Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

hapa inazungumziwa TISS kuegemea chama kimoja, ww unaleta mambo ya CIA kupanga nani aongoze nchi, democratic na republican wanabadilishana uongozi bila matatizo nyie mnakumbatia chama kimoja. maendeleo mtasubir miaka 1000
Maturity ya chama kwenye kuongoza nchi ndio vinasababisha watu wapokezane ofisi kubwa bila shida . .. . . Tutafika huko ila kuna kazi kubwa sana ya kufanyika
 
Kama hii ilikuwa kazi ya kitengo mi naiunga mkono. Kazi yao wanaijua,

Ifikie mahali watu au idara zijue kazi zake. Na magufuli mwenyewe akija pewa ikulu aje awe anafanya kazi kitaalamu. Na wengine pia chini yake hivo hvo - tusipotoka tutakuwa na gundu

Yule jamaa mwingine angechukua nchi angekuwa haambiliki wala hashikiki - kutwa kucha kujaribu kurudisha hela zake alizotumia kwenye kampeni na kuwakomesha wenzie. Na wa kuwakomesha ilikuwa wawe wengi. Tanzania isingekuwa salama tena kwa weng wao

We umeona wapi mtu anakomalia na kushupalia jimboni kwa mbunge mwenzie eti asichaguliwe muhula ujao? Hii ni laana. Na kwakuwa vitu hivi viko wazi vitakuwa vime mgharimu. Ni mtu wa vurugu, fitina. Sasa akiwa rais anaweza fanya nini?
 
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka huu John Maguli tayari amekuwa na ziara za kutembelea mikoa mbalimbali kabla na toka ateuliwe na CCM kuwa mgombea urais, kuna mambo kadhaa ambayo nimechunguza na kujiuliza kama kweli CCM ilifanya uamuzi sahihi kumteua Magufuli kuwa mgombea wake waburais.

Kwa mfano
1/Wakati wa uchukuaji fomu za kuomba kuteuliwa kugombea urais ndani ya CCM, Magufuli hakuonekana sana kama ni miongoni mwa watu wanaofaa kupeperusha bendera ya CCM, hakukuwa na mshtuko wala hamasa yoyote kutoka kwa wanaCCCM au wasio wanaCCM kuhusu ugombea wa Magufuli. Tofauti kabisa na wagombea wenzake kadhaa. Hakuna mwanasiasa asiyetaka kushangiliwa au kushabikiwa, na hatuamini kabisa kuwa Magufuli hakutaka kushangiliwa au kushabikiwa bali huenda ni mvuto duni wa kisiasa ndani ya CCM au vinginevyo.

2/Hata baada ya Magufuli kuteuliwa rasmi kuwa mgombea urais wa CCM na kufanya mikutano ya Hadhara mjini Dodoma, Dar, Zanzibar na Mwanza bado hatukuona mwangwi mzito wa mwitikio wa watu.
Kwa ujumla mikutano yote hiyo ilijaa makada wa CCM wakiwa na sare zao za kijani(wengi wao walikuwepo kwenye harakati za kumshabikia Lowassa wakati wakusaka wadhamini) wakiwa na sura zenye mashaka makubwa na tabasamu za kutengeneza. Wengi wetu tulitegemea makundi makubwa sana ya watu mbalimbali hususani wasiokuwa wanaCCM.

3/Mpaka sasa hatujaona kishindo cha mtikisiko wa kisiasa kwa upande wa upinzani katika kuhofia ujio wa Magufuli katika mbio za urais mwaka huu. Japokuwa UKAWA hawajatangaza rasmi mgombea wao lakini hatuoni Presha yoyote katika kuhofia nguvu za Magufuli kisiasa.

4/Mwitikio wa Makundi makubwa ya kijamii bado uko chini sana baada ya Magufuli kuteuliwa. Mpaka sasa wingu la kisiasa limegubikwa na kukatwa kwa jina la Lowassa tu, badala ya uteuzi wa Magufuli.
Kila mtu alishuhudia namna Lowassa alivyokuwa akitikisa kila mahali alipopita wakati tu, amechukua fomu kugombea urais.
Tukio la Lowassa kutangaza nia jijini Arusha lilikuwa ni tukio kubwa sana kiasi cha kusimamisha kabisa shughuli za watu katika Miji ya Arusha, Moshi na Manyara. Lakini huwezi amini Tukio la Magufuli kuteuliwa kugombea irais na CCM na kuja Dar na Mwanza halikushtua kitu chochote katika shughuli za watu za kila siku.

Hivi wewe haujapata soma kwenye biblia takatifu ile aya isemayo" jiwe walilolikataa waashi ndilo limekua jiwe kuu la pembeni". Unajua maana yake!
 
Kitengo hawakutaka JK awe rais 2005 lakini Mkapa baada ya kuona hawezi kuzima Moto wa JK wa 2005 hakukubaliana na kitengo.

JK baada ya kuingia madarakani 2005 aliwashiti kiaina kitengo ushauri wao mwingi aliupuuza, baada ya CCM kupitia kwenye mapito ya kujivua gamba kitengo wakamshauri JK amteue Kinana kuwa Katibu mkuu na Mangula kuwa makamu mwenyekiti , Kikwete alikubali alishindwa kuwakatalia baada ya kuona Chama kinakwenda mrama.

2015 kitengo hawakumtaka EL , Kikwete hakuwa na jinsi, kitengo walimpa taarifa ambayo hata ungekuwa wewe mleta Mada ndio JK ungelikata tu jina la EL.
 
Ni wakati gani Vetting inafanyika? Ni muhimu kiasi gani? Ni kwa maslahi gani na ya nini?

Wapiga kura kwa uwingi wao tunaongelea quantity, kitengo kwa uchache wao ni "Quality" based, now chagua mwenyewe unataka kiongozi wako apatikane vipi, kwa quality au quantity. Kwa kilichotokea katika kipindi cha miaka kumi iliyopita nadhani kitengo kimejifunza kazi yake na kutorudia kosa ambalo wananchi walikuwa just about kufanya! Am glad kitengo is getting back to basics!

Hakuna lolote, kitengo kilitaka kumuweka mwenzao, mjomba mbona vetting yao imeshindwa, na hiyo quality yao imeshindwa hata kwenye chama tu? Ni ujinga kufikiri usalama ndo wanatakiwa wachagulie watu rais. Obama alichaguliwa na CIA? nijibu wewe..! Toa pumba hapa
 
Na hakuna anaetaka kujadili hili
huu ni mwiko mkubwa demokrasia

Hakuna demokrasia kwa vi nchi kama hivi, wananchi hawako informed kina lowasa wanawanunua kwa sh elfu kumikumi unategemea waachiwe wafanye maamuzi magumu. Waacheni usalama wafanye kazi zao, hatuwezi kuyaachia nchi magenge ya kifamilia!
 
Hakuna demokrasia kwa vi nchi kama hivi, wananchi hawako informed kina lowasa wanawanunua kwa sh elfu kumikumi unategemea waachiwe wafanye maamuzi magumu. Waacheni usalama wafanye kazi zao, hatuwezi kuyaachia nchi magenge ya kifamilia!
​Nawe upo KITENGO eenh?
 
Km kuna pahala TISS walicheza kwa ufanisi na busara ni pale walipohakikisha jina la Lowasa linakatwa.Ingekuwa enzi zile,Edo angelikwisha pata ajali siku nyngi.Hyo iko pote duniani hata Us.Hata opp. Kunyimwa ushndı ni kazi ya TISS, to be fair hauwezi kukabidhi nchi kwa watu km Mbowe.TISS ndo inasaidia kuwajengea uwezo opp na baada ya muda nadhani watawapa nafasi wakishnda.Wanaimprove kila siku na watu wenye akili wanawajoin, tutafika.
We unafikiri edo ni mjinga kama wewe? Wewe unafikiri apson ambae ni mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa mstaafu alikuwa ana kazi gani? Watu wapo extra smart..
 
Je Kitengo kipo kikatiba?Kama jibu ni hapana mbona kina nguvu sana hadi Mzee Kingunge anakihofia?Labda Kitengo ni baadhi ya vyombo vya usalama wa Taifa ambavyo vipo very invisible but very powerful and untouchable.Mh Lowassa amekuwa Waziri Mkuu,na amekuwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama Bungeni,hivi hakujua nguvu ya kitengo kabla ya kutangaza nia?
Uchaguzi Mkuu ujao Ngazi ya raisi na wabunge hauna maana kwa wananchi ni kupoteza pesa za walipa kodi kwani kitengo kimeisha maliza kazi yake.
 
Nakubaliana na mtoa mada, Tanzania usalama wa taifa unahusika sana kupanga mbinu mkakati nyingi sana katika kuongoza nchi, lakini tunajua pia hata kusambaratisha upinzani wanahusika pia.

Na hii sio kwa Tanzania tu bali hata Marekani, tunajua kilichotokea kwa JF Kennedy na nduguye Andrew Kennedy, pia hapa bongo tunajua kilichomkuta Sokoine, kolimba, Gnl Imran Kumbe na wengineo.

Ninashuku hata Mwang'onda kwenye team Lowassa alikuwa pale kwa mkakati maalumu lakini sio kumsaidia Lowassa.

Tukirudi kwenye mchakato wa kumpata mgombea kwa ticket ya CCM, kwa kweli mchezo walioucheza hawa jamaa kumpata John Joseph Pombe Magufuli nawapa credit kubwa sana, maana laiti kama angechaguliwa Lowassa basi nchi ingewekwa rehani, na kama angechaguliwa Membe basi tungeshuhudia makundi, mpasuko, ukanda na visasi, unakumbuka wale maadui zake 11 aliyosema akishinda watakimbilia Kenya?!

Kumchagua Magufuli imekuja kama suprise na kwa kweli pamoja na mambo yote kwa record yake nzuri na ya kutukuka ya nyuma nivigumu sana kumchafua Magufuli, pili hana makundi wala ukanda kama Membe na Lowassa!

Hapa nawapa HEKO kitengo!
 
Je Kitengo kipo kikatiba?Kama jibu ni hapana mbona kina nguvu sana hadi Mzee Kingunge anakihofia?Labda Kitengo ni baadhi ya vyombo vya usalama wa Taifa ambavyo vipo very invisible but very powerful and untouchable.Mh Lowassa amekuwa Waziri Mkuu,na amekuwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama Bungeni,hivi hakujua nguvu ya kitengo kabla ya kutangaza nia?
Uchaguzi Mkuu ujao Ngazi ya raisi na wabunge hauna maana kwa wananchi ni kupoteza pesa za walipa kodi kwani kitengo kimeisha maliza kazi yake.

Yameanza leo??!!
Waliokuwa viongozi mbona hakuna aliyewahi kuhoji uteuzi wake??!!!
 
Badirisha title umenikera mambo ya ccm kuyahusisha na taifa/nchi mojakwamoja, we sema ccm inaendeshwa na KITENGO
 
Huu mzimu wa maneno ya mkosaji tu kwani palipo ushindan lazima mshindi apatikane sasa kama yule upendae mtu hajapitishwa hakuna haja haja ya kuanzisha maneno ya mbaazi kukosa maua na kuanza maneno mara ooh kitengo tuache maneno kama hayo nadhan ya dodoma yamekwisha kama watanzania tugange yajayo na pia kama mgombea wako hakushinda usizushe,kitengo hicho inamaana kijan yote ya wapiga kura dodoma ilikuwa kitengo,tuache utoto kama mgombea wako alikuwa mhimu sana awe kiranja wa nyumba yako,tusianzishe mambo ya uongo na ukweli ila nafurah watanzania wako macho sana maneno ya kichochez si tz bwana
 
Ndio maana mi naamini hii nchi haitapiga hatua kidemokrasia wala kiuchumi hadi nafasi za kiutendaji zitakapoachwa kuongozwa kisiasa...

Usalama wa taifa, polisi, jeshi, TAKUKURU, mahakama, watendaji wa bunge, wakuu wa mashirika na taasisi za umma nk ... wote wapo affiliated kwa chama kimoja cha siasa...

Ili hali hii iweze kuondoka ni lazima wananchi wawezeshwe kukidhoofisha chama hiki kwa kukipunguzia sauti kwenye vyombo vya maamuzi kuanzia chini kabisa kwenye ngazi za halmashauri za vijiji, za wilaya na bunge...

Well said!
Hapa tatizo ni mfumo huu ulioasisiwa na chama 1!.
Lkn watu hawaelewi
Ooh magufuli jembe sijui nn!
Hakuna jipya chini ya huu mfumo!!
 
Back
Top Bottom