Ndoa yangu ipo ICU !dah

Ndoa yangu ipo ICU !dah

Mwanaume kukaa unalia kisa mwanamke anakusumbua ni ujinga kwa kiwango kilichopitiliza.

Ningekuwa nilishaoa mke mwingine siku nyingi Sana.
Wanawake wako wengi Sana na wengine hawataki hata hivyo vinaitwa vyeti vya ndoa.

Ndio maana wazee wetu walikuwa wanaoa mke zaidi ya mmoja. Inapunguza uzinguzi Kama huu.
Ndugu yangu mkeo keshapata wa kumkuna Tena Ni mume wa mtu.
Muache uone Kama naye ataendelea.
Huwa inatokea hivyo kwa Sababu anakuwepo wa kumtunza. Asipokuwepo tu na sie huwa tunakula Kona maana majukumu yote unaachiwa wewe
 
Pole brother ,Mungu akiwa upande wetu ni Nani aliye juu yetu,Bibilia inasema Hakuna.
Brother,endelea kuwa mpole na kuendelea kufanya majukumu Kama baba wa Familia.
Note.Endelea kumpenda mke wako vizuri kabisa mwisho wa siku,Mungu atamrejesha na huo uovu wake.
Kitu ambacho unateseka nacho ktk kipindi hichi unapoona mwanamke Hana utii Maana wanaume wengi wanapenda utii kutoka kwa wake zake.

Turudi kwenye maandiko ya Neno la Mungu kidogo.
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.
28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.
30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake.
31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.
Efeso5:------
Mungu hapendi watu wanaoishi kwa shida na dhambi wanatenda.
Kila siku kuchukiana kisa nini?
Mtu mwenyewe mmekutana ukubwani ndio akukoseshe raha duniani!?
 
Mkuu pole sana
Huyo mwanamke mapenzi yameshaisha kwako ndio shida za kutokula ujana enzi za usichana hizi ukiamua kuingia kwenye ndoa ushamaliza kila kitu unatulia na ndoa yako hakuna cha kukusumbua

Huyo sasa hivi anajiuliza alikuwa wapi siku zote hajakutana na raha hizo anajuta ata kwa nn aliolewa pole sana mkuu
Kuna mahusiano kweli shemeji kati ya kuto kula ujana na kutokutulia katika ndoa
 
pole sana mkuu. Cha msingi achananae, wew sio Wa kwanza kama utamuacha...
 
Dah kiukweli mie nina wasifu kama wa mtoa mada, nina moyo wa kusamehe sana na mzito kuvunja mahusiano ila too bad sie ndio aina ya vidume tunaosumbuliwa sana na wanawake! Unakuwa very gentle ila unapata mtu asiejua ana nini ukimuacha anakuja kulia lia very lately!
Wanawake wanapenda badboys ,,,wakuwapelekesha pelekesha
 
mkuu to be honesy kila nikifikiria hii road naumiaga sana na niombe niwe imara kwa hili
Kuna siku nilikuta vyakujipimia ngoma anavyo..niliishiwa pozi kumuuliza nilisubir tupo outing tukiwa tume refresh nikamuuliza angependa tukapime sote maana nilikuta kachukua hatua mwenyew maana sijajua kama either mimi nilisababishia ahofie au yeye tu mwenyewe aliniuliza umeaza lin kupekua vitu vyangu..nikachoka
Ujue alitoka namtu ambae hamwamini alipata mashaka baada ya kudo nae take care lakini
 
Yaan wanawake wote hawa nchi hii bado unalazimisha penzi kiasi hicho?yaan umemkuta mkeo ana vifaa vya kupimia ukimwi bado unalazimimsha eti kisa watoto?yaan mkeo analetwa na gar eti alikua outing bado unalazimsha kuish nae..yaan mkeo anakwambia umuache bado unalazimisha..daahh subir magonjwa sasa maana hakuna namna ..
 
Back
Top Bottom