Hamjambo wajukuu zangu.
Tangu nimeanza kuwa mtu mzima(18yrs) katika miaka ya 1970s sijawai ona maajabu kama haya yanayotokea sasa katika medani za siasa ya nchi ya viwanda na kutumbua majipu.
Namzungumzia Mhe Edward Ngoyai Lowasa, nguli la siasa tangu enzi za Mwlm JK Nyerere. Edward Lowasa ni mwanasiasa aliyepitia magumu mengi pengine kuliko mwanasiasa yeyote katika siasa za Tanzania. Lowasa aliwahi kuhusishwa na kashfa ya ubadhirifu AICC, Richmond, Jengo la UVCCM na kashfa nyingine nyingi nje ndani ya ccm na serikali ya Tanzania.
Ajabu lenyewe ni hili hapa. Lowasa baada ya kuhama CCM na kugombea urais kupitia UKAWA amekua ni nyota inayong'aa ambayo ina tumaini tele mbele ya watanzania wanyonge. Amekuwa kama Musa aliyewatoa wanawaisrael utumwani Misri kuelekea nchi ya ahadi.
Linalonishangaza zaidi kila aliyeinua/anayeinua kinywa chake na kumnena vibaya mtu huyu maono huwa yanamrudia mwenyewe. Kumbukeni kauli za watu mbalimbali waliomtusi na kukashifu afya mtu huyu lkn wao ndo wamekuwa wa kwanza kuchungulia kaburi. Lakini pia chunguzeni kwa makini matamko yenye utata ya Mhe RC ambaye alitumia muda mwingi kumnanga na kumsimanga Lowasa ndani ya UVCCM. Mhe RC hv sasa ameanza kupoteza mwelekeo kila kauli inayotoka kinywani mwake ina ukakasi dhidi ya wananchi ama watumishi wenzake.
Namuhurumia sana mjukuu wangu wa ACT aliyemtukana Lowasa pale mbagala zakhem sijui naye itakuaje tusubiri muda tu.
Babu yenu
Tanaluza
Tangu nimeanza kuwa mtu mzima(18yrs) katika miaka ya 1970s sijawai ona maajabu kama haya yanayotokea sasa katika medani za siasa ya nchi ya viwanda na kutumbua majipu.
Namzungumzia Mhe Edward Ngoyai Lowasa, nguli la siasa tangu enzi za Mwlm JK Nyerere. Edward Lowasa ni mwanasiasa aliyepitia magumu mengi pengine kuliko mwanasiasa yeyote katika siasa za Tanzania. Lowasa aliwahi kuhusishwa na kashfa ya ubadhirifu AICC, Richmond, Jengo la UVCCM na kashfa nyingine nyingi nje ndani ya ccm na serikali ya Tanzania.
Ajabu lenyewe ni hili hapa. Lowasa baada ya kuhama CCM na kugombea urais kupitia UKAWA amekua ni nyota inayong'aa ambayo ina tumaini tele mbele ya watanzania wanyonge. Amekuwa kama Musa aliyewatoa wanawaisrael utumwani Misri kuelekea nchi ya ahadi.
Linalonishangaza zaidi kila aliyeinua/anayeinua kinywa chake na kumnena vibaya mtu huyu maono huwa yanamrudia mwenyewe. Kumbukeni kauli za watu mbalimbali waliomtusi na kukashifu afya mtu huyu lkn wao ndo wamekuwa wa kwanza kuchungulia kaburi. Lakini pia chunguzeni kwa makini matamko yenye utata ya Mhe RC ambaye alitumia muda mwingi kumnanga na kumsimanga Lowasa ndani ya UVCCM. Mhe RC hv sasa ameanza kupoteza mwelekeo kila kauli inayotoka kinywani mwake ina ukakasi dhidi ya wananchi ama watumishi wenzake.
Namuhurumia sana mjukuu wangu wa ACT aliyemtukana Lowasa pale mbagala zakhem sijui naye itakuaje tusubiri muda tu.
Babu yenu
Tanaluza