Ndoa yangu iko njia panda, nifanyeje?

Ndoa yangu iko njia panda, nifanyeje?

du! pole mkuu, mtangulize Mungu kwenye maamuzi yako utakayochukua pia usiwe na hasira. kwa muda wote mliooana, mmevumiliana mengi mpaka mmefika hapo hivyo mfanikiwe kutatua tatizo hili.
 
Kuna uwezekano mkeo akawa limbukeni au amejiona sasa anaweza kuwa kila kitu bila wewe. Ingawa stori yako ni upande mmoja, uwezekano wa kukudhuru ni mkubwa hasa kama anatoka kwenye makabila yanayojulikana kwa tabia hiyo. Muhimu kaa ufikiri na umuite umpe ukweli wa moyoni bila vitisho wala kugusia kuwa unataka kuachana naye. Akijua kuwa una mpango huo atakuwahi na kukuharibia maisha. Ningekuwa wewe ningebadili usimamizi wa mali kiasi cha kupunguza kipato chake. Ningeweza hata kujaribu kumpunguzia hiyo biashara nikimpa somo kuwa kukaa nyumbani ni jambo muhimu. Kama anakunyima chakula cha bwana basi kuna kidudu mtu ambaye ameishamuingia. Fanya utafiti ujue kiburi chake kinatoka wapi ili ujue jinsi ya kupambana naye. Waweza kuanza ku-diversify miradi yako ili kuanza kukusanya nguvu mpya in case if anything happened. Nadhani kwa leo haya yanatosha mwanangu. POLE SANA KWA YANAYOKUKUTA.

Father of All,
Nashukuru kwa uchambuzi na ushauri ulitoa. Maana haiwezekani anichanjie ghafla, najua simulizi inaonekana ya upande mmoja lakini huwa na kaa na kufikiri ni wapi nimekosea, naona mbona sina kosa linalolingana na adhabu ninayopewa, Asante kaka
 
du! pole mkuu, mtangulize Mungu kwenye maamuzi yako utakayochukua pia usiwe na hasira. kwa muda wote mliooana, mmevumiliana mengi mpaka mmefika hapo hivyo mfanikiwe kutatua tatizo hili.

BelindaJacob,
Nikushukuru, maana huwa naona hata aibu kusema eti nimeachana na mke wangu kwa umri niliofikia. Naendelea mimi mwenyewe kufanya yaliyosahihi mbele yake angalau kum-attract naye ajue wajibu wake kwa mume wake. Ile dhana ya kifo ndicho kitutenganisha yaonekana nikaikosa. Asante kwa ushauri wako
 
Inauma sana kama ni mume wa namna hiyo halafu Mkeo anakunyima mchezo kwa miaka miwili. Kama binadamu lazima nawe utakuwa na mapungufu yako lakini miaka miwili unatoka kapa!!! Duh! Una moyo sana Mkuu!! Mie hata sijui nikushauri nini maana mengi inaelekea mmeshayafanya kuinusuru ndoa yenu lakini bila mafanikio. Pole sana Mkuu.
 
Father of All,
Nashukuru kwa uchambuzi na ushauri ulitoa. Maana haiwezekani anichanjie ghafla, najua simulizi inaonekana ya upande mmoja lakini huwa na kaa na kufikiri ni wapi nimekosea, naona mbona sina kosa linalolingana na adhabu ninayopewa, Asante kaka
Mwanangu Fugwe usijali. Maisha ni kusaidiana. Huyu ajua hili na yule lile ilmradi maisha yanakwenda. Nimefurahi kusikia kuwa angalau nimeweza kutoa mchango. Usikubali kushindwa wala kutoa maamuzi kwa hasira au kukomoana bali kujinasua na janga ulilomo.
 
Nina uhakika wewe ndio kikwazo kwenye hiyo ndoa na sio mkeo.jirekebishe.
1.punguza majukumu uliyompatia nusu
2.kuna kidume kinahudumiwa pembeni kama huoni hela na zilichofanyia.
3.hiyo miaka yenu imeanza kugonga life expectancy pataneni mfaane uzeeni jamani ni hayo tu.ila angalia wanawake noma asijekuwekea sumu ufe.kama ni wakristo mkonsult mchungaji wako tapika yote naye atapike yote mkaanze maisha upya.unategemea ukimbie nyumba mwanaume ujana umeulia hapo ,hapo umevallia jeans na kaptula ,nani atakupokea ukamvalie msuli weye!!!
 
Rafiki yangu aliyesimamia arusi yangu aliniambia kipindi fulani kuwa mke wake alimnyima tendo la ndoa kwa miaka 3 nikadhani ni uongo ni sehemu ya mazungumzo yakuniandaa kwa ajili ya ndoa kumbe inatokea..Da sijui kwangu ikianza kutokea itakuwaje..
 
Pole sana, unahitaji kuyaishi haya maisha ndio ujue cha kushauri, huyo mkeo keshajiunga na timu asikudanganye mtu kuwa mta -reconcile, huyo keshapanga mgawane mali, makosa ni uhuru uliompa, nasema haya yamenikuta. Tafuta mwanasheria ujue pa kuanzia, natamani nikuulize maswali mengine lakini hapa kwenye public sio sehemu yake, waweza ni pm tuweze ku-brainstorm
 
Nahitaji ushauri wenu wanaJF,
Ndoa yangu ina umri wa miaka 21 na mimi mwenyewe nina umri wa miaka 46. Katika ndoa yetu tumejaliwa kupata watoto 3. Mke wangu yeye ni mjasiria mali (siwezi kusema ni mama wa home) kwani anasimamia vijimiradi vya familia na mimi nimwajiriwa wa seriakli. Katika maisha ya ndoa mimi kama baba nimejenga nyumba 2, nina usafiri mzuri magari 3, nina mashamba 2 ya nguvu na vimifugo kidogo si haba. kati ya hivyo vyote hakuna senti iliyotoka mfukoni mwa wife. Nyumbani kama mnavyofahamu kuna facilities za kumuwezesha wife aihudumie familia kwa urahisi, kule kitchen kila kifaa cha kurahisisha mapishi kipo.

Sikilizeni tatizo lilipo, kama mnavyojua sahani zikikaa pamoja lazima zigongane, sasa ikitokea kutoelewana wife hawajibiki kwa maana sipikiwi chai, hakuna kusimamia mafundi na vibarua wataachwa wachakachue wapendavyo, achilia mbali tendo la ndoa ambalo lazima nisahau. Kaenda mbali ndugu kawaambia ninavyomnyanyasa nao bila kuuliza wameungana naye. mambo hayo ni karibu miaka 5 na zaidi hakuna maelewano ndani ya nyumba. Labda nijisemee na mimi, kweli najijua nina hasira lakini pamoja na hayo kwa miaka yote hiyo 21 ya ndoa sijawahi kunyosha mkono kumpiga wife, kurudi nyumbani usiku sio tabia yangu, sina mtoto wa nje wala small house na sijawahi lala nje hata siku moja. Nilikuwa nikipokea mshahara namkabidhi, then naomba hela ya matumizi lakini yeye hela inayopatikana kwenye vijimradi vyetu sijui inatumikaje.

Hatua tulizochukua kujaribu kupata muafaka, sisi wenyewe tumekaa several time hakuna kusikilizana ikabidi tushirikishe family friend tunakaa kidogo yanajirudia, ndugu wa pande zote wamejaribu hakuna muafaka, Hali iliyopo sisi wenyewe hatuwezi tena kuyamaliza ingawa ndio tulikuwa na dhamana ya kuyamaliza.

Nipeni ushauri, ni-sacrify kila kitu niondoke zangu? maana naona uchungu eti tugawane mali wakati najua nina madeni bank kwa ajili ya mali hizo ambapo yeye hakuchangia achilia mbali usemi wa sasa hivi kwamba mali ya ndoa ni ya wanandoa wote. Nitafute small house maana tunda nimeshanyimwa takribani mk2 sasa. Nisiwachose, maoni yenu tafadhali


Relax kaka. Hivi kweli huyo shetani unamruhusu avunje ndoa yako hivi hivi? Wewe kwa sababu ni muelewa endelea kutafuta suluhu ya hayo matatizlo, nina imani yataisha tena very soon. Bila wewe hao watoto wataathirika sana, watendeeni haki watoto wenu.

Huyo mama nahisi ni wakati wako wa kunyoosha mkono umchape makofi tena mengi ila usimtie ngeu. Omba likizo uanze kufatilia kimoja baada ya kingine, usione aibu. Ainisha makosa yake ya kishenzi yote halafu ita ndugu, jamaa na marafiki waamulie ugonvi.

Narudia tena usimruhusu shetani akakuongoza kwenye maamuzi. Mwanaume unahama unaena wapi?

Mungu akutie nguvu sana.
 
kaka pole sana kwa makubwa hayo yanayokusibu ndani ya ndoa yako....nimesoma btwn lines na nimegundua machache ambayo yanaweza kuwa chanzo cha matatizo yako ya ndoa.

1- sijajuwa vizuri age difference kati yako na mkeo...isijekuwa umeoa mtoto mdogo ukilinganisha na umri wako na yeye akawa damu inamchemka wakati wewe inapoa..ndo maana 2years kakunyima ndoa unakutoa anapata huduma kwa sharobaro wa jirani kwako

2-hasira zako pia zinaweza kwa asilimia kubwa kuwa chanzo cha tatizo na kutopiga/kupigana hakumaanishi kuwa humuumizi mwenzako na hasa psychological torture kitu ambacho kwa wenzetu huwa kinawakaa sana moyoni na kuwaumiza sana...na naamini kwa hasira zako huwa unatoa kauli zinazomfanya yeye (kama mama wa nyumbani na msimamizi wa miradi unayoibuni wewe) kujiona akinyanyaswa.

3- ndoa yako hapo ilipofikia ni matunda ya uzembe wenu wote kwa pamoja kutokuwa karibu katika kushirikishana kipato na matumizi ya mapato ya miradi yenu... sio jambo jema na la hekima kusema kuwa hujui pesa ya miradi anayoisimamia mama inakwenda wapi na hasa ukiwa kama baba na kichwa cha familia...hata kama unampatia mshahara wako wote ni lazima ujuwe pia miradi imeingiza kiasi gani na kinatumikaje na yeye analipwa kiasi gani kwa usimamizi wa miradi hiyo.

4- nachokiona pia ni uoga wako wa kutaka kugawana mali mlizochuma pamoja na mkeo wa ndoa in 26 years. unanipa picha kuwa mngekuwa hamjachuma mali basi ulikuwa tayari kuachana na mkeo...hii inamaanisha upendo hakuna na uvumilivu umekushinda.

NASHAURI YAFUATAYO:-
1-KWANZA HUJACHELEWA BADO...JIFANYE MJINGA PIGA GOTI MUOMBE MSAMAA MKEO KWA YOTE YALE ANAYOAMINI KUWA UMEMKOSEA NA MWOMBE AKUPE NAFASI YA KUJIREKEBISHA MUANZE UPYA.

2-MPUMGUZIE KIPATO KISICHOKUWA NA MATUMIZI KWA KUMPATIA MAJUKUMU ATAKAYOYATEKELEZA KUPITIA MAPATO YA MIRADI YENU IKIWAMO KULIPIA KARO ZA WATOTO NA KULIPIA VITU KAMA INSURANCE ZA MAGARI, AFYA NA MENGINEYO ..HII ITAMFANYA AJIONE MWENYE MAJUKUMU NA KUMPUNGUZIA PESA AU KIPATO CHA YEYE KUMILIKI PASI MATUMIZI YASOJULIKANA.

3-MKUMBUSHE KUWA MULIPOFIKIA SIO TENA UMRI WA KUGOMBANA NI UMRI WA KUJENGE MAISHA YENU NA HASA YA UZEENI NA MAHUSIANO YAKO NA NDUGUZE YAWE KARIBU NA JITOLEE NA JITOE KATIKA SHUGHULI ZA SHIDA NA RAHA KWA UPANDE WA MKEWE..AMINI NDUGUZE WATAKUPENDA NA KUWASUPPORT NYOTE NA SIO KAMA SAHIVI WANAMSUPPORT YEYE NA KUONA WEWE UNAMNYANYASA.

4- KUWENI WACHAMUNGU NA MUNGU ATAWABARIKI NINYI NA UZAO WENU...KAMA NI MKRISTO MZURI UTAKUWA UNAFAHAMU HABARI ZA AYUBU.
 
Kweli wewe ni bushoke mwingine miaka miwili unanyimwa wakati mke wako anagawa kwingine tafuta small house coz na yeye ana marioo mwingine..
 
Relax kaka. Hivi kweli huyo shetani unamruhusu avunje ndoa yako hivi hivi? Wewe kwa sababu ni muelewa endelea kutafuta suluhu ya hayo matatizlo, nina imani yataisha tena very soon. Bila wewe hao watoto wataathirika sana, watendeeni haki watoto wenu.

Huyo mama nahisi ni wakati wako wa kunyoosha mkono umchape makofi tena mengi ila usimtie ngeu. Omba likizo uanze kufatilia kimoja baada ya kingine, usione aibu. Ainisha makosa yake ya kishenzi yote halafu ita ndugu, jamaa na marafiki waamulie ugonvi.

Narudia tena usimruhusu shetani akakuongoza kwenye maamuzi. Mwanaume unahama unaena wapi?

Mungu akutie nguvu sana.

CAROLINE DANZI...hapo nilipo-bold naona unataka ndugu yetu achezee mvua za kutosha....

kati ya kitu asichotakiwa kufanya ni hicho na kwa kosa hilo naona kina mama ananilea nkya na kijo helen bisimba na usu mallya wanavyo-mtolea uvivu ndugu yetu na kuishia segerea kwa miaka mi-5.

na akirudi anakuta mkewe keshaolewa na anawatoto wengine wa-3 na baba mpya na mali zote zishauzwa then anakuwa chizi au anakufa hapohapo.

WANAHARAKATI WA JINSIA WANASEMA MVUMO DUME NI MBAYA...ILA DONT EVEN THINK OF TRYING OTHERWISE...MVUMO JIKE UNAUWA SI MZURI KWA MATUMIZI YA BINADAMU HASA HUKU KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA.
 
CAROLINE DANZI...hapo nilipo-bold naona unataka ndugu yetu achezee mvua za kutosha....

kati ya kitu asichotakiwa kufanya ni hicho na kwa kosa hilo naona kina mama ananilea nkya na kijo helen bisimba na usu mallya wanavyo-mtolea uvivu ndugu yetu na kuishia segerea kwa miaka mi-5.

na akirudi anakuta mkewe keshaolewa na anawatoto wengine wa-3 na baba mpya na mali zote zishauzwa then anakuwa chizi au anakufa hapohapo.

WANAHARAKATI WA JINSIA WANASEMA MVUMO DUME NI MBAYA...ILA DONT EVEN THINK OF TRYING OTHERWISE...MVUMO JIKE UNAUWA SI MZURI KWA MATUMIZI YA BINADAMU HASA HUKU KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA.

hakuna watu wajinga kama hao wana harakati, hawana msaada wowote wanapenda kuonekana kwenye TV ili wajulikane wapo. Chapa kofi moja uone mambo yanavyokimbia.

Whocares inafika wakati mtu inabidi utumie mbinu mbadala.
 
Mungu wangu . . . . . !!Ngoja nikamalize haka ka shughuli nije,jamani katika jambo gumu ni kuishi na mtu!
"
Dah!Kweli huu ni mtihani mkubwa!Nitarudi . . . . . !!
 
Nahitaji ushauri wenu wanaJF,
Ndoa yangu ina umri wa miaka 21 na mimi mwenyewe nina umri wa miaka 46. Katika ndoa yetu tumejaliwa kupata watoto 3. Mke wangu yeye ni mjasiria mali (siwezi kusema ni mama wa home) kwani anasimamia vijimiradi vya familia na mimi nimwajiriwa wa seriakli. Katika maisha ya ndoa mimi kama baba nimejenga nyumba 2, nina usafiri mzuri magari 3, nina mashamba 2 ya nguvu na vimifugo kidogo si haba. kati ya hivyo vyote hakuna senti iliyotoka mfukoni mwa wife. Nyumbani kama mnavyofahamu kuna facilities za kumuwezesha wife aihudumie familia kwa urahisi, kule kitchen kila kifaa cha kurahisisha mapishi kipo.

Sikilizeni tatizo lilipo, kama mnavyojua sahani zikikaa pamoja lazima zigongane, sasa ikitokea kutoelewana wife hawajibiki kwa maana sipikiwi chai, hakuna kusimamia mafundi na vibarua wataachwa wachakachue wapendavyo, achilia mbali tendo la ndoa ambalo lazima nisahau. Kaenda mbali ndugu kawaambia ninavyomnyanyasa nao bila kuuliza wameungana naye. mambo hayo ni karibu miaka 5 na zaidi hakuna maelewano ndani ya nyumba. Labda nijisemee na mimi, kweli najijua nina hasira lakini pamoja na hayo kwa miaka yote hiyo 21 ya ndoa sijawahi kunyosha mkono kumpiga wife, kurudi nyumbani usiku sio tabia yangu, sina mtoto wa nje wala small house na sijawahi lala nje hata siku moja. Nilikuwa nikipokea mshahara namkabidhi, then naomba hela ya matumizi lakini yeye hela inayopatikana kwenye vijimradi vyetu sijui inatumikaje.

Hatua tulizochukua kujaribu kupata muafaka, sisi wenyewe tumekaa several time hakuna kusikilizana ikabidi tushirikishe family friend tunakaa kidogo yanajirudia, ndugu wa pande zote wamejaribu hakuna muafaka, Hali iliyopo sisi wenyewe hatuwezi tena kuyamaliza ingawa ndio tulikuwa na dhamana ya kuyamaliza.

Nipeni ushauri, ni-sacrify kila kitu niondoke zangu? maana naona uchungu eti tugawane mali wakati najua nina madeni bank kwa ajili ya mali hizo ambapo yeye hakuchangia achilia mbali usemi wa sasa hivi kwamba mali ya ndoa ni ya wanandoa wote. Nitafute small house maana tunda nimeshanyimwa takribani mk2 sasa. Nisiwachose, maoni yenu tafadhali


Rafiki,
Ndoa haina ushauri wa nje.
 
Kiukweli tatizo lipo,kama wewe umekua muungwana na umekuja hapa,inaonekana kuwa unahitaji suluhu.
"
Lakini suluhu hupatikana pale ambapo pande zote mbili zinapokuwa tayari kuitafuta,hili kwa mkeo kwa kiasi inaonekana halipo.
"
Kwa mujibu wa maelezo yako mkeo inaonekana na mtu pembeni,na pia haithamini tena familia.
"
Nimesema hivyo kwa kuwa umesema mnapogombana anakuwa hajishughulishi sana na mambo ya familia.Haya ni matokeo ya mtu mwenye ushirika na mtu mwingine.
"
Anaona familia sio yake na huduma yake kwenye familia hiyo ni kama msaada,hii inasababishwa na ushirika wake kwenye familia nyingine anayoithamini kwa sasa.
"
Kwa sasa ni kuwa kutokana na mambo yalivyo huenda akawa anafanya mambo kwa maelekezo kutoka kwa mtu mwingine,kuna uwezekano wa kukudhuru kama ni mpenda mali au huyo mtu mwingine ni mpenda mali.
"
Siwezi kukuambia uachane na mkeo,ila endelea kutafuta suluhu huenda ikapatikana ikishindikana,utaamua mwenyewe
"
"Mwanamke ni mtihani mwingine kwa mwanaume baada ya pesa",maneno haya yalizungumzwa na Lucky Dube alipokua anahojiwa na chanel 0 mwaka 2001!!
 
Mimi si mshabiki wa nyumba ndogo lakini mazingira yako hayo yanaweza kushawishi uwe na nyumba ndogo. Maana kuvunjwa kwa ndoa huko sishauri kabisa. Kinachoweza kufanyika ni kujikausha tu, na kujifanya kama huoni kinachoendelea, focus kwenye watoto kuhakikisha mahitaji yao yote wanapata lakini huduma nyingine za upendo na ndoa uzitafute mahali pengine.
Kama akiona hujali, anaweza kuanza kutafuta namna ya kureconcile. Kuna watu wengi hapa mjini wanaishi kwa style hiyo. Yeye home anarudi kulala na kwa ajili ya watoto na miradi yake tu. Ila ni jambo gumu pia, though ni nafuu zaidi kuliko kuachana.

LUKOLO,
Nakushukuru sana kwa ushauri huo, sijakata tamaa naendelea kusaka muafaka, option uliyonipa inafanya kazi pia ingawa ni ya uchungu kama ulivyosema mwenyewe
 
Back
Top Bottom