Ndoa miaka 11 naomba ushauri

Ndoa miaka 11 naomba ushauri

Ndugu zangu ambao mpo kwenye ndoa naombeni ushauri kabla sijafanya maamuzi yangu mwenyewe.

Nipo kwenye hii ndoa kwa miaka 11 ila mwanamke ambaye nilikutana nae alikuwa na mtoto tayari ila naomba niseme alikuwa mwenyewe na mtoto wa miaka 2 mwanaume wake alimkimbia, sasa baada ya hapo mwanaume wake wa zamani kufahamu huyu mwanamke ana mwanaume mwingine siku moja akaniambia kwamba huyu mwanamke huwezi kuja kumzalisha maisha yako yote hata iweje.

Ndugu zangu mpaka leo huyu mwanamke amepata mimba mara 3 ila zote zimetoka. Sasa baada ya hapo mwanamke akaanza kunidharau na kuniambia kwamba sina mbegu za kumzalisha. Me kama mwanaume nikapoteza confidence nikaenda kupiga nje na nimepata mtoto vizuri bila shida kabisa

Sasa amekuja kugundua kwamba me nimezaa nje ila nilivumilia mateso yote na maneno yote ya mateso na alikuwa muda wote ananidharau sana na kusema hata iweje umenikuta na mtoto na taka usitake siwezi kuacha kuongea na baba wa mtoto.

Akinikuta nakunywa anamwaga drinks zote kwenye sink.

Sasa jana usiku nimepigwa vyupa vibaya sana damu nyingi zimetoka sababu anataka tuwe tunatumia password moja, ameingia kwenye simu amekuta yule mwanamke mwingine mwenye mtoto amenitumia picha za mtoto.

Baada ya hapo akanitukania wazazi wote na kuwaita Idiots familia nzima pamoja na mimi...

Nilikuwa tu naomba ushauri nini cha kufanya ila tumeenda hospitali tumegundua zile mimba 3 alipata moja imeziba mirija yake ya uzazi so hawezi pata mimba kwa njia ya kawaida.

Naombeni ushauri wenu tafadhali kwa hili suala.

Je, bora niondoke?
Wewe ni mdhaifu.

Anakutawala huyo.
 
Hapo hamna ndoa ndugu
Uneshaambiwa hauwezi kuzaa naye ina maana jamaa kashamuendea kwa wataalamu
Mwanamke kashakwambia hawezi kuacha kuongea na mzazi mwenzake inamaanisha kwamba jamaa anamla unayemuita mke wako
Mshaanza kupigana chupa na kumwagana damu utakuja upigwe bisu la tumbo au uwekewe sumu ufe
Nenda kaishi na mwanamke uliyezaa naye huyo hakufai
 
Wanawake wasio na watoto wako wengi sana dunia hii,ikawaje ukaoa Single Maza?
 
Kila tukigombana anasema ndoa imeisha mda mrefu sana
Sasa kwanini bado unataka kuwa nae, mna watoto? Hata kama kakuambia tangu...

Sasa hata unyumba hatoi tena anakataa kabisaa
Sasa si hana hisia na wewe tangu aanze kukupa kwa kujilazimisha na sasa hivi ni live anakukataq, hisia zake zipo huko umeona tayari na labda kwa mwingine au wengine. Mwanamke akikata hisia kabisa ni ngumu kukutaka hata kiuongo.
Si umeisha iba nje... au alikuwa sukari kwako?..

kabisaa...Anasema anajuta hata baba wa mtoto wake alikuwa ana mtreat vizuri kuliko mimi
Mwanamke akifika kukufananisha hata hayo maneno basi ujue hakutaki kakuchoka, anatamani umuache au muachane ila bado hautaki kuachanq. Maneno kama haya huwa yanamaanishwa kwa asilimia kubwaa. Wanawwke wengine hawata tamka kujipotezea muda ni bye bye live unabaki mataa..ila huyu kakupa ukweli nawe bado hutaki kukubali

Na jamaa alikuwa anampiga vibaya sanaa sio kidogo
mmmmh halafu anakuambia hayo maneno juu..kuna ambayo haufahamu. Inawezekana aliachwa huku bado anampenda nawe ukawa kipoozeo au wa kukutumia kumkomoa huyo.. sasa labda wameona hawawezi kuishi bila kuwa pamoja..
....ila amejaribu kwangu na ni professional nikimgusa ataniharibia kazi ambayo nafanya....
Achana nao usijiharibie maisha yako kisa mwanamke hakutaki..au umewekeza kwwke sana au anakusaidia pesa hauwezi kuishi bila yeye.

Jipende ukiamua uondoke bila ugomvi wowote, utajua cha kuongea naona kukaa utakuja pandisha hasira upate matatizo wewe. Una mtoto wa kulea hata kwa mbali kama haumpendi uliyezaa nae..

Pole soma story zingine utqjiona haupo peke yako kukataliwa na mwanamke au kuishi hivyo.
 
Uzoefu tu, nipo kwenye ndoa kwa muda mrefu, watoto wa ndoa idadi inaridhisha na huko nje pia nimezaa na wanawake tofauti tofauti idadi ya watoto inayoridhisha. Nakupa ushauri wa kiume, huyo mkeo hana makosa, mwenye makosa ni yule aliyekutangulia, alimuacha huyo demu huku akiwa bado anampenda, akitegemea labda ateseke ili waweze kurudiana au laa. Ulipoingia wewe kwenye hayo mahusiano, wewe ukawa umempa huyo mwanamke kiburi, ambacho ndio kilichomuumiza aliyekutangulia na kuja kukuambia maneno ya ajabu. Yale maneno aliyafanyia vitendo kwa mambo ya kiswahili na kupelekea hizo mimba zako kutokamatika, na huyo mwanamke kuvishwa sura nyingine ya kukuchukia wewe. Kama bado unampenda sana huyo mkeo, kutana na watu wa kiroho; na kama hiyo vita uiwezi, achana na huyo mwanamke endelea na maisha yako.​

Ndugu yangu nashukuru sana ulivyosema hivyo na ndivyo ilivyokuwa kabisaaa hamna hata kitu umekosea hivyo hivyo ilivyokuwa kaka....ila sasa hapo ndio nimekwamba nimetafuta njia zote za msaada kila mahali nimekwama kabisaa....Unaweza kunisaidia kukutana na watu wa kiroho please kama inawezekana??
 
Ukimwangalia ana mapenzi nawe japo ana dharau? Pengine dharau inatokana ns masuala ya kipato.
1). Kuna kumpenda na Kumtegemea huyu mdada(mke) sio kama anampenda mumewe ila anahitaji huduma zake.

Huyo alie mzalisha hatoi huduma kama huyu alie nae, Mwanamke anae mpenda mume wake hawezi kuongea na mwanaume alie mzalisha na kumtekeleza.

Mume ndio msemaji na msimamizi wa familia baba mtoto akitaka kuongea au kumuona mtoto amtafute msemaji wa familia(mume) sio ex wake. Hii inaonesha Mwanamke bado ana hisia na mzazi mwenziwe.

2). Mwanaume usikubali kufanyiwa dharau na mke au Mwanamke kwasababu hii ni ishara ya usaliti. Anakufanya uanze kujishuku mwenyewe ili anapo kusaliti awe na sababu ya kusema si nilikwambia wewe dhaifu sasa niwachie anae weza afanye nitakavyo.
 
Ndugu zangu ambao mpo kwenye ndoa naombeni ushauri kabla sijafanya maamuzi yangu mwenyewe.

Nipo kwenye hii ndoa kwa miaka 11 ila mwanamke ambaye nilikutana nae alikuwa na mtoto tayari ila naomba niseme alikuwa mwenyewe na mtoto wa miaka 2 mwanaume wake alimkimbia, sasa baada ya hapo mwanaume wake wa zamani kufahamu huyu mwanamke ana mwanaume mwingine siku moja akaniambia kwamba huyu mwanamke huwezi kuja kumzalisha maisha yako yote hata iweje.

Ndugu zangu mpaka leo huyu mwanamke amepata mimba mara 3 ila zote zimetoka. Sasa baada ya hapo mwanamke akaanza kunidharau na kuniambia kwamba sina mbegu za kumzalisha. Me kama mwanaume nikapoteza confidence nikaenda kupiga nje na nimepata mtoto vizuri bila shida kabisa

Sasa amekuja kugundua kwamba me nimezaa nje ila nilivumilia mateso yote na maneno yote ya mateso na alikuwa muda wote ananidharau sana na kusema hata iweje umenikuta na mtoto na taka usitake siwezi kuacha kuongea na baba wa mtoto.

Akinikuta nakunywa anamwaga drinks zote kwenye sink.

Sasa jana usiku nimepigwa vyupa vibaya sana damu nyingi zimetoka sababu anataka tuwe tunatumia password moja, ameingia kwenye simu amekuta yule mwanamke mwingine mwenye mtoto amenitumia picha za mtoto.

Baada ya hapo akanitukania wazazi wote na kuwaita Idiots familia nzima pamoja na mimi...

Nilikuwa tu naomba ushauri nini cha kufanya ila tumeenda hospitali tumegundua zile mimba 3 alipata moja imeziba mirija yake ya uzazi so hawezi pata mimba kwa njia ya kawaida.

Naombeni ushauri wenu tafadhali kwa hili suala.

Je, bora niondoke?
Pole Mr. Idiot
 
Back
Top Bottom