Nchi imekauka, mambo hayaendi...

Nchi imekauka, mambo hayaendi...

1550515232797.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa ni kiboko alisemaga lakini tusitupe suruali za zamani baadaye zitatutosha leo nimevaa suruali niliofanya date ya kwanza kwa mke wangu pale Blue palm kwa nyerere.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa Dar unayoizungumzia:
1) Barabara ambazo hazikuwa gazipitiki zinafanyiwa ukarabati
2) Shule za Serikali ambazo kawaida ya watoto kusongamana, kukaa chini, walimu kufanyia kazi chini ya miti au chumba kimoja, hali inabadilika.
3) Hospitali, Vituo vya Afya, na Zahanati ambako kila aina ya uovu usiolingana na usafi wa afya ulionekana, mambo siyo hivyo tena.

Kwa Tanzania bakuri lilokuwa linatalembezwa kuomba misaada, sasa limesafishwa na kufungiwa kabatini.

AU unaishi nchi gani ambayo umetembelea mitaa hiyo?


Sent using Jamii Forums mobile app
hivi unaijua DAR vizuri???

ulishatembelea shule zote uone watoto wanavyokaa chini?? walimu je?? mmeajiri lini baada ya kutumbua??

kule mahospitalin wajawzito wanapoambiwa wakajinunulie vifaa na bado wanalala 3 kitanda kimoja hujaona??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani wananchi wa kipato cha chini walie na hali ngumu ya maisha halafu wewe useme walikuwa wanadeka?
Sijawahi kuona ukitoa kauli insensitive kama hii!.



Acha dharau mkuu, unaweza kuitetea serikali ya CCM kwa mambo mengine lakini siyo at the expense ya well being ya watu!

Hivi mtu maskini unamnyang'anya nini hadi alie? Maskini anakosa nini? maskini anachotamani ni kwenda juu.. watu wa chini wanalalamika nini wakati walikuwa tayari chini; wao matumaini yao ni kwenda juu. Angalia maelfu ya vijana walioajiriwa kwenye miradi mbalimbali ya ujenzi... watu ambao walikuwa hawajui wataishi vipi leo wanaweza kufanya kamradi kao kakalipa..na hapa ndio watu wanakosea.. wanafikiria kulalamika "maisha magumu" kunatosha kubadilisha tu serikali.. watu wakiona mahitaji yao mbalimbali yanaanza kutimizwa wataona tofauti...

Hakuna maisha magumu ambayo watu wanalalamika sasa hivi ambayo yameanza juzi tu; uwe mwangalifu kudhania kuwa watu wote Tanzania hasa walio wengi wanaonalalamika na kuwa kwao maisha yamekuwa magumu zaidi sasa hivi kuliko wakati wa JK. Hili si kweli...
 
hivi unaijua DAR vizuri???

ulishatembelea shule zote uone watoto wanavyokaa chini?? walimu je?? mmeajiri lini baada ya kutumbua??

kule mahospitalin wajawzito wanapoambiwa wakajinunulie vifaa na bado wanalala 3 kitanda kimoja hujaona??

Sent using Jamii Forums mobile app

Hapa sasa ndio unatakiwa useme na kutoa ushahidi wa hili ili watu washughulikie... usilalamike pembeni. Hospitali gani wa kina mama Dar wanalala watatu watatu kitanda kimoja.. embu tutajie ili kina Ndungulile wapate taarifa hapa hapa...
 
Mzee Mwanakijiji; with due respect to you. Ninaelewa mtu kama stroke au jingalao kuandika ulichokiandika. You may have changed your views -for that you commanded respect and admiration- rightly and I dare say deservedly.

But I never thought you would stoop so low that you would insult so many Tanzanians that way! Kuna mkulima gani (na tunaambiwa 70% ya Watanzania ni small-hold farmers) aliezoea vya kunyonga? Ina maana workforce yote kabisa nchi hii (waalimu, field agronomists, manesi na lower cadres wote) walikuwa "wapiga dili". Am sorry Sir, but I thought you were more intelligent than that!!

Inawezekana kabisa hukujua ni kwa kiasi gani ufisadi ulikuwa unaendesha uchumi; hivi mnafikiri tulikuwa tunapinga ufisadi ili ili kila mtu aishi tu kwa raha.. au mlidhani ukiushambulia ufisadi nini kitatokea. Tanzania haijafika mahali bado kabisa pa kuweza kuwa pepo ya wengi... ufisadi uliharibu siyo tu watu wa serikali; uliathiri hadi wakulima na watoto ambao hawajazaliwa bado. Madhara ya ufisadi yalikuwa ni mapana mno na hata sasa bado hazijachukuliwa hatua zote sahihi na stahiki kusahihisha mfumo wetu. Kwamba hali ni ngumu ili lilitarajiwa.
 
Hivi mtu maskini unamnyang'anya nini hadi alie? Maskini anakosa nini? maskini anachotamani ni kwenda juu.. watu wa chini wanalalamika nini wakati walikuwa tayari chini; wao matumaini yao ni kwenda juu. Angalia maelfu ya vijana walioajiriwa kwenye miradi mbalimbali ya ujenzi... watu ambao walikuwa hawajui wataishi vipi leo wanaweza kufanya kamradi kao kakalipa..na hapa ndio watu wanakosea.. wanafikiria kulalamika "maisha magumu" kunatosha kubadilisha tu serikali.. watu wakiona mahitaji yao mbalimbali yanaanza kutimizwa wataona tofauti...

Hakuna maisha magumu ambayo watu wanalalamika sasa hivi ambayo yameanza juzi tu; uwe mwangalifu kudhania kuwa watu wote Tanzania hasa walio wengi wanaonalalamika na kuwa kwao maisha yamekuwa magumu zaidi sasa hivi kuliko wakati wa JK. Hili si kweli...

Kwa mujibu wa takwimu, zaidi ya Watanzania milioni mbili wameingia katika umasikini wa kutupwa tangu mwaka 2015-2018 (Kwa mujibu wa kauli ya mbunge Zitto Kabwe bungeni, serikali haikukanusha)

Wakati wa J.K uchumi ulikuwa unakuwa kwa wastani wa 7% sasa hivi tunaambiwa ni 6 point something percent, hiyo reduction japo ni ya points kadhaa inawakilisha nini interms of kipato cha watu?

Kipindi cha JK kulikuwa na watu masikini, lakini kipindi cha huyu mheshimiwa Umasikini wao umezidi zaidi, na wale waliokuwa na nafuu kipindi cha JK sasa wengi wao wamegeuka masikini.

Biashara zinakufa kwa kasi ya kutisha!
 
Hivi mtu maskini unamnyang'anya nini hadi alie? Maskini anakosa nini? maskini anachotamani ni kwenda juu.. watu wa chini wanalalamika nini wakati walikuwa tayari chini; wao matumaini yao ni kwenda juu. Angalia maelfu ya vijana walioajiriwa kwenye miradi mbalimbali ya ujenzi... watu ambao walikuwa hawajui wataishi vipi leo wanaweza kufanya kamradi kao kakalipa..na hapa ndio watu wanakosea.. wanafikiria kulalamika "maisha magumu" kunatosha kubadilisha tu serikali.. watu wakiona mahitaji yao mbalimbali yanaanza kutimizwa wataona tofauti...

Hakuna maisha magumu ambayo watu wanalalamika sasa hivi ambayo yameanza juzi tu; uwe mwangalifu kudhania kuwa watu wote Tanzania hasa walio wengi wanaonalalamika na kuwa kwao maisha yamekuwa magumu zaidi sasa hivi kuliko wakati wa JK. Hili si kweli...
Wanaoibeza Serikali iliyoko madarakani hawana hoja dhabiti ni kulalamika tu. Isitoshe hawatoi sera/mikakati mbadala ya maendeleo au kukuza uchumi. Wanaamini mchawi wa matatizo yao ni Rais Magufuli badala ya kuchambua kwa kina ubora na udhaifu wa Ilani ya CCM ya Uchaguzi, 2015 na kwa kiwango gani imetekelezwa na Serikali yake.

Upinzani ungetanabahi kuwa katika kipindi hiki kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu, 2020, CCM inatathmini kiwango cha utekelezaji wa Ilani yake, nao wangejipanga ipasavyo kutathmini kiwango cha kutimiza ahadi zao katika majimbo na halmashauri wanazongoza. Badala yake wanahangaika kuikosoa Serikali kwa maneno ya ulalamishi, kebehi na matusi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom