Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

Nchi yangu inaniandaa kuwa muasi

Kama kijana nayeipenda nchi yangu, nayependa amani, demokrasia na maendeleo nafanyaje?

Nafanyaje Askari wanaposherehekea ushindi wa dhulma wa chama tawala kwa kuimba 'soldier nyakua'?

Nafanyaje mheshimiwa rais anapotoa ilani ya kumshughulikia Mkurugenzi atakayemtangaza mpinzani kuwa mshindi kwenye uchaguzi?

Nafanyaje napoona viongozi wangu wa chama, wapenda demokrasia na amani, wakidhalilishwa na polisi kila leo,wakinyang'anywa Mali zao kwa nguvu, wakilazimika kuzunguka mahakamani kila uchao na wakidhalilishwa wao na familia zao?

Nafanyaje napoona vijana wenzangu wa Rika wakishawishiwa na kushawishika kwamba demokrasia haina nafasi Bali siasa za visasi, hujuma na matumizi ya nguvu ya dola ndio mtindo wa kileo?

Nitaendeleaje kuamini katika uchaguzi huru na wa haki wakati tume yenyewe ya uchaguzi haiamini Wala vyombo vya dola haviamini?

Kwanini wakati wa apartheid vijana wa Afrika kusini walikuja kujifunza hapa mbinu za uasi?
Kwanini hawakuitisha tu mikutano ya siasa nchini kwao na kwenda kupiga kura?

When democracy has no chance, it is the responsibility of everyone and anyone to give it a chance!

SOLDIER NYAKUA, NYAKUA!
Mkuu japo jukumu la kujenga nchi ni la kila mwananchi,wengi wetu wanadhani ni la viongozi tu.
Lakini kibaya zaidi hata ule utaratibu wakuwachagua viongozi kupitia njia ya kura umebuma kwani ni vijana wachache wanajiandikisha kupiga kura na ni wachache zaidi wanaokwenda kupiga kura.
Mimi naami kwa kuwa walio wengi tumepiga kisogo demokrasia na kuwaachia watu wachache wafanya watakavyo.Tumegeuza nchi yetu shamba la majaribio tokea nchi yetu kupata uhuru.
 
Kama kijana nayeipenda nchi yangu, nayependa amani, demokrasia na maendeleo nafanyaje?

Nafanyaje Askari wanaposherehekea ushindi wa dhulma wa chama tawala kwa kuimba 'soldier nyakua'?

Nafanyaje mheshimiwa rais anapotoa ilani ya kumshughulikia Mkurugenzi atakayemtangaza mpinzani kuwa mshindi kwenye uchaguzi?

Nafanyaje napoona viongozi wangu wa chama, wapenda demokrasia na amani, wakidhalilishwa na polisi kila leo,wakinyang'anywa Mali zao kwa nguvu, wakilazimika kuzunguka mahakamani kila uchao na wakidhalilishwa wao na familia zao?

Nafanyaje napoona vijana wenzangu wa Rika wakishawishiwa na kushawishika kwamba demokrasia haina nafasi Bali siasa za visasi, hujuma na matumizi ya nguvu ya dola ndio mtindo wa kileo?

Nitaendeleaje kuamini katika uchaguzi huru na wa haki wakati tume yenyewe ya uchaguzi haiamini Wala vyombo vya dola haviamini?

Kwanini wakati wa apartheid vijana wa Afrika kusini walikuja kujifunza hapa mbinu za uasi?
Kwanini hawakuitisha tu mikutano ya siasa nchini kwao na kwenda kupiga kura?

When democracy has no chance, it is the responsibility of everyone and anyone to give it a chance!

SOLDIER NYAKUA, NYAKUA!
Umenibadirisha mawazo, Umenifanya nianze kuifikiria upya, mwanzo nilidhani kuwa adui namba moja wa nchi yetu ni ccm, nadhani I was totally wrong, adui wa kwanza wa nchi hii si ccm bali ni watanzania wenyewe, ndiyo ni watanzania wenyewe, kwani wafanyakazi wa tume ya uchaguzi si watanzania? Je wafanyakazi wa vyombo vyetu vya dola si watanzania? Je wakurugenzi wa halmashauri zetu si watanzania? Yes ni watanzania, sasa kwani hayo unayoyaona kiasi cha kukufanya ujiandae kuwa muasi wao hawayaoni, hivi hawajui kuwa chama cha siasa, kwa mfano ccm ni kikundi cha watu wachache ndani ya nchi yetu?
 
Wenzako walijaribu wakaishia kuasiwa, hebu na wewe jaribu bahati yako, mapori ni mengi Sana
Fikira hizi zinatudanyanya, watu wakifikia Level ya kuona hawana cha kupoteza, basi wewe fundi wa kuhasi jiandae kuhasi wote ila ukishidwa kuwahasi wote basi jua kichwa chako ni halali yao. Kwa Tanzania ilipofikia, watu kumi tu wakifa kwa mpigo kwenye furugu za kisiasa,siasa za nchi yetu zitabadirika kabisa, yaani hatasikia tena habari za chama tawala wala ccm, just mark my word
 
Tuongee yote, lakini tukubaliane kabisa, mleta mada ameona mbali.
 
Msio ijua history na Ukweli wa mambo hua nawaonea huruma Sana.
Gaddafi hakutolewa na nguvu ya umma, bali ni mabeberu wakitumia NATO, na walibya wanajuta kwa sasa, kama hujui Jambo ni bora kunyamaza kulinda heshima yako kuliko Kuonyesha uzuzu wako hadharani
sasa tunahitaji mabeberu watumie NATO, watusaidie kuifurusha CCM. tutatoa ushirikiano tu
 
Shetani ameiteka hii nchi tangu ingali changa kabisa. Ni Mkono wa Mungu Mwenyezi pekee utatuokoa!

Hekima imefanyika ujinga na ujinga umefanyika hekima.

Ila naona viongozi wetu wakiwekwa tayari (kwa kunyimwa hekima) for a very, very, very rude awakening.
 
Wewe ni jambazi na nyumbani mwako ni jela milele walahi!
Unacho waza ndio utakachopata mfungwa wewe walahi!
Samahani dada, una mtindio wa ubongo (are you a retard) ?

Wewe na mwenzako cocochanel mna tatizo kubwa la kisaikolojia. Nawashauri mkawaone viongozi wenu wa kiroho mpate rigourous counselling.
 
Mkuu japo jukumu la kujenga nchi ni la kila mwananchi,wengi wetu wanadhani ni la viongozi tu.
Lakini kibaya zaidi hata ule utaratibu wakuwachagua viongozi kupitia njia ya kura umebuma kwani ni vijana wachache wanajiandikisha kupiga kura na ni wachache zaidi wanaokwenda kupiga kura.
Mimi naami kwa kuwa walio wengi tumepiga kisogo demokrasia na kuwaachia watu wachache wafanya watakavyo.Tumegeuza nchi yetu shamba la majaribio tokea nchi yetu kupata uhuru.
siyo kweli! kila mtu anaona kinachoendelea ktk chaguzi zetu. hata wakijitokeza hawataweza kupambana na policy wenye bunduki.
 
Ameuliza anafanyaje kama mambo ndo hayo? Mpeni jibu badala ya kumkebehi na kumtisha...
Swali la kijana jepesi tu
NAFANYAJE NINAPOYAONA HAYA YANAYOTENDEKA?
Kijana labda nikusaidie kitu
Wanaofaidi maisha sio wenye akili nyingi wala wenye nguvu nyingi ... bali wenye uvumilivu na fikra pevu.
Si ameshasema ataingia msituni, aingie sasa.
 
Kujenga taifa na utaifa siyo kazi nyepesi inayoweza kufanywa na mbilikimo (lilliputs) wa kisiasa. Nyerere alipata kusema ni ujinga Watanzania kudhani kuwa nchi yao ni tulivu na haiwezi kwenda njia ya Sierra Leone, Liberia, Somalia, Burundi, Rwanda, nk. Alitoa mfano wa Somalia, nchi ya kabila moja na dini moja lakini bado ikasambaratishwa na tofauti za kiukoo.
Somalia kuna kabila moja? Lies. Come again
 
"When people are voiceless, they will've temper tantrums.... And riots are massive temper tantrums from neglected and voiceless people.." Martin Luther King Jr
 
Msitu sahihi wa kuingia ni ule wa maendeleo binafsi familia yako na mke wako wapate mkate unaostahili. Upinzani gani wenyewe hauna hatua? Kila mwaka wao tumeibiwa tumeibiwa, jamani wananchi tumeibiwa. Sisi kama kambi ya upinzani tumeibiwa na tunalaani. Hizi laana haziwapati tu wahusika?
 
Back
Top Bottom