Nataka kumuacha mke wangu

Nataka kumuacha mke wangu

Pole sana, naona unatafta jinsi ya kumpiga chini. Watakuja tu
 
Bora umuache akateseke kwa kipindi kifupi sababu pasipo shaka wala mawaa wewe ni mwanaume gubu

Narudi tena baada ya kupata maana ya neno GUBU, kulingana na chanzo nilicho kisoma, mtu mwenye gubu ni yule mwenye tabia ya kukumbushia makosa ya nyuma aliyokwisha samehe na kuanza kuyakomalia upya.

Ktk kesi yetu, hakuna msamaha wowote niliowahi kutoa maana sijaombwa, iwe ni tukio la zamani au hili jipya na sidhani kama ni sahihi kutoa msamaha kwa mtu asiejutia wala kulitambua kosa lake. Vinginevyo LIMBWATA linahusika.
 
masikini ya mungu hivi huyo dada anajua kuwa yuko karibuni kuachwa????
najiuliza tu kwani huko kwa mama ulikuwa ukiishi naye???
je ni mke wako wa ndoa???
una amini vip kwamba ni kweli ameonesha utovu wa nidhamu? maana kwa kusimuliwa tu haitoshi??
 
Nemefurahi ila ningefurahi zaidibkama ningewekewa na picha zao yani.ya mama yako na ya mke wako
 
naona unafanya maskhara na uzazi eeh. Mimba na uzazi ni kitu kikubwa. vinakuja na hormones kubadilika badilika na usipoangalia zina-create long term problems. hapo mkeo anahitaji support ya kisaikolojia, emotional, etc. tatizo mijianaume ya kibongo haitaki kujielimisha na mambo haya. MSAIDIE MKEO ACHA KUBWABWAJA!
 
masikini ya mungu hivi huyo dada anajua kuwa yuko karibuni kuachwa????
najiuliza tu kwani huko kwa mama ulikuwa ukiishi naye???
je ni mke wako wa ndoa???
una amini vip kwamba ni kweli ameonesha utovu wa nidhamu? maana kwa kusimuliwa tu haitoshi??

Huyo dada hajui lolote
Yap huko kwa mama nilikua naliishi nae kwa wiki 3 za mwisho kabla hajajifungua
Aliyoyafanya nimeyaona mwenyewe
 
Fedora;
Nimejitahidi kukufikiria mpaka nikashindwa. Weye ni mtoto au mtu mzima? Uliozwa huyu mke au ulioa kwa kujipima kwako ukaona unatosha majukumu hayo??
Mke ulimuoa mwenyewe, hukuomba ushauri wa kuoa, iweje leo uje hapa kuomba ushauri wa kumwacha? Pili; Unasema kulikuwa hakuna option ndo maana ulimpeleka kwenu japo alikuwa hataki; kwa hivyo ulimpeleka kwa lazima? Hiyo option ulio ikosa ni ipi? Kwani angeshindwa nini kujisaidia mwenyewe hapo ndani na jiko la mchina baada ya siku chache ambazo ungeomba ruksa kazini ukae naye wiki ya mwanzo?
Hujui kuchemsha nyama umtolee supu? Hujui mahali pa hoteli uweke order ya supu nyeupe mzinga mmoja kwa siku? Mbona mnajiletea balaa wenyewe?
Hukuoa umzalishe mtoto wa watu halafu umpeleke kwenyu huku ukiujua mdomo mkali wa mamako. Hiyo sio haki, Unachokiona weye ni utomvu wa adabu aliouonesha kwa mamako, yeye mama unadhani hakusema kitu baada ya kuona dharau za mwali wake? Hayo yote umeyataka mwenyewe na kumzalisha mtoto wa watu bila mpango. Miezi 9 yoote hukuwaza la kufanya. Pole sana.
Mwache wenzio wafaidi. Wadhani mtoto mmoja tu tayari kawa mzee? Wenzio wenye akili watamchukua tena very fast. Utabaki kuoa mwingine awezaye kuhimili mikiki ya huyo mamako. Oa mke utakayeweza kukaa naye weye. Akiugua umwoshe si kumpenda akiwa mzima tu
 
Kama sheria itanitaka nifanye hivyo ntatoa

Hivi wewe nae kweli ni mume! Dah hivi unafikiri kwa kutumia nn? Mmeoana lini? Running away from a problem isnot a solution to solve it! Tafuta njia ya kuyamaliza hayo matatizo hakuna mtu aliekamilika hapa duniani pengine na wewe Una matatizo yako nani ajuaye?
 
Wanajamvi, ni kama wiki tatu hivi tumebahatika kupata mtoto wa kwanza lkn kabla wife hajifungua nilimpeleka kwa mama yangu kwaajili ya huduma baada ya kujifungua, ndo ilikua mara yake ya kwanza kwenda kuishi na mama mkwe, cha ajabu kwa kipindi chote alichokaa nae ameonesha utovu wa nidhamu mkubwa.

Hivyo nimedhamilia kuachananae muda tu atakapo pata nguvu. Hivyo wanaojua sheria za ndoa na jamii naomba mnijuze ni sheria gani inaweza kunibana ktk hayo maamuzi yangu.

Asante nawasilisha tafadhali.
ukishamuacha nipm namba yake ya simu. wewe hujui kuishi na mwanamke labda kaishi na mama yako. kosa kubwa ulilolifanya ni kumpeleka mke wako kwa mama yako. sisi wenzio huwa tunawaacha hapahapa tunawatunza sisi kama kuna mtu anataka kumsaidia anatakiwa aje hapohapo kwako akae mwezi au miwili halafu asepe, usingempeleka kwa mamako kwasababu lazima angegombana tu labda kama hana akili. hakuna mwanamke unayeweza kumpeleka kwa mamako asigombane. nikwasababu mamamkwe huwa ni namba moja kuvunja ndoa za watoto wao wa kiume. hivyo naomba ukimuacha tuletee namba hapa atapata bwana mwema tofauti yako na wewe urudi kaishi na mama yako. nyambafuuuu
 
Huwa najiuliza...kwa hiyo siku zote mtu anakuwa ametulia zinaibuka baada ya ndoa? Kama ndivyo, basi itakuwa ngumu kuwalaumu kwa uchaguzi mbaya manake tabia hizi zimeshindikana kuonekana kabla. Ingawa mimi binafsi huwa naona kama tabia zinaonekana tu, huwa hazijifichi. Kosa letu huwa tunaamini kuwa...aaah..hilo tu mbona linarekebishika? Thubutuuu...

Very true.
Na waliowengi pia hufanywa vipofu kwa mvuto na upendo walionao kwa mtu. Its very good when you love by mind first before your heart because your mind will define and identity weaknesses of a person and weigh if you can tolerate them but when you put your heart to love automatically your brain won't reason even if what happens.
The results you will see them in marriage when you'll start seeing what you didn't expect.

Make sure your love is definable, you love her/him bcose of 1, 2,3 ....
 
Nifafanulie nilipokosea ili next time nisirudie kosa

1 mke hupelekwa kwao kujifungua kwani ndiko atakapopewa huduma za kutosha na mzazi wake
2 tumezowea mkeo amnapolala kwa mzazi wako anatakiwa yeye ndo aamke mapema na kusafisha nyumba kama ni tabia yetu ya mila, kwani wazazi wako wanahitaji kunyenyekewa sana na mkwe wao. ujauzito unamsumbua atawezaji kuwasaidia
3 siku zote wazazi hawakusema kua mkeo hana adabu isipokua kipindi cha kujifungua, jua kwamba ni ujauzito
4 waulize wazazi wako ni mambo gani aliyokua akiyafanya huyo mkeo, halafu mkae na kuongea. kumuacha sio solution
 

Asante kwa maelezo yako marefu na mazuri lkn bahati mbaya hukusoma vizuri hii thread, naomba urejee post chache za nyuma, zina majibu ya maswali yote uliyouliza, utapata picha nzuri kisha tuma post ingine.
Asante
 
Hivi wewe nae kweli ni mume! Dah hivi unafikiri kwa kutumia nn? Mmeoana lini? Running away from a problem isnot a solution to solve it! Tafuta njia ya kuyamaliza hayo matatizo hakuna mtu aliekamilika hapa duniani pengine na wewe Una matatizo yako nani ajuaye?

Asante kwa mchango wako.
Inaonekana bado unaishi kwa classical ideas, ukipata muda endelea kusoma post za huu uzi, kunakitu utajifunza.
 
ukishamuacha nipm namba yake ya simu. wewe hujui kuishi na mwanamke labda kaishi na mama yako. kosa kubwa ulilolifanya ni kumpeleka mke wako kwa mama yako. sisi wenzio huwa tunawaacha hapahapa tunawatunza sisi kama kuna mtu anataka kumsaidia anatakiwa aje hapohapo kwako akae mwezi au miwili halafu asepe, usingempeleka kwa mamako kwasababu lazima angegombana tu labda kama hana akili. hakuna mwanamke unayeweza kumpeleka kwa mamako asigombane. nikwasababu mamamkwe huwa ni namba moja kuvunja ndoa za watoto wao wa kiume. hivyo naomba ukimuacha tuletee namba hapa atapata bwana mwema tofauti yako na wewe urudi kaishi na mama yako. nyambafuuuu

Asante kwa ushauri wako
Hapa inaonekana ww ni mtu wa kukurupuka tu kama zuzu, Ulicho kipost ni out of point tena hata hujui wapi Pa kujenga hoja. Ukipata muda soma post chache za nyuma utapata picha nzuri nakujua nn cha kusema. Open your mind before opening your mouth.
 
1 mke hupelekwa kwao kujifungua kwani ndiko atakapopewa huduma za kutosha na mzazi wake
2 tumezowea mkeo amnapolala kwa mzazi wako anatakiwa yeye ndo aamke mapema na kusafisha nyumba kama ni tabia yetu ya mila, kwani wazazi wako wanahitaji kunyenyekewa sana na mkwe wao. ujauzito unamsumbua atawezaji kuwasaidia
3 siku zote wazazi hawakusema kua mkeo hana adabu isipokua kipindi cha kujifungua, jua kwamba ni ujauzito
4 waulize wazazi wako ni mambo gani aliyokua akiyafanya huyo mkeo, halafu mkae na kuongea. kumuacha sio solution

Asante sana kwa huu ufafanuzi mzuri japo hayo yote nimekwisha yaelezea vizuri acha nirudie tena kwa kuheshimu jitihada zako na kwa faida ya wengine.
1. Natambua kua mke hupelekwa kwao kwa huduma baada ya kujifungua, lkn kwao walikataa kwa hoja ya mila zao haziruhusu.
2. Hakupaswa kufanya shughuli yoyote ambayo mjamzito hapaswi kufanya au hata kama hajisikii, nilimuongezea muhudumu mwingine wa kumsaidia mbali na mama
3. Mpaka leo wazazi wangu hawajasema kama anatabia mbaya ila nimejionea mwenyewe hata kabla ya ujauzito na wakati wa ujauzito, maana nilikuwepo wiki 1 kabla hajajifungua na kuendelea kuwepo kwa wiki nyingine 2 baada ya kujifungua
4. Nimekua nikimuelekeza na kumuongoza juu ya hiyo tabia yake mbaya kwa muda mrefu bila mafanikio, tukio hili la sasa ni kama climax ya mfululizo wa uozo mwingi alioanza kuufanya muda mrefu.
 
Back
Top Bottom