Natafuta mtu wa Kuniloga.

NGULI Mkuu waziri mtarajiwa MziziMkavu, huyu jamaa anataka kuwa ndege au nyoka (anataka kurogwa), utamsaidiaje ili apotee duniani kwani kachoka na maisha ya kuongozwa na CCM.
 
Last edited by a moderator:
NGULI ....ndugu yangu umeenda wete-pemba mji wa kitalii?mimi nakushauri uende huko huko pemba kuna sehemu moja inaitwa Muwambe(kengeja)then fanya lolote baya kwa wakaazi wa pale,hapo utajua kurogwa kupo au hakupo jaribu kwenda kufanya hio risachi yako huko
 
Last edited by a moderator:
Mi nafanya research juu ya limbwata hivyo natafuta mwanamke wa kunipa libwata ili kukamilisha utafiti wangu
 
Ni pm majina yako matatu na ya mama yako

Unataka kurogwa ni kati ya :

1:kifafa
2:kichaa
3:kukosa haja zote

Au upigwe na radi

NB lawama na hasara ni juu yako wewe uliejitakia
 
NGULI kukuroga huko uliko kwenda yaani ( Tanga, Sumbawanga, Pemba na Bagamoyo) Kama wewe Mkuu NGULI ni Mwanamke

ungelitembea na Mume wa Mtu moja kati ya hiyo miji au kama wewe ni Nguli ni Mwanamme ungelitembea na mke wa Mtu

basi ungelirogwa kiurahisi kabisa, Halafu ukatafuta mtu wa kukuopowa. Mimi ninakufundisha Dawa moja fanya hivi

Ukitaka kuwaona Wachawi, Mashetani na kila kitu kilichojificha duniani cha siri. Tafuta Tongo tongo za mbwa mweusi

mtoe kwenye macho kisha chukuwa hizo tongo tongo za huyo Mbawa Mweusi jipake kwenye macho yako. Basi nenda

Sokoni lenye watu wengi utawaona wachawi usiku na mchana hata mashetani utwaona. Lakini usije kujaribu shauri yako

mwenyewe ni hatari sana wakikujuwa unawaona watakudhuru.
 
Last edited by a moderator:
BINADAMU (WACHAWI) WANAORUKA HEWANI:

Kwa wale wanaofahamu haya wala hawana wasiwasi kabisa kwa kuwa wanajua kuwa mambo haya yapo na yanatokea kila siku.

Mfano katika kitabu cha " The Encyclopedia of Witchcraft and Demonology" uk 511 kuhusu Transvection (Binadamu kupaa hewani) sehemu hii inatoa uthibitisho wa namna gani binaadamu mbalimbali wanavyopaa hewani na kusafiri kwenda katika shughuli zao, ambapo wakati mwingine huwa wanasafiri kwa kupanda wanyama.

Mambo haya ya binadamu kusafiri kwa kupaa Hewani hayakuanza leo bali ni tokea siku nyingi sana hapa duniani.

Mfano kuna mtu mmoja aliyekuwa mashuhuri sana ambaye aliitwa Canon Episcopi, huyu alisema kwamba kuna baadhi ya watu ambao huwa wanaruka hewani usiku aidha kwa kujigeuza maumbo yao na kuwa kama ya wanyama au kwa kuwapanda wanyama au kwa kutumia miili yao wenyewe.

Alisema ya kuwa hao ambao huwa wanaruka na kupaa angani usiku huwa wanasaidiwa na Jini anayeitwa Diana ambaye wao huwa wanamwita Mungu wao wa Kike.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Mwanasheria wa Mfalme wa Scotland aliyeitwa Sir Charles Mackenzie mnamo mwaka 1678 na kuchapishwa katika waraka uliojulikana kama Laws and Customs of Scotland,...

Yeye alisema kuwa kuna watu ambao huwa wanapaa hewani usiku ambapo kwa wengine huwa wanajiona kama ni ndoto lakini ndio ukweli huo kuwa wanapaa na kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine.

Ulrich Molitor mnamo mwaka 1489 alisema ya kuwa kwa msaada wa Jini mtu anaweza akawepo sehemu mbili tofauti kwa wakati mmoja wengine wakamuona ya kuwa amelala na wakati huo wengine wakamuona anapaa hewani.

Watafiti mbalimbali walisema ya kuwa katika kusafiri au kupaa hewani kuna baadhi ya vitu vinavyotumika sana katika kuwasafirisha au kuwapaisha hewani.

Baadhi ya vitu hivyo ni pamoja na Ungo (au chombo chenye mfano wa Ungo mkubwa), Fimbo ya Mfagio, Kuti la Mnazi au Fimbo ndefu, Mnyama, Beleshi (Koleo) na aina ya vitu vingine vya aina mbalimbali.

Mtafiti Errores Gazariorum mnamo mwaka 1450 katika utafiti wake, alisema ya kuwa kwa watu waliokuwa wanataka kupaa hewani walikabidhiwa aina falani ya Fimbo iliyopakwa aina fulani ya Dawa ambayo ndiyo inayowawezesha kupaa hewani wale waliotaka.

Boguet mnamo mwaka 1602 alisema ya kuwa alimuona Mchawi mmoja wa kike aliyekuwa anapaa kwa kutumia aina fulani ya Fimbo nyeupe ambayo alikuwa ameiweka katikati ya miguu yake.

Kitabu kilichoandikwa na Lambert Daneau kilichofahamika kama Les Sorciers cha mwaka 1564 alisema ya kuwa Majini huwa wanawasaidia wale watu ambao huwa hawajawa wazoefu katika kupaa angani kwa kuwapa aina fulani ya Fimbo au Dawa.

Wachawi wengine huwa wanatumia wanyama kama Mbuzi, Fisi, Mbwa au Ng'ombe katika kusafiria na kupaa nao angani.

Kabla ya kuanza kusafiri Wachawi huwa wanajikapa wao pamoja na vyombo vyao wanavyosafiria aina fulani ya Dawa ambayo wengine wanakuwa wamepewa na Jini ili kuwarahisishia safari zao.

Katika safari zao za kupaa hewani kuna baadhi ya vitu ambavyo huwa vinawasababishia matatizo na mikwamo ya hapa na pale.

Mfano sehemu ambazo kuna nyumba za Ibada au sehemu ambayo watu wanafanya sala au maombi kwa Mwenyezi Mungu huwa ni vigumu kwao kupita na hata wakijaribu huwa wanapata matatizo na hata kuanguka kutoka hewani hadi ardhini.
Ili kukwepa kuanguka wanapopita katika sehemu za Kumwomba Mungu huwa wanapita kwa Spidi kubwa zaidi kuliko kawaida ili waweze kupita sehemu hizo bila ya kuanguka au kupata madhara.
Mchunguzi mmoja aliyeitwa Guazzo katika mwaka 1608 alisema ya kuwa inabidi watu watambue ukweli ya kuwa kuna watu ambao wana uwezo wa kusafiri hewani kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa msaada wa Majini.

Katika kusafiri kuna wakati ambapo wao wenyewe wanasafiri kwa kutumia vyombo mbalimbali na kuna wakati wanapanda wanyama ambao mara nyingi huwa ni Majini ambao wamejigeuza na kuchukua umbo la wanyama ili kuwasafirisha hao wachawi kwenda kule wanakotaka.

Alisema ya kuwa hiyo ndivyo jinsi inavyojulikana katika sehemu mbalimbali kama vile Italy, Spain, nchini Ujerumani na sehemu mbalimbali duniani.

Katika kuthibitisha ya kuwa watu wanaweza kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine alisema ya kuwa Mfumo wa dunia jinsi ulivyo umbwa ni kwamba unafuata amri ya Malaika bila ya kujali kama hao Malaika ni wazuri au wabaya.

Walizidi kusema ya kuwa hata kwenye Vitabu vitakatifu imeandikwa ya kuwa watu wanaweza kusafirishwa kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwani hata Biblia nayo inasema ya kuwa Shetani anao uwezo wa kumsafirisha Mtu kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.

Walitoa mfano ambao upo kwenye kitabu cha Mathayo 4: (1 – 11) Mlango wa Nne Mstari wa kwanza hadi wa kumi na moja. Ambapo panaelezwa juu ya jinsi ambavyo Yesu alivyojaribiwa na Shetani na jinsi ambavyo Shetani alivyokuwa anamsafirisha kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.

Biblia yenyewe inasema hivi:

MATHAYO 4: (1- 11)

1. Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani ili ajaribiwe na Ibilisi

2. Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa

3. Mjaribu akamjia akamwambia, ukiwa ndiwe mwana wa Mungu amuru kwamba mawe haya yawe mikate

4. Naye akajibu akasema Imeandikwa, mtu hataishi kwa mkate tu ila kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu

5. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu.

6. Akamwambia, ukiwa ndiwe mwana wa mungu jitupe chini kwa maana imeandikwa, atakuagizia Malaika zake na mikononi mwao watakuchuka, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

7. Yesu akamwambia, tena imeandikwa usimjaribu Bwana Mungu wako

8. Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake

9. Akamwambia, haya yote nitakupa ukianguka kunisujudia

10. Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako shetani, kwa maana imeandikwa, msujudiee Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake

11. Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.


Kwa mujibu wa hao watafiti walichukua sehemu hiyo ya kwenye Biblia kuonyesha ya kuwa Malaika na Shetani na hata Majini wote wana uwezo wa kumchukua mtu na kumsafirisha kutoka sehemu mojawapo kwenda nyingine.

Walisema ya kuwa Ibilisi alikuwa anamtembeza Yesu kwa kumpeleka sehemu mbalimbali katika muda mfupi kama vile Juu ya Hekalu, Juu ya Mlima mrefu kabisa na hata Roho wa Mungu naye alimpandisha akampeleka Jangwani ili ajaribiwe.

Hivyo hata Majini wanaweza kumsafirisha mtu yeyote yule kwenda sehemu yeyote ile anayoitaka tena katika muda mfupi sana kama jinsi ambavyo Wachawi na Watu wengine tofauti tofauti wanavyofanya kwa kuruka juu hewani na kusafiri, mwishoni walisema ya kuwa suala hilo ni la kweli na wala halina ubishi.

Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti yaliyoitwa Antidote Against Atheism yaliyotolewa mwaka 1653 na Henry Moore alielezea jinsi ambavyo mwanamke mmoja aliyekuwa anaitwa Magdalena Crucia alivyokuwa anaruka juu na kusafiri hewani mchana huku watu wakimuona, lakini baadae baada ya kuhojiwa sana alikuja kukiri ya kuwa alikuwa anafanya hivyo kutokana na msaada wa Majini kwani alikuwa ameolewa na kuishi na Jini kwa muda wa zaidi ya miaka Thelathini. (30).

Katika uchunguzi mwingine uliofanyika mwaka 1560 na Giambattista Porta alisema ya kuwa katika kusafiri kwa kupaa hewani, kuna baadhi ya watu au wachawi ambao wao huacha mwili wao ukiwa umelala na wao husafiri kwa roho zao tu wakati ambapo wengine wao husafiri pamoja na miili yao.

Baadhi ya watu waliuliza inakuwaje iwapo mwanamke ni mchawi alafu anasafiri kwenda kwenye shughuli zake za kichawi sasa inakuwaje kwa mume wake hawezi akaamuka na kumkuta hayupo usiku wa manane?

Katika kutafula Jibu la suala hilo, wachunguzi walisema ya kuwa hao wachawi huwa kwanza wanawapaka aina fulani ya Dawa hao waume zao kiasi kwamba hawawezi kuamka hata ikiwa vipi mpaka wao warudi kwenye shughuli zao.


Na wengine waliongeza kusema ya kuwa Mtu anapokuwa ameondoka usiku kwenda kwenye shughuli zake za kichawi basi huwa anamuacha Jini wake hapo kwenye kitanda chake ambae anakuwa anamuangalizia mambo yake yasivurugike mpaka hapo atakaporudi mwenyewe, ingawa wengine walisema ya kuwa si lazima ya kuwa huyo mchawi awe anajua ya kuwa kuna Jini pale kwani katika mkataba wao wa mwanzo ni kwamba Yeye Jini atamlinda na kumsaidia katika shughuli zake zote.




JINI HIEPATCH:
Jini huyo Ana uwezo wa kukuletea mtu aliye mbali papo hapo.

mtu akikutoroka muite huyu atamrudisha....
...................





JINI FRIMOST
• JINI Huyu Ana uwezo juu ya Wake na Wanawali na ana uwezo wa kukusaidia kuwafurahia na kukufanya umpate mwanamke yoyote au mwanamme yoyote unayemtaka

kazi kwenu mnaopenda ............................





Huyu ni JINI MAHABA wa Kike anaitwa SUCCUBI huwajia wanaume na kufanya nao Mapenzi




Jini Mahaba wa kiume akiwa Kazini ni hatari sana hawa





JINI MINOSON

Jini Minoson, ana uwezo wa Kumhakikishia Mtu kushinda katika Michezo yeyote ukiwepo wa Kamari.

Kazi kwenu mpendao abracadabra unaweza kuhimili kuzungumza nae akikukubalia huyu kila siku wewe unashinda.





Jini anayetumiwa kiuchawi huyu hapa

251979_556525097709212_1370283980_n.jpg


Haya tena Mkuu NGULI kazi kwako chaguwa unaye mtaka hapo uwe nae kila siku.
 
Nilikutana na padri mmoja aliyekuwa anafanya utafiti kwa ajili Phd yake.
Anasema alizunguka kwa waganga wote maarufu nchini, mpaka nchi za jirani kujalibu kupata taafa zake ila kati ya mambo ambayo alisema hayapo ni "UCHAWI". Anasema kuna sumu, na mazingaombwe lakini uchawa kama ule wa kudai mtu kuruka na ungo ni uongo na kwamba hakuna anayeweza.
Ni mchango wangu tu.

Huyo padri hajui kutafiti.Hivi unazunguka kwa mwizi halafu unauliza eti wewe ni mwizi akikujibu kuwa sio mwizi unatoa matokeo ya utafiti kuwa hakuna mwizi! utafiti gani huo?

Ngoja tumwambie tuliobobea kwenye hayo mambo.Kama ni padri kweli bila shaka anamjua mtu anaitwa Francis Wa ASIZI.Huyu watu waliobobea kwenye uchawi wanamjua sana.Ni katika watu wanaoheshimika sana katika fani ya uchawi.Sababu alikuwa ana uwezo wa kichawi wa kuongea na ndege hasa BUNDI NA POPO.

Na maandishi yake ya siri yanatumika sana na wachawi wapenda kutumia ndege wa kichawi aina ya bundi na popo katika uchawi.
 
Pasco huyu MziziMkavu kila mada za namna hizi lazima atuwekee mapicha yake ya kutisha!!! huyu MziziMkavu kama anatumia ile nguvu kutoka ndani basi atakuwa anatumia uchawi kuipa nguvu na sio nguvu za ki Mungu!!
Mkuu U-Tube, yote aliyosema Mzizi Mkavu kule juu ni kweli, ila hiyo listi ya majini na hizo picha ni uongo.

Hayo ya wachawi, pia kwenye mada yangu kule nimeieleza mpaka jinsi ya kutengeneza uchawi wa kuruka hewani!.
Pasco
 
Pasco huyu MziziMkavu kila mada za namna hizi lazima atuwekee mapicha yake ya kutisha!!! huyu MziziMkavu kama anatumia ile nguvu kutoka ndani basi atakuwa anatumia uchawi kuipa nguvu na sio nguvu za ki Mungu!!
Mkuu YouTube Usiogope hizo picha sio za ukweli ni picha za kutisha lakini ni uongo mtupu usiogope mimi ninatumia Dawa za Mitishamba situmii nguvu za giza usiogope kabisa Muogope Mungu kila kitu kitakuogopa wewe Dawa zangu hizi hapa chini angalia


spices.jpg
 
Ndugu zangu nawashukuru sana wote kwa data mlizoshusha hapa nimepata elimu kubwa katika huu mjadala. Na naendelea kujifunza special thanks to Pasco na Mzizi mkavu
 
Last edited by a moderator:
kuna mbunge mmoja no hatarii anaroga hadi PANYA mtafute anatokea KIGOMA
 
Ni pm majina yako matatu na ya mama yako

Unataka kurogwa ni kati ya :

1:kifafa
2:kichaa
3:kukosa haja zote

Au upigwe na radi

NB lawama na hasara ni juu yako wewe uliejitakia

Tobaaaaa..!!!
Mkuu, kuna mtu alinifanyia kitu mbaya sana mpaka leo siwezi kumsahau maishani mwangu, naomba msaada wa kumroga akose haja zote mbili, majina yake matatu nayajua ila majina ya mama yake siyajui na alishafariki tangu miaka ya 80's.
 
NGULI Acha kelele rudi tena zenji mtafute jamaa anaeitwa adui chongo(kwao donge) gegeda/tongoza waifu/binti yake halafu mjulishe then ndio tutasikiliza vizuuri hadith zako!wewe unafikiri mungu anaweza akakataza kitu kisicho kuwepo?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu U-Tube, yote aliyosema Mzizi Mkavu kule juu ni kweli, ila hiyo listi ya majini na hizo picha ni uongo.

Hayo ya wachawi, pia kwenye mada yangu kule nimeieleza mpaka jinsi ya kutengeneza uchawi wa kuruka hewani!.
Pasco

mkuu ule uzi nimeupitia sana mwanzoni na hadi kitabu (bring out the magic in your mind)nimeki order online, hope kitakuwa kimeshafika posta. lakini nimeipitia tena huo uzi leo nimekuta umevamiwa na wadini hadi nimekasirika!!! why kila kitu wana wanaleta udini udini!! hadi uelekeo wa mada umeshakwenda alijojo.

labda tumwambie Invisible asafishe wadini kwenye huo uzi , au lbd ndio vile jukwaa lake maalaum la hayo mambo "muujiza ya kweli" kama ulivyopendekeza litengwe na liwe p8.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu zangu nawashukuru sana wote kwa data mlizoshusha hapa nimepata elimu kubwa katika huu mjadala. Na naendelea kujifunza special thanks to Pasco na Mzizi mkavu

Hao uliowapa special thanks wanafundisha ushirikina sio uchawi.Ushirikina unaweza kuujua hata kupitia internet uchawi huwezi kujua kupitia internet hata siku moja.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom