Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Kuamini kuna maisha baada ya kifo ni umasikini wa fikira...the strongest will survive, that's why we have to fight for our rights mambo ya utalipiwa na mungu ni kukubali kuonewa ambalo ni kosa kikatiba.

In this occurrence we have different perception according to the thread..mfano kuna yule mama alie sema Binti wa mkulu alijiua, wakati tuliofahamu ugonjwa mpaka mauti tulibaki tumepigwa butwaa mzee wake wakati ule alihangaika sana kujaribu kunusuru maisha yake mmpaka kwa TB Joshua walifika then kuna mama zima linaleta uongo bado Max analilinda.

huko kungine sikujibu nakujibu Hapa...

huyo mama wala hakuleta jf sio kweli aliandik instagram kuna mtu alileta huku tena kwa kuuliza mbona yule Dada anashutuma sana vtu asivyo na uhakika Nazo

hapo unamsingizia max

Mimi imani yangu inanituma kuna maisha baada ya kufa na kuna hukumu pia kwa kila utakalolitenda hapa duniani linaandikwa

Kila mtu aamini kwa imani yake....!!
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
Ashindwe vipi tena?
Watu huku mtaani wanafurahia maisha ya kutumbuliwa na "maisha ya kimalaika".
Huyu ndie kiongozi "aliyesubiriwa kwa miaka mingi" na wadanganyika, "ni zawadi kutoka kwa Mungu" ili kuwafanya wadanganyika waamke kutoka usingizini.

Ametuletea "mabadiliko tuyatakayo" kama nitaazima msemo wa wapambiaji.

Link Serikali ya Tanzania yathibitisha ununuzi wa Ndege aina ya boeing 787

Huyu ni kiongozi anayemtanguliza "Mungu" mbele kwa yale ayatendayo, ni mpole na mwenye huruma kwa walio chini yake.

Ni kiongozi mpenda DOMO-krasia na mapangaboi. Ni mpenzi wa ndege kiasi ambacho ujengaji wa viwanja vya ndege unachapiwa kazi ya mwendokasi.

Anawapenda wapinzani na amejenga jeshi la polisi imara na wanajeshi kwa ukakamavu wao na utendaji kazi wao wa utii bila kuuliza maswali wanaingizwa kwenye utumishi wa umma (kazi za kiraia, sio kijeshi) badala ya kubakizwa makambini na maporini.

Sasa tuangalie "movie" tu itakavyoishia. Huyu Kiongozi alituomba tumwombee kwa Mungu awe na angalau robo au nusu ya uvumilivu wa walalahoi anaowaongoza sijui kama tumefanya hivyo. Kama hatukufanya ni vyema tuanze sasa kwa sababu inawezekana ametishwa kwa maono ya baadhi ya wabunge.

Lakini nini kinachokushangaza juu ya utendaji kazi au (hapana kazi tu) ya mtukufu? Mwenyewe amekiri tena kadamnasi kwamba "yeye ali-beep tu urais" na Kivuitu akapokea simu.

Sasa badala ya kuiombea amani ya nchi, inapasa tuelekeze nguvu na maombi yetu kwenye kujiombea nafsi zetu kwa sababu polisi inaomba ushirikiano kutoka kwa wamiliki wa mitandao, watu wanapotea na maiti zinaokotwa huku maisha ya kitaa yakiwa ni ya ku-enjoy wote.

Je inawezekana kwamba wanaopotea na kuonekana kwenye visandarusi ni kwa sababu ni wahamiaji haramu au ni wale walioshindwa kupiga dili? Au ni watu walioshindwa kuimba mapambio?
Haya tumsifu Mungu.
Kila nafsi itaoja mauti na ipo siku ya hukumu. Tusijisahau.


 
Kwanza huyu Magufuli hakushinda kihalali uchaguzi, nilimpinga sana na naomba sana pia ashindwe na alegee kuliongoza hili taifa, huyu jamaa tangu awekwe pale Ikulu na tume ya Lubuva amekuwa jeuri, kiburi na amejifanya kuwa mungu mtu asiyetaka kukosolewa pindi pale anapofanya makosa. Anaiongoza nchi kama anaongoza familia yake, ajue hii ni nchi sio familia na hii nchi inaitwa Tanzania ina zaidi ya watu millioni 50 kwa hiyo asijifanye ana akili kuliko watu 50m.

Naunga mkono Magufuli ashindwe na alegee, ni worst president ever

Na akijifanya kiburi zaidi tuaanza kumuandika kwa Kiingereza ili malaika (Wasaidizi) wake wamdanganye wanapomtafsiria.
mkuu, yote hayo yanakutoka kwa kuwa mkuu wa Jf amekamatawa na polisi au yanakutoka kwa kuwa unaagenda yako binafsi,binafsi nafurahi kwa kuwa unatumia uhuru wa kutoa yako ya moyoni hapa tena bila kusumbuliwa lakini bahati mbaya unautumia vibaya kwa kujaribu kuchanganya na mihemko ,yu mkini wewe ni shabiki wa upinzani umechukia magufuli kushinda ,lakini braza maneno au kauli uliyotumia kuonyesha hisia zako ni makali sana,kumbuka unayemshukia ni Rais wa nchi na hata kama wew hupendezwi naye sio kwamba unazuia kuonyesha hisia zako,lakini jaribu kuwa na staha ,jua kuna wenye mioyo kama wewe walimpenda na kumchagua na hata kama huyo lubuva alimpitisha jua na nyeye pia alimpenda ndio maana kampitisha ,

Braza uhuru huu tulionao wa walau kuandika hisia zetu tusiutumie vibaya kiasi hiki,kiasi cha kukosea heshima nafasi ya Urais kiasi hiki,Uungwana ni dawa kuliko mihemko
 
Atokeee, tumemchoka jamani, kama vipi nipeni bomu nikajitoe mhanga, nipo tayari kwa sababu sina furaha yoyote duniani hapa,, nipeni bomu
 
Dah...mambo yapo simpo tu...sheria iliishapitishwa na bunge....kazi ya polisi ni kuhakikisha sheria zinafuatwa ...Tatizo lipo wapi??..Hii sharia haiilindi serikali tu...pia mtu binafsi au Taasisi...sasa kama umevunja sheria halali unashitakiwa....unajitetea....mahakama inaamua....sasa hii fichaficha sijui hata ni ya nini.... 😡😡😡
 
Miezi michache iliyopita rais Magufuli alisema anatamani malaika ashuke [sijui ashuke toka wapi] aje kuizima mitandao ya kijamii ambayo tumekuwa tukiitumia kupashana habari na kubadilishana maoni na mawazo kuhusu mambo mbalimbali.

Baadhi yetu tuliyachukulia maneno hayo kama ishara ya mambo yajayo kuhusu uminywaji wa hii mitandao na haki ya watu kuitumia kwa kujieleza, kutoa maoni, na kuikosoa serikali.

Sasa kitendo kilichotokea jana cha kukamatwa kwa Max kimethibitisha kuwa huu utawala wa Magufuli umeazimia kutuziba midomo kwa kutumia mabavu ya dola.

Kwa hilo mimi nataka huyo Magufuli ashindwe na alegee kabisa. Sitaki kabisa afanikiwe hata kidogo na watu wote wenye akili zao timamu hawana budi kumpinga na kuifanya hizo azma yake iwe muhali.

Kupinga udhalimu ni jambo la adhama. Na huyu mtu tayari keshaonyesha dalili zote za udikteta. Hivyo tumpinge kwa pumzi na nguvu zetu zote. Kwanza ni mtumishi wetu na si vinginevyo.

Hizi siyo zama za kupelekeshana kwa vitisho. Haogopwi mtu zama hizi.

Akichemka tutamkosoa tu. Akichapia Kiingereza tutamcheka tu. Kama hana ngozi nene ya kuweza kumudu na kuvumilia kuongelewa kwa namna yoyote ile basi aondoke. Aachie ngazi.

Mtu mwenyewe kwanza hafai kuwa rais. Hana haiba ya urais, hana hekima wala busara zinazotakiwa mtu wa kiwango cha rais kuwa nazo. Kila akifungua mdomo wake mtu unaanza kuombea asiongee maneno ya kuaibisha.

Sikuwahi hata siku moja kudhani kuna mtu angekuja kumpiku JK kwenye ubomu lakini ndani ya mwaka tu huyu jamaa keshamuacha mbali mno JK. Pata picha hiyo miaka minne iliyobaki hali itakuwaje.

Huyu mtu tumdindie. Tukinywea atavimba kichwa na kujiona ana nguvu nyingi ilhali hana. Hana nguvu za kuweza kuzidi nguvu ya umma.

Kwa hiyo mimi nataka ashindwe. Tena ashindwe vibaya. Je wewe mdau wasemaje?
U.S.A Baby
 
Dah...Hata profesa!!
emoji40.png
emoji40.png
emoji40.png
emoji40.png
emoji40.png
emoji125.png
emoji125.png
emoji125.png
emoji125.png
emoji125.png
😀😀😀😀😀😀
 
Kushindwa kwa Magufuli ni kushindwa kwa watanzania wote, kufanikiwa kwa Magufuli ni mafanikio kwa watanzania wote. Nawaomba ndugu zangu tuweke utaifa mbele. Ni mawazo yangu lakini nisiwakwaze
 
Inasikitisha kuona unanukuu halafu unatua maneno yako binafsi nakudhani kuwa hiyo ndiyo maana na kusudio la Mwl. Nyerere, hambo ambalo siyo kweli, mwalimu Nyerere hawezi kuwa na maana ya kijinga kama hiyo unayojaribu kuileta, eti TANU imaanishe Jamii, n.k, kaa nakutokuelewa kwako . Sisi Wtz tunasonga mbele, hatuhangaiki na makaburi.
 
Kwa kwel mambo mengne yanayofanywa na huu uongoz unauzi sana mtu anakamatwa kwa kosa la kuikosoa serikal hiv serikal n nin jamani mbona hata sie ni serikal tunakushaul mweshimiwa legeza kamba wtu tutoe maoni yetu na tunahaki ya kuikosoa serikal kikatiba.
 
Nipo tayar kuingia barabarani muda wowowte
Yaaa ingia tu barabara ukafagie na kufyeka nyasi hakuna wa kumwingiza chaka humu hata kwenye vitabu vitakatifu Biblia imeandikwa asiyefanya kazi na asile na mikono milegevu hujenga paa bovu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom