Natafuta kazi, maji yamenifika shingoni

X_INTELLIGENCE

JF-Expert Member
Mar 25, 2014
9,667
12,238
ndugu zangu wanajamiiforums, poleni kwa majukumu mazito yanayotukabiri kila kukicha. maisha yamenipiga Mtanzania mwenzenu, hali yangu kiuchumi inazidi kuwa mbaya kila kukicha nipo kwenye ajira sekta binafsi, lakini naishi nikiwa nimeshaumaliza mshahala kabla sijaupokea. Naona kabisa kwenye hii ajira niliyopo sitotimiza malengo yangu.

Watanzania wenzangu, nawaomba kwa moyo mnyoofu kabisa kwa yeyote mwenye kujua sehemu ambayo naweza nikafanya kazi anipe ramani hali inazidi kuwa ngumu sana kwangu.

Ujuzi wa ziada nilio nao ni Diploma ya uandishi wa Habari. Nina mke na mtoto ambao wananitegemea. Kwa mshahara ninaopata hivi sasa ikitokea bahati mbaya mmoja wetu ameumwa nitaumbuka vibaya sana kwani pesa zote zitatumika kutoa huduma za hospitali bajeti haitokidhi kabisa.

Ki makazi nipo Dar es Salaam.

Ieleweke kuwa nipo tayari kufanya kazi yoyote. Nitafurahi sana kama nitapata msaada haraka iwezekanavyo.
 
Prince Mhando,

Mwaka huu lengo kubwa la kila mmoja wetu ni kupigania uhai wake kwa maana ya kuhakikisha hupati maambukizi ya CORONA. Swala la ajira mpya mmmmm kila mtu yuko vitani kupigania uhai wake.

Kuhusu ughali wa matibabu, ishi kulingana na mshahara wako; kuna BIMA za afya za TZS 30,000 ambako utatibiwa nadhani kwenye hospitali ya Wilaya yako; ni kukosa akili ukiwa na mawazo ya kutibiwa Aga Khan wakati hata usafiri wa kukufikisha pale huna.
 
Mwaka huu lengo kubwa la kila mmoja wetu ni kupigania uhai wake kwa maana ya kuhakikisha hupati maambukizi ya CORONA. Swala la ajira mpya mmmmm kila mtu yuko vitani kupigania uhai wake.

Kuhusu ughali wa matibabu, ishi kulingana na mshahara wako; kuna BIMA za afya za TZS 30,000 ambako utatibiwa nadhani kwenye hospitali ya Wilaya yako; ni kukosa akili ukiwa na mawazo ya kutibiwa Aga Khan wakati hata usafiri wa kukufikisha pale huna.
Asante kwa ushauri. Kwa Dar es Salaam bima ya kaya ni kuanzia 150,000/=
 
Ndugu Prince Mhando

1. Je, kazi yako ya sasa unapokea take home kiasi gani?

2. Ungependa kazi unayoitamani walau wakulipe kiasi gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu, nafanya kazi kwenye kampuni ya ulinzi. Mshahara baada ya makato unafikia 230,000/= kweli kidogo cha halali lakini kwa maisha ya Dar es Salaam huku nina familia inayonitegemea, inanipa mawazo sana. hapo hapo kodi, usafiri wa kunifikisha kazini, bado kazini sijala na nyumbani hiyo hiyo ndio tunayoitegemea. Nawaza hadi nachanganyikiwa.
 
N- dugu yangu nafanya kazi kwenye kampuni ya ulinzi...mshahala baada ya makato unafikia 230,000/= kweli kidogo cha halali lakini kwa maisha ya dar es salaam huku nina familia inayonitegemea ... inanipa mawazo sana...hapo hapo kodi, usafiri wa kunifikisha kazini, bado kazini sijala...na nyumbani hiyo hiyo ndio tunayoitegemea....nawaza hadi nachanganyikiwa
Hapo kweli ndugu mshahara ni mdogo sana.

Inabidi upate plan better, namaanisha tafuta chanzo cha ziada kupata kipato zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lakini mkuu nadhani bado maji hayafika shingoni Kama unavyodhani. mimi hata mlo wa Mara moja kwa siku sometimes nakosa. Nimehangaika Hadi nimekata tamaa ya kuishi. Wewe una uhakika wa laki mbili kwa mwezi alafu unasema majiyamefika shingoni?! Acha kabisaa kufuru mkuu

Sent from my Infinix X650B using Tapatalk
 
Ishi kulingana na kipato chako, punguza matumizi yasio ya lazima naamini hiyo hiyo dar wapo ambao wanaishi kwa pungufu ya huo mshahara unaopata kwa mwezi na wanafamilia pana zaidi yako.

Ukifanikiwa kupata kazi ya ziada ni vyema zaidi lakini ishi kulingana na hicho kipato chako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sana ndugu yangu kwa mawazo yako
 
Back
Top Bottom