roselina john
JF-Expert Member
- Aug 17, 2017
- 758
- 942
Jamani mambo zenu, Niko katika wakati mgumu
Mimi ni binti wa miaka 29 kwa sasa, nimempata mwanaume ambaye tulipanga mengi sana hadi kupanga jinsi ya kufunga ndoa,
Mwaka fulani niliingia kwenye mahusiano na kijana mmoja toka Mbeya, ila kwa sasa anaishi Afrika ya Kusini kwa shughuli zake ,
Tulikubaliana kuanza kutambulishana kwao, na kwetu
Nakumbuka alinilipia nauli ya ndege nikaenda kwao kutambulishwa nikamshukuru Mungu kwamba nimepata mme sasa,
Tumeendelea na utaratibu na mshenga akatumwa kwetu kusema, baada ya kuondoka nikamweleza mama kuwa kijana sawa ananipenda ila hapendi jambo fulan ambalo kwa ukweli sitalisema hapa, mama akasema kama ndo hivo sitak habari zako za kuolewa,
Ikabidi mchakato uendelee kawaida, wakaleta kishika uchumba mama akawa hataki kushiriki hata kidogo, anasusa, sasa shangazi yangu akaniambia kwamba kwakuwa huna baba naomba ili suala tuwashirikishe baba wadogo na wajomba tuendelee na nchakato,
Baada ya muda tukapanga wataletaje mahari na siku ya send off tukaipanga,
Sasa kabla ya send off siku moja kabla tukapata habari kupitia kwa mjomba kwamba Mwanaume anayeenda kunioa kumbe ana mke mi naenda kuwa mke wa pili, taarifa hii ikawachanganya wote hata wajomba wakasema ngoja wajiweke pembeni, maandalizi ya send off yakavurugika wakati huo wakwe wakiwa njiani kuhudhuria sherehe hiyo , walikodi Costa na magari kadhaa kutoka mbeya hadi Ngara,
Wakanikimbia ndugu zangu wote nami nikachanganyikiwa kwa hasira sikutokea kwenye send off na maandalizi ikawa hasara, wakapiga simu nikazima nilikuwa na hasira sana,
Baadaye nikawasha simu nikakuta mama mkwe mtarajiwa amenitumia meseji kwamba "Sikutegemea kama ungetufanyia haya, sisi tunajiandaa kesho tunarudi lakini baki na amani"
Niliumia sana Akaendelea kunitumia meseji za machungu nikijua naye anajua kuwa Mwanae ana mke na mama huyu tumeongea kila siku niliumia,
Sasa yule mchumba wangu akawa ananitafta sipokei nikamwambia sina Muda mchafu wa kuolewa na wewe, hapo sikumwambia kwanini nimebadili mawazo,
Sasa nakumbuka siku kadhaa baadae naitwa nyumbani kwamba kuna kikao,
Kumbe kuna taarifa kwamba yule kijana hakuwa ameoa ila alichumbia sehemu akalipa mahari ila kumbe hakuoa,
Habari zilisononesha sana
Nikaenda kwa askofu mmoja akanishauri
1.Ama tuombe radhi kwao kuendelea na mchakato
2.Ama tuwape kishika uchumba chao maana mahari alikuwa bado angetoa siku ya send off asubuhi yake,
Naomba ushauri wenu plz
Nimeikosea Sana familia ile, pia hasira baada ya kupungua natamani niolewe naye japo nashindwa naanzaje
-----------------------------------
Nimeamua kuwaambia ukoo wangu, Kuanzia Mama sina Baba R.I.P
Mashangazi, Baba Mdogo na wajomba nia yangu ya dhati kuiomba msamaha familia ya ambaye alikuwa mchumba wangu,
Naenda kuomba msamaha nikitegemea maswali magumu,
Naenda Kuomba msamaha nikijua maumivu na uchungu hata hasara waliyopata kutoka Mbeya hadi Ngara,
Hatua ya Kwanza
Nimeamua niangalie upepo ndani ya familia yangu, idadi ya wanaonisapot,
Niangalie mtazamo wao juu ya kwanini nasukumwa kuomba msamaha,
Tatu naangalia dhamira yangu na msukumo wa moyo wa dhati,
Nne Nimeamua kuwashirikisha ndugu na kuwaambia sitaenda moja kwa moja kwa wakwe ila ntaenda kwa mshenga
Tutaenda timu ya watu 7 watu wazima sita na mimi nikiwa wa saba, katika timu hiyo mama aneendelea kugoma kutoshiriki, Nimepata shangazi mama mdogo na baba mkubwa,na wengine
Tutaelekea kwa mshenga kuomba radhi, na kueleza sababu za kutokuwapo kwenye send off alafu tumuombe atuombee msamaha,
Baada ya wao kujua tunaomba msamaha kup kwa mshenga
Nimeandaa kishika uchumba walicholipa na nimeandaa wazee 5 na wanisindikize Mbeya kutoka Ngara kwenda kuomba msamaha na pia kabla ya kufika kwenye familia ya wakwe, tutapitia kwenye parokia iliyokaribu kumuona kiongozi wa dini atupe mwongozo na kumuomba atupe ushirikiano kufika kule, pia tutaomba aambatane na wazee wa heshima wa Kanisa, hii nitaifanya tu hata wasipotoa jibu pitia kwa Mshenga
Nikifika nitakuwa na maombi mawili
1.Kuomba kusamehewa na kurudisha kishika uchumba chao
Ama
2.Kuomba kusamehewa na kuendelea na mchakato wa harusi kama watakua bado hawajapata mtu.
Naombenii mawazo yenu mengine pia
asante
Mimi ni binti wa miaka 29 kwa sasa, nimempata mwanaume ambaye tulipanga mengi sana hadi kupanga jinsi ya kufunga ndoa,
Mwaka fulani niliingia kwenye mahusiano na kijana mmoja toka Mbeya, ila kwa sasa anaishi Afrika ya Kusini kwa shughuli zake ,
Tulikubaliana kuanza kutambulishana kwao, na kwetu
Nakumbuka alinilipia nauli ya ndege nikaenda kwao kutambulishwa nikamshukuru Mungu kwamba nimepata mme sasa,
Tumeendelea na utaratibu na mshenga akatumwa kwetu kusema, baada ya kuondoka nikamweleza mama kuwa kijana sawa ananipenda ila hapendi jambo fulan ambalo kwa ukweli sitalisema hapa, mama akasema kama ndo hivo sitak habari zako za kuolewa,
Ikabidi mchakato uendelee kawaida, wakaleta kishika uchumba mama akawa hataki kushiriki hata kidogo, anasusa, sasa shangazi yangu akaniambia kwamba kwakuwa huna baba naomba ili suala tuwashirikishe baba wadogo na wajomba tuendelee na nchakato,
Baada ya muda tukapanga wataletaje mahari na siku ya send off tukaipanga,
Sasa kabla ya send off siku moja kabla tukapata habari kupitia kwa mjomba kwamba Mwanaume anayeenda kunioa kumbe ana mke mi naenda kuwa mke wa pili, taarifa hii ikawachanganya wote hata wajomba wakasema ngoja wajiweke pembeni, maandalizi ya send off yakavurugika wakati huo wakwe wakiwa njiani kuhudhuria sherehe hiyo , walikodi Costa na magari kadhaa kutoka mbeya hadi Ngara,
Wakanikimbia ndugu zangu wote nami nikachanganyikiwa kwa hasira sikutokea kwenye send off na maandalizi ikawa hasara, wakapiga simu nikazima nilikuwa na hasira sana,
Baadaye nikawasha simu nikakuta mama mkwe mtarajiwa amenitumia meseji kwamba "Sikutegemea kama ungetufanyia haya, sisi tunajiandaa kesho tunarudi lakini baki na amani"
Niliumia sana Akaendelea kunitumia meseji za machungu nikijua naye anajua kuwa Mwanae ana mke na mama huyu tumeongea kila siku niliumia,
Sasa yule mchumba wangu akawa ananitafta sipokei nikamwambia sina Muda mchafu wa kuolewa na wewe, hapo sikumwambia kwanini nimebadili mawazo,
Sasa nakumbuka siku kadhaa baadae naitwa nyumbani kwamba kuna kikao,
Kumbe kuna taarifa kwamba yule kijana hakuwa ameoa ila alichumbia sehemu akalipa mahari ila kumbe hakuoa,
Habari zilisononesha sana
Nikaenda kwa askofu mmoja akanishauri
1.Ama tuombe radhi kwao kuendelea na mchakato
2.Ama tuwape kishika uchumba chao maana mahari alikuwa bado angetoa siku ya send off asubuhi yake,
Naomba ushauri wenu plz
Nimeikosea Sana familia ile, pia hasira baada ya kupungua natamani niolewe naye japo nashindwa naanzaje
-----------------------------------
Nimeamua kuwaambia ukoo wangu, Kuanzia Mama sina Baba R.I.P
Mashangazi, Baba Mdogo na wajomba nia yangu ya dhati kuiomba msamaha familia ya ambaye alikuwa mchumba wangu,
Naenda kuomba msamaha nikitegemea maswali magumu,
Naenda Kuomba msamaha nikijua maumivu na uchungu hata hasara waliyopata kutoka Mbeya hadi Ngara,
Hatua ya Kwanza
Nimeamua niangalie upepo ndani ya familia yangu, idadi ya wanaonisapot,
Niangalie mtazamo wao juu ya kwanini nasukumwa kuomba msamaha,
Tatu naangalia dhamira yangu na msukumo wa moyo wa dhati,
Nne Nimeamua kuwashirikisha ndugu na kuwaambia sitaenda moja kwa moja kwa wakwe ila ntaenda kwa mshenga
Tutaenda timu ya watu 7 watu wazima sita na mimi nikiwa wa saba, katika timu hiyo mama aneendelea kugoma kutoshiriki, Nimepata shangazi mama mdogo na baba mkubwa,na wengine
Tutaelekea kwa mshenga kuomba radhi, na kueleza sababu za kutokuwapo kwenye send off alafu tumuombe atuombee msamaha,
Baada ya wao kujua tunaomba msamaha kup kwa mshenga
Nimeandaa kishika uchumba walicholipa na nimeandaa wazee 5 na wanisindikize Mbeya kutoka Ngara kwenda kuomba msamaha na pia kabla ya kufika kwenye familia ya wakwe, tutapitia kwenye parokia iliyokaribu kumuona kiongozi wa dini atupe mwongozo na kumuomba atupe ushirikiano kufika kule, pia tutaomba aambatane na wazee wa heshima wa Kanisa, hii nitaifanya tu hata wasipotoa jibu pitia kwa Mshenga
Nikifika nitakuwa na maombi mawili
1.Kuomba kusamehewa na kurudisha kishika uchumba chao
Ama
2.Kuomba kusamehewa na kuendelea na mchakato wa harusi kama watakua bado hawajapata mtu.
Naombenii mawazo yenu mengine pia
asante