Fugwe
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 1,676
- 664
- Thread starter
- #41
Kiukweli tatizo lipo,kama wewe umekua muungwana na umekuja hapa,inaonekana kuwa unahitaji suluhu.
"
Lakini suluhu hupatikana pale ambapo pande zote mbili zinapokuwa tayari kuitafuta,hili kwa mkeo kwa kiasi inaonekana halipo.
"
Kwa mujibu wa maelezo yako mkeo inaonekana na mtu pembeni,na pia haithamini tena familia.
"
Nimesema hivyo kwa kuwa umesema mnapogombana anakuwa hajishughulishi sana na mambo ya familia.Haya ni matokeo ya mtu mwenye ushirika na mtu mwingine.
"
Anaona familia sio yake na huduma yake kwenye familia hiyo ni kama msaada,hii inasababishwa na ushirika wake kwenye familia nyingine anayoithamini kwa sasa.
"
Kwa sasa ni kuwa kutokana na mambo yalivyo huenda akawa anafanya mambo kwa maelekezo kutoka kwa mtu mwingine,kuna uwezekano wa kukudhuru kama ni mpenda mali au huyo mtu mwingine ni mpenda mali.
"
Siwezi kukuambia uachane na mkeo,ila endelea kutafuta suluhu huenda ikapatikana ikishindikana,utaamua mwenyewe
"
"Mwanamke ni mtihani mwingine kwa mwanaume baada ya pesa",maneno haya yalizungumzwa na Lucky Dube alipokua anahojiwa na chanel 0 mwaka 2001!!
EIYER,
Nakushukuru, kweli option ya kuachana sio priority lakini yakinizidi basi. Nashukuru naendelea kuyafanyia kazi kweli inaniuma na kunipotezea heshma kwa watu wanaonizunguka