Hii ni dalili ya watu waliokuwa wamedeka katika mfumo wa utawala wa kifisadi... kama ulikuwa unanyongewa kila siku sasa unaambiwa chinja... hujui kisu kinashikwa vipi.. Jiji la Dar lina matatizo yake na hayaishi leo.. mojawapo ni kuwa watu wake wamezoea uchafu kiasi kwamba kuishi bila uchafu kunaonekana ni kama kuwa "mzungu" au kuwa majuu!
Yaani wananchi wa kipato cha chini walie na hali ngumu ya maisha halafu wewe useme walikuwa wanadeka?
Sijawahi kuona ukitoa kauli insensitive kama hii!.
Hali ngumu ya Maisha mtaani ni result ya sera za uchumi zilizofeli na uendeshaji wa mambo vibaya wa mheshimiwa na si kudeka kwa watu!.
1. Kutokuongeza mishahara na nyongeza za kila mwaka ambazo ni stahiki za wafanyakazi kwa mujibu wa sheria
2. Kumismanage ishu ya korosho, kawatia umasikini wakulima
3. Kutokulipa wafanyabiashara kwa huduma zao walizotoa kwa serikali/taasisi zake
4. Kuhamisha serikali Dodoma bila kujipanga, matokeo yake makusanyo dar yameshuka na Dodoma haijajipanga kuweza kuaaccomodate hospitality business kwa hiyo overall makusanyo kushindwa kufikia malengo
5. Sera zake alipoingia tu mara ya kwanza ziliiyumbisha bandari naona sasa ndo wanakumbuka kuondoa tozo mbalimbali kwa mizigo ya congo, wacongo walishatuhama , wakagamia mombasa
6. Sera zake za kuminya uhuru na demokrasia matokeo yake wahisani kuacha kutoa hela
7. Kutumia pesa bila kuwa na malengo yaliyofanyiwa tafiti vya kutosha, ukijisikia mradi huu unapeleka hela bila hata kufanya money for value analysis ya kutosha, kuipitisha bungeni na kupata mawazo na kuwa allocated budget, matokeo yake baadhi ya miradi kama ndege imepeleka nje mihela yetu mingi tu ya kigeni
Sasa katika hali kama hiyo utamlaumu vipi raia anayeshindia karanga za mia mbili kutwa kuwa alikuwa anadeka?
Acha dharau mkuu, unaweza kuitetea serikali ya CCM kwa mambo mengine lakini siyo at the expense ya well being ya watu!