Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Wewe ndo umeongea point kabisa.....watu hapa wanachangia kisiasa zaidi..,
Ikitokea UKAWA walete mgombea maslahi mfukoni, pia CCM watuleteee mwingne kuipeleka nchi shimoni ndo tuwaache tu kisa nini?
Kuna mambo wananchi hawawezi kuyasikia na ikitokea wakafaham juu ya hao wanaowashabikia wanaweza wakastajaabu na kupata stroke
Hii nchi bado changa sana hata huo upinzani inabidi ujengewe uwezo kuongoza nchi.....Mtauzwa hadi mayai yaliyo tumboni kwa ushabiki watanzania ....tulieni tujenge hii nchi yetu sote si ya kuendeleza kusini, Kaskazini, wala kanda yeyote ile..tunahitaji maendeleo na tuache propaganda tusizozijua kwa undani wake...hatuwezi kabidhi nchi kwa mtu kisa mahaba ya siasa



Wewe kweli ni mzalendo halisi, umeongea kizalendo sana bila kuweka ushabiki wowote ule, nimeipenda sana hii point yako, laiti kama watanzania wote tungewaza kama Wewe nchi hii ingekuwa mahali pazuri sana pakuishi, big up sana!
 
Je Kitengo kipo kikatiba?Kama jibu ni hapana mbona kina nguvu sana hadi Mzee Kingunge anakihofia?Labda Kitengo ni baadhi ya vyombo vya usalama wa Taifa ambavyo vipo very invisible but very powerful and untouchable.Mh Lowassa amekuwa Waziri Mkuu,na amekuwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama Bungeni,hivi hakujua nguvu ya kitengo kabla ya kutangaza nia?
Uchaguzi Mkuu ujao Ngazi ya raisi na wabunge hauna maana kwa wananchi ni kupoteza pesa za walipa kodi kwani kitengo kimeisha maliza kazi yake.
Top 5 ya awali ilikuwa na majina mengine lakini kitengo kikayabadili na kuwaingiza Membe na January wakiamini wangepenya kwenye wajumbe lakini wakadunda Membe wao akakatwa . Sasa wamejipanga kumpa uwaziri mkuu Membe kisha nape atakuwa waziri wa Utawala bora au mambo ya ndani . Kitengo wana uhakika magufuli ni Rais Hata Kama watanzania wote watapiga kura Kwa DP ya mtikila .
 
Wakuu, kwanza naomba nikiri kuwa 'kitengo' kipo! Kwa mara nyingine kimeshindwa kumpitisha rais (Membe) ila kama kinashindwa kufanya hivyo, system yote inayofuata huamuliwa na kitengo. Mathalan Membe anaenda kuwa waziri mkuu.
 
Kuna wapiga kura mil 20, ccm ina wanachama mil6 , ukawa wa jitahidi kuvuna wana chama at least wawe mil 8 kwa mwaka 2025, waende kwenye matawi chini huko , then watafute suppor ya kitengo , kitengo hakiwezi kumpa mbowe nchi au slaa. Tanzania sio uingereza au marekani , demokrasia yetu inavyoendeshwa ni kama urusi na China , hizo nchi zote vyama Vya upinzani havijawahi shika nchi , comrade kinana amekirudisha chama huko hadi kapeleka watu kwenye mafunzo China kwanini haendi uingereza hadi Balozi wa China kasimama jukwaa la ccm , kitengo kina nguvu sana ila kwa ugomvi wa membe na lowassa kumteua magufuli aisee Jamaa wamecheza

Ni kweli kabsa kuwa wajumbe wengi walimpigia kura Magufuli Kwa Nia ya kumwonyesha kuwa hawamtaki kabsa Membe ndiyo maana alikuwa wa mwisho Kati ya wale top 5 licha ya kuambatana na waganga wa kienyeji 100 toka mataifa mbalimbali lakini kitengo walidunda Kwa Membe sasa wanamwandalia cheo cha Uwaziri mkuu huku mwakyembe naye anautaka Kwa udi na uvumba Simjui kitengo watawezaje huo mtiti.
 
Wakuu, kwanza naomba nikiri kuwa 'kitengo' kipo! Kwa mara nyingine kimeshindwa kumpitisha rais (Membe) ila kama kinashindwa kufanya hivyo, system yote inayofuata huamuliwa na kitengo. Mathalan Membe anaenda kuwa waziri mkuu.

Na Nape atakuwa waziri wa Utawala bora ili wawakomeshe wafuasi wa Lowasa
 
Membe keshasema siasa basi na hagombei.Keshakubali kushindwa
 
You are naive if you think power is in the hands of the "people"

Decisions kubwa zote zinafanywa na kikundi cha watu wachache

Na hii sio kwa Tanzania tu ni dunia nzima.Russia wana wa kwao wanaitwa silovik

Marekani ni ruling class Anglozionists au unaweza ukawaita Neoconservatives(Neo-Cons)

China ni Communist Party.Katika historia ya mwanadamu hakuna kipindi power ilikuwa kweli kwa umma

Democracy ni illusion.Mfano mzuri ni Greece.Juzi Syriza Party iliitisha referendum kuchagua austerity measures wananchi wakakataa,kesho yake viongozi wao wakachagua the opposite
 
Na Nape atakuwa waziri wa Utawala bora ili wawakomeshe wafuasi wa Lowasa

Kazuga tu yupo bado hajastaafu siasa japo ana mapesa mengi ya Gafafi lakini bado anatamani kuiba zaidi
 
Wakuu, kwanza naomba nikiri kuwa 'kitengo' kipo! Kwa mara nyingine kimeshindwa kumpitisha rais (Membe) ila kama kinashindwa kufanya hivyo, system yote inayofuata huamuliwa na kitengo. Mathalan Membe anaenda kuwa waziri mkuu.

Nasikia wanamuweka LUKUVI...
 
Sasa why wasitumie nguvu yao kuwapa zaidi wananchi sauti?
why wasiwabane CCM waruhusu Tume ya Uchaguzi huru ili wananchi wawe na final say?
why wao wajipe 'mandate' ya kuwaamulia wananchi?
una uhakika gani wao hawana udini na ukabila kwenye maamuzi yao?
wao sio part yahiyo middleclass inayo waburuza wanyonge?

Wananchi wenyewe hawana maana, wakichangiwa pesa za wizi na ufisadi baaasss wamejisahau wanatoa nchi!
 
Mkuu safari ya matumaini ndo umekubali iishie njiani au?

Mkuu unanitega ee!

Sikuridhishwa kabisa na mchakato wa kumpata mgombea wa CCM.


Binafsi sikubali kabisa safari hii ikome ghafla hivi, ila tusubiri kidogo majibu yatapatikana hivi punde!

Cha kutumaini sina!
 
Mkuu unanitega ee!

Sikuridhishwa kabisa na mchakato wa kumpata mgombea wa CCM.


Binafsi sikubali kabisa safari hii ikome ghafla hivi, ila tusubiri kidogo majibu yatapatikana hivi punde!

Cha kutumaini sina!

Binafsi sikufurahishwa pia na mchakato ulivyokwenda though nilijua kitakachojiri....

Ila vyovyote itakavyokuwa... iwe leo au kesho... masika au kiangazi ipo siku CCM italipa hii gharama ya kupandikiza chuki za kikanda....
 
Kitengo hawakutaka JK awe rais 2005 lakini Mkapa baada ya kuona hawezi kuzima Moto wa JK wa 2005 hakukubaliana na kitengo.

JK baada ya kuingia madarakani 2005 aliwashiti kiaina kitengo ushauri wao mwingi aliupuuza, baada ya CCM kupitia kwenye mapito ya kujivua gamba kitengo wakamshauri JK amteue Kinana kuwa Katibu mkuu na Mangula kuwa makamu mwenyekiti , Kikwete alikubali alishindwa kuwakatalia baada ya kuona Chama kinakwenda mrama.

2015 kitengo hawakumtaka EL , Kikwete hakuwa na jinsi, kitengo walimpa taarifa ambayo hata ungekuwa wewe mleta Mada ndio JK ungelikata tu jina la EL.
Mkuu ni taarifa gani hiyo? Unajua kuna watu wengine hawakuwa wanampenda Lowassa, lakini hisia za kwamba kaonewa zinawafanya wawe upande wake... bora zingetajwa hizo taarifa. Binafsi japo siko kwa Lowassa, lakini ningependa haki... Kama ana mabaya si yawekwe wazi tu. Kwanini kulindana.
 
Kweli inaumiza sanaa rais ambaye ndie jimedari mkuu kupangiwa maamuzi na the so called kitengo..! Najaribu kufikiri tuu hilo dubwana kitengo ni zimwi gani hilo???..

Ni bora hata wangetupangia rais au viongozi wenye kuleta maendeleo kwa kasi, kukemea ufisadi, kuboresha huduma za afya, maji safi, nk na nk...sasa kitengo cha tz ni kuweka viongozi watakao wabeba mafisadi na wabadhilifu wa mali za uma si bora kisiwepo tuu....

lakini yote yanamwisho kama ulivyo koma utumwa ndivyo utakuwa mwisho wa kitengo watakapolia na kusaga menoo siku yaja...haijawahi kutokea ktk historia ya ccm kuanza kupingana wenyewe kwa wenyewe hadharani kama tulivyo ona kwa inchimbi na mzee kingunge hizo ni dalili za kufikia mwisho kwa the so called kitengo....
 
Binafsi sikufurahishwa pia na mchakato ulivyokwenda though nilijua kitakachojiri....

Ila vyovyote itakavyokuwa... iwe leo au kesho... masika au kiangazi ipo siku CCM italipa hii gharama ya kupandikiza chuki za kikanda....
Mkuu uko sahihi, kwa hili tuko pamoja!
 
Mkuu unanitega ee!

Sikuridhishwa kabisa na mchakato wa kumpata mgombea wa CCM.


Binafsi sikubali kabisa safari hii ikome ghafla hivi, ila tusubiri kidogo majibu yatapatikana hivi punde!

Cha kutumaini sina!
MUSSA ALLAN sikuwa napenda Lowassa awe mgombea Urais kupitia CCM hasa nilipojua makundi yaliyokuwa nyuma yake. Sijapenda namna alivyonyimwa haki kama wale wengine 33 pasipo kupewa maelezo. Lakini ninaamini anapaswa kutulia kwa sasa, ayaache yaliyopita. Si kila mtu atakuwa Rais... Alipofika panamtosha.
Yeye kama mlutheri anaweza akawa anaukumbuka wimbo huu, kwa mtu aliyekosa matumaini...



Cha kutumaini sina, Ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha, Dhambi zangu kuziosha,
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye Mwamba: ni salama
Ndiye Mwamba: ni salama


Njia yangu iwe ndefu, Yeye hunipa wokovu,
Mawimbi yakinipiga, Nguvu zake ndiyo nanga.
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye Mwamba: ni salama
Ndiye Mwamba: ni salama


Damu yake na sadaka, Nategemea daima,
Yote chini yakiisha, Mwokozi atanitosha.
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye Mwamba: ni salama
Ndiye Mwamba: ni salama


Nikiitwa hukumuni, Rohoni nina amani,
Nikivikwa haki yake, Sina hofu mbele zake.
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye Mwamba: ni salama
Ndiye Mwamba: ni salama
 
Back
Top Bottom