Miss Champagne
JF-Expert Member
- Sep 2, 2020
- 2,157
- 6,309
Haswa za kizazi hiki.
Usaliti umekuwa kitu cha kawaida, magomvi kama yote, wengi wanafeki furaha ila ndani kunafurukuta. Matukio ya kutisha, najiuliza walewale waliokuwa wanacheza romantic songs sijui blues kwa hisia na upendo ndo hawahawa leo wanakimbizana na mapanga?
Wamechafukwa hawatamani kuonana tena, ndo hawa kila mmoja kamchoka mwenzake? Wanapigana wengine wanauana.
Ndoa imekuwa kifungo cha maumivu, nimeshuhudia wengi wakiteseka kihisia, kimwili, kiroho nk
Ndoa sio salama tena imekuwa njia ya kujipatia magonjwa ya kila aina, ukitaka magonjwa yote ingia kwenye ndoa na malaya asiejua kuridhika wala kutulia. Ndoa zimegeuka tanzi na mtego.
Hata ukiweka vigezo 100 lakini ukweli watu hubadilika kutokana ma situations zinazotokea maishani. Mpaka baba mchungaji anachepuka. Ukiyumba kiuchumi kidogo tu mwenzio kakukimbia. Ukipata hata ajali ukilala tu kitandani mwenzio anaomba talaka ama anahamia kwa mwingine.
UKITAKA KUINGIA KWENYE NDOA JIPANGE NA UWE NA ROHO NGUMU!
Usaliti umekuwa kitu cha kawaida, magomvi kama yote, wengi wanafeki furaha ila ndani kunafurukuta. Matukio ya kutisha, najiuliza walewale waliokuwa wanacheza romantic songs sijui blues kwa hisia na upendo ndo hawahawa leo wanakimbizana na mapanga?
Wamechafukwa hawatamani kuonana tena, ndo hawa kila mmoja kamchoka mwenzake? Wanapigana wengine wanauana.
Ndoa imekuwa kifungo cha maumivu, nimeshuhudia wengi wakiteseka kihisia, kimwili, kiroho nk
Ndoa sio salama tena imekuwa njia ya kujipatia magonjwa ya kila aina, ukitaka magonjwa yote ingia kwenye ndoa na malaya asiejua kuridhika wala kutulia. Ndoa zimegeuka tanzi na mtego.
Hata ukiweka vigezo 100 lakini ukweli watu hubadilika kutokana ma situations zinazotokea maishani. Mpaka baba mchungaji anachepuka. Ukiyumba kiuchumi kidogo tu mwenzio kakukimbia. Ukipata hata ajali ukilala tu kitandani mwenzio anaomba talaka ama anahamia kwa mwingine.
UKITAKA KUINGIA KWENYE NDOA JIPANGE NA UWE NA ROHO NGUMU!