Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

When democracy has no chance, it is the responsibility of everyone and anyone to give it a chance!
kuongea ukiwa umejificha kwa id feki ni rahisi sana,ukitaka kua muasi huna haja ya kuandika JF hiyo ni mikwara mbuzi tu
 
mkuu umewaza kwa fikra huru na umevuka upeo wa kawaida wa fikra.. mawazo yako yamejaa ukweli mtupu... nakwambia hata Gaddafi hakuijua nguvu ya umma kabla pamoja na jeshi na polisi kumuunga mkono unaambiwa hakupata pa kutorokea japo alipewa visting offer ya kwenda uhamishoni na marafiki zake. nakuahidi TUTAWANYAKUA TU.
Unachokisema si cha kweli.....Gaddafi alitaka mwenyewe kupambana hadi umauti akiwa pale Libya, si kwamba hakuwa na nafasi ya kutoroka au kukimbia.

Gaddafi hakuwa coward kwa taifa la Libya na ndio maana alikuwa tayari kwa lolote....

Na kuanguka kwa Gaddafi ni matokeo ya usaliti wa ndani, miongini mwa raia wake na watu wake wa karibu wenye viroho vya kwann!

Na leo wanaona faida ya roho ya usaliti na tamaa ya kukomoa.......
 
Kama kijana nayeipenda nchi yangu, nayependa amani, demokrasia na maendeleo nafanyaje?

Nafanyaje Askari wanaposherehekea ushindi wa dhulma wa chama tawala kwa kuimba 'soldier nyakua'?

Nafanyaje mheshimiwa rais anapotoa ilani ya kumshughulikia Mkurugenzi atakayemtangaza mpinzani kuwa mshindi kwenye uchaguzi?

Nafanyaje napoona viongozi wangu wa chama, wapenda demokrasia na amani, wakidhalilishwa na polisi kila leo,wakinyang'anywa Mali zao kwa nguvu, wakilazimika kuzunguka mahakamani kila uchao na wakidhalilishwa wao na familia zao?

Nafanyaje napoona vijana wenzangu wa Rika wakishawishiwa na kushawishika kwamba demokrasia haina nafasi Bali siasa za visasi, hujuma na matumizi ya nguvu ya dola ndio mtindo wa kileo?

Nitaendeleaje kuamini katika uchaguzi huru na wa haki wakati tume yenyewe ya uchaguzi haiamini Wala vyombo vya dola haviamini?

Kwanini wakati wa apartheid vijana wa Afrika kusini walikuja kujifunza hapa mbinu za uasi?
Kwanini hawakuitisha tu mikutano ya siasa nchini kwao na kwenda kupiga kura?

When democracy has no chance, it is the responsibility of everyone and anyone to give it a chance!

SOLDIER NYAKUA, NYAKUA!
Vipi mkuu.
 
unawaza misitu tu , jiongeze mjomba , usije kusema hatukusema .
Hao ndio wale wanakula na kulala kwa shemeji na wanaona maisha ni kawaida na miguno wanayosikia usiku toka chumbani kwa dada hawajui ndiyo inayo fanya wasiambiwe wakajitegemee
 
Back
Top Bottom