Nataka Rais Magufuli ashindwe

Nataka Rais Magufuli ashindwe

Status
Not open for further replies.
Kwahiyo Juliana Shonza na Bashe walivyosema bungeni kwamba ule muswada haugusi mitandao ya jamii walikuwa ni waongo/walilidanganya bunge?
Cybercrime Act Imepitishwa na Bunge Tarehe 1 April 2015..By the time hao shonza na Bashe hawakuwa bungeni...Othrwise unaongelea mswaada wa sheria ya vyombo vya habari,2016
 
Unadhani hata anapoua kama kule mto Ruvu anatoa taarifa,wewe ni kichaa kama yeye.
Dada nakuona umejipinda kweli kutumia cm yako.

Watu kama ninyi ndio mmemponza Max.

Sasa kama hiki ulichoandika hapa ukikamatwa utatoa ushahidi?

Alafu kumuita rais kichaa nayo ni ukosoaji,? Ukikamatwa utasema unazibwa mdomo kweli,?
 
Huwa mm nasema kila siku wakosoaji wa Magufuli hawana hoja kabisa, wanajifanya ma griti thinka kumbe ni ujinga mtupu.

Hoja zao mara nyingi zinaegemea kwenye kumkejeli rais na kumbatiza majina ya dhihaka. Na ona mleta mada yeye amajikita kwenye hekima mara kukosea kingereza, sasa nikuulize wewe mleta mada huo ustaarabu ni upi unaotaka?

Kama ni viongozi wastaarabu alikuwepo JK na tulitokwa mapovu hivihivi.

Tujifunze sisi kwanza kuwa na heshima. Haiwezekani unachukua tu kisimu chako unaorodhesha jejeli kibao kwa rais wa nchi alafu unasema eti huo ndio ukosoaji!
Tulia huko jikoni umpikie mzee
 
Hahahaaaa....


Hahahahahahahahahahahaha
Hahahajhahahahahahahahaha
Hahahahahahahahahahahaha.

Wewe nyaningabu leo umeamka vibaya,

Aya ya 8 hiyo ,hahahahahahah.


Halafu umeamua kuweka mziki.duh!!

Nimecheka kweli leo,tena kwa sauti ya juu kabisa.
hahahahahaha
Ila mimi sichangii.
 
Magufuli ana weakness kama Kiongozi. Lazima ajifunze ku-accommodate hata wale wanaompinga au wenye tofauti na mawazo yake. Kitu ambacho ni kigumu kwa viongozi wengi wa Africa.

Having said that, bado naamini kwa dhati kabisa Magufuli ana nafasi kubwa ya kuwa kiongozi bora Tanzania. Kwa sababu anaweka maslahi ya taifa mbele. Hatujawahi kuwa na Kiongozi wa namna hiyo.

Haya ya kukamata waandishi wa habari na mengine ya kuminya wigo wa demokrasia, yanazungumzika.
 
Kwanza huyu Magufuli hakushinda kihalali uchaguzi, nilimpinga sana na naomba sana pia ashindwe na alegee kuliongoza hili taifa, huyu jamaa tangu awekwe pale Ikulu na tume ya Lubuva amekuwa jeuri, kiburi na amejifanya kuwa mungu mtu asiyetaka kukosolewa pindi pale anapofanya makosa. Anaiongoza nchi kama anaongoza familia yake, ajue hii ni nchi sio familia na hii nchi inaitwa Tanzania ina zaidi ya watu millioni 50 kwa hiyo asijifanye ana akili kuliko watu 50m.

Naunga mkono Magufuli ashindwe na alegee, ni worst president ever

Na akijifanya kiburi zaidi tuaanza kumuandika kwa Kiingereza ili malaika (Wasaidizi) wake wamdanganye wanapomtafsiria.
 
Kwanza huyu Magufuli hakushinda kihalali uchaguzi, nilimpinga sana na naomba sana pia ashindwe na alegee kuliongoza hili taifa, huyu jamaa tangu awekwe pale Ikulu na tume ya Lubuva amekuwa jeuri, kiburi na amejifanya kuwa mungu mtu asiyetaka kukosolewa pindi pale anapofanya makosa. Anaiongoza nchi kama anaongoza familia yake, ajue hii ni nchi sio familia na hii nchi inaitwa Tanzania ina zaidi ya watu millioni 50 kwa hiyo asijifanye ana akili kuliko watu 50m.

Naunga mkono Magufuli ashindwe na alegee, ni worst president ever

Na akijifanya kiburi zaidi tuaanza kumuandika kwa Kiingereza ili malaika (Wasaidizi) wake wamdanganye wanapomtafsiria.
Mkuu punguza hasira kidogo, sisi ni binadamu tunapaswa kusamehana.
 
Dada nakuona umejipinda kweli kutumia cm yako.

Watu kama ninyi ndio mmemponza Max.

Sasa kama hiki ulichoandika hapa ukikamatwa utatoa ushahidi?

Alafu kumuita rais kichaa nayo ni ukosoaji,? Ukikamatwa utasema unazibwa mdomo kweli,?
Mbona mnatishatisha watu, ili iww nini? Kwani mmezuiwa kujenga hivyo viwanda? Au ndio mnatafuta sababu ya kujitetea. Na hamtajenga hata kiwanda cha toothstick kwa woga huu mliouanza mapema hivi.
 
Kuamini kuna maisha baada ya kifo ni umasikini wa fikira...the strongest will survive, that's why we have to fight for our rights mambo ya utalipiwa na mungu ni kukubali kuonewa ambalo ni kosa kikatiba.

In this occurrence we have different perception according to the thread..mfano kuna yule mama alie sema Binti wa mkulu alijiua, wakati tuliofahamu ugonjwa mpaka mauti tulibaki tumepigwa butwaa mzee wake wakati ule alihangaika sana kujaribu kunusuru maisha yake mmpaka kwa TB Joshua walifika then kuna mama zima linaleta uongo bado Max analilinda.
Jpm wewe sio Mungu na kumbuka kuna maisha baada ya kufa
 
Sisi ni watu wazima .
Kwa nini Hawa viongozi wanatuchezea kama watoto wa chekechea? Kwa nini wanatulazimisha kufanya mambo ambayo hatuyataki?

Wanachosahau hii ni miaka ya utandawazi. Obama anasemwa vibaya sembuse Magufuli?
Waache kukandamiza watu

[HASHTAG]#freemaxencebringbackourben[/HASHTAG]
 
Hivi kwani uzush ukipotezewa shida iko wapi si muwaache watu watoe madukuduku yao jamani maana hatufanani .Mangapi yamepotezewa?Maana hata uzushi nao unaeza ukawa na ka ukweli kakifanyiwa kazi.Kusingiziana kupo ktk maisha ya kawaida na hii inatufanya tuish tukiwa makini.Hayo ya machafuko waachieni wenyewe huko.
embu jaribu kufikiria hili,wewe unasingiziwa au unazushiwa jambo ambalo halipo,mfano unaambiwa jambo baya ambayo litakuchukia na hata kukukoseshea stasha mbele ya jamii,utachukuliaje? na wakati huo jamii tayar nimeshaanza kuamini juu ya hilo jambo na kuanza kuwa na mihemko nalo,si utachukia siyo? au utafurahi na kuona ni jambo la kawaida? tafakari kwanza usione kawaida wakifanyiwa wenzako ,wewe je?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom