Zakumi
JF-Expert Member
- Sep 24, 2008
- 5,063
- 2,492
Gaijin,
..umeshaona Balozi wa nchi yoyote ile akiwasilisha hati za utambulisho kwa "raisi" wa Zanzibar??
..Pinda aliwaambia ukweli kwamba ZNZ siyo nchi, lakini kwasababu kwa miaka mingi mmekuwa mkidekezwa na nyie kubweteka mkadhani amekosea.
..kama kuna uraia wa ZNZ, nionyeshe passport ya nchi inayoitwa ZNZ iliyotolewa baada ya mwaka 1964.
..Nyerere aliwahi kuulizwa swali kuhusu wa-Tanganyika kuingia Zanzibar kwa passport. Swali hilo aliulizwa miaka ya 60 na Arcado Ntagazwa wakati huo akiwa mwanafunzi wa shule ya msingi ktk mkoa wa Kigoma. Mwalimu Nyerere alisema walikuwa wanafanya hivyo kwasababu za KIUSALAMA.
..kosa lenu, au tatizo lenu nyinyi ni UBAGUZI, hicho ndicho kinachowasukuma kujitenga na kuukana Utanzania.
Mbona unakuja kwa hasira mkuu. Mada ni Kenya kuidharau Tanzania. Mara tupo kwenye Zanzibar na Tanganyika. Hizi drama zitakwisha lini?