Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Ili ujue atakayofanya magufuli huhitaji kufumba macho na kuanza kuyafikiria aliyoyafanya kwa taarifa yako yapo bayana kabisa,kila mtanzania anayajua,sema kinachowauma wachache ni ile wagombea wao kushindwa hilo ndo naweza kuelewa kuwa hoja nyingine hapa ni maumivu ya moyo,na nitoe ushauri hapa kwamba kama hamtoi uchungu wenu wa mioyo na kukubali matokeo mtaumia sana lakini jembe litaendelea kuchapa kazi na bahati mbaya yenu ni kwamba the majority wanafahamu uwezo wa magufuli,mie nikimlinganisha na hata hao mnaowaombolezea na kufikia hadi kuzusha kwa niaba yao haotasaidia kikubwa kubalin yaishe tujenge taifa
 
Well said!
Hapa tatizo ni mfumo huu ulioasisiwa na chama 1!.
Lkn watu hawaelewi
Ooh magufuli jembe sijui nn!
Hakuna jipya chini ya huu mfumo!!

Mfumo ni watu mmoja mmoja na taasisi waziundazo. . . . .Ukipata key palyer mzuri anaweza badili mchezo mkaacha kufungwa mkaingia kwenye kutoa droo. . . . .

So far apewe benefit of doubt. . . . . sababu anaweza akiamua sasa asipoamua tutaanzia hapo japo tutakuwa tumeumia. . . .
 
Asante The Boss kwa mada hii muhimu. Nimepitia michango ya wenzangu waliotangulia, ni kweli kuwa ni wakati muafaka sasa tujadili na kushiriki kutengeneza nchi na taifa letu na historia itatuhukumu hivyo.

1. Kwa CCM suala la Urais kwao halina mjadala ni LAZIMA awe wa kwao hata kama italigharimu Taifa hili uhai wake wote. Hiyo ni siri iliyo wazi kwa miaka mingi tu.

2. Je ni mara ngapi tumewahi kusikia au kuona "viongozi wakuu" kama Rais, Waziri Mkuu, Wabunge na Mawaziri wakisema/kulalamika au kuonyesha "laiti kama ingekuwa ni uwezo/mamlaka yangu basi ninge......." Mifano iko mingi; mfano kauli ya Waziri Mkuu Pinda kuwa "wakiwashughulikia mafisadi nchi itayumba..." Hii inaonyesha kuwa kuna "nguvu" nyuma yao hao wanaonekana kwa macho kuwa "wakuu"; ambayo wao wenyewe wanaiogopa na kutumikia hiyo "nguvu" kwa hiari au shuruti, kwa kujua au kutokujua.

3. Kauli ya Kingunge ni nzito na ya ajabu sana kwa kuzingatia historia, uhusiano na hadhi yake CCM.
Kwangu mimi kauli ile ina vitu vikubwa vine (tofauti na watu waliojitokeza kusema kuwa mzee yule alikuwa anaitishia CCM nyau).
a) Kitengo ni kitu halisi "real"
b) Kitengo, pamoja na kuwa ni halisi, lakini sio kinachofikiwa na wengi (not accessible to all except for a selected few)
c) Kitengo ni fumbo pana na refu (codeword and terible mystery)
d) Kitengo hakina mipaka (kinaweza kuanzia ndani ya CCM lakini hakiishi huko na kinyume chake)

4. Matunda yake yako wazi katika historia ya nchi yetu. Ujinga umeendelea kutusumbua, umaskin umeendelea kuongozeka, maradhi, madawa ya kulevya, rushwa na ufisadi vimeongezeka kila siku na sasa vinatishia mustakabali wa nchi nzima.

5. Ugumu wa fumbo ni pale (kwa mujibu wa Kingunge) Kitengo ndio "kilipika/kilitengeneza" kashfa ya Richmond ili kumtoa Lowassa kutoka kuwa WM (hatujui hasa kwanini), lakini kwa jinsi kilivyo cha ajabu, nusura kiiangushe kabisa Serikali ya Kikwete mwaka 2006! Inaonesha kitengo kiko nje/juu ya mamlaka ya Mkulu. Ni kama vile duara (cycle) huoni mwisho na mwanzo ni mgumu pia kuuona!

HITIMISHO (kwa sasa)
i. TISS, Idara ya Ulinzi/Usalama/Ujasusi wa Chama, Ikulu, Bunge ni sehemu ya Kitengo lakini Kitengo sio Umma (Wananchi wa Tanzania.
ii. Kitengo kipo kiuhalisia ingawa hakipo kwa mujibu wa Katiba yetu ya JMT.

Fumbo bado linataka tuendele mbele zaidi kuchunguza, kudadisi na kuwa wajasiri zaidi ili tusimezwe na "Kitengo"
 
Kwa hali ilivyo ni bora iwe hivyo kwa muda. . . . . . " kuna mambo labda hayahitaji mjadala na labda kuna mambo yakiwekwa wazi kabisa itahitajika nguvu kubwa zaid kutuliza jamii" hizi ni aasumptions ambazo zinaweza sababisha nchi kuelekezwa nini cha kufanya . . . . .

Naamini ni kwa faida ya wengi na ya muda mrefu. . .

Wewe ndo umeongea point kabisa.....watu hapa wanachangia kisiasa zaidi..,
Ikitokea UKAWA walete mgombea maslahi mfukoni, pia CCM watuleteee mwingne kuipeleka nchi shimoni ndo tuwaache tu kisa nini?
Kuna mambo wananchi hawawezi kuyasikia na ikitokea wakafaham juu ya hao wanaowashabikia wanaweza wakastajaabu na kupata stroke
Hii nchi bado changa sana hata huo upinzani inabidi ujengewe uwezo kuongoza nchi.....Mtauzwa hadi mayai yaliyo tumboni kwa ushabiki watanzania ....tulieni tujenge hii nchi yetu sote si ya kuendeleza kusini, Kaskazini, wala kanda yeyote ile..tunahitaji maendeleo na tuache propaganda tusizozijua kwa undani wake...hatuwezi kabidhi nchi kwa mtu kisa mahaba ya siasa
 
Unless kuna mapinduzi, hiyo ni standard practice dunia nzima.
Fuatilia kilichompata Princess Diana yule wa Uingereza aliyetaka kuolewa na mwarabu, alipatiwa ajali na akamalizwa haraka sana.

Hakuna ushahidi kwamba aliuliwa, kule kuna waandishi wa habari wanojua kufuatilia habari in deep. Kwa hiyo hizo habari unazosema sio za kweli na huna ushahidi nazo, ni habari za vijiweni.
 
Sasa hao usalama wa taifa si waingie na kwenye michakato ya vyama vingine ili kuweka usawa katika kupata mtu safi mbele ya wananchi?

Hapa ndipo tunapotofautiana, Usalama wa taifa iachwe ifanye kazi zake kiuweledi bila ya kuingilia siasa. Kama kuna mtu fisadi basi wanatakiwa wamshughulikie kama muhalifu hata kama ni Waziri au mtu yoyote aliyevunja sheria za nchi. Wasisubiri mpaka huyo mtu anapotaka kugombea nafasi kwenye chama chake. hapo ni kuingilia kazi za vyama vya siasa. Sasa hivi Usalama wa Taifa umeshajisahau kuwapo kwa ajili ya kulinda taifa, badala ya kufanya ukachero wa kulinda taifa sasa wanafanya ukachero kulinda ccm.
 
Mfumo ni watu mmoja mmoja na taasisi waziundazo. . . . .Ukipata key palyer mzuri anaweza badili mchezo mkaacha kufungwa mkaingia kwenye kutoa droo. . . . .

So far apewe benefit of doubt. . . . . sababu anaweza akiamua sasa asipoamua tutaanzia hapo japo tutakuwa tumeumia. . . .

Na km kuumia ni Miaka 10 tena!!!

Siamini km ataweza,kwenda kinyume na matakwa ya "kitengo" sidhani km ni rahisi!!!
 
Kuna vitu vinajitokeza kipindi hiki cha uchaguzi
ambavyo vinapaswa kuulizwa
je nikweli wananchi wa Tanzania ndio wasemaji wa mwisho wa masuala ya nchi hii?
au kuna watu kwa aakili zao na utashi wao wamejipa 'jukumu' hilo?

Kingunge alisema 'KITENGO' ndio kiliamua nani awe mgombea wa CCM na sio
wanachama......na Ukisoma gazeti la Raia Mwema wanasema watu wa 'usalama'
walimwambia Ngeleja awaambie wazanzibar kumchagua 'mgombea wa kitengo'
ndio akashinda....maswali yanajitokeza
1.kitengo kinaendeshwa na nani hasa?
2.Ni watu wangapi wanaofanya hayo maamuzi?
3.Ni kweli maamuzi yao yote ni kwa faidaya Taifa?
4.Wananchi wakipishana maamuzi na 'kitengo' maamuzi ya wananchi yataheshimiwa?
5.Nguvu ya 'kitengo' kwa tume ya uchaguzi ni halali?
6.kuna faida ya kushiriki uchaguzi huku 'kitengo' kimeshafanya maamuzi?
7.Je tuna demokrasia kweli au tunaruka ruka ttu na maigizo?

========
Some interesting comments:

Umeshaambiwa kitengo walashapanga Rais awe membe lakini wajumbe wakakigomea kitengo wakaamua kupiga kura Kwa magufuli , kitengo sasa wote wapo Kwa magufuli watahakikisha anakuwa Rais mpende msipende hata kama kura za wananchi zitakwenda Ukawa lakini wajue Rais ni magufuli tu.
 
Wewe ndo umeongea point kabisa.....watu hapa wanachangia kisiasa zaidi..,
Ikitokea UKAWA walete mgombea maslahi mfukoni, pia CCM watuleteee mwingne kuipeleka nchi shimoni ndo tuwaache tu kisa nini?
Kuna mambo wananchi hawawezi kuyasikia na ikitokea wakafaham juu ya hao wanaowashabikia wanaweza wakastajaabu na kupata stroke
Hii nchi bado changa sana hata huo upinzani inabidi ujengewe uwezo kuongoza nchi.....Mtauzwa hadi mayai yaliyo tumboni kwa ushabiki watanzania ....tulieni tujenge hii nchi yetu sote si ya kuendeleza kusini, Kaskazini, wala kanda yeyote ile..tunahitaji maendeleo na tuache propaganda tusizozijua kwa undani wake...hatuwezi kabidhi nchi kwa mtu kisa mahaba ya siasa
Well nailed. . . . .
 
Kwenye maelezo yako umesema kwa kumuweka mtu anaweza leta hayo mabadiliko
Sasa Magufuli sidhanikama nimsikivu enough hata kwa hao KITENGO
na power ya urais inampa nguvu hata ya kukisuka KITENGO kwa malengo yake
ni gamble ambayo watu wenye uzalendo wa kutosha wasingeifanya
We need people like John Edgar Hoover katika ofisi za Usalama wa Taifa. Mtu akayepigania Usalama wa taifa uwe na nguvu kama walizokuwa nazo enzi za Nyerere au zaidi ya hapo. Wawe na misuli ya kwenda sehemu yoyote ya nchi na nje ya nchi bila ya kuingiliwa na wanasiasa. wakatae kutumika kisiasa kama John Edgar Hoover, wajikite kwenye ufanisi wa kazi zao.

 
kitengo ndicho chenye kuamua mpaka hesabu za kura ziendee kwa nani.

Ndiyo maana yake kitengo wana matokea tayari hapo wanasubiri mda watangaze Rais magufuli , kule Zanzibar tokea 1995 CUF imekuwa ikishinda Uchaguzi lakini kitengo hubadilisha matokeo na ccm kupewa ushindi wa mezani kirahisi ina maana Zanzibar hata wana ccm wasipopiga kura ccm itashinda tu kupitia Kwa njia za kitengo.
 
ha ha ha...naona sasa vijana wamelipwa kuja mitandaoni kutuletea porojo.
ACHENI POROJO NA KUTUMIKA...
Lowasa mwenyewe ni hatari kwa afya yake binafsi...sembuse familia yake na watanzania.

Hivi kweli bado kuna WaTz wa namna hii? yaani umeshindwa kuziona logic zote, umeona Lowasa tu...

Chukua yale mazuri, ya Lowasa yaache.
 
Ah wapi! Ukibahatika kutembelea sehemu mbalimbali za nchi ndo utagundua kwamba maamuzi 'yao' mengi wala si kwa manufaa ya taifa.

Sina uhakika sana na hili la kiinua mgongo cha wabunge na sijalisikia tena tokea karibu wiki mbili zilizopita lakini kama kweli hicho kitengo dhima yake kuu ni kulinda maslahi ya taifa basi kingeingilia kati ili hayo mabilioni ambayo yanadaiwa wabunge watalipwa yaende sehemu ambazo zina uhitaji mkubwa zaidi.



Thubutu! Watanzania wa kizazi hiki hawana ujasiri wala uthubutu wa kupishana na maamuzi ya 'kitengo'. Majuzi tu hapa tumeona jinsi ambavyo rafu imechezwa hadi Magufuli akawa railroaded kuwa mteule wa chama na yule ambaye iliaminika ndiye aliyekuwa chaguo la wengi kutoselewa mbali tena kwa udhalilishaji wa hali ya juu. Walipojitokeza watu wawili watatu kujaribu kupinga kilichotokea walizimwa haraka sana na wakarudishwa mstarini.



Sisi hatuna tume huru ya uchaguzi. Hiyo ambayo tunayo sasa ni extension ya 'kitengo' tu. Hebu tumia tu hata busara zako za kawaida [common sense]. Ni nani ambaye huiunda hiyo tume? Mwenyekiti wa hiyo tume na hao wenzake huwa wanapatikanaje?



Kwa ujumla mimi sioni faida yoyote ile hususan kwenye urais. Kwa jinsi ambavyo mambo yalivyo hivi sasa CCM kuja kushindwa na wapinzani haiwezekani hata kidogo. Kutegemea mwenyekiti wa tume ya uchaguzi aliyeteuliwa na rais/ mwenyekiti wa CCM kumtangaza mshindi wa kiti cha urais mgombea wa upinzani ni sawa na kutegemea ngamia apite kwenye tundu la sindano.

Kama kuna anayedhani hiyo tume ya uchaguzi siyo extension ya kitengo namsihi arudi kumwangalia mmoja wa watangaza nia wa CCM - Jaji Agustino Ramadhani. Huyu bwana nadhani alikuwa ni makamu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kuanzia mwaka 1993 hadi 2002 na kuanzia 2002 hadi 2007 alikuwa makamu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar [eti hawa watu nao wana tume yao ya uchaguzi!!].

Hiyo inatueleza nini kuhusu hiyo inayoitwa tume ya uchaguzi? Je, ina maana tume nzima imejaa makada wa CCM? Mimi nadhani ni hivyo.



Ni maigizo tu. Demokrasia gani hiyo isiyotoa fursa sawa kwa washindani wote? Hata katiba ya nchi inayoendana na misingi mikuu ya kidemokrasia hatuna. Eti juzi juzi tu hapa ndo tumestuka na kuona umuhimu wa kuandika katiba mpya.

Kwa nini hilo halikufanyika hapo awali kabisa mwaka 1992 tulipoingia kwenye siasa za vyama vingi?

Na kusema ukweli Tanzania wala hatuna siasa za vyama vingi. Siasa zetu ni za chama kimoja ila kuna mazingaombwe yanayofanya watu wadhani kwamba tuna siasa za vyama vingi. Hatuna.

Wiki ilopita tumeshuhudia jinsi ambavyo nadhari karibu ya Watanzania wote ilivyoelekezwa huko Dodoma katika shauku ya kutaka kujua rais ajaye atakuwa nani.

Hakuna ubishi wowote ule kuwa rais wa 5 wa Tanzania ni John Magufuli.

Hata kupatikana kwake hakukuwa kwa demokrasia. Kinachosubiriwa sasa ni kukamilishwa tu kwa taratibu [igizo la uchaguzi mkuu hapo Oktoba] na yeye kuapishwa, basi.

Nyani Ngabu Umemaliza kila kitu hapo, tanzania hakuna demokrasia ya vyama vingi bali kuna kiini macho cha demokrasia. Uchaguzi unakuwa sio wa haki. tatizo kubwa tunalo sisi wenyewe watanzania, tunachezewa vibaya sana na hawa wahuni
 
Kubali ukatae kitengo ni kila kitu hapa Tanzania japo kuna sehemu wanashindwa mfano wameshindwa kumpenyeza Membe na January machaguo ya Jk na Nape , sasa wanajipanga kumpa Membe uwazi Mkuu na Nape atakuwa waziri wa Utawala bora au mambo ya ndani ili waanze kuwakomesha timu Lowasa , kitengo wana uhakika Kwa 1000% magufuli atakuwa Rais na membe atapewa ulaji sanjari na Nape .
 
Kuna wapiga kura mil 20, ccm ina wanachama mil6 , ukawa wa jitahidi kuvuna wana chama at least wawe mil 8 kwa mwaka 2025, waende kwenye matawi chini huko , then watafute suppor ya kitengo , kitengo hakiwezi kumpa mbowe nchi au slaa. Tanzania sio uingereza au marekani , demokrasia yetu inavyoendeshwa ni kama urusi na China , hizo nchi zote vyama Vya upinzani havijawahi shika nchi , comrade kinana amekirudisha chama huko hadi kapeleka watu kwenye mafunzo China kwanini haendi uingereza hadi Balozi wa China kasimama jukwaa la ccm , kitengo kina nguvu sana ila kwa ugomvi wa membe na lowassa kumteua magufuli aisee Jamaa wamecheza
 
Back
Top Bottom