Natamani Kujiua

Natamani Kujiua

Habari Wana JF, Kama Heading Inavyosomeka Hapo Juu, Mimi Ni Kijana wa Miaka 29, Nimeajiriwa, Kazi Imenitenganisha Na Familia,( Mzazi Mmoja ambaye Ni Mama, Maana Baba Alifariki Kipindi Nikiwa Mdogo, Nimekua Mlevi Kupindukia, Simu Sipigi Nyumbani, Hela Siioni Inakoelekea, Mama Sina Mahusiano Nae Mazuri, Mahusiano Yangu Hayaeleweki.
Misuko Suko Kibao, Ajali Haziishi, Sioni Wapi Naelekea, Asubuhi ya Leo Wakati Natoka Club , Nikiwa Na Mwanamke Niliempata Huko, Nimepata Ajali Mbaya Sana, Nimepata Majeraha Madogo Tu, Ila Gari Imeumia Sana, Na Kwa Vile Nilikua Nimelewa, Nikampigia GF Wangu Akaja Kushughulikia Kuivuta Gari, Mimi Na Yule Mwanamke Tukawa Tumeshaondoka, Hata Sikufikiria Kama Nitakutwa.

Mbaya Zaidi Nikafumaniwa Na Yule Mwanamke, Ilikua Aibu tupu Mtaani, Naona Siheshimiki Tena, Nyumba Ninayoishi Ni Ofisi Nipo Na Baadhi ya Staff Wenzangu wapo Na Familia Zao, Sijatoka Nje Siku Nzima ya Leo, Kilicho Kichwani Kwangu Ni Kujiua Tu, Sitamani Tena Kuishi, WHY ALWAYS ME? Nimemkosea Nini Mungu, Najua Natenda Dhambi, Ila Niende Huko Labda Nitapumzika. Samahanini Kwa Maelezo Yangu Marefu
Ila Hili Lipo Moyoni Mwangu na Lazima Nilitekeze, Napokea Maoni Yenu Wadau, NAKOSEA WAPI?
Hizi swaga ni za kilevi usituchore wewe
 
Habari wanaJF, kama heading inavyosomeka hapo juu, mimi ni kijana wa miaka 29, nimeajiriwa, kazi imenitenganisha na familia,( mzazi mmoja ambaye ni mama, maana baba alifariki kipindi nikiwa mdogo, nimekua mlevi kupindukia, simu sipigi nyumbani, hela siioni inakoelekea, mama sina mahusiano nae mazuri, mahusiano yangu hayaeleweki.

Misuko suko kibao, ajali haziishi, sioni wapi naelekea, asubuhi ya leo wakati natoka club , nikiwa na mwanamke niliempata huko, nimepata ajali mbaya sana, nimepata majeraha madogo tu, ila gari imeumia sana, na kwa vile nilikua nimelewa, nikampigia gf wangu akaja kushughulikia kuivuta gari, mimi na yule mwanamke tukawa tumeshaondoka, hata sikufikiria kama nitakutwa.

Mbaya zaidi nikafumaniwa na yule mwanamke, ilikua aibu tupu mtaani, naona siheshimiki tena, nyumba ninayoishi ni ofisi nipo na baadhi ya staff wenzangu wapo na familia zao, sijatoka nje siku nzima ya leo, kilicho kichwani kwangu ni kujiua tu, sitamani tena kuishi, why always me? Nimemkosea nini mungu, najua natenda dhambi, ila niende huko labda nitapumzika. Samahanini kwa maelezo yangu marefu.

Ila hili lipo moyoni mwangu na lazima nilitekeze, napokea maoni yenu wadau, nakosea wapi?
Kila mtu ana njia yake yake ya kufia,wengine watakufa na ukimwi, ajali, malaria, kuuawa nk.Wewe unaepanga kufia kwa kujiua unaweza ukashindwa kwa sababu Mungu ndie anaepanga tarehe ya mtu kufa.Omba watu wakusaidia kuepukana na matendo yanayoashiria kukuletea matatizo.
 
Unatoka club mlevi kupindukia hujui pesa zinaelekea wapi na umemkasirisha mama kwa sababu ya ulevi wako na kutojali familia...pombe na wanawake mbona unaweza kuwaacha tu tatizo liko wapi au ndio umeanza kunywa pombe na hao kutafuta wanawake ukubwani baada ya kupata kazi...sina ushauri wowote walevi wengi wanajitambua utatupa mrejesho...
Ni Kweli Usemacho Kaka, Nimeanza Kunywa Baada ya Kuwa na Kazi, Asante kwa Ushauri
 
Pale unapoona binadamu wote wamekuacha na kukutenga usisahau kuna mungu muumbaji,kumbuka umeanguka wapi mludie yeye naye atakuponya pia muombe msamaha mama yko weka mambo sawa kwa watu wako .naamini utafanikiwa na utarudi kama zamani .
Amina! Ubarikiwe Sana
 
Yani natamani ningekuwa karibu nikuchape vibao acha upuuzi,mtoto wa kiume usirudie kusema upuuzi huu tena,Kuwa na moyo mgumu kama chuma cha pua.
Hope in the face of uncertainty!
Asante, Nitajitahidi
 
Pole sana. Kujiuwa sio suluhisho la maisha yako. Tubu kwa mola wako. Jiepushe na mambo ya kishetani kama kulewa na kutia malaya. Utafanikiwa tu
 
Hili nalo la kuomba Ushauri..'!???? Sasa unajua unapokosea unataka ushauri wa nin...!??? Rekebisha makosa yako songaa mbelee mzee...
 
Unategemea kujiua lini? Huu ni msiba wa kujitakia eti pombe na ngono! Shukuru Mungu una hela za kulewa na za kununulia malaya.
 
Kiutaalam mtu akishakua na suicidal thoughts ni vyema kukaa nae karibu sana
 
Halafu wazazi bana aliyesema ni miungu ya pili duniani nadhani hawakukosea, mi nkizinguanaga na washua home hata kidogo tu, aisee nakosa amani kabisa hadi nikae nao tufanye resolution. Go n talk to your moms
 
Be like Bro
Bro.jpeg
 
Umri wako bado, ukikua utaacha huo ujinga...

Ngoja uianze 30+ na akili itatulia utakua huna stress...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom