Nategemea kuvuta fiber internet ya TTCL

Nategemea kuvuta fiber internet ya TTCL

Hawa jamaa nilienda ofisini kwao, Nikauliza nipate details vizuri kuhusu huduma ya Fiber. Nikajibiwa kwa mbinu za kibiashara kumvutia mteja.
Waliniambia kuna fomu watanipa nijaze then watanipigia simu waje kufanya survey then ndio watakuja kufunga, Nikawauliza hiyo process yote hadi kufungiwa inaweza kuchukua siku ngap? Wakaniambia hadi siku 7 nakuwa tayari nishafungiwa.

Niko nasubiri simu ya survey hapa , Leo ni siku ya 9 ya kazi, sikutaka kuhesabu weekend, nimeassume tu hawafanyi kazi weekend.
Apo ungecheki Voda chap tu anafunga supakasi internet kwako mkuu
 
Mkuu naomba kuuliza tena hao wanaotoa huduma ya Isp wao Internet yao wanatoa wapi
ISP si kama Vodacom ye ananunua toka Europe kupitia world wide ISP then using Fiber anasafilisha ad center ake pale south so toka apo south ndo anaenda Kwa inch zingne so far fiber cable inapita chini ya ardhi au chni ya bahari
 
Hizi IT zetu...wewe badala uwape watu miongozo jinsi ya kuingiza hela matokeo yake imekuwa kinyume...

Tumia bando la kawaida mpka utakapoona uhitaji wa hizo fiber, hiyo hela ya kulipia mwezi inabid uingize kwa siku ikizid sana siku mbili .
Huyu jamaa fala kweli. Unafikiri ukijua IT ndo umejua kila kitu nonsence kabisa
 
ISP si kama Vodacom ye ananunua toka Europe kupitia world wide ISP then using Fiber anasafilisha ad center ake pale south so toka apo south ndo anaenda Kwa inch zingne so far fiber cable inapita chini ya ardhi au chni ya bahari
Kwa mfano nikitaka kuanzisha ISP co kama sina uwezo wa kutoa Internet uko Europe naweza kutoa kwa vodacom
 
Fiber yenyewe ni Ghali, kilomita moja inacost mamilioni cable tu, bado miundombinu mingine kama inachimbiwa chini ya Ardhi ama ni nguzo etc. Na kuna mambo mengine kama software, Modem/routers, repeaters na makorokoro kibao.

Ndio maana huoni kampuni yoyote ndogo ina compete kwenye Fiber.
Je haya mashindano ya Zuku na TTCL kwenye Fiber unahisi Zuku atatoboa?
 
Wana miundombinu yao, na miundombinu yao inapoishia kunakuwa na isp mwengine.

Kwenye long distance kunakuwa na Cable za baharini.

Mfano kama Halotel kasambaza fiber zake nchi nzima zina connect, then hizo fiber zipo connected na fiber nyengine Africa nzima na chini ya bahari.
Angalia ramani ya Fiber Kusini mwa jangwa la sahara
View attachment 2306860

So isp analipa kwa hizo kampuni zenye fiber hapo ndipo linapokuja suala la route.

Kama umewahi kucheza game online utaona mitandao haifanani, kama unacheza game lipo Usa unaweza ukatumia voda ping ikawa 150ms na ukatumia Tigo ping ikawa 200ms kwa maana voda inafikia isp wa Marekani haraka kuliko Tigo, hio inatokana na route anayotumia Voda ni fupi, pengine inakatiza tu congo mpaka Atlantic ocean faster inaenda Usa, ila mwengine labda mpaka izunguke North Africa itokee ulaya iende Usa.

Hivyo kila ISP anachagua mwenyewe Route zake na Kampuni Gani atatumia kutoa data Nchini kuingia mifumo ya Dunia.
Hiv hiv fiber ndio nn wakuu au ni unaenda ttcra wanakupa internet yako mwenyew unakuwa unauza msaa please
 
Mashindano yao faida kwetu, Zuku wana Huduma nyingi za kujitofautisha, sidhani kama atatolewa sokoni, ila soko lake litamegwa.
Hivi kwann nchi kama marekani ukiangalia kampuni kubwa la Internet kama AT&T halija dominate Internet provider kwa majimbo yote lakini ni more powerful ISP kwa bongo ttcl ndo ka cover asilima kubwa lakini haliendelea kukua kiuchumi
 
Hivi kwann nchi kama marekani ukiangalia kampuni kubwa la Internet kama AT&T halija dominate Internet provider kwa majimbo yote lakini ni more powerful ISP kwa bongo ttcl ndo ka cover asilima kubwa lakini haliendelea kukua kiuchumi
Isp wa marekani ni kama maduka makubwa ya simu, wanauzia watu simu kwa mikataba wanalipa kila mwezi huku wakipewa dakika na gb za kupimiwa kwa mijali. Ile system inafanya kazi Marekani tu.
 
Back
Top Bottom