watu wa dunia ya leo wanatazama mbele sio nyuma.
watu wanajiuliza juu ya uraia wa nchi mbili au zaidi, sisi tunajiuliza uraia wa nusu nchi!
watu wanazungumza namna ya kuvutia uwekezaji wa kimataifa, uondoshwaji wa masharti ya visa, sisi tunazungumzia kichefuchefu cha neno "bara" kwenye utambulisho wetu, tunataka turejee kwenye nchi mbili na kurudisha masharti ya passport na visa
watu wanahangaika na mazungumzo ya ushirikiano/uundwaji wa shirikisho, soko la pamoja, ushirikiano katika masuala ya sayansi na tekinolojia, umoja wa forodha, sarafu moja nk sisi tunazungumza namna ya kuvunja muungano!.
jambo la msingi la kujiuliza ni je, tunapiga hatua kimaendeleo au tunarudi nyuma? tunakwammishwa na jina hili tanzania, au ni kitu gani kinatukwamisha tusiendelee kwa kasi tuliyotazamia? kama hatupati maendeleo tunayohitaji kwa kasi tunayotazamia, je, tatizo ni nini, ni jina la Tanzania?
Miss Judith.
Umesema mengi mazuri katika mchango wako.
Lakini mengine umeyatoa nje ya "context"
Zaire imerudi katika jina lake la zamani...sijui wamerudi nyuma?
Lakini hapa wengi hawasemi turudi kwenye nchi mbili kwa maana ya utengano, nilivyowaelewa mimi.
Watanganyika wanataka jina Tanganyika litumike kwa sehemu ya iliyokuwa nchi ya Tanganyika kabla na sio Tanzania bara na pia yale mambo ambayo si ya muungano, yaitwe mambo ya Tanganyika badala ya kuitwa mambo ya Tanzania bara au wizara za mambo ya Tanzania bara. na wazanzibari wanahoji kupotea kwa Tanganyika. wao wanauliza wajadiliane na nani?
Kumbuka muungano huu si muungano wa kila kitu au jambo. Jikumbushe historia ya muungano.
Kwa hiyo malalamiko hasa yapo kwa sababu mbia mmoja wa muungano kapotea au kajipoteza. Inapotokea upande uliobaki unataka kuzungumza au kujadiliana tena kuhusu jambo lolote ajadiliane na nani?
Umetoa mfano wa nchi kuungana na kuondosha visa. kweli hili ni jambo zuri lakini pia wao wameweka utaratibu mzuri. kama mfano wa EU hawa wote ni europeans lakini kila european ana utambulisho mwengine kama ni mjerumani,mfaransa ,mgiriki au mbelgiji.
Majina ya nchi zao au utaifa wao haukufa na bado wamepiga hatua hizo unazosema.
Tatizo la kwetu ni usanii mwingi na utaratibu mbovu au misingi mibovu ya muungano tulionao. na kwa sababu "viongozi" hawataki kusikiliza vilio vya wananchi ndio wengine wanafikia kusema muungano uvunjwe lakini wengi wanataka iwekwe misingi ya muungano wa haki na usawa. na vilio hivi viko Tanganyika na Zanzibar.
Au wewe unaelewa muungano ulioua wanachama wake?
Au sisi kwa kuliua jina Tanganyika ndio tumepiga hatua za kwenda mbele zaidi ya hao unaoona wamepiga hatua kubwa kimaendeleo na ushirikiano?