Nataka kujenga, nina laki 5 mkononi

Nataka kujenga, nina laki 5 mkononi

Mafundi wengi wanajenga tofali moja sh.200 kwahiyo 400 x 200 = 80,000
Hivyo fundi waweza kumpa 120,000 akaanza kukujengea kuanzia msingi hadi kukumalizia chumba kimoja. Kuwa na moyo then epuka matumizi yasiyo na msingi ufikie malengo.

"ᵂᵒʳʳʸ ⁱˢ ᵃ ʷᵒʳᵈ ᵗʰᵃᵗ ᴵ ᵈᵒⁿᵗ ᵃˡˡᵒʷ ᵐʸˢᵉˡᶠ ᵗᵒ ᵘˢᵉ"
Kwa makisio ya kujenga kwa tofari moja Tshs. 200 hapa inategemea na project. Kwa kujenga chumba kimoja hapa mafund huwa hafanyi kaz kwa gharama hizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimenunua tofali 400 nimebakiwa na laki 5 natafuta mtu mwenye akili nyingi aniambie jinsi ntakavyokamilisha hata chumba kimoja na kuhamia ikibidi kabaki kachenchi hata elfu 5.
Pia nina mifuko 10 ya cement na mchanga wakutosha Karibuni
Bravo!! kwa jitihada zako.., kweli mwanzo mgumu ila utakamilisha ndoto na azma yako....hongera ndg !!
 
Hebu anza na choo kwanza alafu tuone kama kuna kinachobaki.
 
Jenga full suti ya mabati rejects mkuu....utatumia kama laki moja.....iliyobaki rudisha heshima iliyobaki baa
 
Nimenunua tofali 400 nimebakiwa na laki 5 natafuta mtu mwenye akili nyingi aniambie jinsi ntakavyokamilisha hata chumba kimoja na kuhamia ikibidi kabaki kachenchi hata elfu 5.
Pia nina mifuko 10 ya cement na mchanga wakutosha Karibuni
Kwa sababu mchanga na cement unavyo fanya hivi

Fundi = 100,000
Bati 6 = 119,000
Mbao 4×2 6 = 39,000
2×2 6 = 21,000
Mbao za kukodi kwaajili ya linta 8 = 10,000
Nondo 2 = 40,000
Misumari 2kg = 7,000
Bainding wire = 3,000
Mlango wa kawaida pamoja na frem yake = 70,000
Dirisha la mbao = 35,000

Hapa itakua bado choo tu

Achana na watu wenye misongo ya mawazo maana fedha ya kula tu utakuta inawashinda.. Ndio wajue bei ya cement?

20190124_111803.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama huyo kwenye avatar ndio wewe, nitakusaidia kujenga hiyo hela ifanyie matumizi mengine. Jukumu lako ni kunionyesha kiwanja kilipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa sababu mchanga na cement unavyo fanya hivi

Fundi = 100,000
Bati 6 = 119,000
Mbao 4×2 6 = 39,000
2×2 6 = 21,000
Mbao za kukodi kwaajili ya linta 8 = 10,000
Nondo 2 = 40,000
Misumari 2kg = 7,000
Bainding wire = 3,000
Mlango wa kawaida pamoja na frem yake = 70,000
Dirisha la mbao = 35,000

Hapa itakua bado choo tu

Achana na watu wenye misongo ya mawazo maana fedha ya kula tu utakuta inawashinda.. Ndio wajue bei ya cement?

View attachment 1003443

Sent using Jamii Forums mobile app
Zungumza ukweli utamuweka huru muomba ushauri!
Gharama zako ulizoweka hapo hakuna hata sehemu moja ya gharama za ubebaji mpaka hivyo vitu vifike sehemu ya ujenzi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesoma vizuri alichokiandika? Amevitaja vifaa alivyonavyo
Wewe utakuwa ni mmoja wa wagonjwa aina ya Tundu. Matofali 400 ndio unaita vifaa vya Ujenzi? Hata banda la kufugia nguruwe hujengi.
 
Garama ya Fundi ni 300 kwa tofali, 400 × 300 = 120000/ hiyo Hela ni nyingi sana . milango unaenda used bati una pata safi tu dukani. mbao chache plas mirunda Kazi imeisha .
 
Nenda kabet hiyo laki 5, odds zako 10 hapo ushapata M5 unaanza kujenga. Thats the risk worth taking.
 
hivi wabongo tumedanganywa na nani maendeleo ni kujenga tu,mbona wahindi wengi ni matajiri na wana biashara kubwakubwa tu lakini wanaishi nyumba za NHC.kajitu kamepata hela ya kubadilisha mboga kanataka kajenge chuma kama choo ili aonekane nae kajenga mi nilidhani utaomba ushauri wa biashara gani ufanye ili ukuze mtaje baadae utumie profit kujiendeleza hatimae ujenge ukiwa umerelux .akili ya kukremishwa mbaya sana

Jamaa sio mhindi sasa aisee ni mbongo man
 
Inawezekana . Mtafute fundi ambae ni rafiki yako kabisa alafu
Mwambie kwa sasa sina pesa ila utampa elfu hamsini 50000
Lakini utamlisha chakula
Kibarua wa kuchanganya udongo na kusogeza tofari utakuwa wewe mwenyewe
Nunua mchanga wa laki moja na nusu
Nunua cement
Na kokoto
Anzeni kazi
Bati, mlango na madirisha je anatoa wapi?
Hapo bado hesabu ya choo, kuchimba karo n.k

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujenzi kwanza . Kwa bati inategemea anajenga vyumba vingapi. Pia mlango ni rahisi anaweka wa bati tu
 
Back
Top Bottom