Kwn umelazimishwa kucomment mijitu mingine bhana!?Mkuu ulivyo kuwa unataka kuoa ungetupa taarifa ni muhimu sana
Maana tunaona kama hayatuhusu mambo yenu
Muwe mnatoa taarifa
Vyovyote utakavyochukulia.. Nina experience kubwa sana na welfare za mahusiano kitaaluma n.kNi ukweli mchungu ila pls usiite uboya, yamkini yalishakukuta ama yanaweza kukufika hata wewe siku moja! Pia kumbuka huyu wa jamaa ni mke sio hawara!
mkuu kuanzia uhusiano wetu yeye ndo alikomaa tuwe serious(kipind hiko alikua anatoka kwenye uhusiano na mimi nilikua nipo nipo tu)nilikua namkwepesha nakuwa nae karibu sana kwasabab nilielewa maybe ni maumivu aliyotokea nayo..basi kiutani utani kweli niliamua kudate nae maana nilikua nampenda pia -nilimpenda awali nikajenga ukaribu nae nilivyogundua anapitia a break up nikapunguza mazoea apite salama ila yeye akazidisha eventually tukadateMtoa mada pole sana, ila kabla sijakushauri naomba nkuulize..kumbuka kipindi kile ndo unamtongoza mkeo kwa mara ya kwanza, alikusumbua sana kwa mda mrefu ndo ukampata? Kama alikusumbua kwa mda mrefu alikusumbua kwa mda mrefu kiasi gani? Au ulimpata kirahisi.
Kwenye mwanzo mahusiano yenu kabla hamjaoana, huyo mkeo alikuwa na tabia ya kukuomba pesa hovyo bila mpangilio? Hata kama mizinga yake ilikuwa haikukeri, au Midogo, specify kiasi cha pesa alchokuwa anakuomba. simon baker
mkuu kuanzia uhusiano wetu yeye ndo alikomaa tuwe serious(kipind hiko alikua anatoka kwenye uhusiano na mimi nilikua nipo nipo tu)nilikua namkwepesha nakuwa nae karibu sana kwasabab nilielewa maybe ni maumivu aliyotokea nayo..basi kiutani utani kweli niliamua kudate nae maana nilikua nampenda pia -nilimpenda awali nikajenga ukaribu nae nilivyogundua anapitia a break up nikapunguza mazoea apite salama ila yeye akazidisha eventually tukadateMtoa mada pole sana, ila kabla sijakushauri naomba nkuulize..kumbuka kipindi kile ndo unamtongoza mkeo kwa mara ya kwanza, alikusumbua sana kwa mda mrefu ndo ukampata? Kama alikusumbua kwa mda mrefu alikusumbua kwa mda mrefu kiasi gani? Au ulimpata kirahisi.
Kwenye mwanzo mahusiano yenu kabla hamjaoana, huyo mkeo alikuwa na tabia ya kukuomba pesa hovyo bila mpangilio? Hata kama mizinga yake ilikuwa haikukeri, au Midogo, specify kiasi cha pesa alchokuwa anakuomba. simon baker
Mkuu i am a very emotional person yani nasoma hii huku dah...asante sana mkuuPole brother ,Mungu akiwa upande wetu ni Nani aliye juu yetu,Bibilia inasema Hakuna.
Brother,endelea kuwa mpole na kuendelea kufanya majukumu Kama baba wa Familia.
Note.Endelea kumpenda mke wako vizuri kabisa mwisho wa siku,Mungu atamrejesha na huo uovu wake.
Kitu ambacho unateseka nacho ktk kipindi hichi unapoona mwanamke Hana utii Maana wanaume wengi wanapenda utii kutoka kwa wake zake.
Turudi kwenye maandiko ya Neno la Mungu kidogo.
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.
28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.
30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake.
31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.
Efeso5:------
Omba waihamishie wodi nyingine hata ya watotoBinafsi nipo kwenye ndoa takribani miaka mine na tumebarikiwa watoto wawili. Changamoto zilianza mke alipohamishwa kikazi mwaka juzi kutoka Dar kwenda Morogoro.
Kutokana na ukaribu nikawa najituma sana kutwa kwenda halafu isitoshe huyu mtoto wa pili alikua mwaka mmoja. Umbali ukasababisha mimi niwe mnywaji kidogo kuondoa upweke kuliko niwe nachepuka. Nikawa napunguza safari za kwenda weekend na yeye akazidisha mahusiano ya simu na mfanyakazi mwenzie(sijui kama walitembea ila nilijua wana uhusiano baada ya kunasa chat maana ilifika kipindi anajua weekend nalala ndo anakua busy kwa simu wakiongea na huyo mpaka nilivyombana na chats aka admit wanamahusiano via simu na huyo mtu yupo Dar).
Siku moja nikaenda Moro ghafla nikakuta anachat nae bado na isitoshe kuna mwingine wa Moro; nilimdunda hatari. Tukasuluhishwa na familia baada ya hapo kila tukikwaruzana kidogo anakimbilia kusisitiza tuachane yaani ndo ukawa wimbo.
Sasa nikaona kuondoa usumbufu na yeye kuhamia Dar aligoma kwa kusema maisha nafuu Moro nikatafuta kazi Moro nikahamia(nilipata kazi half the pay ya Dar) ila nilimweleza la msingi tuwe pamoja tuweze nusuru ndoa.
Sasa tangu tumeamua kukaa pamoja mambo hayajawa mepesi. Mimi na-cover basic needs kama kawaida yangu na napambana na biashara ila mwenzangu amekuwa amepotea kabisa kimapenzi. Tangu mwaka huu tunaweza kuwa tumesex si zaida ya mara 15 am sure maana mwenzangu hayupo kabisa anaona nimembana sana.
Kila kitu anatupia lawama nivomdundaga na matatizo ya nyuma. Nimejitahid kumpa space sana ila naona kitu kidogo anakimbilia kutaka talaka.
Sasa kilichonipelekea kuandika uzi huu ni majuzi nilimwambia naenda Dar maana alikua yupo moody sikujua ni sababu yangu au lah. Nikamwambia tu nina safari ya Dar week nzima; aisee alifurahii sana.
Safari ilikuwa ya siku mbili nikarejea jioni nikamtafuta kwenye simu akawa hapokei alivyotoka kibaruani. Jirani yetu ni mfanyakaz mwenzie akarudi tukapishana nikamuuliza vipi shoga yako akasema tumeachana amesema anapita sokoni mara moja (nikaona very rare kutorudi na shoga yake).
Wife akanitumia meseji akasema ametoka outing na shoga zake. Nikasema fine mimi nikanyuti nje mtaa wa pili kuona nani angerudi nae.
Kuna gari ikaja ikapaki kwa jirani ikakaa dakika kama 15 akashuka halafu gari ikaondoka. Alivyoingia ndani nami nikamfwata kwa nyuma
akashtuka sana. Nikamuuliza nani akasema rafiki yake tu walienda pata wine.
Nikamwambia naomba uwe makini tu kuna maradhi. Kama tumefikia huko naomba basi uwe na amani ufanye yako na si hapa kwangu na isitoshe tuna watoto wadogo usilete jazba kwenye haya mambo(maana tulivoingia ndani akaanza kuwaka kama simuamini alivyosema yupo outing nikamweleza outing sio issue ishu umetoka huko mkaweka kambi kwenye gari mie nawaona tu mnapiga story hamkumaliza huko outing)
Nimegundua hana mapenz kwa sasa na nimevumilia sana vituko vyake ila nawaza niwashirikishe wazazi wake na wadhamini wetu nataka niwachukue wanangu nirudi Dar nimpe nafasi tu.
Mkewangu ananiuma sana kila nikikumbuka nilivyompata, mahusiano yetu nk. Yeye ndo alikuwa kipaumbele kunitia sana moyo pale nilipokwama au kusita jambo(hii naandika kwa majonzi sana)
Umri wake haujazidi 30 bado na kuna muda naamini alingia ndoani akiwa mdogo sijui kuna mambo hajafanya? Ila mimi ni mtu wa kuwa huru sana namwambiaga nishirikishe nikupe kibali sina hiyana wala nini cha msingi ni imani tu kwamba hatavuka mipaka.
Suala la uwezo sijalitilia uzito maana yeye binafsi ana kazi na mshahara wake kwakweli huwa simgusiagi hata kidogo anafanya atakavyo. Mimi nina nyumba Dar ndo nimepangisha kuja kuishi naye huku. In short majukumu yangu nayajua na nayamudu.
Suala la kitandani lilikuwa zuri tu sote tunafurahi nk. Mwaka huu lilianza kususasua penzi la kubembeleza yeye ata enjoy ila mpaka nimemuandaa nimemconvince mbona shughuli.
Kwa upande wangu sio mnywaji sana na anajua. Nikinywa tu wine nikiwa nae ntajitahid kumueleza kiu yangu juu ya mambo ambayo hanitimizii hapo nae atarukia "si uniache"bas mkibishana atasema mlevi tatizo.
Weekend ndo tunakaa na kujadili mambo ila mara chache sana maana katikati ya wiki akirudi home yeye kachoka ni kula kulala tu.
Mimi ni mwanadamu pia naweza kuwa na mapungufuyangu ila all i know kuachilia mbali kila jambo nimekuwa nikijitahid kuomba msamaha ninapokosea nk.
Ndugu zangu ndo wanaona nimekamatwa kwelikweli ila nakuwa najitahid niishi ki maadili maana mke mwenyewe mmoja.
Nimesali sana mpaka nimeona kama ni watoto hata nikisema nimpotezee nitahitaji kuwaona wanangu ambapo itapelekea nimwone labda na yeye kitu ambacho mda mwingi kinaniwia ngumu kuvunja familia. Ila nikisema nibebe watoto(namjua kwa sasa majibu yake atasema nenda nao tu la msingi tuachaneee nk) nitabeba ila nataka niombe nisingependa kusikia pua yake na wakwe ndo watakua gia ya kuwaona. Ninataka full right ya wanangu nina uwezo wa kuwalea vizuri. Yani naumia sana ila naona ndo best option kwa sasa.
Naomba ushauri wenu wakuu
30 mkuuUna umri gani mkuu?
HakikaVyovyote utakavyochukulia.. Nina experience kubwa sana na welfare za mahusiano kitaaluma n.k
Nasema hivi , msimamo wangu ni ule ule. Unapoona dalili za kuumizwa na mwanamke tafuta mikakati ya kujinasua either
1. Kumpiga chini
2. Kuendelea kuwa nae ila potezea na vumilia kila Kitu (Ni wanaume wachache wanaweza hii)
Kinyume na hapo utakufa na kuacha wanao wanateseka bure huku mkeo akiendelea kuliwa uroda na mabazazi. Ifike muda nyeusi tuseme nyeusi tusipake rangi. Wanaume tunajitfutia vifo kwa mikono yetu.
Hakuna maamuzi magumu yasiyokuja na maumivu. Apige moyo konde atapata mtu sahihi. Sio kuendelea kulialia huo sio uanaume. Uanaume ni maamuzi magumu. Maamuzi magumu sio kuruka sarakasi ubungo mpaka chanika pekee. Kuwa imara kwa nyakati kama hizi kunapima "Uanaume" pia.
Please mkuu nikuombe tena kwa Ustawi Wa maisha yako achana na huyo mke kabla hali haijawa mbali. Kama MTU hakutaki anashindwaje kukuwekea hata sumu ?? Angalia hili kwa jicho la tatu. Unaweza kuishi na simba lakini sio Mke au Mme asiekutaka. Ni kujitafutia mabalaa tu.
Najua maumivu anayopitia Mkuu ila siku zote lazima uhalisia Wa mambo ndio uakisi maamuzi. Kama anaona hali anazopitia anaweza kuendelea na Mke wake , namuomba aendelee na Mke wake. Mimi macho na masikio Yangu natega Redion na habari za magazetini.
Dah kweli halafu mwanamke wa kupishana nae umri kidogo hivyo ndio huwa wanakuwaga viburi sana! At least umuache 5 years and above wanakuwaga na hali ya kuogopa kufanya ujinga!30 mkuu
Mwenzangu 27
Mkuusalama?Pole mkuu binafsi nilikuwa sielewi kwa nini wanasema wanaume tumeumbwa mateso...but hapo mwisho umeweka vitisho acha watu wakupe nyeusi na nyeupe ili ujue wapi palekebishwe....kwa mfano sijaona sababu ya wewe kuhamia Moro na nyumba unayo Dar hilo tu linaonyesha hukusimama imara....