Mwizukulu mgikuru
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 4,730
- 11,085
Wakuu mimi ni miongoni mwa vijana wa kitanzania ambao tulijitahidi kuipata elimu huku tukiamini kupata ajira aidha sekta binafsi au serikalini, lakini mambo yakawa tofauti ni miaka saba sasa imepita na wengine tumeshaanza kusahau hata tulichokisomea kwa sababu tuliamua kufanya mambo mengine nje na elimu zetu ili maisha yaende.
Kiukweli alipokufa magufuli mimi nilikuwa ni miongoni mwa vijana waliofurahi sana, nakumbuka siku hiyo walipotangaza kifo cha magufuli mida ya saa sita usiku.
Mimi nilibubujikwa machozi ya furaha nikiamini kuwa sasa na mimi nakwenda kulamba asali, kwa sababu yule aliekuwa anazibana sector binafsi na kubana kutoa ajira serikalini ametangulia kwa hiyo mambo yatakuwa mtelezo.
Sio siri kwa sasa mambo ndio yamekuwa magumu zaidi huwezi kupata kitu mpaka utoe chochote sio tamisemi wala wizarani sio utumishi wala sector binafsi mambo ni magumu zaidi ya jana.
Kiukweli alipokufa magufuli mimi nilikuwa ni miongoni mwa vijana waliofurahi sana, nakumbuka siku hiyo walipotangaza kifo cha magufuli mida ya saa sita usiku.
Mimi nilibubujikwa machozi ya furaha nikiamini kuwa sasa na mimi nakwenda kulamba asali, kwa sababu yule aliekuwa anazibana sector binafsi na kubana kutoa ajira serikalini ametangulia kwa hiyo mambo yatakuwa mtelezo.
Sio siri kwa sasa mambo ndio yamekuwa magumu zaidi huwezi kupata kitu mpaka utoe chochote sio tamisemi wala wizarani sio utumishi wala sector binafsi mambo ni magumu zaidi ya jana.