Ndege huwa inaongozwa vipi angani?

Ndege huwa inaongozwa vipi angani?

bush crazy

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
773
Reaction score
1,087
poleni na majukumu wakuu! wakati nasoma nilifundishwa kuwa dunia ni oblate sipheriod kwa maana ina umbile la mviringo. Leo nimepata swali kichwani mwangu, je ndege ikipaa angani na kuanza safari, pilot akiinyosha kwa maana ya kuto kupanda juu au kwenda chini ndege haiwezi toka nje ya dunia ( chukua rula ilaze juu ya mpira utaelewa nini na maanisha) karibuni!
 
poleni na majukumu wakuu! wakati nasoma nilifundishwa kuwa dunia ni oblate sipheriod kwa maana ina umbile la mviringo. Leo nimepata swali kichwani mwangu, je ndege ikipaa angani na kuanza safari, pilot akiinyosha kwa maana ya kuto kupanda juu au kwenda chini ndege haiwezi toka nje ya dunia ( chukua rula ilaze juu ya mpira utaelewa nini na maanisha) karibuni!

Labda tuanze kwa kukuuliza kama uliwahi kusoma Sayansi na Geography?
 
Simu yangu inazima chaji hapa panastahili comments zangu, na siyo moja,

Ndege uongozwa katika minajili au aina.mbili

Kuna mfumo wa kujiendesha, (Auto pilot)
Kuna na mfumo wa kuendeshwa au kuongozwa na Pilot,
Maelezo mengi hapa inabidi ya base kwenye uendeshaji wa pilot kama binadamu,
Ngoja nakuja
 
Ndege haiwezi kwenda kwnye space haiwez tokea kuna urefu wake standard inauruka ndio maana ikaitwa ndege yani inapopanda juu zile wings ndio huipa support ku flow angani bila zile gravitation force ina i pull kurudi chini ndio maana unaona space ship znafungwa rockets zenye high power kuweza kuishinda gravity ya dunia mpaka kutoka kwnye orbit after hapo zna de attach ship inaelea ynyewe knye space na kuongozwa kwa manova ya ki sayansi ila ndege inasaidiwa na wings tu na kuhitaji power ndogo wakati inaruka kama walivyo ndege viumbe ndio exactly ndeke chombo kinavyo operate

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama uliweza kusoma kwamba dunia ni mviringo, naamini mambo ya longitude na latitude unafununu nayo. Pia kuna nguvu ya uvutano ya dunia inayovuta vitu kuelekea kati kati ya dunia ndio maana ukaambiwa ukirusha kitu juu, lazima kitarudi chini.

Ndege inapoanza safari, inaruka juu ikiongeza zaidi uelekeo wa wima hadi kufikia kimo kitakachofaa ili ianze safari yake kuelekea inapotarajia kwenda kutua, itakapofika huko itashuka. Kama inaenda umbali mrefu, itaenda juu zaidi, kwa safari ya karibu, haiendi kimo kirefu sana juu.

Ndege za kawaida hazina uwezo wa kuzifanya ziishinde nguvu ya uvutano wa dunia zitoke nje ya eneo lake, vifaa maalum vinavyoenda sayari zingine vina nguvu na huo uwezo.

Kwa muktadha huo, kimo au umbali gani ndege itaenda juu inategemea na masafa ya umbali wa safari yake. Na kwenye ndege kuna vifaa vya kuonyesha makadirio ya vipimo sahihi kutokana na umbali wa safari husika.

Umewahi kujiuliza kitu gani kinamjulisha rubani kwamba aanze kuishusha ndege kwa kuwa mmekaribia kiwanja mnachotarajia kutua?
 
Simu yangu inazima chaji hapa panastahili comments zangu, na siyo moja,

Ndege uongozwa katika minajili au aina.mbili

Kuna mfumo wa kujiendesha, (Auto pilot)
Kuna na mfumo wa kuendeshwa au kuongozwa na Pilot,
Maelezo mengi hapa inabidi ya base kwenye uendeshaji wa pilot kama binadamu,
Ngoja nakuja

Nunua powerbank mkurugenzi...usalama upo lakini?
 
Simu yangu inazima chaji hapa panastahili comments zangu, na siyo moja,

Ndege uongozwa katika minajili au aina.mbili

Kuna mfumo wa kujiendesha, (Auto pilot)
Kuna na mfumo wa kuendeshwa au kuongozwa na Pilot,
Maelezo mengi hapa inabidi ya base kwenye uendeshaji wa pilot kama binadamu,
Ngoja nakuja
ahsante!!! nasubiri kwa hamu coment zako mkuu once ukichaji simu!
 
ahsante mkuu kwa majibu mazuri, kwahiyo route za ndege zipo curved from point a to b as dunia ni sphere?

Kwa kifupi tunaweza kusema hivyo mkuu. Wajuvi watakuja kumwaga maelezo mujarabu
 
Kwa kifupi ndege kabla haijaruka angani hupewa umbali wa kuruka kwenda juu na waongoza ndege (Air traffic control) umbali huu hupimwa kwa futi (feet) kutoka usawa wa bahari na rubani huwa ana feed kwenye computer ya ndege, umbali huu, ikiwa ni pamoja na speed na uelekeo wa ndege (Direction) anakokwenda. Rubani anapobonyeza Auto Pilot, ndege hufuata maelekezo hayo bila kukosea na kuifanya ndege iendelee ku maintain umbali ule ule, hivyo hata kama dunia ni duara kwa kuwa ndege inasafiri angani kwa umbali uleule toka usawa wa bahari itaendelea kuzunguka na dunia kwa usawa uleule, ku maintain usawa huu ni muhimu ili kuepusha ndege kugongana kwani kila moja hupewa usawa wake, na pia huepusha ndege isipotee, vilevile kila ndege imetengenezwa na umbali wake wa mwisho kwenda juu angani (Altitude ceiling) ndege inaporuka juu kama inakwenda mwezini (Outer space) ikifikia ile Maximum ceiling haiwezi kuendelea zaidi ya pale, itaingia kwenye Aero-Dynamic-Stall, itakosa lift na kuanguka..na pia umbo la ndege pia linaundwa kuvumilia Pressure kwa ceiling yake, ijulikane kuwa kila unavyozidi kwenda juu, pressure inazidi kuwa kubwa, hivyo ndege ikipita kwenye ceiling yake ita katika katika haiwezi kustamili..na kwa kawaida Rubani huwa anawatangazia abiria umbali ambao ndege yao itasafiri kutoka usawa wa bahari (eg 35,000 feet) from sea Level

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali la nyongeza: kwanini tuliita ndege hatukuiita mbuzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata ungeeita kijiko ingekua sawa tu.Lugha ni SAUTI ZA NASIBU. Hata leo baba angekua anaitwa mti ingekua sawa tu.

The problem with the world is that the intelligent people are full of doubts, while the stupid ones are full ofconfidence.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom