Natafuta binti Salaf wa kuoa

Natafuta binti Salaf wa kuoa

SIYO KILA ANAYEVAA HIJABU ANAZOSIFA ZA KUWA MKE TU KWASABABU NI MUISLAMU. WENGINE NI WASHENZI KULIKO HATA MA BAR MAID. KUWA MAKINI SANA NA HIVYO VIGEZO

Yeye anataka mwanamke anayefuata Manhaj Salaf. Hajasema mwanamke tu Muislam anayevaa Hijaab. Au umeona kasema hivyo? Halafu unataka kusema nini? Yaani kwa sababu tu kuna baadhi ya wanawake Waislam wanaovaa Hijaab na wana tabia mbaya ndio asitafute Mwanamke Muislam aliyeikamata Dini yake na anayeufuata Uislam sahihi (wa Qur-aan na Sunnah juu ya Ufahamu wa Wema waliotangulia)?

Yeye anazingatia usia wa Mtume (Swala na Salamu ziwe juu yake) wa kutafuta mke mwenye Dini. Allah Amfanyie wepesi kwa hilo.
 
Masharti mengi, si uzae wako..

Unaanza kututajia maneno ambayo hata hatujawahi sikia, mahajil salaf sijui, Kwanza utakuwa gaidi wewe..

Ndiyo mliofurumishwa gaza, utasemaje unapatikana dar na mikoa ya karibu.. yaani huna makazi maalum..

Kwanza ningekuwa nakufahamu ningekulisha🐷🐖

Uzi haukuhusu achana nao. Sio unakuja kuwamalizia watu stress zako hapa.
 
Wako wengi misikiti ya ki Sunna wanasoma jion utawakuta wamevaa nikab tengeneza bond na Imam akuonyeshe alietulia upambanie huku jf hachelewi mwanaume kuvaa nikab akajifanya ndo huyo mwanamke Salafi
Yaah njia rahisi ni hii.

Japo pia wengi huangukia pabaya, hawa wanawake wa kutafuta kwa namna hii, huwa inakua jau sometimes.
 
Huenda huujui Usalafi. Wengi wanaouchukia Usalafi ni kwa sababu hawaujui na wamemezeshwa chuki. Masalafi wanaupiga vita mno ujinga katika Dini. Elimu ya Dini kwao ni kipaumbele.

Halafu tuache kumharibia ndugu yetu uzi.
Kama unae dada yako mpe😀
 
Kama wewe ni Muislam mche Allah ndugu yangu. Chuki zisikuendeshe
Ni kama hao wakujiita salafi dini waliipokea moja kwa moja kutoka kwa mtume....KWANI YEYE HANA SALAFI WENZIE? HAWANA WANAWAKE? Hata wao kwa wao sasa hivi hawaozani kwa misimamo yao ya hovyo hovyo!
 
Ni kama hao wakujiita salafi dini waliipokea moja kwa moja kutoka kwa mtume
Masalafi wanaufuata Uislam ulioachwa na Mtume (Swala na Salamu ziwe juu yake) ambao hata mimi na wewe wote tunalazimika kuufuata na kuacha yaliyozushwa katika Dini. Sijui kwanini umeandika hivyo hapo! Kwani sisi tunatakiwa kumfuata nani kwenye hii Dini Tukufu ya Uislam? Unajuwa kuwa Uislam aliouacha Mtume (Swala na salamu ziwe juu yake) na wakaushikilia Maswahaba zake (Allah Awaridhie) bado upo na ukahifadhiwa kizazi kwa kizazi mpaka leo? Wapo watu waliosimama katika njia ya Maswahaba tokea enzi zao mpaka leo na wakapambana na kubainisha yaliyozushwa na yaliyotaka kuingizwa katika Uislam ambayo hayapo na Uislam Sahihi ukabaki mpaka leo.


....KWANI YEYE HANA SALAFI WENZIE? HAWANA WANAWAKE?
Kaamua kuja hapa akidhania wapo Masalafi ambao watamsaidia katika jambo hili jema.
Hata wao kwa wao sasa hivi hawaozani kwa misimamo yao ya hovyo hovyo!

Nani kakuambia hili kwamba hawaozani wao kwa wao?


Usalafi ndio Uislam Sahihi. Mapungufu binafsi ya Masalafi mtu mmoja mmoja hayaondoi ukweli kuwa Usalafi ndio Uislam Sahihi na ndio Haqq na Masalafi ndio watu wa Haqq hata kama wao sio infallible.




Hata hivyo tungeacha uzi ubaki katika lengo lake.

Allah aniongoze mimi na wewe katika njia iliyonyooka, Allahumma Aamiin.
 
Sheikh nakuombea Allah akufanyie wepesi ila kwa kupitia humu sidhan,wanawake wa hzo sifa ulizotaja majukwaa kma Haya ni nadra sana kumkuta....labda mtu wa humu aone Hili tangazo Amwambie huyo mlengwa ila si directly kumpata humu.
Sheikh kwa uzoefu wangu wanawake walioonyooka hivyo Huwa Sio watu wa mitandao,humu utapata tu "waigizaji"....utapewa intro Pale mwanzo tu,kivumbi subiri kma miezi mitatu hv utaelewa na utajuta kutafuta wanawake kupitia humu.
Humu Labda tafuta mke upambane umkunje/umfunze mwenyewe,hzo sifa za huyo uliyemchora hapo juu utakaa sana sheikh wangu.
kusema ukweli huyo hata mtaani kumpata ni shughuli.
 
Mashariti yote hayo utakuta huyu sheikh ubwabwa, kazi kuuza uji msikitini.
Muache watoto wa watu wapate watu sahihi nyie endeleeni kupiga soga vijiweni.
 
Mbona hujaweka bank statement sheikh 😜
 
Akisha kuepo anaolewa chap sana mtaani maana nyuki wanapenda maua mazuri matulivu.
Inshort binti akiishika Manhaj salafy vzr haswaaa, basi ndoa kwake ni swala la kugusa tu.
Hahah halafu shughuli ni kwamba hakuna atakayekwambia ukimtuma mtu akienda akiona mazingira yalivyo anakuzunguka anachukua yeye, vinginevyo ndoa simple ataipata mtwara na lindi tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom