Usawa huu waajiri wengi naona wamesitisha ajira, cha kufanya ndugu jitahidi kumaliza madeni na kata bajeti yako.
Kama unapoishi kodi ni kubwa sana nenda sehemu nyingine ambapo itakua nafuu.
Kwa kipato chako usiendekeze kula nje... Jitahidi uwe unakula vya kutosha nyumbani. Mzee wangu alikua anafanya hivyo na sio kwa sababu hakua na hela ila alijijengea tu hiyo tabia baada ya kuona hela nyingi inatumika kununua vyakula akiwa kazini. Utazoea tu.
Ukipata mshahara, nunua yale mahitaji muhimu ya ndani... Mf. Unga wa sembe, ngano, mchele, mafuta, dagaa, maharage.
Cha muhimu zaidi, Ongea na mkeo aanze biashara. Apike vitafunio asubuhi (skonzi, maandazi, mihogo etc.) Chochote kile... Hamtakosa vihela vya mboga. Pia afungue genge. Kama mtaji mdogo atembeze vitu vya genge ata kwenye beseni. Afanye chochote ili msaidiane.
Hakikisha unatunza vihela na huvigusi ata kidogo kwa ajili ya dharura kama ugonjwa. Yaani ata ukiweka 50 kila mwezi unaweza shangaa n mshahara huo huo unaanza kujenga.
Kuna mtu kazungumzia tenda za kubeba mizigo n.k jaribu na huko ujiongezee kipato wakati unaendelea kutafuta hiyo kazi ya kuajiriwa nyingine.
Kila la kheri mkuu!
Tusichoke kupambana.
Sent using
Jamii Forums mobile app