Ndoa zina matukio jamani

Ndoa zina matukio jamani

Haswa za kizazi hiki.

Usaliti umekuwa kitu cha kawaida, magomvi kama yote, wengi wanafeki furaha ila ndani kunafurukuta. Matukio ya kutisha, najiuliza walewale waliokuwa wanacheza romantic songs sijui blues kwa hisia na upendo ndo hawahawa leo wanakimbizana na mapanga?

Wamechafukwa hawatamani kuonana tena, ndo hawa kila mmoja kamchoka mwenzake? Wanapigana wengine wanauana.

Ndoa imekuwa kifungo cha maumivu, nimeshuhudia wengi wakiteseka kihisia, kimwili, kiroho nk

Ndoa sio salama tena imekuwa njia ya kujipatia magonjwa ya kila aina, ukitaka magonjwa yote ingia kwenye ndoa na malaya asiejua kuridhika wala kutulia. Ndoa zimegeuka tanzi na mtego.

Hata ukiweka vigezo 100 lakini ukweli watu hubadilika kutokana ma situations zinazotokea maishani. Mpaka baba mchungaji anachepuka. Ukiyumba kiuchumi kidogo tu mwenzio kakukimbia. Ukipata hata ajali ukilala tu kitandani mwenzio anaomba talaka ama anahamia kwa mwingine.

UKITAKA KUINGIA KWENYE NDOA JIPANGE NA UWE NA ROHO NGUMU!
Ukipewa certificate bila kufaulu mitihani kwanza uwe na uhakika huko kwenye hiyo kazi kuna kazi. Ndoa ni kwa ajili ya watu wazima, wenye akili tu sio fashion ya kupendezesha kila mtu.
 
Nlifumaniwa dada nkapigwa ndoa ya mkeka...
emoji38.png
emoji38.png

Kidding
🤣🤣🤣🤣Ningekuja Sasa hivi na pambe yangu nikufanyie single
 
Hakuna raha yoyote kutafuta papa kwa tochi, yaani utoke huko mara unakuja paaap simba wanacheza, hakuna raha, mnasema tu lakini hakuna rahaaaa
Yan bwana wangu afu hajui lini naingia period? Huyo hawezi kuwa bwana angu mimi 😂😂

Raha kuifata
Unafika kila kitu ON…

Sasa nyie, mkikasirikiana kdg hampeani? Mara unapewa huku amekasirika?
Mara unamvizia unadumbukiza
Woi
 
Back
Top Bottom