Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Nashukuru kwa ufafanuzi... imani hapo tu ndio huwa namkumbuka athari za ujuo wa wamishionari jukumu lao kuu kutuandaa kutawaliwa kifikira kwa kigezo cha imani... ukipigwa kofi shavu la kulia geuza na kushoto. Wakati wao ukimgusa mwenzao mmoja wanawakaanga nyie 1000 anyway baki na imani yako wengine fighting for our right and reputation ndio maisha yetu.
huko kungine sikujibu nakujibu Hapa...

huyo mama wala hakuleta jf sio kweli aliandik instagram kuna mtu alileta huku tena kwa kuuliza mbona yule Dada anashutuma sana vtu asivyo na uhakika Nazo

hapo unamsingizia max

Mimi imani yangu inanituma kuna maisha baada ya kufa na kuna hukumu pia kwa kila utakalolitenda hapa duniani linaandikwa

Kila mtu aamini kwa imani yake....!!
 
Kwani mtu ukitoa maoni yako pasipo kutoa matusi au ukianzisha uzi wenye uhalisia na usio wa kichochezi unakuwa na hofu ya nini?

Tatizo lililopo kuna baadhi yetu tumekuwa maarufu kutunga stori za uongo na kuzijengea hoja then tunataka jamii iamini kama ni kweli kumbe ni upotoshaji

Mtu kama umeanzisha mada yako na ushahidi unao kwa nini uogope? Endapo utahitajika polisi si unapeleka ushahidi?

Fikiria mtu anayeanzisha uzi hapa eti Dangote anahamishia kiwanda Kenya na hizo habari zinasambaa dunia nzima kumbe ni uonge pasipo kufikiria negative impacts kwa wawekezeji walioko huko nje. Mtu kama huyu leo hawezi fanywa kitu sababu tu anatumia ID feki sishangai kesho akaibuka na jambo jingine

Watu wa namna hii lazima washughulikiwe hakuna kulea ujinga. Watanzania tumekuwa maarufu sana wa kupika majungu

Ninakubaliana na wewe kabisa uhuru wa kutoa maoni lazima uheshimiwe na watawala kwani ni takwa la kikatiba lakini uhuru huo lazima uzingatie utu na nidhamu.

Leo mtu akimchukia mtu flani sababu za kiitikadi za vyama au jambo lolote, kesho anamtungia tuhuma na kusambaza kwenye mitandao. Vitu vya namna hiyo siyo vya kulea
Hivi Dunia ikisikia kua rais hayuko tayari kushirikiana n.a. upinzani unajua impact yake kiuchumi n.a. kisiasa?
Wawekezaji wanaotokea kwenye nchi zenye Demokrasia wakisiakia kua vyama vya siasa vimekatazwa kufanya kazi zao za kikatiba unajua impact yake katika uwekezaji n.a. Uchumi kwa ujumla?
Rais anaendelea kuifanya Tanzania kua hostile country for capital importation /foreign investment kama hujui ilo
 
Kaka ubarikiwe...vichwa vya namna hii ndio vinapaswa kuwa hapa JF.

Unajenga hoja yako bila dhihaka na matusi.

JF inaharibiwa na watu wachache ambao tafsiri ya uhuru wa kutoa maoni/mawazo kwao ni kujenga na kutoa propaganda za uongo zenye kujenga chuki na uhasama ktk jamii na wasiguswe. Kwakuwa taifa hili linaongozwa kwa mujibu wa sheria...inatupasa kutii sheria za nchi zilizopo hata kama sheria hizo hatuzitaki.

Haiwezekani uje hapa jukwaani ubwabwaje unavyotaka bila kupima athari za kauli zako halafu wakuache tu. Hio Serikali hata sisi wananchi tutaishangaa...haipo hapa duniani.

Uhuru bila mipaka ni fujo.

JF bila nidhamu ya kuongea ni fujo...tusikubali watu wachache wakatuharibia JF yetu.....
#Ashindwetu#
 
Wajukuu zako watakuja kukulaumu sana.kama babu zetu wangekuwa waoga kama wewe.mpaka leo hata uhuru huu wa bendera tusingeupata.

Sijaamini kama hayo uliyoandika ni ya kwako! Yawezekana hujui maana halisi ya 'woga' au 'uhuru'!

Ni mtu mwehu, teja au punguani awezea kujifanya jasiri pasipo kupima athari zake!

Ni mtu asiye mstaarabu, kutokujua mipaka ya "uhuru"!
 
"Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha"

Daa we jamaa ni noma...hadi nmeogopa kwenye hiyo paragraph
 
Mbona mnatishatisha watu, ili iww nini? Kwani mmezuiwa kujenga hivyo viwanda? Au ndio mnatafuta sababu ya kujitetea. Na hamtajenga hata kiwanda cha toothstick kwa woga huu mliouanza mapema hivi.
Ndio maana Nagufuli anaamua kuwabana watu wajinga kama ninyi sasa ishu ya viwanda hapa inatoka wapi? Mpinge Magufuli kwa hoja siyo unakuja hapa kwa vimaneno vyako vya jejeli alaf eti unasema ndio unakisoa
 
Nyie nyote mnaompinga JPM ndiyo mtashindwa vibaya sana kwakua mnashindana na mamlaka itokayo kwa Mungu.Huyo aliyekamatwa kakamatwa kwa mujibu wa Sheria na si kwa maagizo ya JPM.Tuache Sheria ichukue Mkondo wake na si kila kitu kumsingizia Rais.
Ni lini Mungu alihusika kwenye uchaguzi hapa nchini,acha uongo na usiwe unamhusisha Mungu kwenye vitu vya aina hii.
 
..umekumbusha vita ya majimaji mkuu,sema saa hizi tushashtuka risasi tunajua hazitageuka maji!
 

Attachments

  • images-8.jpeg
    images-8.jpeg
    13.7 KB · Views: 31
  • images-6.jpeg
    images-6.jpeg
    11.3 KB · Views: 28
  • images-9.jpeg
    images-9.jpeg
    11.3 KB · Views: 34
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
Ashindwe kwa lipi sasa?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom