Nawaunga Mkono Madaktari

Nawaunga Mkono Madaktari

Watanzania tuandamane kuwaunga mkono madaktari, peke yao hawawezi, kwa sababu jamaa ni viziwi hat hawaambiliki, wao wanatibiwa Appolo- India, tunaoumia ni sisi wananchi walala hoi. Tuwasaidie madaktari kugoma, tutakaokufa ni sisi.

Pinda mwehu tu ameacha kuwaita madaktari anaita waandishi wa habari kwani wao ndiyo wamegoma, angeenda TBC na kutangaza kuomba kukutana au kutoa wito wa kukutana na madaktari, au atembelee muhimbili awone si wapo kwenye kikao?? Huyu mtoto wa mkulima ameshiba sasa.
 
Napenda kusikia PM atakavyoshughulikia swala la mojawapo "kupeleka viongozi nje kutibiwa" maana inasababisha sekta hii ya afya vitendea kazi kuonekana sio kipao mbele. Wanaosimamia na kuatibu sera wote wanatibiwa nje hata kama ni babu wana access na rufaa za pale wizarani kwend India.
Wanatibiwa nje machine za kutoa vipimo ziinaharibika mwezi hamna mwenye uchungu maana hamna anayetibiwa hapa. Eti mara X ray mashine ni mbovu mwezi hospitalifulani, mara machine fulani kifaa hamna mwezi..

Hili swala naungana na madaktari kabisa.
viongozi wanafanya check up sijui mara ngapi kwa mwaka nje ya nchi. Kwa nini kusiwe na mipango ya kuleta hizo machine kwenye hospitali zete ili kuondoa mzigo kwa serikali?

Naunga mkono kwa sababu hii maana watakuwa na uchungu na hospitali zetu.


Ukitaka kujua kwenda nje ni dili angalia pale muhimbili wanapasua moyo lakini bado wanapeleka wagonjwa nje na serikali inapitisha, hii ni DILI za watu.

inauma sana.
 
tatizo ni fumuko wa bei na ugumu wa maisha. Apa serikali itafute namna then mambo ya nyongeza za mishahara yatakuwa yametatulika.
 
Mimi siwaungi mkono kwani wanavunja sheria hata Kama ni mbovu. Pili hawana umoja wako disunited kinoma. Hakika mgomo wao sio planned technically kwa hiyo kuna kila dalili ya kudhoofika. Pinda jana amekaa na wahariri kaongea utumbo na wao wakaandika.

Pinda is the most hopeless prime minister tangu tupate Uhuru wa bendera ambao CCM wameutumia kudumaza maendeleo. The PM has always been a government boy all his life. To him GVT first kwani amekuwepo Ikulu awamu zote just saying yes. Inachefua akijua fika hao madokta hawana umoja anasema yuko tayari kukutana na wawakilishi wao anytime.

Doctors ni wasomi wanapasa kuwa na plan za kugoma and if hawatasikilizwa then what next. Sijaona agenda ya msingi for sure it definately going to crack sooner or later.
 
Mwanakijiji, SIUNGI MKONO hoja yoyote inayolenga kumpa kuongeza kipato kwa sekta moja na nyingine kuwa hoi. Kama ambavyo siungi mkono wabunge kuongeza posho zao NAPINGA DAKTARI KUOMBA aongezwe mshahara.

Hoja zangu ni kwamba hakuna fani iliyobora zaidi ya mwingine, daktari ni muhimu sana, lakini anajua vifaa anavyotumia zinatengezwa na wahandishi (aibu kwamba ni wa nje ya TZ), anajua anatumia mifumo mbalimbali ya kompyuta kufanya uchunguzi, anajua yeye amekuwa dakatari kwa hiari lakini vile vile wote tusingeza kuwa madaktari ndo maana tukagawana kwa hiari hizi fani, lengo ni kuhakikisha tunasaidiana kwa pamoja kujenga nchi na watu wake. KIPATO ni kidogo ama kwa ajili ya wizi wa Serikali na Wazungu au kwa maana tu ya kidogo hivyo ni vema kama Serikali inapandisha mishahara itumie formula fulani kupandisha kwa Watumishi wote.

SIKUBALI SEKTA MOJA KUWA BORA KULIKO NYINGINE NAAMINI KATIKA MGAWANYO WA KAZI, hivyo maslahi yakaribiane kwa sekta zote, hasa kwa ukweli kwamba soko na mfumko wa bei ni moja tu kwetu sote
 
Siungi mkono madaktari kugoma kwanza hawana uzalendo hasa wa muhimbili. Huwa hawawatendei haki wagonjwa wa hali ya chini. Mtu ukiwa wa hali ya chini ukaenda muhimbili utashangaa make unaweza ishia kupata ugonjwa wa frustration hasa ukilazwa.
 
Kuna daktari mmoja alikuwa anahojiwa na kituo kimojapo cha Redio, akasema kuwa wao walianza kugoma siku nyingi kushinikiza kupewa stahili zao na kuboreshwa kwa mazingira ya utabibu nchini hususan katika hospitali za Serikali. Kwakuwa, Serikali ikaweka ngumu...sasa ndio wamerasmisha mgomo wao!

Viongozi wamezidi dharau...na ndio maana wamepuuza kuwasikiliza...

Viongozi wa bongo ni watu tunaopaswa kuwachukia kwa dhati! Naunga mkono mgomo endelevu wa madaktari...kwani hata wakati mgomo ulikuwa haujatangazwa, go slow ilikuwa inaendelea na wagonjwa walikuwa wanaendelea kuteseka na kufa!!
 
Hapa tutapiga makelele tu, kama tunataka kuwasaidia madaktari wetu ambao watatusaidia kwa afya yetu ni wote kuingia mtaani. Mfanyakazi yoyote wa umma tuunge mkono kwa kushinikiza wenzetu wasikilizwe madai yao. Imefika wakati sasa wafanyakazi (kama si wananchi wote) tujenge umoja. Sisi wote tu watoto wa baba mmoja (serikali) tena si watoto tu tu pacha, mmoja akionewa tunaathirika wote. Imefika wakati sasa serikali ielewe kuwa iko hapo ilipo si kwa matakwa yao bali imetumwa, imewekwa na kulindwa na sisi wananchi wake. Sisi ni clients ambao tumewacomission wao kazi ya kuleta maendeleo ya nchi yetu ikiwa ni pamoja na kutupatia huduma muhimu katika kiwango kinachokubalika na sisi turidhike nacho. Tuache kulia lia kama ombaomba ilhali tuiomayo ni haki yetu wenyewe. Tunakatwa kodi, ndugu zetu wanakatwa kodi kwa ajili ya maboresho mbalimbali na hata bila ya kodi kitendo cha kupata ridhaa ya mwananchi ya kukaa madarakani ni kodi tosha.

Mbona wakiwa wanaomba kura, wanatuahidi mengi? au kwa vile usemi wa "Never make a promise that you can't keep" ulizaliwa kwa wazungu??
 
ikiwa takribani siku ya tatu mfululizo madatari tanzania kuigomea serikali kutoa huduma kwa wagongwa kwa madai:

1. Kuitaka serikali kuboresha huduma kwa wagonjwa ( kutokulala chini, kukosa vipimo muhimu, dawa, oxygeni, vitendea kazi vinavyopelekea kutoa huduma duni)

2. Kuipiga marufuku serikali kutumia hospitali kuu nchini kama stand za kuwapeleka wakubwa nje ya nchi kutibiwa na kutelekea kutohamasika kuboresha hospitali nchini.

3. Kupewa masilahi yao kama ilivyoandikwa kwenye nukuu za serikali.

4.kupewa huduma bora za afya pale wanapougua kama wawatendeanyo wagonjwa. (green card)

5. Kuwatoa madarakan wakuu wa wizara maana ndio kikwao.

6. Kuwarudisha interns waliofukuzwa bila hatia muhimbili bila mashariti.

Mimi binafsi kwa tafasiri ya haraka yote yalianisha ni madai halali na ni haki ya mgonjwa na daktari pia wanachofanya ni wajibu wao, naiomba serikali isijifanye kiziwi ndugu zetu wanaumia, ilishungulikie shala hili bila ubabaishaji.
 
Aliyeweka roho zetu rehani wala si Madaktari wetu.

Wenye kufanya hivo ni watunga sera zetu hapo sekta ya afya, ukaidi wa Blandina Nyoni na kujiona Katibu Mkuu wa kwanza na wa mwisho Tanzania hii.

Nasema wenye kuweka roho zetu rehani ni Mizengo Peter Pinda anayeinuia kuwaongeza wabunge posho za kufa mtu licha ya sisi walipakodi kugomea jambo hili.

Ndio, nasema Waziri Mkuu anaonyesha kila dalili ya KWENDA KINYUME na matakwa ya umma huku akiendelea kuwuzia kiswahili kirefu Madaktari wetu huku asijue kwamba waalimu na University Lecturers naao wako njiani na madai mazito zaidi miezi si mingi sana.

Tunamtakia Mhe Pinda kheri katika hatua yake hiyo huku tukimsubiri njia panda tukamalizane cash cash juu ya huo ukaidi wa maoni ya umma wa nchi hii.
 
Ikiwa serikali inatoa billioni 90 kila mwaka kwa kanisa mlitegemea itapata fedha wapi zaidi za kuboresha Hospital zake..
huyu ni Mkandara kweli!!?? this is too low kwa level yako, hivi hapa tunaweza kukutofautisha na Maralia Sugu? kwa hiyo solution ya matatizo haya ni kuwa na Mahakama ya kadhi na tujiunge na OIC?
 
posho za wabunge nazo unazisemeaje?
 
safi sana docs, kazeni uzi muda sim refu kitaeleweka
 
Madai haya ni ya msingi. Yatekelezwe haraka. Je nini tamko la chadema kuhusu hawa wapigakura?
 
Back
Top Bottom