Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

Nchi inaendeshwa na 'KITENGO'?

mkuu nchi sio begi ukampa kila mtu , kitengo ndio kinaendesha nchi siku zote , ukawa sijui chadema ni maigizo tu na kujipa moyo , kwa kuwa so far kitengo kinataka ccm iendelee kuwepo basi kitengo kimemchagua yule inaonekana atauzika kirahisi na kuhakikisha nchi ipo salama kwa miaka 10 ijayo , kusema ule ukweli kabisa profile za wagombea urais kitengo lazima wapiti na ripoti yao ni muhimu kwenye maamuzi , wakisema mgombea anakufa miaka 4 ijayo ana cancer je ? au mgombea anapata ufadhili toka kwa magaidi .sio tatizo hawa watu wa kitengo kupitia majina tatizo linakuja tu pale viongozi wa ccm wanapotumia vibaya kitengo .
 
mkuu nchi sio begi ukampa kila mtu , kitengo ndio kinaendesha nchi siku zote , ukawa sijui chadema ni maigizo tu na kujipa moyo , kwa kuwa so far kitengo kinataka ccm iendelee kuwepo basi kitengo kimemchagua yule inaonekana atauzika kirahisi na kuhakikisha nchi ipo salama kwa miaka 10 ijayo , kusema ule ukweli kabisa profile za wagombea urais kitengo lazima wapiti na ripoti yao ni muhimu kwenye maamuzi , wakisema mgombea anakufa miaka 4 ijayo ana cancer je ? au mgombea anapata ufadhili toka kwa magaidi .sio tatizo hawa watu wa kitengo kupitia majina tatizo linakuja tu pale viongozi wa ccm wanapotumia vibaya kitengo .


Zambia marais wamekufa tu zaidi ya mmoja nchi iko salama bado
Kuhusu kupokea pesa za nje,hata Kikwete alipewa pesa za nje kwa uchaguzi na wanajua
Kama hakuna demokrasia basi tufute tu vyama tujue moja
 
Nami nimejiuliza sana, hicho KITENGO ni nini na ni kina NANI wamo ndani yake?
Hivi hiki KITENGO ndio kinataka maamuzi yao (wachache) yahesabike kama maamuzi yanayojumuisha na wale walioko nje ya KITENGO (waliotengwa) kwa makusudi japo walistahili kuwa ndani sehemu ya mfumo rasmi kabla ya KITENGO kujitwalia mamlaka..?!

Je inawezekana ile thamthilia ya nchi ya kusadikika inaelekea kuwa uhalisia Tz...?!! Naendelea kujiuliza tu!!

Ni kweli Kitengo (system) imefanya makosa mengi sana,kilishindwa kuzuia kifo cha Sokoine,kilishindwa kumshauri Mkapa kuhusu uuzaji na ubinafsishaji wa viwanda na mashirika ya umma kwa wawekezaji wa kigeni,kilishindwa kudhibiti matendo ya ufisadi serikalini,kilishindwa kudhibiti biashara ya unga na ya nyara za taifa na pia kilishindwa kulidhibiti genge la akina Kikwete na Lowassa kuingia madarakani mwaka 2005.Lakini mwaka huu 2015 walau wamejitahidi kuwadhibiti akina Lowassa wasiingie ikulu,tungejuta.
 
Kwanza kitengo anachozungumzia mzee kingunge si usalama wa taifa bali kitengo cha watu sita wa kumpa mgombea wao nafasi,kilfanyakazi usiku na mchana na kamati ya maadili
 
mkuu nchi sio begi ukampa kila mtu , kitengo ndio kinaendesha nchi siku zote , ukawa sijui chadema ni maigizo tu na kujipa moyo , kwa kuwa so far kitengo kinataka ccm iendelee kuwepo basi kitengo kimemchagua yule inaonekana atauzika kirahisi na kuhakikisha nchi ipo salama kwa miaka 10 ijayo , kusema ule ukweli kabisa profile za wagombea urais kitengo lazima wapiti na ripoti yao ni muhimu kwenye maamuzi , wakisema mgombea anakufa miaka 4 ijayo ana cancer je ? au mgombea anapata ufadhili toka kwa magaidi .sio tatizo hawa watu wa kitengo kupitia majina tatizo linakuja tu pale viongozi wa ccm wanapotumia vibaya kitengo .

This we call it playing politics kwenye maisha yetu, poor you. Usalama waachwe wafanyekazi zao, si kitengo cha kutafuta wagombea wa ccm. mambo ya siasa wawaachie wenyewe ccm na vyama vingine. we foot their bills not ccm
 
Zambia marais wamekufa tu zaidi ya mmoja nchi iko salama bado
Kuhusu kupokea pesa za nje,hata Kikwete alipewa pesa za nje kwa uchaguzi na wanajua
Kama hakuna demokrasia basi tufute tu vyama tujue moja

Sidhani kama kuna umuhimu wa kuwa na vyama vingi wakati uchaguzi wenyewe sio wa haki. hata uandikishaji wenyewe pia unadosari
 
Kwanza kitengo anachozungumzia mzee kingunge si usalama wa taifa bali kitengo cha watu sita wa kumpa mgombea wao nafasi,kilfanyakazi usiku na mchana na kamati ya maadili

Soma vizuri usalama wa Taifa walimuagiza Ngeleja amfanyie kampeni Magufuli kwa wajumbe wa Zanzibar
 
Ni wakati gani Vetting inafanyika? Ni muhimu kiasi gani? Ni kwa maslahi gani na ya nini?

Wapiga kura kwa uwingi wao tunaongelea quantity, kitengo kwa uchache wao ni "Quality" based, now chagua mwenyewe unataka kiongozi wako apatikane vipi, kwa quality au quantity. Kwa kilichotokea katika kipindi cha miaka kumi iliyopita nadhani kitengo kimejifunza kazi yake na kutorudia kosa ambalo wananchi walikuwa just about kufanya! Am glad kitengo is getting back to basics!
 
3.Ni kweli maamuzi yao yote ni kwa faidaya Taifa?

Ah wapi! Ukibahatika kutembelea sehemu mbalimbali za nchi ndo utagundua kwamba maamuzi 'yao' mengi wala si kwa manufaa ya taifa.

Sina uhakika sana na hili la kiinua mgongo cha wabunge na sijalisikia tena tokea karibu wiki mbili zilizopita lakini kama kweli hicho kitengo dhima yake kuu ni kulinda maslahi ya taifa basi kingeingilia kati ili hayo mabilioni ambayo yanadaiwa wabunge watalipwa yaende sehemu ambazo zina uhitaji mkubwa zaidi.

4.Wananchi wakipishana maamuzi na 'kitengo' maamuzi ya wananchi yataheshimiwa?

Thubutu! Watanzania wa kizazi hiki hawana ujasiri wala uthubutu wa kupishana na maamuzi ya 'kitengo'. Majuzi tu hapa tumeona jinsi ambavyo rafu imechezwa hadi Magufuli akawa railroaded kuwa mteule wa chama na yule ambaye iliaminika ndiye aliyekuwa chaguo la wengi kutoselewa mbali tena kwa udhalilishaji wa hali ya juu. Walipojitokeza watu wawili watatu kujaribu kupinga kilichotokea walizimwa haraka sana na wakarudishwa mstarini.

5.Nguvu ya 'kitengo' kwa tume ya uchaguzi ni halali?

Sisi hatuna tume huru ya uchaguzi. Hiyo ambayo tunayo sasa ni extension ya 'kitengo' tu. Hebu tumia tu hata busara zako za kawaida [common sense]. Ni nani ambaye huiunda hiyo tume? Mwenyekiti wa hiyo tume na hao wenzake huwa wanapatikanaje?

6.kuna faida ya kushiriki uchaguzi huku 'kitengo' kimeshafanya maamuzi?

Kwa ujumla mimi sioni faida yoyote ile hususan kwenye urais. Kwa jinsi ambavyo mambo yalivyo hivi sasa CCM kuja kushindwa na wapinzani haiwezekani hata kidogo. Kutegemea mwenyekiti wa tume ya uchaguzi aliyeteuliwa na rais/ mwenyekiti wa CCM kumtangaza mshindi wa kiti cha urais mgombea wa upinzani ni sawa na kutegemea ngamia apite kwenye tundu la sindano.

Kama kuna anayedhani hiyo tume ya uchaguzi siyo extension ya kitengo namsihi arudi kumwangalia mmoja wa watangaza nia wa CCM - Jaji Agustino Ramadhani. Huyu bwana nadhani alikuwa ni makamu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi kuanzia mwaka 1993 hadi 2002 na kuanzia 2002 hadi 2007 alikuwa makamu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar [eti hawa watu nao wana tume yao ya uchaguzi!!].

Hiyo inatueleza nini kuhusu hiyo inayoitwa tume ya uchaguzi? Je, ina maana tume nzima imejaa makada wa CCM? Mimi nadhani ni hivyo.

7.Je tuna demokrasia kweli au tunaruka ruka ttu na maigizo?

Ni maigizo tu. Demokrasia gani hiyo isiyotoa fursa sawa kwa washindani wote? Hata katiba ya nchi inayoendana na misingi mikuu ya kidemokrasia hatuna. Eti juzi juzi tu hapa ndo tumestuka na kuona umuhimu wa kuandika katiba mpya.

Kwa nini hilo halikufanyika hapo awali kabisa mwaka 1992 tulipoingia kwenye siasa za vyama vingi?

Na kusema ukweli Tanzania wala hatuna siasa za vyama vingi. Siasa zetu ni za chama kimoja ila kuna mazingaombwe yanayofanya watu wadhani kwamba tuna siasa za vyama vingi. Hatuna.

Wiki ilopita tumeshuhudia jinsi ambavyo nadhari karibu ya Watanzania wote ilivyoelekezwa huko Dodoma katika shauku ya kutaka kujua rais ajaye atakuwa nani.

Hakuna ubishi wowote ule kuwa rais wa 5 wa Tanzania ni John Magufuli.

Hata kupatikana kwake hakukuwa kwa demokrasia. Kinachosubiriwa sasa ni kukamilishwa tu kwa taratibu [igizo la uchaguzi mkuu hapo Oktoba] na yeye kuapishwa, basi.
 
mkuu mi nimesema kinachoendelea tu Tanzania sio marekani wala uingereza , hapa tumezungukwa na watu wanapigana kila siku sisi tuna Amani ni vizuri tukawapa pongezi hawa jamaa wa vyombo vya usalama pamoja na mapungufu yao , naamini kingunge alikuwa anaongelea wale wazee wa kamati ya ushauri na wale wa kamati ya maadili sidhani kama alimaanisha vyombo vya usalama , jiulize tu mgombea wa ccm alikuwa jaji mkuu pia makamu wa tume ya uchaguzi ...utajuaje kama huyu wa sasa sio ? demokrasia bado sana sisi hata huko upinzani kuna watu wao ambao mimi na wewe hatuwezi jua ,cha maana ukawa wakaze sana buti kwenye bunge , kupata wabunge wengi ,
 
Sasa why wasitumie nguvu yao kuwapa zaidi wananchi sauti?
why wasiwabane CCM waruhusu Tume ya Uchaguzi huru ili wananchi wawe na final say?
why wao wajipe 'mandate' ya kuwaamulia wananchi?
una uhakika gani wao hawana udini na ukabila kwenye maamuzi yao?
wao sio part yahiyo middleclass inayo waburuza wanyonge?

1. Labda hiyo sauti itapatikana kwa kuweka mtu anayesikiliza wananchi. . .
2. Labda waliyemuweka kama kweli kawekwa ndio mwenyekiti na rais sasa huoni tume itakaa sawa na final say itatoka kwa majority. . .
3. Udini na ukabila kila mtu anao cha maana tu visiingilie malengo mahususi na ya jumla katika mipango na utekelezaji. . .
4. Wao kama ni elites na middle class inayoamua on behalf, for a common good basi waendelee. . .mandate akipewa dikteta mzalendo ni bora kuliko democratic bourgeoisie. . . .
 
The Boss

Mkuu hii nchi inaongozwa na 'Kitengo', ndio maana rais anaweza kuwa nje apendavyo, hata batizo ama dedications za watoto wa marais wengine hakosi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kweli nchi inaongozwa na ' Kitengo ' ndio maana rais anaweza kuwa nje apendavyo, hata batizo ama dedications za watoto wa marais wengine hakosi.
 
Nyani Ngabu ume nail tu ....

Watu huwa nawaambia Uchaguzi mkuu ni ule wa Dodoma
October ni maigizo tu hawaelewi
cha kushangaza wapinzani nao wanashiriki haya maigizo vizuri saana
halafu watakuja kulalamika later..wanashangaza
 
Last edited by a moderator:
The Boss kwanza hongera kwa kuja kivingine.Pili ninachofikiri "KITENGO" si usalama wa Taifa.Kuna watu wachache ambao sidhani kama wanazidi hata kumi ndani ya CCM yenyewe ndiyo iliyofanya uamuzi wa nani awe sababu za kibinafsi kabisa.Hata Makufuli amepata bahati ya mtende baada ya PANZI KUANZA VITA.Kwa hiyo yawezekana usalama wa Taifa ukasingiziwa tu ili kukidhi haja ya wachache.

Tujiulize haya maswali:

1.Hivi kama ni TISS hawa wafuatao ni wachafu kiasi kwamba walishindwa kuingia kwenye mchujo?Judge Tqmadhani,Pinda,Ghalib Bilali,Chikawe,uadilifu wao ukazidiwa hata na January Makamba asiyejua chochote kuhusu CCM?Kwa kujiuliza hivi kwa uhakika kabisa ninapata majibu kwamba TISS wanasingiziwa tu.

Akili za kuambiwa changanya na za kwako..Kitengo si TISS ni wachache wNaojua bei ya Makufuli...
 
Kitengo ndani ya CCM ni muungano wa Kamati ya Maadili na Usalama ya CCM na Baraza la Usalama la Taifa!

Baraza la Usalama la Taifa lina nguvu kisheria ya kupata ushauri wowote kutoka kwenye vyombo vya ulinzi wa Taifa.
 
Back
Top Bottom