Nchi yetu inaitwa Tanganyika

Nchi yetu inaitwa Tanganyika

WanaJF nisaidieni tafadhali:
  1. Hivi Canada, Australia na New zealand nd ni nchi huru?
  2. Kuna tofauti gani kati ya kupata uhuru na nchi kuwa jamhuri?

1. ni huru.
uhuru ni hali ya kujitegemea kimaamuzi (kujiondoa katika utegemezi), kufanya mambo yako bila kuingiliwa.

2. kupata uhuru ( soma maana ya uhuru hapo juu)
jamhuri ni mfumo/aina ya serikali ambayo wananchi wanakuwa na haki ya kuchagua viongozi wao (uongozi sio wa kurithi), mara nyingi serikali hizi huongozwa na rais (aliyechaguliwa na watu).

hitimisho, canada, australia na new zealand ni huru ila zimeamua kuchagua mfumo wa serikali wa kidominioni ambapo waziri mkuu anakuwa mkuu wa serikali na malikia/mfalme wa uingereza anakuwa mtawala wa nchi.
 
Hakuna kukusanyika kwan al-shababu wataujumu, na kova alisha sema hivyo sherekehen majumbani mwenu tuuu.

pamoja sana..na wole wenu mtakao thubutu kwenda uwanja wa uhuru al shabaab na kile kikundi wamejizatiti..lol
 
Goma usigome maisha yanaendelea tu mkuu..

Sikumbuki lini nimewahi kwenda kwenye sherehe ya so called taifa labda nilipokuwa primary

Kama hakuna kazi inakuwa fursa nzuri ya kufanya misele yangu mjini..
 
Tunasherekea uhuru wa Tanganyika mwaka huu 2011 au mwaka kesho 2012 kufuatana na mada hapo juu??????:lol:
 
Kuelekea sikukuku ya Uhuru inayoenda na Matumizi makubwa ya pesa za walipa kodi maskini Watanzania wengi wapo njia panda kuelewa kuwa wanakwenda kusherekea Uhuru wa Nchi inayoitwa Jina lipi? Katika pitapita mtaani wananchi wengi wamekuwa na mtazamo tofauti juu ya maadhimisho ya Uhuru wa taifa lenye utata kwani baadhi ya Watu wanasema kusherekea miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania, wengine miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara na kundi kubwa likisema kusherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.

Kotokana na mambo yanaendelea kujiri serikali inatakiwa kutoa tamko rasimi ya sherehe hizo na kuweka wazi ni Taifa lipi linaloenda kusherekea Uhuru aidha katika kufanikisha tamko hilo ukiwa kama mwananchi toa maoni yako juu ya Taifa linaloenda kusherekea Miaka 50 ya Uhuru pamoja na mafanikio na changamoto linalolikabili Taifa ambalo unafahamu likwenda kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru
 
historia, nimesoma japo si sana inaonekana hukunielewa vizuri kwa vile post imekaakaa kaa shairi fulani hivi, laki my point is:

1. Tanganyika ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wakoloni

2. Tanzania ni nchi iliyobuniwa na kubatizwa jina hilo na wazalendo

3. mimi na wingine wenye umri usiofikia miaka 47, tumezaliwa Tanzania na sio Tanganyika

4. muungano ni kielelezo cha umoja wetu na licha ya mapungufu yake, ni bora kuliko kutengana

5. changamoto tuliyonayo ni kuondoa mapungufu yake, iwe ni kwa kuunda serikali moja, tatu au kubaki na mbili za sasa, vyovyote vile, muhimu tuondoe kero zinazohusiana na muungano

kilichotufanya tusindwe kuijenga Tanzania si muungano uliopo, bali masuala mengi tu tunayojadili hapa kila siku kama ufisadi nk. kwa hiyo hata tukiuvunja muungano, tutashindwa kuijenga Tanganyika pia kama hatutapambana na matatizo haya (ufisadi nk)

nna wasiwasi na 'biology' ya mwili wako kwa tarehe ya leo, sio bure wewe!
 
Nafikiri kwa wakati huu kama utanikazania niiitwe mtanganyika nitakukatalia mimi ni Mtanzania, so baki na uzanzibar wako sisi tutaendelea na utanzania wetu usitutie ujinga. hamkawii kubadilika mara mtakapoona mtanzania anaendelea mtaomba turudiane so mimi nilizaliwa wakati wa Tanzania na nitaendelea kuwa mtanzania,

heee! Kuzaliwa ndio utaifa? Hujiulizi nyerere aliomba kujitawala kwa nchi gani? Sio Tanganyika! iko wapi sasa? kamuuzia zenj kinyemera, au!
 
Katika kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika, kwa nini wale woote wanaosema hawatashiriki wasichukue nafasi ya siku hii KUANDAMANA kupinga utawala uliopo? at least fanyeni la maana kuonyesha hisia zenu siku hiyo, lakini kugoma tu kushiriki kuadhimisha siku hiyo hakuwezi kuwaletea sifa yoyote zaidi ya kuwadhalilisha zaidi..

Desember 9 iwe siku ya maandamano nchi nzima mkipinga yoote mnayoyalaaani na ndio iwe siku ya kudai huo UHURU muutakao..
 
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa Tanganyika,
maana ya neno Tanganyika, siijui,
Tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui

nilizaliwa Tanzania,
nilizaliwa Afrika
nilizaliwa duniani
nlizaliwa na mwanadamu

kwa hiyoÿ

mimi ni mtanzania
mimi ni mwafrika
mimi ni mdunia
mimi ni mwanadamu

maana ya Tanzania, najua
maana ya Afrika, najua
maana ya Dunia, najua
maana ya mwandamu, najua

nawauliza wazanzibari,
nini maana ya Zanzibari,
nani aliipa jina Zanzibari,
kwa nini wajivunie uzanzibari?
kwa nini wasijivunie utanzania?

Taifa, Kabila, na lugha ni mapenzi ya Mungu! Muombe Mungu atakuonyesha kuhusu tanzania isivyo mapenzi ya Mungu, bali ya binadamu na ushirikina mtupu kama wa mwenge!
 
ukisoma kwenye mitandao(sitaki kutaja)wenzetu wa visiwani hawautaki muungano hata kuna threats zinahamasisha kuvunjwa,pia kuna kero za muungano hizi nazo zina nafasi yake.lakini imefikia watu wanachomewa maduka nk huko visiwani ,sababu ni mtanganyika!!kwa kweli kuna vitu vya kutazama, pia nakuimbuka kulikua na mjadal mkubwa miaka ya 90 kuhusu serikali tatu!!nazan ndio chaguo bora maana ukisema moja itabidi sehemu fulan iwe mkoa,zikiwa tatu kutakua na cost and benefit sharing na si fulan kumpa fulan. pia kwa undani ukiangalia watu wa bara hawalidhiki na mabo yanavyokwenda hasa kuzuiwa zuiwa kumiliki maeneo au kuishi visiwani,
 
Usidharau watu simply kwa kuwa wana mtizamo tofauti na wa kwako! Washabiki wa u-Tanganyika bahati mbaya sana haelezi faida zitakazopatikana mara baada ya kuanzisha Serikali tatu! Je, ufisadi utatoweka? Je, umaskini utaondoka? Je, vifo vya mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka 5 vitapungua? Kama hakuna majibu, basi sioni haja ya hiyo Serikali ya Tanganika ambayo nahisi itaongeza matatizo badala ya kupunguza!

Nikuulize, nawe ujiulize! kwa nini kusiwe na serkali moja?
jee mzenj yuko tayari kukubali serkali moja?
 
Nikuulize, nawe ujiulize! kwa nini kusiwe na serkali moja?
jee mzenj yuko tayari kukubali serkali moja?

Hakuna kitu wazanzibari wanapinga kama serikali moja
 
Mmemsikia Seif Sharif Hamad ati rais ajaye lazima atoke Z'bar. Nani atashughulikia mambo yasiyo ya muungano kama tunakuwa na mkulu kutoka kule?
 
mimi sio mtanganyika,
sikuzaliwa Tanganyika,
maana ya neno Tanganyika, siijui,
Tanganyikailitoka wapi, sijui,
ilibatizwa jina na nani, sijui

nilizaliwa Tanzania,
nilizaliwa Afrika
nilizaliwa duniani
nlizaliwa na mwanadamu

kwa hiyo;

mimi ni mtanzania
mimi ni mwafrika
mimi ni mdunia
mimi ni mwanadamu

maana ya Tanzania, najua
maana ya Afrika, najua
maana ya Dunia, najua
maana ya mwandamu, najua

nawauliza wazanzibari,
nini maana ya Zanzibari,
nani aliipa jina Zanzibari,
kwa nini wajivunie uzanzibari?
kwa nini wasijivunie utanzania?

MISS sikuelewi unaposema Tanganyika huijui na hapo hapo unasema Tanzania Unaijua.... Mimi naamini kama huijua Tanganyika basi hata Tanzania huijui (soma definition ya Tanzania). Pili Najua majuzi kodi yako kubwa badala ya kununua vitanda Muhimbili ili kinamama wasijufungulie chini ilitumika kusherehekea miaka hamsini ya nchi wanayoita Tanzania Bara huku wakihakisha neno Tanganyika halitamkwi. Ila cha ajabu hapa UN hamna nchi inayoitwa Tanzania Bara na Wala hamna nchi iliyowahi kuitwa Tanzania Bara... Nilipata shida sana nilipokuwa naulizwa na watu Tanzania Bara ni nchi gani hiyo?????. Ila kwenye Data Zao wana nchi iliyopatata Uhuru 9 Dec 1961 inaitwa Tanganyika na 1964 ikaungana na Zanzibar kuwa Tanzania (Ila shida nyingine wakaniuliza mbona nchi mbili zikiungana hutoa nchi moja ila kwenu naona imetoa nchi mbili?????????....Kwa kukatisha mazungumzo ilibidi nianze kuzungumzia xmass ah ah ah)
 
Hakuna Tanzania pasipo Tanganyika na Zanzibar. Hivi kwa nini wenzetu hawayaiti yale mapinduzi kuwa ni ya Tanzania Visiwani?
 
Tanganyika ipo na kamwe hatuko tayari kuipoteza,Tanganyika bila zanziba inawezekana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom