Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Na hakuna anaetaka kujadili hili
huu ni mwiko mkubwa demokrasia

Hili swala gumu...

Idara ya Usalama wa Taifa ina stake kubwa sana kwenye siasa. Kiuhalisia chombo hiki kinapaswa kuwa independent and doing a continuous job ya kulinda nchi regardless of the times.

Hebu tuchukue mfano wewe ungekuwa Mkurugenzi wa hii idara halafu ukaamua kuacha watu wafanye siasa watakavyo i.e wachague hata watu ambao unafahamu kuwa hawana maadili, huoni kama utakuwa ume-fail kwenye jukumu la msingi?

Mimi naamini tunawahitaji kwenye processes ndani ya vyama. Making sure kunakuwa na vetting ya kutosha, wanapaswa kufahamu kuliko sisi. Na ifanyike kwenye vyama vyote, kuwe na uadilifu wa kutoa wasiotufaa, ila baada ya hapo waachwe wakafanye siasa in a level playing field.

It's a difficult balancing act
 
ai
Hujaona connection ya Magufuli na Ngeleja na TISS ambayo
RaiaMwema waliisema?

Hakuna kitu hapo.Wanamsafisha Mukulu.Ngeleja ni mwizi tena kuliko hTa huyo Lowassa.Kitengo hicho kimeratibiwa ndani ya CCM kwa manufaa ya viongozi wachache.Huko ndani ya CCM kuna kitengo cha usalama lamini si TISS.Kaka siasa za Afrika ni majungu,uongo,mauaji yaani ushenzi wote uko huko.
 
TISS included!

Jamani siamini ila najua CCM wanakitengo cha usalama lakini hapa tukiwaincule Tiss tunawaonea.Hili limetengenezwa na ukoo w.kifalme ili kuisafisha wakatengeneza stori ya tiss.
 
Nasikitika kusikia usalama wa taifa 'kitengo' mlihusika kukatwa majina ya wagombea urais ccm.Tiini matakwa ya umma.

Unapokuwa na umma ambao akili zao zimejaa upofu kama wewe lazima wahusike tu. Maana hamumjui huyo mgombea nyie ndo maana mnaongea utumbo utumbo hapa.
 
Usalama wa Taifa au TISS kama wanavyoitwa ni moja ya majeshi ya nchi kama vile Polisi, JWTZ, Magereza au JKT. Watumishi wa majeshi haya kwa mujibu wa Katiba ya nchi hawapaswi kuwa wanachama wa vyama vya siasa. Lakini chini ya zuria ni wanachama. Hii nathibitishwa na mifano ya watumishi wengi wa majeshi haya kuteuliwa kushika nafasi za uongozi wa kisiasa kama Issa Machibya na J. Agustino Ramadhani kugombea kwa nafasi ya uraisi kupitia CCM.
Usalama wa taifa wana sub standards sana.
Wanaacha mambo muhimu ya nchi wanafanya siasa.
Hiko Kitengo kinatakiwa kijulikane ni kina nani hasa?
Wao ni kama nani watuamulie rais wa nchi?
 
The Boss Hata mimi nilishangazwa katika hiki kipindi cha demokrasia ya vyama vingi eti Usalama wa taifa wanaingia kwenye vikao vya ccm kumchambua mgombea atakayepeperusha bendera ya ccm.

Kama taifa bado kazi tunayo. Naamini mwaka huu 2015 wa uchaguzi, hautokuwa wa haki kama ulivyokuwa wa 2010
unauhakika na ulichoandika!? Au ni chuki na mihemuko ndo inakusumbua!?
 
You are naive if you think power is in the hands of the "people"

Decisions kubwa zote zinafanywa na kikundi cha watu wachache

Na hii sio kwa Tanzania tu ni dunia nzima.Russia wana wa kwao wanaitwa silovik

Marekani ni ruling class Anglozionists au unaweza ukawaita Neoconservatives(Neo-Cons)

China ni Communist Party
.Katika historia ya mwanadamu hakuna kipindi power ilikuwa kweli kwa umma

Democracy ni illusion.Mfano mzuri ni Greece.Juzi Syriza Party iliitisha referendum kuchagua austerity measures wananchi wakakataa,kesho yake viongozi wao wakachagua the opposite

Uko sahihi kiasi fulani. Lakini usichanganye nchi na mifumo. Mambo ya Urusi/China yana tofauti kubwa na yale ya Marekani/Ugiriki. Kote kuna hivyo vinavyoitwa vitengo lakini miundo, majukumu na mamlaka ni tofauti. Kwa Urusi na China kama hapa kwetu, vina mamlaka kamili (absolute powers). Hata kuhusu uamuzi wa matokeo ya kura katika chaguzi za kisiasa. Yaani vinaamua hesabu ya kura aliyopata kila mgombea na chama. Ndio maana hapa kwetu hicho kikundi kinahakikisha ni yule mgombea anayekubalika na wenyewe ndani ya CCM pekee ndiye anayeshinda u-rais na si vinginevyo.

Huko Marekani, Ulaya Magharibi (EU block) na kwingineko kwenye mlengo sawa wa kidemokrasia km Japan na Korea Kusini, hivyo vikundi havina mamlaka kiasi hicho. Vinaweza kuangusha baadhi ya wagombea wanaoonkena hatari kwa mustakabali mkubwa wa taifa lakini, hatimaye, ni hesabu halisi za kura zilizopigwa na wananchi ndizo huamua ni nani na chama kipi ndio mshindi kati ya wagombea waliopitishwa na tume (huru) ya uchaguzi. Tena hufanya hivyo kimkakati sana si wazi kama huku kwetu ambapo hawajali kazi zao kujulikana. Kwa wenzetu, utasikia tu habari ya "conspiracy theories" katika mambo kama hayo.

Ndio maana kwa wenzetu, kura katika uchaguzi bado zina maana sana kuonyesha kukubalika au la kwa vyama na wagombea wake. Wanaweza hata kuendesha "opinion polls" zinazoshawishi kuonyesha mwelekeo wa umaarufu wa vyama na wanasiasa wake katika mazingira mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi, kiusalama, n.k. Huku kwetu hatuna hizo zaidi ya kuangalia ni nani anakubalika zaidi na rais aliyeko madarakani (na familia yake), wafanya biashara wakubwa, kamati kuu ya chama, n.k. ili tuhitimishe uwezekano wake kufika popote kisiasa. Vyama vya upinzani ndio hatuvifikirii kabisa. Ni kama vile vyama hivyo, wafuasi na mashabiki wake vimebakia kuwa "jokers in the pack"!
 
Napenda substance iliyoko kwenye uzi wako,ila umetumia maneno makali mno.
Unapokuwa na umma ambao akili zao zimejaa upofu kama wewe lazima wahusike tu. Maana hamumjui huyo mgombea nyie ndo maana mnaongea utumbo utumbo hapa.
 
Mkuu sometimes inabidi. Sababu watu wanalalamika sana hawajui hata hatari wanazoepushwa nazo

Hujaelewa kitu kabisa
Mimi binafsi nimempinga Lowasa humu sana
hapa ishu si Lowassa..ishu hapa ni kikundi cha watu kuwa na nguvu ya kuchagulia watu Rais
tuseme Lowasa hafai,Je Mwandosya hafai? Mahiga hafai?Augustine Ramadhan hafai?Mwakyembe hafai?Sitta hafai?
Mwele hafai?Monica hafai? why wao hawakupita tano bora?kitengo kilitumia vigezo vipi?
 
Hujaelewa kitu kabisa
Mimi binafsi nimempinga Lowasa humu sana
hapa ishu si Lowassa..ishu hapa ni kikundi cha watu kuwa na nguvu ya kuchagulia watu Rais
tuseme Lowasa hafai,Je Mwandosya hafai? Mahiga hafai?Augustine Ramadhan hafai?Mwakyembe hafai?Sitta hafai?
Mwele hafai?Monica hafai? why wao hawakupita tano bora?kitengo kilitumia vigezo vipi?
Mkuu sijakuzungumzia wewe.
 
Mkuu, kwa wataalam wa saikolojia, mtu anapokuwa katika maruwe ruwe kuna nyakati husema yanayoonekana kama maruwe ruwe, ukweli ni kuwa anachosema ndicho alicho nacho moyoni.

Ni maruwe ruwe'delirium' ndiyo humusukama kusema bila kukusudia

Baada ya kufanikiwa kumtengeneza mfalme,mzee alijisahau au alijivika kofi ya ubaba wa Taifa.

Akawekeza sana , mwisho wa siku tunajua yaliyomkuta. Hapa namnukuu JK akisema 'naomba yaliyomkuta mzee X yasije yakanikuta''

Mzee alikuwa ndani ya 'Kitengo' tulichokuwa hatukijui hadi alipoapatwa na mkasa.

Hivi leo analalamikaje, ikiwa sisi wananchi wenye nchi hatukujua kitengo isipokuwa yeye na wana kitengo? Thanks to CCM

Kuhusu hoja zako

Kwanza, mzee anatueleza hatuna demokrasia. Hata hivyo, hatuwezi kukaa tukilalamika bila kufanya jambo.

Oktoba 25 tubadili mwenendo ili tuwape watu wa nje nafasi ya kutueleza kitengo kinafanyaje kazi

Pili, ninashangaa usalama wa taifa wanaingia katika kitengo cha CCM. Hapa napo pana jambo

Tatu, tume ya uchaguzi ni sehemu ya 'kitengo' nikupe mfano. CCM waliosema kura ya maoni ipo, tume ikashikilia msimamo huo.

CCM wakasema kura ya maoni ni pamoja na uchaguzi, tume ikashikilia msimamo.

CCM wakasema wameagiza BVR na kazi itamalizika kwa wakati, tume wakasema hayo.

Rais akarudia kule Washington kuwa kura ya maoni ipo pale pale, mwenyekiti wa tume akarudia maneno hayo hayo.

CCM wakasema wameshauri serikali iharishe kura yao ya maoni, tume wakasema nao wanaahirisha.

Yaani tume iliyopaswa kuongozwa kitaalumu, imekuwa inapokea maagizo ya ''kitengo''

Ndiyo maana tunasema, kama tutalalamika bila kuleta mabadiliko, 2020 tutakuwa hapa tunazungumzia hicho hicho

Tatu,kitengo kinaendeshwa na nani? Hapa mzee atusaidie maana hatukujua uwepo wa kitengo

Nne,Watu wangapi wanafanya maamuzi? Mzee anajua kitengo kimeundwaje na kina watu wangapi

Tano,maamuzi ya kitengo ni ya kitengo, na huwa ya kitaifa kupitia vyombo husika.
Kimoja ni hicho tulichoambiwa, kingine ni Bunge. Hivi watu hawajui mswada wa gesi na mafuta ni kazi ya kitengo?

Uliletwa haraka na serikali, ukapigwa mhuri haraka haraka na bunge ili watu waende kwenye kampeni, tumeondoa mafuta na gesi tupeni kura wazanzibar. Hili nalo linajibu hoja ya maamuzi kwa manufaa ya taifa

Sita,kuna fiada gani kushiriki uchaguzi? Tukikaa pembeni kitengo kinaimarika.

Tumekaa miaka 50 na kitengo, hatuwezi kuendelea kukaa mingine 50 tukisubiri kitengo kitatuhurumia.

Lazima lifanyike jambo, kazi hiyo ipo kwetu na si kwa kitengo. Oktoba 25 tukiendelea na ugonjwa wa kusahau, hewalaa!

Mwisho mzee wetu kasoma Urusi. Anajua vema falasafa za vanguard party na Polituburo.
Sina uhakika nani ameanzisha kitengo, ninachojua kitengo ni mfumo uliopo unaondeana na anachokieleza mzee



Ahsante kwa your insight
 
Mkuu umeisoma sheria ya 1996 inyoongoza shughuli. . . . ??!!!
Unajua mtu mzima unamshauri mtaa huu sio salama kupita usiku. . . . .Akipita badala ya kuacha vijana wamkabe unaweza andaa mazingira akamwagiwa maji ya ukoko tu kesho hapiti. . . . . .Ila pia anaweza amua pita huku kavaa rain coat kabisa. . . . .

Unawatetea sana KITENGO
kama vile unawajua au kuwaelewa sana
Au ndio 'utetezi wa wana Kitengo' ?ha haa
 
Asante The Boss kwa mada hii muhimu. Nimepitia michango ya wenzangu waliotangulia, ni kweli kuwa ni wakati muafaka sasa tujadili na kushiriki kutengeneza nchi na taifa letu na historia itatuhukumu hivyo.

1. Kwa CCM suala la Urais kwao halina mjadala ni LAZIMA awe wa kwao hata kama italigharimu Taifa hili uhai wake wote. Hiyo ni siri iliyo wazi kwa miaka mingi tu.

2. Je ni mara ngapi tumewahi kusikia au kuona "viongozi wakuu" kama Rais, Waziri Mkuu, Wabunge na Mawaziri wakisema/kulalamika au kuonyesha "laiti kama ingekuwa ni uwezo/mamlaka yangu basi ninge......." Mifano iko mingi; mfano kauli ya Waziri Mkuu Pinda kuwa "wakiwashughulikia mafisadi nchi itayumba..." Hii inaonyesha kuwa kuna "nguvu" nyuma yao hao wanaonekana kwa macho kuwa "wakuu"; ambayo wao wenyewe wanaiogopa na kutumikia hiyo "nguvu" kwa hiari au shuruti, kwa kujua au kutokujua.

3. Kauli ya Kingunge ni nzito na ya ajabu sana kwa kuzingatia historia, uhusiano na hadhi yake CCM.
Kwangu mimi kauli ile ina vitu vikubwa vine (tofauti na watu waliojitokeza kusema kuwa mzee yule alikuwa anaitishia CCM nyau).
a) Kitengo ni kitu halisi "real"
b) Kitengo, pamoja na kuwa ni halisi, lakini sio kinachofikiwa na wengi (not accessible to all except for a selected few)
c) Kitengo ni fumbo pana na refu (codeword and terible mystery)
d) Kitengo hakina mipaka (kinaweza kuanzia ndani ya CCM lakini hakiishi huko na kinyume chake)

4. Matunda yake yako wazi katika historia ya nchi yetu. Ujinga umeendelea kutusumbua, umaskin umeendelea kuongozeka, maradhi, madawa ya kulevya, rushwa na ufisadi vimeongezeka kila siku na sasa vinatishia mustakabali wa nchi nzima.

5. Ugumu wa fumbo ni pale (kwa mujibu wa Kingunge) Kitengo ndio "kilipika/kilitengeneza" kashfa ya Richmond ili kumtoa Lowassa kutoka kuwa WM (hatujui hasa kwanini), lakini kwa jinsi kilivyo cha ajabu, nusura kiiangushe kabisa Serikali ya Kikwete mwaka 2006! Inaonesha kitengo kiko nje/juu ya mamlaka ya Mkulu. Ni kama vile duara (cycle) huoni mwisho na mwanzo ni mgumu pia kuuona!

HITIMISHO (kwa sasa)
i. TISS, Idara ya Ulinzi/Usalama/Ujasusi wa Chama, Ikulu, Bunge ni sehemu ya Kitengo lakini Kitengo sio Umma (Wananchi wa Tanzania.
ii. Kitengo kipo kiuhalisia ingawa hakipo kwa mujibu wa Katiba yetu ya JMT.

Fumbo bado linataka tuendele mbele zaidi kuchunguza, kudadisi na kuwa wajasiri zaidi ili tusimezwe na "Kitengo"


cc OLESAIDIMU Nyani Ngabu ....
naona jamaa kauliza very hard questions
 
Last edited by a moderator:
Kwa hali ilivyo ni bora iwe hivyo kwa muda. . . . . . " kuna mambo labda hayahitaji mjadala na labda kuna mambo yakiwekwa wazi kabisa itahitajika nguvu kubwa zaid kutuliza jamii" hizi ni aasumptions ambazo zinaweza sababisha nchi kuelekezwa nini cha kufanya . . . . .

Naamini ni kwa faida ya wengi na ya muda mrefu. . .

asante.
 
kama kitengo anachokisema kingunge ni kile kilichomng'oa jicho na kucha kibanda na ulimboka,basi kinajulikana.Kingunge alistaafishwa au kastaafu kwa hiari kitengoni?maana tukizungumzia unyama wa kitengo,kingunge alibobea humo!!!!now that they have turned on each other,dirty lingeries are washed in public now....the pirates' ship is sinking.
 
Hawajijui nafasi yao
badala ya kuwa 'loyal subject to the Republic'
wao nao ni loyal subjects to CCM......so shameful

The Boss,

Huoni kwamba kwa wao kupendekeza taarifa za kukatwa kwa Lowassa walikuwa loyal subject to the Republic?. Umewahi kujiuliza nini kingetokea endapo wangeruhusu Lowassa apitishwe?

Ndiyo 2005 walishindwa kutimiza wajibu wao, lakini mwaka huu wameweza. Isitoshe wao wako better placed kujua nyendo za ndani kabisa za wagombea wote.

By the way, hivi kwani vyama vingine wamezuiwa kutumia huduma za "kitengo" kupata taarifa sahihi za wagombea wao? Au ni muendelezo wa malalamio ya watanzania kama ilivyozoeleka?
 
Back
Top Bottom