Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,850
- 62,291
- Thread starter
- #161
Inawezekana kabisa hukujua ni kwa kiasi gani ufisadi ulikuwa unaendesha uchumi; hivi mnafikiri tulikuwa tunapinga ufisadi ili ili kila mtu aishi tu kwa raha.. au mlidhani ukiushambulia ufisadi nini kitatokea. Tanzania haijafika mahali bado kabisa pa kuweza kuwa pepo ya wengi... ufisadi uliharibu siyo tu watu wa serikali; uliathiri hadi wakulima na watoto ambao hawajazaliwa bado. Madhara ya ufisadi yalikuwa ni mapana mno na hata sasa bado hazijachukuliwa hatua zote sahihi na stahiki kusahihisha mfumo wetu. Kwamba hali ni ngumu ili lilitarajiwa.
Kama ufisadi ulikuwa mkubwa kiasi hicho hao mafisadi waliopigwa vita wapo katika magereza gani na walihukumiwa katika hukumu zipi?
Mimi ninachokiona ni kuwa kuna rhetoric tu majukwaani ya kupiga vita ufisadi lakini sioni mafisadi hao kukamatwa na kuhukumiwa vifungo!
Alitwambia kuwa kwenye CCM kuna mafisadi lakini sijamuona mwanaCCM yeyote mzito kufikishwa mahakamani.
Tumeshuhudia ufisadi katika chaguzi za marudio na kununua wapinzani, serikali ya chama kinachonunuanunua wapinzani kwa vihela hivi kinatumiatumia hakiwezi kuwa serious kwenye kupambana na ufisadi.
Au labda wewe mwenzetu kuna Tanzania yako iliyoko ndotoni unaiota, lakini Tanzania ya leo, kupambana na ufisadi ni kibwagizo tu cha kisiasa lakini hakuna genuine fight, ingekuwepo basi kishindo kingekuwepo badala ya maneno matupu.
Tungepambana na ufisadi, Rostam angeenda Ikulu kunywa chai?
Chenge angekuwa mwenyekiti wa bunge?
Karamagi angekuwa uraiani?
Waliobeba hela kwenye Sandarusi wangekuwa wapo huru uraiani wanakula bata?
Acha utani wewe!

