Athari zilizoletwa na ukoloni juu ya damu, vichwa vya wazee wetu

Gily Gru

JF-Expert Member
Jul 4, 2016
7,798
20,743
ATHARI ZILIZOLETWA NA UKOLONI JUU YA DAMU, VICHWA VYA WAZEE WETU

MZUNGU
(Mkoloni) ni mtu mbaya sana na utawala wa kitumwa ulikuwa mbaya na kwani familia nyingi zilitengwa na wenzao na kupelekwa wasipokujua. Watoto walitengwa na wazazi wao, mume na mkewe kwa kweli inaonyesha ni uchungu kiasi gani babu zetu walipitia. Wanaume waliochukuliwa kwenda kufanywa watumwa ughaibuni, walichukuliwa na KUHANISIWA ili wasiwazalishe wanawake wa huko. Ndugu zetu wakiwa huko nchi za ugenini walipigwa MNADA na KUNUNULIWA kama bidhaa. Mambo haya waliyoyapitia ni ya uchungu mkubwa mno kuyaelezea, hakuna atakayefurahia kumkuta

MWARABU (Mkoloni) ni mtu mbaya sana kwani ni moja yapo ya watu wabaya kuleta utumwa, nakumbuka nilisimuliwa na bibi, waliwagawanya watu katika matabaka. Ilifika kipindi watu wakawa wanauza watoto wao kwa fitina za waarabu. Mfano pwani (Tanga mpaka Tabora maeneo haya yalijulikana kama pwani kipindi cha ukoloni) mtoto alikuwa ni mali ya mjomba, ikimaanisha bba hakuwa nanguvu zaidi ya mjoimba. Wajomba wengi waliuza watoto wao kwa waarabu ili wapate ujira. Kwa watoto waliokuwa na damu ya kiarabu wao na waarabu wenyewe walikuwa wezi wakubwa, tena waliiba watu wengi hususani watoto. Usipomchunga mwanao basi atanyakuliwa na hawa waarabu na mamluki yake na kwenda kuuzwa kama bidhaa.

Wazee wetu walijazwa hofu ndani ya mioyo yao ili wauone mzungu kama mungu, wengine waliwazania ni mungu. Wakoloni waliwafanya mababu na mabibi zetu wajione wako chini yao, kuwafanya kutekeleza mambo ya kikoloni (watu kuuza watoto wao wenyewe kwa Waarabu) na kumwabudu mkoloni kama miungu dunia. Bibi zetu WALIBAKWA sana tena sio mbele ya kadamnasi, walifanywa kama chombo cha starehe, wanawake walizalilishwa na kuzalishwa na watawala hawa wa mabavu. Ilipelekea wengine kutengwa na familia zao na kuteseka sana kwa uchungu mkubwa pale walipozalishwa na wakoloni.

Walipigwa fimbo kama wanyama, na kushurutishwa kufanya shughuli mbali mbali zenye kuwazalishia makoloni zikiwemo kulima mashamba ya wazungu. Mbali na hayo walinyimwa haki zao za kibinadamu mfano walishindishwa njaa bila kupewa chakula chochote, walifanyishwa kazi kupita uwezo wao wa kibinadamu, walitiwa chapa za alama kama wanyama n.k. Mababu zetu walitia sahihi mikataba ya kilaghai kwa shuruti na wengine kwa kupenda kuwauza wa-Tanganyika wenzao. Hapo unaona jinsi walivyotugawanya sisi wenyewe kwa wenyewe.

Hata baada ya kupata uhuru, dhambi ya utumwa haikukoma, ikaendelea kuwatafuna jamaa zetu kupitia UKOLONI MAMBOLEO. Nchi nyingi barani Africa hata baada ya uhuru bado ziliathirika na ukoloni mamboleo unaoendelezwa na watawala wenyeji. Tumeona wazungu wakipora utajiri wa nchi nyingi barani Afrika hata baada ya utumwai, hasa mafuta na madini. Ukoloni umeathiri FIKRA za ngozi nyeusi, ndo maana unaona watu wamekuwa wavivu kujiajiri, fitina, uvivu wa kufikiri nk. Je, kitu gani unaona tufanye kufuta ukoloni mamboleo jwa vizazi vyetu vinavyokuja?

Kuna watu wanajiona juhudi zao binafsi zilitupa uhuru, lakini harakati za uhuru zilianza toka kwa wote walipigana kutetea haki zao na familia zao (UHURU HAUKULETWA NA JUHUDI TANU PEKE YAKE). Shukrani zatu za dhati zinaenda kwa Chifu Mkwawa (1891 and 1894), Kinjekitile Ngwale kuwaunganisha watu katika vita vya Maji Maji (1905 – 1907), ma chifu wengi, taasisi za dini (WAKRISTU, WAISLAMU, DINI ZA KIJADI), na watu wote waliopigania uhuru kwa namna moja au nyingine. SHUKRANI ZA KIPEKEE zimwendee HAYATI MWALIMU NYERERE, kwa kuunganisha Tanganyika kuwa nchi moja yenye ushikamano mmoja pasipo UDINI, UKABILA, UKANDA, UBAGUZI WA RANGI N.K. Nawapongeza Maraisi wote waliopita na wa sasa kwa kufata nyayo hizi na kupiga kabisa chembe chembe hizi za chuki na kudumisha umoja wetu.

Kuna baadhi ya viongozi wa kipindi kile walitaka kudai uhuru wa maeneo yao binafsi na mfano mzuri ni Mangi Thomas Marealle. Kazi kubwa ilifanywa na Mwalimu J K Nyerere kuwaunganisha viongozi wa mikoa mbali mbali nchini Tanganyika na kuwaweka chini ya utawala mmoja. Isingekuwa juhudi na fikra za Mwalimu Nyerere basi kungekuwa na ushindani mkubwa sana kila mtu angevutia kwake. Kwa yeyote anayebeza kuwa yeye si MUASISI halali, mbona babu zao hawakupewa nchi watawale wao? Mbona babu zao hawakuunganisha Tanganyika? Kuna watu wengi walidai uhuru, kuna watu ndugu zao walidai uhuru kwa kiasi kikubwa leo hawako kutafuta ujiko. Mwalimu Nyerere hakudai uhuru wa wakatoliki, alidai uhuru wa wa-Tanganyika, hakupewa uraisi kwa sababu ya ukatoliki wake. Kwanza idadi ya WAKRISTU na WAISILAMU haikuzidi hata nusu ya WATANGANYIKA (wengi hawakuwa na dini za kuletewa).

Tahadhari: Naomba sana wana Tanzania wenzangu tupinge kwa sauti moja dhambi za kibaguzi; na yeyote anayepinga dhambi hizi aweke neno lake. Mimi siko hapa kubishana, kutukanana na mtu yeyote, ukoloni mamboleo umetawala fikra za watu wengi. Kupinga ukoloni mamboleo tena wanasiasa, kwa wasomi wanaojitafutia majina, wanaopayuka tu kuuharibu umoja wetu WAPE NENO LA KUJENGA. Swali, sio unakaa chini kila siku unawaza Tanzania imekufanyia nini, wewe umeifanyia nini Tanzania?
 

Attachments

  • images.jpg
    images.jpg
    9.2 KB · Views: 4
  • index 1.jpg
    index 1.jpg
    8.2 KB · Views: 3
  • index 2.jpg
    index 2.jpg
    4.5 KB · Views: 3
  • index.jpg
    index.jpg
    12.7 KB · Views: 5
Ndio maana nasema hakuna Uchawi wowote wa watu weusi, ni Imani tu ya kijinga ya kutishana...ni kama ilivyokuwa blah blah za majimaji

Kama watu weusi au waafrika wangekuwa wachawi kweli wasingefanyiwa haya yote, wanaume lukuki na nguvu zao mbele ya wazee wao tena wengine ni wazee wa kimila walichukuliwa wakaswagwa mkoa hadi mkoa mfano Kigoma hadi Kilimanjaro kulima mkonge n.k

Wengine waliwabeba wazungu mabegani huku wakilambwa mijeledi haswa, kisa mzungu mmoja ana kagobole tu.

Hawa Waganga so wangewaroga hawa watu mpaka wakome warudi kwao?

Pia kingine hatuna hata ubunifu wala akili wala teknolojia. Wazungu walitutawala kwa karne nzima yaani miaka 100 wakiwa na silaha aina moja tu ya gobole, sisi ambao tulishakuwa na wafua vyuma na vyuma kila mahali tulishindwaje kutengeneza hata bunduki tupambane nao?

Je hata leo baada ya kuwa na wasomi haswa wahandisi especially mechanical engineers tunatengeneza hata gobole?

Viongozi nao Hamna kitu.

Watu weusi waliumbwa ili kutawaliwa na Wazungu.
 
Ndio maana nasema hakuna Uchawi wowote wa watu weusi, ni Imani tu ya kijinga ya kutishana...ni kama ilivyokuwa blah blah za majimaji

Kama watu weusi au waafrika wangekuwa wachawi kweli wasingefanyiwa haya yote, wanaume lukuki na nguvu zao mbele ya wazee wao tena wengine ni wazee wa kimila walichukuliwa wakaswagwa mkoa hadi mkoa mfano Kigoma hadi Kilimanjaro kulima mkonge n.k

Wengine waliwabeba wazungu mabegani huku wakilambwa mijeledi haswa, kisa mzungu mmoja ana kagobole tu.

Hawa Waganga so wangewaroga hawa watu mpaka wakome warudi kwao?

Pia kingine hatuna hata ubunifu wala akili wala teknolojia. Wazungu walitutawala kwa karne nzima yaani miaka 100 wakiwa na silaha aina moja tu ya gobole, sisi ambao tulishakuwa na wafua vyuma na vyuma kila mahali tulishindwaje kutengeneza hata bunduki tupambane nao?

Je hata leo baada ya kuwa na wasomi haswa wahandisi especially mechanical engineers tunatengeneza hata gobole?

Viongozi nao Hamna kitu.

Watu weusi waliumbwa ili kutawaliwa na Wazungu.

Wazungu wachawi sasa uchawi upo dunia nzima. Majini uarabuni ndio nyumbani

Sanduku hilo lilifukwa na wajerumani ufukweni mwa bahari ya hindi pwani ya Tanga. Kwa kuwa bahari inakuja nchi kavu likafukua hilo sanduku, likawa linaonekaja kwa juu lakini ilitegemea kupwa na kujaa kwa bahari. Maji yakijaa lilikuwa linafunikwa na maji & maji yakipwa lilikuwa linaonekana sehemu ya juu. Wana kijiji walishindwa kulifungua sanduku japo lilionekana ufukweni mwa bahari.

Mambo mengi ya ajabu yalikuwa yanatokea pale walipotaka kulifungua sanduku hilo mfano maskari wawili wa kijerumani wakiwa wamebeba bunduki walikuwa wanatokea na kuwawatimua mbio. Watu walikuwa wanakuja na waganga ili watengue lile zindiko, wengine walitoa kafara za wanyama nawengine wanamwaga mitama ya bisi na kubanja nazi zilizokuwa na maneno ya kiarabu lakini yote ilikuwa bure

Watu wanaamini kuwa yale masanduku ya hela yalikuwa yamewekwa kichawi ndio maana walishindwa kuyachukua kwa mda mrefu. Kuna baadhi ya wajerumani huja kuchunguza baadhi ya vitu vyao walivyoacha kipindi cha utawala wao Africa mashariki. Sanduku la Tongoni lilichukuliwa na wajerumani wenyewe mwanzoni mwa miaka ya tisini, jambo la kushangaza hakuna jambo lolote la ajabu lilitokea wakati wanalifukua
 
Ndio maana nasema hakuna Uchawi wowote wa watu weusi, ni Imani tu ya kijinga ya kutishana...ni kama ilivyokuwa blah blah za majimaji

Kama watu weusi au waafrika wangekuwa wachawi kweli wasingefanyiwa haya yote, wanaume lukuki na nguvu zao mbele ya wazee wao tena wengine ni wazee wa kimila walichukuliwa wakaswagwa mkoa hadi mkoa mfano Kigoma hadi Kilimanjaro kulima mkonge n.k

Wengine waliwabeba wazungu mabegani huku wakilambwa mijeledi haswa, kisa mzungu mmoja ana kagobole tu.

Hawa Waganga so wangewaroga hawa watu mpaka wakome warudi kwao?

Pia kingine hatuna hata ubunifu wala akili wala teknolojia. Wazungu walitutawala kwa karne nzima yaani miaka 100 wakiwa na silaha aina moja tu ya gobole, sisi ambao tulishakuwa na wafua vyuma na vyuma kila mahali tulishindwaje kutengeneza hata bunduki tupambane nao?

Je hata leo baada ya kuwa na wasomi haswa wahandisi especially mechanical engineers tunatengeneza hata gobole?

Viongozi nao Hamna kitu.

Watu weusi waliumbwa ili kutawaliwa na Wazungu.

Unatakiwa ukiwa unasali hata Rosali, usali mpaka na vidole vya miguu. Usibeze yale mambo ambayo babu zetu walipitia. Kutojitambua kuwa tunatakiwa tufanye nini, kunaweza uturudisha nyumba kwenye ukoloni na utumwa. Kusema kuwa watu weusi waliumbwa kutawaliwa na wazungu, ni kutudhalilisha na kujidhalilisha mwenyewe.

Unaonaje kama mahakama ingekupa hukumu ya kuwa mtumwa kwa mwezi mmoja tu, nadhani usingetoa lawama bila kufikiri. Unataka kusema kuwa babu zetu hawakupigana na mzungu? Walipenda kuotelewa na watoto na ndugu zao? Watoto walipenda kukua bila baba? Ukiona mkeo au mumeo anabakwa unajisikiaje? Ni kitu kibaya sana

Naanza na wewe, kuonyesha unapinga hili tupia neno la kupinga ukoloni leo hii
 
ATHARI ZILIZOLETWA NA UKOLONI JUU YA DAMU, VICHWA VYA WAZEE WETU

MWARABU
(Mkoloni) ni mtu mbaya sana kwani ni moja yapo ya watu wabaya kuleta utumwa,
Naunga mkono hoja


P
 
Naunga mkono hoja


P
Nakupongeza sana kwa hoja yako imejieleza kwa inavyotakiwa
 
Tatizo kubwa nnalo liona hapa ni Akili ya Watu weusi kusimamiwa na hao Wakoloni ,na hiyo ipo mpaka leo ktk mambo ambayo tumeaminishwa na kuyafuata.

Ni vigumu sana kumtawala Mtu anae jitambua ,walio jaribu kwa kutenda ili kuwatoa Watu weusi ktk Giza waliuwawa kikatili na wengine waliozea Gerezani kwa kutumikia Adhabu.
 
Tuweni wakweli,
Wazungu na Warabu wote lao moja. Kimtazamo hawa watu wa rangi including Indians wanajiona wao ni superior race ukilinganisha na waswahili.

Na wakati wa mkoloni Muingereza Mzungu alikuwa class one; Indians na Arabs class 2; Somali somewhere in the middle na waswahili daraja la mwisho.

Muingereza aliwapa Indians mitaji ya kuanza biashara baada ya kumaliza kazi ya kujenga reli toka Tabora mpaka Mwanza.

Kihistoria ubaguzi wa rangi ulianzishwa na wakoloni waarabu na wazungu.

Sasa hivi umeingia ubaguzi mwingine taratiiibu. Kuna watu wana degree kadhaa na sasa wanajiona wana akili/weledi mkubwa kuliko wale wanajua kusoma na kuandika.

Ubaguzi huwa ni ubaguzi pale mtu mmoja anapojiona yeye ni bora kwa rangi ya ngozi, wingi wa vyeti au unene wa wallet.

Kipimo cha utu mwl. Nyerere alituonesha, japo alikuwa msomi sana, yet alikaa meza moja na bmBibi Titi Mohamed kwenye kamati kuu.

Hivi leo watu wenye wingi wa digrii hata kama hawana ubunufu wowote wa ku-solve matatizo ya Watanzania; washafikia wakati wa kuwanyamazisha wengine in the name of no research no right to speak
 
Juu ya kinachoitwa "Ukoloni" kwa upande mmoja na "Harakati za kupigania Uhuru kwa nchi za Afrika" kwa upande mwingine, ni jambo linalohitaji utafiti wa kina.

Pasipo kufanya utafiti yatabaki mawazo na kimsingi mitazamo.

Lakini ukweli wa kinachoitwa ukoloni na harakati za kupigania Uhuru ndilo suala lisilopaswa kuwa mawazo au mitazamo, bali utafiti.

Historia ya dunia ni muhimu sana katika kuelewa ukweli wa kinachoitwa ukoloni na harakati za kupigania uhuru Afrika.

Suala la historia ya eneo ambalo hii leo linajulikana kama Afrika ni muhimu sana, ili kuelewa ukweli wa kinachoitwa ukoloni na harakati za kupigania uhuru.
 
ATHARI ZILIZOLETWA NA UKOLONI JUU YA DAMU, VICHWA VYA WAZEE WETU

MZUNGU
(Mkoloni) ni mtu mbaya sana na utawala wa kitumwa ulikuwa mbaya na kwani familia nyingi zilitengwa na wenzao na kupelekwa wasipokujua. Watoto walitengwa na wazazi wao, mume na mkewe kwa kweli inaonyesha ni uchungu kiasi gani babu zetu walipitia. Wanaume waliochukuliwa kwenda kufanywa watumwa ughaibuni, walichukuliwa na KUHANISIWA ili wasiwazalishe wanawake wa huko. Ndugu zetu wakiwa huko nchi za ugenini walipigwa MNADA na KUNUNULIWA kama bidhaa. Mambo haya waliyoyapitia ni ya uchungu mkubwa mno kuyaelezea, hakuna atakayefurahia kumkuta

MWARABU (Mkoloni) ni mtu mbaya sana kwani ni moja yapo ya watu wabaya kuleta utumwa, nakumbuka nilisimuliwa na bibi, waliwagawanya watu katika matabaka. Ilifika kipindi watu wakawa wanauza watoto wao kwa fitina za waarabu. Mfano pwani (Tanga mpaka Tabora maeneo haya yalijulikana kama pwani kipindi cha ukoloni) mtoto alikuwa ni mali ya mjomba, ikimaanisha bba hakuwa nanguvu zaidi ya mjoimba. Wajomba wengi waliuza watoto wao kwa waarabu ili wapate ujira. Kwa watoto waliokuwa na damu ya kiarabu wao na waarabu wenyewe walikuwa wezi wakubwa, tena waliiba watu wengi hususani watoto. Usipomchunga mwanao basi atanyakuliwa na hawa waarabu na mamluki yake na kwenda kuuzwa kama bidhaa.

Wazee wetu walijazwa hofu ndani ya mioyo yao ili wauone mzungu kama mungu, wengine waliwazania ni mungu. Wakoloni waliwafanya mababu na mabibi zetu wajione wako chini yao, kuwafanya kutekeleza mambo ya kikoloni (watu kuuza watoto wao wenyewe kwa Waarabu) na kumwabudu mkoloni kama miungu dunia. Bibi zetu WALIBAKWA sana tena sio mbele ya kadamnasi, walifanywa kama chombo cha starehe, wanawake walizalilishwa na kuzalishwa na watawala hawa wa mabavu. Ilipelekea wengine kutengwa na familia zao na kuteseka sana kwa uchungu mkubwa pale walipozalishwa na wakoloni.

Walipigwa fimbo kama wanyama, na kushurutishwa kufanya shughuli mbali mbali zenye kuwazalishia makoloni zikiwemo kulima mashamba ya wazungu. Mbali na hayo walinyimwa haki zao za kibinadamu mfano walishindishwa njaa bila kupewa chakula chochote, walifanyishwa kazi kupita uwezo wao wa kibinadamu, walitiwa chapa za alama kama wanyama n.k. Mababu zetu walitia sahihi mikataba ya kilaghai kwa shuruti na wengine kwa kupenda kuwauza wa-Tanganyika wenzao. Hapo unaona jinsi walivyotugawanya sisi wenyewe kwa wenyewe.

Hata baada ya kupata uhuru, dhambi ya utumwa haikukoma, ikaendelea kuwatafuna jamaa zetu kupitia UKOLONI MAMBOLEO. Nchi nyingi barani Africa hata baada ya uhuru bado ziliathirika na ukoloni mamboleo unaoendelezwa na watawala wenyeji. Tumeona wazungu wakipora utajiri wa nchi nyingi barani Afrika hata baada ya utumwai, hasa mafuta na madini. Ukoloni umeathiri FIKRA za ngozi nyeusi, ndo maana unaona watu wamekuwa wavivu kujiajiri, fitina, uvivu wa kufikiri nk. Je, kitu gani unaona tufanye kufuta ukoloni mamboleo jwa vizazi vyetu vinavyokuja?

Kuna watu wanajiona juhudi zao binafsi zilitupa uhuru, lakini harakati za uhuru zilianza toka kwa wote walipigana kutetea haki zao na familia zao (UHURU HAUKULETWA NA JUHUDI TANU PEKE YAKE). Shukrani zatu za dhati zinaenda kwa Chifu Mkwawa (1891 and 1894), Kinjekitile Ngwale kuwaunganisha watu katika vita vya Maji Maji (1905 – 1907), ma chifu wengi, taasisi za dini (WAKRISTU, WAISLAMU, DINI ZA KIJADI), na watu wote waliopigania uhuru kwa namna moja au nyingine. SHUKRANI ZA KIPEKEE zimwendee HAYATI MWALIMU NYERERE, kwa kuunganisha Tanganyika kuwa nchi moja yenye ushikamano mmoja pasipo UDINI, UKABILA, UKANDA, UBAGUZI WA RANGI N.K. Nawapongeza Maraisi wote waliopita na wa sasa kwa kufata nyayo hizi na kupiga kabisa chembe chembe hizi za chuki na kudumisha umoja wetu.

Kuna baadhi ya viongozi wa kipindi kile walitaka kudai uhuru wa maeneo yao binafsi na mfano mzuri ni Mangi Thomas Marealle. Kazi kubwa ilifanywa na Mwalimu J K Nyerere kuwaunganisha viongozi wa mikoa mbali mbali nchini Tanganyika na kuwaweka chini ya utawala mmoja. Isingekuwa juhudi na fikra za Mwalimu Nyerere basi kungekuwa na ushindani mkubwa sana kila mtu angevutia kwake. Kwa yeyote anayebeza kuwa yeye si MUASISI halali, mbona babu zao hawakupewa nchi watawale wao? Mbona babu zao hawakuunganisha Tanganyika? Kuna watu wengi walidai uhuru, kuna watu ndugu zao walidai uhuru kwa kiasi kikubwa leo hawako kutafuta ujiko. Mwalimu Nyerere hakudai uhuru wa wakatoliki, alidai uhuru wa wa-Tanganyika, hakupewa uraisi kwa sababu ya ukatoliki wake. Kwanza idadi ya WAKRISTU na WAISILAMU haikuzidi hata nusu ya WATANGANYIKA (wengi hawakuwa na dini za kuletewa).

Tahadhari: Naomba sana wana Tanzania wenzangu tupinge kwa sauti moja dhambi za kibaguzi; na yeyote anayepinga dhambi hizi aweke neno lake. Mimi siko hapa kubishana, kutukanana na mtu yeyote, ukoloni mamboleo umetawala fikra za watu wengi. Kupinga ukoloni mamboleo tena wanasiasa, kwa wasomi wanaojitafutia majina, wanaopayuka tu kuuharibu umoja wetu WAPE NENO LA KUJENGA. Swali, sio unakaa chini kila siku unawaza Tanzania imekufanyia nini, wewe umeifanyia nini Tanzania?
Hivi kuna mkoloni mbaya zaidi ya huyu JIWE? Naomba kujuzwa
 
Tatizo kubwa nnalo liona hapa ni Akili ya Watu weusi kusimamiwa na hao Wakoloni ,na hiyo ipo mpaka leo ktk mambo ambayo tumeaminishwa na kuyafuata.

Ni vigumu sana kumtawala Mtu anae jitambua ,walio jaribu kwa kutenda ili kuwatoa Watu weusi ktk Giza waliuwawa kikatili na wengine waliozea Gerezani kwa kutumikia Adhabu.
Nimekuelewa kwamba hata baada ya kupewa uhuru, bado tumekuwa tegemezi kuongozwa na ngozi nyeupe. Unahisi kitu gani kifanyike kwa kizazi kinachokuja kuwaepusha na hili tatizo

Nilitegemea watu kupewa elimu ya ukoloni na mateso waliyoyapitia jamaa zetu, basi inheleta chachu ya kutaka kubadilika. Kuna hata ya kufundisha historia hususani mashuleni kama bado haijamkomboa mtu mweusi?
 
Hivi kuna mkoloni mbaya zaidi ya huyu JIWE? Naomba kujuzwa

Sijajua unamaanisha nini ila naomba nikulize, unadhani tatizo liko wapi? Mabadiliko yanaanza na mtu mwenyewe ndiyo yanahamia kwenye jamii kisha nchi kwa ujumla. Katika jamii yako unaamua kuifanyia nini Tanzania?
 
Wazungu wachawi sasa uchawi upo dunia nzima. Majini uarabuni ndio nyumbani

Sanduku hilo lilifukwa na wajerumani ufukweni mwa bahari ya hindi pwani ya Tanga. Kwa kuwa bahari inakuja nchi kavu likafukua hilo sanduku, likawa linaonekaja kwa juu lakini ilitegemea kupwa na kujaa kwa bahari. Maji yakijaa lilikuwa linafunikwa na maji & maji yakipwa lilikuwa linaonekana sehemu ya juu. Wana kijiji walishindwa kulifungua sanduku japo lilionekana ufukweni mwa bahari.

Mambo mengi ya ajabu yalikuwa yanatokea pale walipotaka kulifungua sanduku hilo mfano maskari wawili wa kijerumani wakiwa wamebeba bunduki walikuwa wanatokea na kuwawatimua mbio. Watu walikuwa wanakuja na waganga ili watengue lile zindiko, wengine walitoa kafara za wanyama nawengine wanamwaga mitama ya bisi na kubanja nazi zilizokuwa na maneno ya kiarabu lakini yote ilikuwa bure

Watu wanaamini kuwa yale masanduku ya hela yalikuwa yamewekwa kichawi ndio maana walishindwa kuyachukua kwa mda mrefu. Kuna baadhi ya wajerumani huja kuchunguza baadhi ya vitu vyao walivyoacha kipindi cha utawala wao Africa mashariki. Sanduku la Tongoni lilichukuliwa na wajerumani wenyewe mwanzoni mwa miaka ya tisini, jambo la kushangaza hakuna jambo lolote la ajabu lilitokea wakati wanalifukua
- Kama ni kweli, ni kwanini hao wazungu walipokuja na kuona hilo sanduku pembeni mwa bahari hawakulichukua?

- Watu walijuaje kuwa kuna pesa ndani yake ilihali hawajawahi kulifungua?

- Utawala wa ujerumani una almost miaka 100 na zaidi sasa, hivyo vitu vilivyopo ndani ya hilo sanduku ni vya materials gani visiharibike hata kwa kutu ama kuisha? Ilihali Coins tu za silver za miaka kadhaa zinafubaa, hela za notes pia zinaisha.

Hiyo habari ya kusema walikuwa wachawi na sijui kuacha masanduku ni uzushi uliosambaa sana, hakuna ushahidi.

Kwahiyo inamaana walituzidi uchawi na kuwazidi hadi wanigeria?

Tangu mwanzo walituzidi kwa MAARIFA NA TEKNOLOJIA, ndio maana hata kwenye management tu wanatuzidi.
 
Nimekuelewa kwamba hata baada ya kupewa uhuru, bado tumekuwa tegemezi kuongozwa na ngozi nyeupe. Unahisi kitu gani kifanyike kwa kizazi kinachokuja kuwaepusha na hili tatizo

Nilitegemea watu kupewa elimu ya ukoloni na mateso waliyoyapitia jamaa zetu, basi inheleta chachu ya kutaka kubadilika. Kuna hata ya kufundisha historia hususani mashuleni kama bado haijamkomboa mtu mweusi?

Elimu yetu Mkuu imetupwa sana na hawa Watawala (Wanasiasa) wenye Mamlaka,mkazo mkubwa ni hapo ili kupunguza Wajinga na Wapumbavu.Nna amini Elimu ni chanzo cha mambo mengi sana yenye Faida.
 
- Kama ni kweli, ni kwanini hao wazungu walipokuja na kuona hilo sanduku pembeni mwa bahari hawakulichukua?

- Watu walijuaje kuwa kuna pesa ndani yake ilihali hawajawahi kulifungua?

- Utawala wa ujerumani una almost miaka 100 na zaidi sasa, hivyo vitu vilivyopo ndani ya hilo sanduku ni vya materials gani visiharibike hata kwa kutu ama kuisha? Ilihali Coins tu za silver za miaka kadhaa zinafubaa, hela za notes pia zinaisha.

Hiyo habari ya kusema walikuwa wachawi na sijui kuacha masanduku ni uzushi uliosambaa sana, hakuna ushahidi.

Kwahiyo inamaana walituzidi uchawi na kuwazidi hadi wanigeria?

Tangu mwanzo walituzidi kwa MAARIFA NA TEKNOLOJIA, ndio maana hata kwenye management tu wanatuzidi.

Nimekwambia walipokuja wajerumani walilichukua wenyewe na hakuna kilichotokea. Mimi mwenyewe nishashuhudia hilo swala mkoani Kilimajaro, wewe unataka kleta ubishi na mie siwezi kubishana.

Kama ujuavyo watu wakiona vitu vya zamani wanajua kuna mali. Kuna kipindi nilikutana na mrangi mmoja yeye alikuwa na wenzake kazi zao kuzunguka Tanzania kutafuta hayo masanduku na mali nyinginezo

Alafu watu wa zamani walikuwa wanatoa makafara sana kwa kutumia mali za kijerumani, sijui kwa nini. Ila mkoani kilimanjaro, hela ya mjeruma mpaka leo inatumika sana mfano mtu akijenga nyumba anaziweka juu ya dari kuzuia rapi isipate nyumba, mtoto mdogo anpozaliwa anafungwa zile hela n.k. Ndo maana inawezekana kila zinapozungumziwa watu wanashindwa kuzikomnoa

Lakini hizo za Tanga, atu walikuja na waganga zao ndugu Azarel mie nakuweleza. Ukiuliza utaambiwa. Mpaka leo kuna watu wananunua hela za kijerumani mpaka moja laki tano kwa mambo yao a kishirikina
 
Elimu yetu Mkuu imetupwa sana na hawa Watawala (Wanasiasa) wenye Mamlaka,mkazo mkubwa ni hapo ili kupunguza Wajinga na Wapumbavu.Nna amini Elimu ni chanzo cha mambo mengi sana yenye Faida.
Ciril unachosema sikipingi ni kweli, Afrika tumeshindwa kutofautisha SIASA na TAALUMA. Elimu yetu imeingiliwa na SIASA sana kinachotakiwa tutofautishe sana hapa. Waalimu wa vyuo vikuu wazalishe TAALUMA na siasa isipate nafasi mashuleni na vyuoni. Umesema nino zuri sana la kujenga nakupongeza
 
Back
Top Bottom