Na hakuna anaetaka kujadili hili
huu ni mwiko mkubwa demokrasia
ai
Hujaona connection ya Magufuli na Ngeleja na TISS ambayo
RaiaMwema waliisema?
TISS included!
TISS included!
Yaani hao huwezi kuwaacha nje ya huo mchezo!!!
Nasikitika kusikia usalama wa taifa 'kitengo' mlihusika kukatwa majina ya wagombea urais ccm.Tiini matakwa ya umma.
Mkuu safari ya matumaini ndo umekubali iishie njiani au?
Usalama wa taifa wana sub standards sana.
Wanaacha mambo muhimu ya nchi wanafanya siasa.
Hiko Kitengo kinatakiwa kijulikane ni kina nani hasa?
Wao ni kama nani watuamulie rais wa nchi?
unauhakika na ulichoandika!? Au ni chuki na mihemuko ndo inakusumbua!?The Boss Hata mimi nilishangazwa katika hiki kipindi cha demokrasia ya vyama vingi eti Usalama wa taifa wanaingia kwenye vikao vya ccm kumchambua mgombea atakayepeperusha bendera ya ccm.
Kama taifa bado kazi tunayo. Naamini mwaka huu 2015 wa uchaguzi, hautokuwa wa haki kama ulivyokuwa wa 2010
You are naive if you think power is in the hands of the "people"
Decisions kubwa zote zinafanywa na kikundi cha watu wachache
Na hii sio kwa Tanzania tu ni dunia nzima.Russia wana wa kwao wanaitwa silovik
Marekani ni ruling class Anglozionists au unaweza ukawaita Neoconservatives(Neo-Cons)
China ni Communist Party.Katika historia ya mwanadamu hakuna kipindi power ilikuwa kweli kwa umma
Democracy ni illusion.Mfano mzuri ni Greece.Juzi Syriza Party iliitisha referendum kuchagua austerity measures wananchi wakakataa,kesho yake viongozi wao wakachagua the opposite
Unapokuwa na umma ambao akili zao zimejaa upofu kama wewe lazima wahusike tu. Maana hamumjui huyo mgombea nyie ndo maana mnaongea utumbo utumbo hapa.
Napenda substance iliyoko kwenye uzi wako,ila umetumia maneno makali mno.
Mkuu sometimes inabidi. Sababu watu wanalalamika sana hawajui hata hatari wanazoepushwa nazo
Mkuu sijakuzungumzia wewe.Hujaelewa kitu kabisa
Mimi binafsi nimempinga Lowasa humu sana
hapa ishu si Lowassa..ishu hapa ni kikundi cha watu kuwa na nguvu ya kuchagulia watu Rais
tuseme Lowasa hafai,Je Mwandosya hafai? Mahiga hafai?Augustine Ramadhan hafai?Mwakyembe hafai?Sitta hafai?
Mwele hafai?Monica hafai? why wao hawakupita tano bora?kitengo kilitumia vigezo vipi?
Mkuu, kwa wataalam wa saikolojia, mtu anapokuwa katika maruwe ruwe kuna nyakati husema yanayoonekana kama maruwe ruwe, ukweli ni kuwa anachosema ndicho alicho nacho moyoni.
Ni maruwe ruwe'delirium' ndiyo humusukama kusema bila kukusudia
Baada ya kufanikiwa kumtengeneza mfalme,mzee alijisahau au alijivika kofi ya ubaba wa Taifa.
Akawekeza sana , mwisho wa siku tunajua yaliyomkuta. Hapa namnukuu JK akisema 'naomba yaliyomkuta mzee X yasije yakanikuta''
Mzee alikuwa ndani ya 'Kitengo' tulichokuwa hatukijui hadi alipoapatwa na mkasa.
Hivi leo analalamikaje, ikiwa sisi wananchi wenye nchi hatukujua kitengo isipokuwa yeye na wana kitengo? Thanks to CCM
Kuhusu hoja zako
Kwanza, mzee anatueleza hatuna demokrasia. Hata hivyo, hatuwezi kukaa tukilalamika bila kufanya jambo.
Oktoba 25 tubadili mwenendo ili tuwape watu wa nje nafasi ya kutueleza kitengo kinafanyaje kazi
Pili, ninashangaa usalama wa taifa wanaingia katika kitengo cha CCM. Hapa napo pana jambo
Tatu, tume ya uchaguzi ni sehemu ya 'kitengo' nikupe mfano. CCM waliosema kura ya maoni ipo, tume ikashikilia msimamo huo.
CCM wakasema kura ya maoni ni pamoja na uchaguzi, tume ikashikilia msimamo.
CCM wakasema wameagiza BVR na kazi itamalizika kwa wakati, tume wakasema hayo.
Rais akarudia kule Washington kuwa kura ya maoni ipo pale pale, mwenyekiti wa tume akarudia maneno hayo hayo.
CCM wakasema wameshauri serikali iharishe kura yao ya maoni, tume wakasema nao wanaahirisha.
Yaani tume iliyopaswa kuongozwa kitaalumu, imekuwa inapokea maagizo ya ''kitengo''
Ndiyo maana tunasema, kama tutalalamika bila kuleta mabadiliko, 2020 tutakuwa hapa tunazungumzia hicho hicho
Tatu,kitengo kinaendeshwa na nani? Hapa mzee atusaidie maana hatukujua uwepo wa kitengo
Nne,Watu wangapi wanafanya maamuzi? Mzee anajua kitengo kimeundwaje na kina watu wangapi
Tano,maamuzi ya kitengo ni ya kitengo, na huwa ya kitaifa kupitia vyombo husika.
Kimoja ni hicho tulichoambiwa, kingine ni Bunge. Hivi watu hawajui mswada wa gesi na mafuta ni kazi ya kitengo?
Uliletwa haraka na serikali, ukapigwa mhuri haraka haraka na bunge ili watu waende kwenye kampeni, tumeondoa mafuta na gesi tupeni kura wazanzibar. Hili nalo linajibu hoja ya maamuzi kwa manufaa ya taifa
Sita,kuna fiada gani kushiriki uchaguzi? Tukikaa pembeni kitengo kinaimarika.
Tumekaa miaka 50 na kitengo, hatuwezi kuendelea kukaa mingine 50 tukisubiri kitengo kitatuhurumia.
Lazima lifanyike jambo, kazi hiyo ipo kwetu na si kwa kitengo. Oktoba 25 tukiendelea na ugonjwa wa kusahau, hewalaa!
Mwisho mzee wetu kasoma Urusi. Anajua vema falasafa za vanguard party na Polituburo.
Sina uhakika nani ameanzisha kitengo, ninachojua kitengo ni mfumo uliopo unaondeana na anachokieleza mzee
Mkuu umeisoma sheria ya 1996 inyoongoza shughuli. . . . ??!!!
Unajua mtu mzima unamshauri mtaa huu sio salama kupita usiku. . . . .Akipita badala ya kuacha vijana wamkabe unaweza andaa mazingira akamwagiwa maji ya ukoko tu kesho hapiti. . . . . .Ila pia anaweza amua pita huku kavaa rain coat kabisa. . . . .
Asante The Boss kwa mada hii muhimu. Nimepitia michango ya wenzangu waliotangulia, ni kweli kuwa ni wakati muafaka sasa tujadili na kushiriki kutengeneza nchi na taifa letu na historia itatuhukumu hivyo.
1. Kwa CCM suala la Urais kwao halina mjadala ni LAZIMA awe wa kwao hata kama italigharimu Taifa hili uhai wake wote. Hiyo ni siri iliyo wazi kwa miaka mingi tu.
2. Je ni mara ngapi tumewahi kusikia au kuona "viongozi wakuu" kama Rais, Waziri Mkuu, Wabunge na Mawaziri wakisema/kulalamika au kuonyesha "laiti kama ingekuwa ni uwezo/mamlaka yangu basi ninge......." Mifano iko mingi; mfano kauli ya Waziri Mkuu Pinda kuwa "wakiwashughulikia mafisadi nchi itayumba..." Hii inaonyesha kuwa kuna "nguvu" nyuma yao hao wanaonekana kwa macho kuwa "wakuu"; ambayo wao wenyewe wanaiogopa na kutumikia hiyo "nguvu" kwa hiari au shuruti, kwa kujua au kutokujua.
3. Kauli ya Kingunge ni nzito na ya ajabu sana kwa kuzingatia historia, uhusiano na hadhi yake CCM.
Kwangu mimi kauli ile ina vitu vikubwa vine (tofauti na watu waliojitokeza kusema kuwa mzee yule alikuwa anaitishia CCM nyau).
a) Kitengo ni kitu halisi "real"
b) Kitengo, pamoja na kuwa ni halisi, lakini sio kinachofikiwa na wengi (not accessible to all except for a selected few)
c) Kitengo ni fumbo pana na refu (codeword and terible mystery)
d) Kitengo hakina mipaka (kinaweza kuanzia ndani ya CCM lakini hakiishi huko na kinyume chake)
4. Matunda yake yako wazi katika historia ya nchi yetu. Ujinga umeendelea kutusumbua, umaskin umeendelea kuongozeka, maradhi, madawa ya kulevya, rushwa na ufisadi vimeongezeka kila siku na sasa vinatishia mustakabali wa nchi nzima.
5. Ugumu wa fumbo ni pale (kwa mujibu wa Kingunge) Kitengo ndio "kilipika/kilitengeneza" kashfa ya Richmond ili kumtoa Lowassa kutoka kuwa WM (hatujui hasa kwanini), lakini kwa jinsi kilivyo cha ajabu, nusura kiiangushe kabisa Serikali ya Kikwete mwaka 2006! Inaonesha kitengo kiko nje/juu ya mamlaka ya Mkulu. Ni kama vile duara (cycle) huoni mwisho na mwanzo ni mgumu pia kuuona!
HITIMISHO (kwa sasa)
i. TISS, Idara ya Ulinzi/Usalama/Ujasusi wa Chama, Ikulu, Bunge ni sehemu ya Kitengo lakini Kitengo sio Umma (Wananchi wa Tanzania.
ii. Kitengo kipo kiuhalisia ingawa hakipo kwa mujibu wa Katiba yetu ya JMT.
Fumbo bado linataka tuendele mbele zaidi kuchunguza, kudadisi na kuwa wajasiri zaidi ili tusimezwe na "Kitengo"
Kwa hali ilivyo ni bora iwe hivyo kwa muda. . . . . . " kuna mambo labda hayahitaji mjadala na labda kuna mambo yakiwekwa wazi kabisa itahitajika nguvu kubwa zaid kutuliza jamii" hizi ni aasumptions ambazo zinaweza sababisha nchi kuelekezwa nini cha kufanya . . . . .
Naamini ni kwa faida ya wengi na ya muda mrefu. . .
Hawajijui nafasi yao
badala ya kuwa 'loyal subject to the Republic'
wao nao ni loyal subjects to CCM......so shameful