Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Wawekezaji wapi unaowazungumzia? Maana kampuni zote kubwa ni wageni wapo na hawana mpango wa kuondoka kutokana na mikataba ya kinyonyaji walio saini... anzia kwenye madini Ashanti, Acacia, Williamson , Mantra nenda vitalu vya uwindaji, mahotel ya kitalii, Gesi, uvuvi na usindikaji, viwanda kama polyplastic, viwanda vyote vya cement nani kaondoka? Unapoongelea , kushirikiana lazima ujue unakataa kipi! Na ndio kinachopimwa na jumuiya , kimataifa
Hivi Dunia ikisikia kua rais hayuko tayari kushirikiana n.a. upinzani unajua impact yake kiuchumi n.a. kisiasa?
Wawekezaji wanaotokea kwenye nchi zenye Demokrasia wakisiakia kua vyama vya siasa vimekatazwa kufanya kazi zao za kikatiba unajua impact yake katika uwekezaji n.a. Uchumi kwa ujumla?
Rais anaendelea kuifanya Tanzania kua hostile country for capital importation /foreign investment kama hujui ilo
 
Nadhani watawala wetu hawajajua vizuri ni wapi tumekwama na vitu gani vipewe kipaumbele. Vita ya ufisadi haikuwahi kuwa agenda ya ccm, ni wapinzani walipiga kelele na kufumua kashfa nzito nzito zilizofanyika. Inashangaza kuona kuwa awamu hii wale waliosaidia kuibua kashfa nzito za uhujumu uchumi ndio wanaonekana adui namba moja na wanafungwa midomo. Mfumo uliolea ufisadi ni ule ule na wakubwa hawataki kuubadilisha kwa kisingizio cha kusafisha nchi. Nchi haisafishiki kwa nguvu za mtu mmoja tu, tunataka katiba mpya ili iweka mfumo madhubuti wa kujitawala na sii kutegemea utashi wa kiongozi aliyeko madarakani.
 
Simpendi huyo jamaa basi tu, dua zangu za kufeli mpaka sasa naamini mungu kazipokea, kishafeli katika Kila mipango yake, tunamuhesabia miaka 3 tu ijayo tukammalize kwenye sanduku,
 
Kwani mtu ukitoa maoni yako pasipo kutoa matusi au ukianzisha uzi wenye uhalisia na usio wa kichochezi unakuwa na hofu ya nini?

Tatizo lililopo kuna baadhi yetu tumekuwa maarufu kutunga stori za uongo na kuzijengea hoja then tunataka jamii iamini kama ni kweli kumbe ni upotoshaji

Mtu kama umeanzisha mada yako na ushahidi unao kwa nini uogope? Endapo utahitajika polisi si unapeleka ushahidi?

Fikiria mtu anayeanzisha uzi hapa eti Dangote anahamishia kiwanda Kenya na hizo habari zinasambaa dunia nzima kumbe ni uonge pasipo kufikiria negative impacts kwa wawekezeji walioko huko nje. Mtu kama huyu leo hawezi fanywa kitu sababu tu anatumia ID feki sishangai kesho akaibuka na jambo jingine

Watu wa namna hii lazima washughulikiwe hakuna kulea ujinga. Watanzania tumekuwa maarufu sana wa kupika majungu

Ninakubaliana na wewe kabisa uhuru wa kutoa maoni lazima uheshimiwe na watawala kwani ni takwa la kikatiba lakini uhuru huo lazima uzingatie utu na nidhamu.

Leo mtu akimchukia mtu flani sababu za kiitikadi za vyama au jambo lolote, kesho anamtungia tuhuma na kusambaza kwenye mitandao. Vitu vya namna hiyo siyo vya kulea

Maneno yote bila mfano ni upuuzi.
 
Wawekezaji wapi unaowazungumzia? Maana kampuni zote kubwa ni wageni wapo na hawana mpango wa kuondoka kutokana na mikataba ya kinyonyaji walio saini... anzia kwenye madini Ashanti, Acacia, Williamson , Mantra nenda vitalu vya uwindaji, mahotel ya kitalii, Gesi, uvuvi na usindikaji, viwanda kama polyplastic, viwanda vyote vya cement nani kaondoka? Unapoongelea , kushirikiana lazima ujue unakataa kipi! Na ndio kinachopimwa na jumuiya , kimataifa
Kwahiyo una amini kua kwakua wapi hao basi hatuitaji wawekezaji wengine
 
ni kweli mkuu... hapa kuna fikra pevu sana na zimewasaidia watawala wengi kujirekebisha. Lakin swala linakuja kwamba, kama kweli tunatoa mawazo ya maana kwa nini tunaogopa kungundulika na vyombo vya usalama? kwa nini kuwaficha vyombo vya usalama kama wakihitaji kujua nani kasema nini? Uoga huu unatoka wapi??

Tazama michango yangu yote katika jukwaa hili, sijawahi kumtukana mtu, hata nikitoa mawazo ya kuikosoa serikali naongea kwa staha, sina hofu yeyote ya kujulikana na vyombo vya usalama.

kabla ya kushambulia vyombo vya usalama tujipime wenyewe.. je tunaongea kwa staha au tunataka jamii forums liwe jukwaa la kujifichia matusi yetu kwa watu??

Max Mello nakuombea umalizane nao hao watu urudi kuendelea na shughuli zako, Mungu ni mwema, utatoka tu bro.
Kama unatoa mchango mzuri na wabusara kwanini Usalama wahitaji taarifa zako?
Usalama wanataka nini hasa kwako?
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?

kukamatwa kwa Melo hakutakiwi kuhusishwa na Magufuli labda kuhusishwe na CYBER CRIME ACT amabayo inawapa mamlaka polisi kupata taarifa za watu fulani kutoka taasisi yeyote ile na polisi walipokataliwa na Melo ndiyo maana walifungua case na jana walimshikilia lakini bado kuna case ya msingi mahakamani ya kupinga vipengele vya cyber crime act vinavyo kinzana na katiba mama.....hivyo ni lazima wamuachie huru leo.

Kwa hiyo kukamatwa kwa Melo hakuna uhusiano na Magufuli kabisa sema hamtaki kutafuta taarifa.
 
mkuu hili jukwaa tunakoelekea na hii serikali yetuu itafikia hatua inapita muswada wa kufungiwa, maana ukiskia huko juuu wanataka kuzima mitandao ya kijamii huwezi amini 99% ni jf na kama kweli tutatafutana mchawi ni nani

*bado tutaendelea kukumbuka past tense*
 
Namaindi kinoma ingekuwa Maisha yanafaa ku forward ningepeleka mpaka 2025 ili mtoto wa
malkia apite aende zake na balaa lake .
 
Ameshashindwa kitamboo mbona mkuu remix unataka he is a specialist in failure
 
Usijidanganye kua Mungu hausiki kwa kuegemea kwenye ushabiki.
Acha unazi na pia acha kufanya vitu kwa mihemko "Siku zote Mungu hapatani na uchafu ,acha kumchafua Mungu kwenye vitu vya aibu " kama unazungumzia yule Mungu wa mzizima uko sawa.

Unaweza kuthibithisha vitu vinne vinavyoonesha yeye ni chaguo la Mungu?
 
Kwani mtu ukitoa maoni yako pasipo kutoa matusi au ukianzisha uzi wenye uhalisia na usio wa kichochezi unakuwa na hofu ya nini?

Tatizo lililopo kuna baadhi yetu tumekuwa maarufu kutunga stori za uongo na kuzijengea hoja then tunataka jamii iamini kama ni kweli kumbe ni upotoshaji

Mtu kama umeanzisha mada yako na ushahidi unao kwa nini uogope? Endapo utahitajika polisi si unapeleka ushahidi?

Fikiria mtu anayeanzisha uzi hapa eti Dangote anahamishia kiwanda Kenya na hizo habari zinasambaa dunia nzima kumbe ni uonge pasipo kufikiria negative impacts kwa wawekezeji walioko huko nje. Mtu kama huyu leo hawezi fanywa kitu sababu tu anatumia ID feki sishangai kesho akaibuka na jambo jingine

Watu wa namna hii lazima washughulikiwe hakuna kulea ujinga. Watanzania tumekuwa maarufu sana wa kupika majungu

Ninakubaliana na wewe kabisa uhuru wa kutoa maoni lazima uheshimiwe na watawala kwani ni takwa la kikatiba lakini uhuru huo lazima uzingatie utu na nidhamu.

Leo mtu akimchukia mtu flani sababu za kiitikadi za vyama au jambo lolote, kesho anamtungia tuhuma na kusambaza kwenye mitandao. Vitu vya namna hiyo siyo vya kulea
Unaongea mambo ya ajabu.
wale mawaziri waliokuwa wkiongelea sakata la Dangote na makaa ya mawe, gesi na dizeli ulisikia wakisema nini?
By the way, kupata kesi hapa si lazima uongee matusi. Ukiikosoa serikali kwa namna yoyote ya wazi jamaa analala na wewe mbele.

Ukitaka kusalimika, isifie serikali, kisha mimina mitusi mikubwa, mizito na minene kuelekea upande wa "wale wenzetu" halafu uone kama utaguswa. Sheria ina macho bwana, inaangalia rangi na sura.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom