Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,947
- 95,237
Twambie basi usiishie kwenye ndoto zako pekee yakoNasikia sauti ktk moyo wangu ina niambia kuna jambo lasiri sana linaendelea ktk siasa za Tanzania.
Jambo hili hata mimi sijuwi ila yatupasa kuliombea taifa kwa machozi na damu.
Kuna kimya chakutisha sana tena kutoka kwa wenye roho za hili Taifa, kuna giza nene limeikumba nchi na tunaiyona nembo ya taifa tu ikiwakawaka ktk moyo wa Taifa...
Ukimya huu huwezi kuuwona wala kuhisi kama nimwanadam wakawaida. Ila mimi naona nakuwathibitishia kalitafute neno au andiko lamzee yeyote unaye mjuwa mwenye hekima na alie shiba siri za taifa hili... Ukiliona rudi hapa uniambie mm nitapeli.
Kama ni mchezo wa draft basi mchezeshaji wa hii draft atakuwa na nguvu za ajabu maana draft inameza kete na draft inatoa mlio wa ajabu pindi kete zinasukumwa....
Hakuna anaye shituka wala kudhania kesho yaweza ikawa juu chini na chini juuu...
Mtikisiko ulio ikumba Dodoma sasa unaenda kuwa mtikisiko mkubwa zaidi kwakuwa serikali inaongozwa kwa siri na wengi hufa na siri zao.
Basi tuliombee taifa.
Epuka kuongea au kumsuta mwenzako ukijuwa unaye msuta hujuwi kama vile wewe hakujuwi.
Nawaona wana kijani wanaongea sana nakudhani kuanguka kwa Ndugai ni fursa ila nataka niwaambie huu ndio mwanzo wa utungu.
Yapo mambo hatuyaoni ila sasa yataonekana.
Yapo mambo hatujuwi ila sasa yatajulikana.
Wakati haya yanaendelea mataifa yenye nguvu duniani yanafuwatilia kwa ukaribu kile kinaendelea ktk siasa za Tz.
Pray for Nation. Amen