Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Nyie mnajibizana na Huyu mtu Yupo USA kila siku kuleta thread za kuwapambanisha vichwa,kwanza hajulikanagi Yupo upande gani siku nyingine anakuja na kelele kibao kumpinga Lowassa,siku nyingine JPM,watu kama hawa wapo kibao nje hata kuja kwao kusalimia huwa hawaji,kazi kuchonganisha watu tu na kuwatia watu hasira na serikali yao.Ishu ya UKUTA Huyu jamaa aliwapamba watu waingie barabarani wapigwe utadhani atakuwepo nchini.Kuweni makini na mleta mada.Mwisho anachosahau dunia ni kijiji siku hizi hata USA Waweza kufatwa tu,system inafika popote tu ikiamua.Its just the matter of time.Ni hayo tu.
Angalia kilicho cha maana kwenye hoja yake achana na mahali alipo Mkuu. Uhuru wa kutoa maoni ni muhimu sana
 
Watu wenye hekima huwa wanawaonya kina Maxence kuhusu kucheka na watu wanaongea pumba na matusi kupitia nyuma ya keyboard lakini hawakusikia, ndiyo malipo ya kulea ujinga wanaanza kuyapata. Watu wanashangaa nini hata Marekani huko mnakotaka kukimbilia ukimbizi mitandao mikubwa kama yahoo inapelekeshwa na serikali itakua hapa? Watu tujifunze kuwa uhuru una mipaka yake, maana kama una uhuru wa kufanya lolote basi ua mtu uone kama huo uhuru wako utafuatwa, sentensi ya Uhuru inasema "una uhuru wa kufanya lolote ili mradi usivunje sheria" kwanini waliongeza hilo neno kuvunja sheria??? lakini MSIMISEKE SENIOR hapa kuna wengi wanajifanya wanajua huko hawajaverify hizo personel details zao. Mbaya zaidi wanaishi bongo na wanatumia mtandao wa bongo. Kwanini wasiende kutapika hizo nyonga zao katika mitandao ya kimataifa maana huko ndiko wataianika serikali labda na wao kiingereza kinawashinda.
Ndugu mipaka kwenye uhuru wa kufikiri na kutoa maoni ni ukoloni Tu. Kwa nini uniwekee mipaka ya kufikiri na kukiishi ninachofikiri. Kama nimefikiri vibaya kwa kuwa uwezo wangu kikfikra ni mdogo chip In mwenye uwezo mkubwa weka fikra zako. Wengi watajifunxa kwa jinsi hiyo.
Tinawka mipaka kwenye uhuru inawezekana ni ujinga Tu wa kutokujua maana au kuwa na mtazamo tofauti kuhusu maana ya uhuru. Hayo yote yaweza tibiwa kwa kuwepo uhuru wa kufikiri
 
"Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha"

Daa we jamaa ni noma...hadi nmeogopa kwenye hiyo paragraph
Naamini binadam yoyte Raia wa nchi mwenye akili tumamu anaweza kuwa rais mambo ya haiba peleka Bongo movies
 
Angalia kilicho cha maana kwenye hoja yake achana na mahali alipo Mkuu. Uhuru wa kutoa maoni ni muhimu sana
Mkuu mkiwa mmezaliwa watoto tisa nyumba moja,wanne wakawa wanaishi mbali na watano mnaishi na familia,walio mbali wakawa wanakuja na hoja za mmojawenu anayewaongoza mliyemchagua hafai wakati haishi humo,pengine tayari ana familia yake inabidi mumtilie shaka,mbaya zaidi hatoi suluhisho ni nani anafaa ila mijadala yake ni kuharibu tu.Hata mkifarakana haishi hapo tena.Mfatilie huyu jamaa,ni mojawapo ambao ni kama wapo nje lakini maisha yamewashinda,ya huko waliko yamewashinda na ya wanakotokea(asili) yamewashinda.Mtu anayesema raisi aachie ngazi kwa kejeli kibao bila kujua gharama na yanayoweza kutokea nchi ambayo hakai ni wa kupuuza kwa gharama yoyote.Ndo maana nimekupa mfano wakati Chadema wanaandaa UKUTA alikuwa anashinikiza watu waandamane waingie mtaani wapigwe tu na wajeda.Fatilia post zake kila anachosema ni kama matokeo ya matakwa yake yawe + au - yeye hana la kupoteza.Bado unaona ni mtu wa maana kumsikiliza?,mtu anayeishi hapa hapa kuna vitu hawezi andika wala kuongea kama anajua madhara yake.Hebu mfatilie thread zake hata tatu au nne halafu nipe jibu mkuu.
 
Nchi imekuwa ya hovyo hovyo, eti akili moja ni bora kuliko akili za watanzania milioni 40.
3bd2c7ceb06384ca57e8396cf31591fa.jpg
 
Mkuu mkiwa mmezaliwa watoto tisa nyumba moja,wanne wakawa wanaishi mbali na watano mnaishi na familia,walio mbali wakawa wanakuja na hoja za mmojawenu anayewaongoza mliyemchagua hafai wakati haishi humo,pengine tayari ana familia yake inabidi mumtilie shaka,mbaya zaidi hatoi suluhisho ni nani anafaa ila mijadala yake ni kuharibu tu.Hata mkifarakana haishi hapo tena.Mfatilie huyu jamaa,ni mojawapo ambao ni kama wapo nje lakini maisha yamewashinda,ya huko waliko yamewashinda na ya wanakotokea(asili) yamewashinda.Mtu anayesema raisi aachie ngazi kwa kejeli kibao bila kujua gharama na yanayoweza kutokea nchi ambayo hakai ni wa kupuuza kwa gharama yoyote.Ndo maana nimekupa mfano wakati Chadema wanaandaa UKUTA alikuwa anashinikiza watu waandamane waingie mtaani wapigwe tu na wajeda.Fatilia post zake kila anachosema ni kama matokeo ya matakwa yake yawe + au - yeye hana la kupoteza.Bado unaona ni mtu wa maana kumsikiliza?,mtu anayeishi hapa hapa kuna vitu hawezi andika wala kuongea kama anajua madhara yake.Hebu mfatilie thread zake hata tatu au nne halafu nipe jibu mkuu.
Umewahi kusikia kuhusu vita ya majimaji au unafikiri waliopigana hawakuwa na mwili na nyama ? Sisemi vita ni nzuri Bali nakukumbusha kuwa watu wengine wanapotaka kusongesha ajenda yao hawaogopi kile wewe unaogopa.
Kihusu ndigu yako aliye mbali akija na hoja kuhusu miongozi wenu wa familia jibu hoja yake na hrshimu exposure yake. Kama mmezaliwa katika ya msitu maisha na dunia yenu ni msitu kwa ukomo. Akija akitevuka msitu akikwambia uongoxi wa kimsitu ni mbovu jenga hoja kinzani dhidi yake usimfunge kinywa au kumpuuza puuza hoja kwa hoja
 
Mkuu mkiwa mmezaliwa watoto tisa nyumba moja,wanne wakawa wanaishi mbali na watano mnaishi na familia,walio mbali wakawa wanakuja na hoja za mmojawenu anayewaongoza mliyemchagua hafai wakati haishi humo,pengine tayari ana familia yake inabidi mumtilie shaka,mbaya zaidi hatoi suluhisho ni nani anafaa ila mijadala yake ni kuharibu tu.Hata mkifarakana haishi hapo tena.Mfatilie huyu jamaa,ni mojawapo ambao ni kama wapo nje lakini maisha yamewashinda,ya huko waliko yamewashinda na ya wanakotokea(asili) yamewashinda.Mtu anayesema raisi aachie ngazi kwa kejeli kibao bila kujua gharama na yanayoweza kutokea nchi ambayo hakai ni wa kupuuza kwa gharama yoyote.Ndo maana nimekupa mfano wakati Chadema wanaandaa UKUTA alikuwa anashinikiza watu waandamane waingie mtaani wapigwe tu na wajeda.Fatilia post zake kila anachosema ni kama matokeo ya matakwa yake yawe + au - yeye hana la kupoteza.Bado unaona ni mtu wa maana kumsikiliza?,mtu anayeishi hapa hapa kuna vitu hawezi andika wala kuongea kama anajua madhara yake.Hebu mfatilie thread zake hata tatu au nne halafu nipe jibu mkuu.

Great! Waste no time na wajinga wa US, Trump ndio Raisi huko. Nawajua wengi US na Uk ni wachovu kifweza. Kazi mbovu huko, wajinga wengi wanalipwa $8 kwa saa halafu ni kazi hasa masaa 12 na gharama za maisha ni kubwa. Wajinga wengi pande hizo wanashea apartments, yaani nyumba twaishi kama bwenini shule za boarding bongo.

Trump.
 
Kwani mtu ukitoa maoni yako pasipo kutoa matusi au ukianzisha uzi wenye uhalisia na usio wa kichochezi unakuwa na hofu ya nini?

Tatizo lililopo kuna baadhi yetu tumekuwa maarufu kutunga stori za uongo na kuzijengea hoja then tunataka jamii iamini kama ni kweli kumbe ni upotoshaji

Mtu kama umeanzisha mada yako na ushahidi unao kwa nini uogope? Endapo utahitajika polisi si unapeleka ushahidi?

Fikiria mtu anayeanzisha uzi hapa eti Dangote anahamishia kiwanda Kenya na hizo habari zinasambaa dunia nzima kumbe ni uonge pasipo kufikiria negative impacts kwa wawekezeji walioko huko nje. Mtu kama huyu leo hawezi fanywa kitu sababu tu anatumia ID feki sishangai kesho akaibuka na jambo jingine

Watu wa namna hii lazima washughulikiwe hakuna kulea ujinga. Watanzania tumekuwa maarufu sana wa kupika majungu

Ninakubaliana na wewe kabisa uhuru wa kutoa maoni lazima uheshimiwe na watawala kwani ni takwa la kikatiba lakini uhuru huo lazima uzingatie utu na nidhamu.

Leo mtu akimchukia mtu flani sababu za kiitikadi za vyama au jambo lolote, kesho anamtungia tuhuma na kusambaza kwenye mitandao. Vitu vya namna hiyo siyo vya kulea
Bila shaka ID yako ni feki we MTU!

Unaposema uchochezi ni vile tu mtu unavyoamua kudefine issue! Na uhalisia wa kitu anaujua anayeleta mada wala si wewe kujidai unafahamu kila kitu na hivyo kukosoa kila mtu.

Anyways, jf siyo gazeti kwahiyo usitake kazi ya uhariri hapa.

Umesema aliyeleta habari za dangote alipotosha,,sawa! Je,hiyo habari ilianzia hapa jf?! Hakuna magazeti yaliyoandika habari hiyo hiyo? Au nayo yalikopi kutoka Jf?

Asiyetaka kuambiwa ukweli ni shetani.
 
Inawezekana kabisa wengi wetu humu tumeathirika na Viroba, kwa uchangiaji huuu sion staha na U great thinker zaidi ni Uhuni na Usela mavi au Kutafuta umaarufu wa vitu vya ovyo ovyo.
Unatafutaje umaarufu ilihali hakuna anayekujua? Can't you think?!

Hebu endelea kunywa gongo yako
 
Upo sahihi kaka kukosolewa ni sehemu ya kujifunza ukiona mtu hataki kukosolewa atakuwa na matatizo binafsi

Kila binadamu tunajifunza kwa kuambiwa na wengine wapi hapafai na wapi tupo sahihi hii ya kujifanya miungu watu anajiaibisha mwenyewe na taifa kwa ujumla
Mimi sipo tayari kuona taifa langu linadharirika kwa ajiri ya mapungufu ya mtu mmoja
Kosoa kwa lugha yenye heshima na adabu. Ukifanya hivyo ukosoaji wako utatiliwa maanani.
 
Upo sahihi kaka kukosolewa ni sehemu ya kujifunza ukiona mtu hataki kukosolewa atakuwa na matatizo binafsi

Kila binadamu tunajifunza kwa kuambiwa na wengine wapi hapafai na wapi tupo sahihi hii ya kujifanya miungu watu anajiaibisha mwenyewe na taifa kwa ujumla
Mimi sipo tayari kuona taifa langu linadharirika kwa ajiri ya mapungufu ya mtu mmoja
Kosoa kwa lugha yenye heshima na adabu. Ukifanya hivyo ukosoaji wako utatiliwa maanani.
 
Mimi sio Mwanasheria lakini sio zwazwa. Sheria na kifungu ulichonukuu kinaelezea kuwepo kwa shitaka au tuhuma lakini sio AFANDE aamke Tu na kumwagiza Max kuwa nataka utambulisho wa H1N1, Nyani Ngabu etc etc
atakuwa amesema kwenye barua waliyomwandikia max
 
Kwa Maana Ulimi nao ni kiungo, nacho kwa udogo kilijipatia sifa yake. Kwa maneno chawaweka watu pamoja kadhalika kwa maneno hayo hayo huwaweka watu mbali. Bali wewe upitato katika mapito yako, Basi uchunge sana Mdomo wako kuliko chochote ukichungacho.

Mfalme mjinga Hushindwa kuuona upepo, nao Watu wapumbavu hujishughulisha na Kazi za upepo wasio uona. Kaburi lilizikwa Aliyehai naye akafukiwa katika Shimo lenye Mchanga Mweupe, Waliolia walilia kwa ujinga Wang nao walioshangilia walishangilia kwa maovu yao.

Ikiwa Mtoto humwogopa Babaye, naye baba kwa Upotevu wa fikra zake huona fahari kwa mwanae kuwa na hofu basi ni kheri Mti uliopandwa jangwani kuliko Baba huyo.

Nchi hutoa mazao ya kila namna nayo huipendezesha Uso wake lakini kwa Waliiharibu nchi. Kwa dini zao za uwongo wakawanyonya Masikini wakijitia maneno matamu kuliko asali ili wapate kudhidhulumu nafsi changa.

Wasiwasi ndio akili nayo Staha ni kwa mwenye hekima. Je utamfanyia Staha Mpumbavu asikudharau? Hasha Usimjibu mpumbavu wala kuongea nae usije ukajitia katika Uchungu mkuu.

Mfalme mwenye hekima huipinga dhuluma, huitetea haki ya wanyonge naye hujilisha maarifa kwa kufuata sheria na hekima. Bali Mfalme mpumbavu nani Asiyemuogopa, Mfalme ajitakiaye mambo yake mwenyewe pasi na Mashauri ya Wazee.

Taifa la Watu wajinga hujilinganisha na Watu wa mataifa mengine. Hujisifia kwa wasiyokuwa nayo, nao hujidharau na kujiponda kwa yale walionayo. Hao ndio watu wajinga niliowaona katika Uvungu wa Jua.

Kilio kingi huuchosha mwili nacho huleta Kwiki itingishayo Mwili.

~Michaelray22
 
Sawa lakini mbele ya wakina Lubuva nk nk hata mshinde watamtangaza wanayetaka ili mradi wao matumbo yanapokea.

Sasa umenielewa. Tunapopiga kelele za uhuru wa habari, tufikirie kujenga upinzani imara wenye mkakati thabiti sivyo ilivyo sasa tunatawaliwa na mihemko
 
Bila shaka ID yako ni feki we MTU!

Unaposema uchochezi ni vile tu mtu unavyoamua kudefine issue! Na uhalisia wa kitu anaujua anayeleta mada wala si wewe kujidai unafahamu kila kitu na hivyo kukosoa kila mtu.

Anyways, jf siyo gazeti kwahiyo usitake kazi ya uhariri hapa.

Umesema aliyeleta habari za dangote alipotosha,,sawa! Je,hiyo habari ilianzia hapa jf?! Hakuna magazeti yaliyoandika habari hiyo hiyo? Au nayo yalikopi kutoka Jf?

Asiyetaka kuambiwa ukweli ni shetani.

Kumbe unajijibu mwenyewe. Sababu hutaki kuambiwa ukweli basi jibu tayari unalo wewe ni nani
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom