Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 118,181
- 219,325
Hebu urudi mkuu , maana next week nataka niitumie fastjet kwenda Mbeya , nina kijisafari cha kwenda Lilongwe lakini nina kazi ya siku mbili ya Chadema pale Kyela , halafu nataka kutumia gari ndogo kuelekea Lilongwe kibiashara .Hapa ndio ingekuwa ATCL,basi watu wangetukana sana na huko insta kusingekalika kabisa leo
Yaani my dear ATCL anaandamwa sana...Nipo mbali na nyumbani,ngoja nitafute vyanzo vyangu,wanambie nini kimeikumba fastjet?Kwamba wanaenda Mwanza lakini si Mbeya?
Ila kama ilifika saa 1625hrs bado mpo Dsm,isingewezekana kwenda Mbeya,maana uwanja wa Mbeya hauna taa,unategemea muda wa Sunset na Sunrise.
Sasa leo jua Mbeya limezama saa 1723 bila shaka,Fastjet isingeruhusiwa kuruka kuja Dsm wakati wa machweo,hata kama kwa macho ya kinyakyusa ungekuwa unauona mwanga.
Nasubiri vyanzo vyangu,nitarudi hapa....
Kama vipi niangalie utaratibu mwingine .