Wizara ya Mazingira fanyeni kazi yenu sawa sawa nchi inageuka Jalala kwa kasi

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,504
51,099
Nimetembelea jiji la Dar es salaam, kwa kweli hali niliyokutana nayo inasikitisha sana. Mpaka ikabidi nijiulize hii wizara inayohusika na mazingira iko wapi na inafanya nini?

1. Mifuko ya Plastic mitaani imekuwa mingi sana.
Miaka michache iliyopita wakati wa Utawala wa Hayati Magufuli serikali ilijaribu kupunguza kiwango cha mifuko ya plastic nchini, kwa kweli hilo lilisaidia sana. Lakini hivi sasa mifuko ya plastic imerudi tena, na inazagaa mitaani.
Kuna mifuko ya aina fulani ya plastic inauzwa kati ya sh 300 na 500, iliyoletwa kureplace mifuko ya nailoni nayo imekuwa kero sana. Imezagaa tele mitaani.
Aina nyingine za mifuko ya plastic niliyoiona ni mifuko ya sabuni ya unga, vifungashio mbalimbali

2. Chupa za Plastic zimekuwa nyingi sana.
Sasa hivi kuna chupa za energy drinks, Vikombe vya plastic vya juice, chupa za plastic za soda, hizi zimezagaa mitaani kama njugu. Kwa kweli kila mtaa unaopita hivi sasa unakuta chupa za namna hiyo zimezagaa

3. Foil za chakula za takeaway
Hili nalo ni tatizo kubwa mno. Siku hizi mtu akiagiza chakula anafungiwa kwenye take away au foil. Hizi taka nazo ni ngumu sana kuoza. Leo hii ukizunguuka mitaani, kumejazana hizi foil

4. Chupa za pombe
Leo hii wauza pombe zikiwemo pubs hawajisumbui kutafuta mahali sahihi pa kutupa chupa zao baada ya wateja kunywa pombe. miongoni mwa chupa hizo ni zile za Wine, Pombe kali kama vile K-Vant na nyinginezo. Matokeo yake wanavizia usiku wanaenda kutupa katika mitaa ya jirani

4. Uchomaji taka usio salama kwa afya wakithiri.
Leo hii ukipita katika mitaa, kwa sababu ya accumulation ya taka, basi raia wanajichomea taka kila mtu kadri anavyotaka. Lakini kitendo hicho ni hatari sana,baadhi ya taka kama vile plastic na foils zinatoa kemikali ambazo ni hatari sana kwa mapafu na inaweza kupelekea magonjwa ya kutopumua vizuri au kansa. Japo kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za serikali za mitaa,lakini serikali insonekana imelala, watu wanachoma taka na kuhatarisha afya ya jamii kwa kiwango cha kutisha sana.

5. Upikaji chakula usiozingatia afya ya walaji.
Leo hii ukizunguuka mitaani kuna staili ya mapishi ambayo ni hatari sana kwa afya. Mama lishe wanapika wali huku wakiufunikia manailoni. Wao wanaamini wakifanya hivyo ndo unaiva haraka.Lakini athari ya hayo ni makemikali ya plastic baasa ya kupata joto kuvujia ktk chakula na kupelekea maradhi mengi ikiwemo kansa. Sasa hivi nchini kuna ongezeko kubwa la ugonjwa wa kansa, huenda miongoni mwa sababu ni lifestyle ya namna hii.

Huu ni wakati wa serikali kuamka. Nchi kwa kasi sana inageuka jalala. Waziri wa Mazingira uko wapi, timiza wajibu wako!
 
Tatizo la kansa kwa kiasi kikubwa linasababishwa na mambo 2 yafuatayo:-
(a) utumiaji mbaya (poor handling) wa kemikali wakati wa uchenjuaji au usafishaji wa madini pamoja na shughuli za shamba.

(b) utumiaji mbaya wa madawa. Hapa watanzania wengi wanajinunulia dawa na kuyatumia bila ya kupima kwanza.

Wengine hawajui kutafsiri maana ya "kutwa mara tatu". Wanadhani wanatakiwa kuwa wamemeza vidonge mara tatu kabla ya jua kuzama.

Huko famasi pia siyo waaminifu, wanauza dawa zilizopitwa na muda.

Utunzaji wa dawa ni tatizo kwa wananchi walio wengi pia.

Hitimisho: Mlundikano wa taka kavu ktk mazingira na ulaji mbovu wa Vyakula unachangia kwa kiasi kidogo sana tatzo la kansa ukimlinganisha na hayo mawili.
 
Hii ni dalili mojawapo ya utawala uli-collapse. Mambo yanafanywa kizimamoto. Kuna njia kadhaa zinazoweza kutumika kupunguza tatizo:

1. Wauzaji wa vinywaji kwenye chupa kulazimishwa ku-recycle chupa, kwa kuongeza bei ya kinywaji, na baada ya matumizi kuwe na sehemu za kununua chupa. Hili litafanya chupa ziwe ''mali'' inayoingiza fedha na watu hawatathubutu tena kuzitupa hovyo. Na hata zikitupwa hovyo waokotaji watakuwa wengi ili kwenda kuuza.

2. Mitaa yote, iwe na vibanda vya kutupa taka. Kila kibanda kiwe na ma-container kama manne au matano ya kuweka taka, hivyo magari ya kusomba taka yawe yanapita kwenye kila kibanda kuzoa. Kila mkazi awe na wajibu wa kutoa taka zake ndani na kupeka kwenye kibanda ambako gari litakuwa linapita mara tatu kwa wiki kuzoa.
 
Mtoa mada umeeleweka sana.

Serikali iweke sheria kali..

Kuhusu energy drinks, zile chupa zao waokota makopo wahazitaki, hivyo jukumu iwe kwa makampuni yazalishayo hizo bidhaa, yaweke wakusanyaji...
Chupa nyeupe zinaokotwa sana.

Karatasi, bado serikali yetu haijaweka msisitizo, yatakiwa isiruhusu mifuko ya aina yoyote ambayo ni poly au plastic

Kuhusu mapishi, wateja ni wengi hivyo ni swala la walaji kuamua kuhusu afya zao
 
Hiyo ni attitude ya watu, sio serikali.
Serikali kuu ikusimamie hadi utupaji wa taka?

Watu wa mtaa husika kama mnajielewa mnajiwekea utaratibu na kuhakikisha unafuatwa tu, sio Waziri

Hiyo wizara ina staff wangapi hadi waje kusimamia kila mtaa!
 
Nilivyosikia jalala basi nikamumbuka maneno haya:

“Mimi Ni Nani?Nimezaliwa Katika Kijiji Cha Vumbi ,Nimeishi Maisha Ya Ufukara Sikutegemea Nitakuwa Hapa Ila Wewe Na Mungu Wako Anajua Kwanini Umenitoa Kwenye Jalala Na Kunifikisha Hapa"
 
Tatizo la kansa kwa kiasi kikubwa linasababishwa na mambo 2 yafuatayo:-
(a) utumiaji mbaya (poor handling) wa kemikali wakati wa uchenjuaji au usafishaji wa madini pamoja na shughuli za shamba.

(b) utumiaji mbaya wa madawa. Hapa watanzania wengi wanajinunulia dawa na kuyatumia bila ya kupima kwanza.

Wengine hawajui kutafsiri maana ya "kutwa mara tatu". Wanadhani wanatakiwa kuwa wamemeza vidonge mara tatu kabla ya jua kuzama.

Huko famasi pia siyo waaminifu, wanauza dawa zilizopitwa na muda.

Utunzaji wa dawa ni tatizo kwa wananchi walio wengi pia.

Hitimisho: Mlundikano wa taka kavu ktk mazingira na ulaji mbovu wa Vyakula unachangia kwa kiasi kidogo sana tatzo la kansa ukimlinganisha na hayo mawili.
Hujafanya reserach yoyote hivyo maoni yako ni kama nadharia isiyothibitishwa. Tatizo la kansa ni jambo pana linalohitaji utaalam kabla ya kuanza kutoa conclusion. Vyanzo viko vingi sana na vingine mpaka sasa hivi havijulikani.
 
Hiyo ni attitude ya watu, sio serikali.
Serikali kuu ikusimamie hadi utupaji wa taka?

Watu wa mtaa husika kama mnajielewa mnajiwekea utaratibu na kuhakikisha unafuatwa tu, sio Waziri

Hiyo wizara ina staff wangapi hadi waje kusimamia kila mtaa!
Nadhani suala kubwa hapa ni elimu kwa wananchi na kuhakikisha kuna mifumo imara ya ukusanyaji taka
 
Hii habari si ya kweli, ni batili.
Chupa ya plastic dar es salaam ukiitupa mahali pa wazi haivuki dk ,60 inaokotwa.
Kwa hoja yako namba 2 Uzi wako umekuwa batili.
Kuhusu mifuko ya plastic Kafanye tena utafiti
 
Nadhani suala kubwa hapa ni elimu kwa wananchi na kuhakikisha kuna mifumo imara ya ukusanyaji taka
Watu wanajua kuwa utupaji hovyo wa taka haufai ila wanatupa,

Na mifumo ya ukusanyaji wa taka pia ipo, kama imelegea ni wananchi na serikali ya mtaa husika
Mfano unaamka asubuhi unakuta mtu kamwaga furushi la pampasi na matakataka mengine barabarani, sasa hapa utamlaumu waziri?
 
Hili ni janga kubwa sana karibia nchi nzima...nipo huku mwanza hali ni mbaya sana

Wananchi wanatupa taka ovyo kwa matarajio eti wafanya usafi watakuja ziondoa.sometimes umepanda daladala mtu anakunywa juisi halafu chupa anairusha barabarani, kwa hali kawaida ungetegemea aiache ndani ya gari ili wakiwa wanafanya usafi waiweke sehemu inapostahili.

Nadhamu kikubwa cha kuzingatiwa ni elimu , elimu , elimu wananchi wapewe elimu ya umuhimu wa kuweka mazingira yao safi iwe ni kampeni ya kudumu kabisa kupitia radio na television na hta simu yaani kila mwananchi atumiwe hta meseji tatu kwenye simu kwa siku khs umuhimu wa usafi

Na mwisho kabisa serikali iweke miundo mbinu mizuri kwa ajili ya ukusanyaji taka yaani kila nyumba iwe na dustbin na kuwepo na utaratibu wa gari kupitia uchafu mara kwa mara.

Na baada ya kufanya hayo yote serikali itengeneze kikosi kazi cha askari wa mazingira hawa kazi kuu itakuwa ni kukamata wachafuzi wa mazingira na kuwapeleka kwenye mkono wa sheria

Na nashauri kuwepo na adhabu kali ya wachafuzi wa mazingira ikibidi iwe faini kuanzia milioni 1 au kifungo cha jela miezi 3

Serikali ikifanya haya yote nadhani suala la uchafuzi wa mazingira litakuwa history.
 
Hii habari si ya kweli, ni batili.
Chupa ya plastic dar es salaam ukiitupa mahali pa wazi haivuki dk ,60 inaokotwa.
Kwa hoja yako namba 2 Uzi wako umekuwa batili.
Kuhusu mifuko ya plastic Kafanye tena utafiti
Chupa za maji ndo zinaokotwa na waokota chupa. Ila za energy drinks hawana mpango nazo!
 
Tatizo la kansa kwa kiasi kikubwa linasababishwa na mambo 2 yafuatayo:-
(a) utumiaji mbaya (poor handling) wa kemikali wakati wa uchenjuaji au usafishaji wa madini pamoja na shughuli za shamba.

(b) utumiaji mbaya wa madawa. Hapa watanzania wengi wanajinunulia dawa na kuyatumia bila ya kupima kwanza.

Wengine hawajui kutafsiri maana ya "kutwa mara tatu". Wanadhani wanatakiwa kuwa wamemeza vidonge mara tatu kabla ya jua kuzama.

Huko famasi pia siyo waaminifu, wanauza dawa zilizopitwa na muda.

Utunzaji wa dawa ni tatizo kwa wananchi walio wengi pia.

Hitimisho: Mlundikano wa taka kavu ktk mazingira na ulaji mbovu wa Vyakula unachangia kwa kiasi kidogo sana tatzo la kansa ukimlinganisha na hayo mawili.
100% upo sahh mkuu
 
Nimetembelea jiji la Dar es salaam, kwa kweli hali niliyokutana nayo inasikitisha sana. Mpaka ikabidi nijiulize hii wizara inayohusika na mazingira iko wapi na inafanya nini?

1. Mifuko ya Plastic mitaani zimekuwa nyingi sana.
Miaka michache iliyopita wakati wa Utawala wa Hayati Magufuli serikali ilijaribu kupunguza kiwango cha mifuko ya plastic nchini, kwa kweli hilo lilisaidia sana. Lakini hivi sasa mifuko ya plastic imerudi tena, na inazagaa mitaani.
Kuna mifuko ya aina fulani ya plastic inauzwa kati ya sh 300 na 500, iliyoletwa kureplace mifuko ya nailoni nayo imekuwa kero sana. Imezagaa tele mitaani.
Aina nyingine za mifuko ya plastic niliyoiona ni mifuko ya sabuni ya unga, vifungashio mbalimbali

2. Chupa za Plastic zimekuwa nyingi sana.
Sasa hivi kuna chupa za energy drinks, Vikombe vya plastic vya juice, chupa za plastic za soda, hizi zimezagaa mitaani kama njugu. Kwa kweli kila mtaa unaopita hivi sasa unakuta chupa za namna hiyo zimezagaa

3. Foil za chakula za takeaway
Hili nalo ni tatizo kubwa mno. Siku hizi mtu akiagiza chakula anafungiwa kwenye take away au foil. Hizi taka nazo ni ngumu sana kuoza. Leo hii ukizunguuka mitaani, kumejazana hizi foil

4. Chupa za pombe
Leo hii wauza pombe zikiwemo pubs hawajisumbui kutafuta mahali sahihi pa kutupa chupa zao baada ya wateja kunywa pombe. miongoni mwa chupa hizo ni zile za Wine, Pombe kali kama vile K-Vant na nyinginezo. Matokeo yake wanavizia usiku wanaenda kutupa katika mitaa ya jirani

4. Uchomaji taka usio salama kwa afya wakithiri.
Leo hii ukipita katika mitaa, kwa sababu ya accumulation ya taka, basi raia wanajichomea taka kila mtu kadri anavyotaka. Lakini kitendo hicho ni hatari sana,baadhi ya taka kama vile plastic na foils zinatoa kemikali ambazo ni hatari sana kwa mapafu na inaweza kupelekea magonjwa ya kutopumua vizuri au kansa. Japo kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za serikali za mitaa,lakini serikali insonekana imelala, watu wanachoma taka na kuhatarisha afya ya jamii kwa kiwango cha kutisha sana.

5. Upikaji chakula usiozingatia afya ya walaji.
Leo hii ukizunguuka mitaani kuna staili ya mapishi ambayo ni hatari sana kwa afya. Mama lishe wanapika wali huku wakiufunikia manailoni. Wao wanaamini wakifanya hivyo ndo unaiva haraka.Lakini athari ya hayo ni makemikali ya plastic baasa ya kupata joto kuvujia ktk chakula na kupelekea maradhi mengi ikiwemo kansa. Sasa hivi nchini kuna ongezeko kubwa la ugonjwa wa kansa, huenda miongoni mwa sababu ni lifestyle ya namna hii.

Huu ni wakati wa serikali kuamka. Nchi kwa kasi sana inageuka jalala. Waziri wa Mazingira uko wapi, timiza wajibu wako!
Umesahau na haya mapampazi sijui,wanayovishwa watoto, yanaharibu mazingira Sana,

Huu uzi watavamia misukule ya dikteta watakuambia angekuwepo yasingetokea
 
Back
Top Bottom