Napinga IGP Sirro kukutana na Vyama vya Upinzani kwasababu hana hadhi ya kuwa mpatanishi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,703
218,239
Kwa miaka yote tangu ateuliwe kuwa IGP, Mtukufu Sirro amejipambanua kuwa upande wa CCM, huyu ndio chanzo cha vurugu kwenye harakati zote za kisiasa za vyama vya upinzani, ameshiriki kuvuruga, kuumiza na kuua Raia wasio na hatia kwenye mikutano na maandamano ya amani ya vyama vya siasa yasiyo na vurugu zozote.

Ametumika sana na Serikali ya CCM kudanganya raia ili kunufaisha chama chake cha CCM, NENDENI TUNDUMA MKAJIONEE UNYAMA WALIOFANYIWA CHADEMA, Mauaji ya Akwilina na utekaji wa MO ni ushahidi wa uongo wa wazi na wa kishamba sana wa Simon Sirro, kama yeye mwenyewe au mpambe wake anabisha ajitokeze hadharani .

Mtesaji mkuu wa Wanasiasa wa Tanzania kwa awamu ya 5 na hii ya 6 ni Simon Sirro kupitia Jeshi analoliongoza la polisi , kwa kadri ya kumbukumbu zangu sijawahi kuona vurugu zozote za kisiasa zilizoanzishwa na upinzani, bali nimeshuhudia utesaji , manyanyaso , wizi wa kura wa aibu sana na utekaji wa viongozi wa upinzani ukisimamiwa na Jeshi la polisi lililo chini ya Sirro.

Mtu wa namna hii hana uwezo wa kuitisha kikao na vyama vya siasa vya upinzani kwa namna yoyote ile si tu kwa vile hana MAMLAKA YA KISHERIA YA KUFANYA HIVYO , Bali pia haaminiki na anao upande wake wa yule aliyemteua ambaye ni Mwenyekiti wa CCM.

NASHAURI CHAMA CHANGU CHA CHADEMA KUTOHUDHURIA KIKAO CHOCHOTE KITAKACHOITISHWA NA SIMON SIRRO akiwa yeye binafsi ama akivaa cheo cha IGP.

NAKALA: John Mnyika

=========
Maoni ya Tundu Lissu kuhusu jambo hili haya hapa .

 
Naunga mkono hoja kwa asilimia 100

Huyo Sirro hana "credibility" ya kuhudhuria kikao hicho.

Ingawa pia huyo Mutungi naye tuhisi kuwa ametokewa na Roho Mtakatifu Hadi kufikia uamuzi huo??

Kwa kuwa na yeye pia hana "credibility" ya kuitisha kikao hicho kwa namna na yeye pia alivyo-side na upande wa Chama tawala Katika kipindi chote, tokea ateuliwe kwenye nafasi hiyo nyeti Sana hapa nchini

Au tuite kuwa kuna shinikizo kubwa kwenye Jumuia ya Kimataifa ndiyo imemfanya huyo Msajili wa vyama vya siasa apige hiyo U-turn yake??

Kuna maswali mengi yanayokosa majibu kwenye huu mwelekeo mpya wa Msajili wa vyama vya siasa
 
Siro hajaitisha kikao na vyama vya siasa. Msajili ndiye aliyeitisha kikao hicho. ( siku nyingine andika vizuri ,uache kupindisha kama gwajiboy)
Bila kujali matokeo ya hicho kikao, nawashauri mhudhurie ili angalau mpate sababu za reactions zenu baadae.
 
Siro hajaitisha kikao na vyama vya siasa. Msajili ndiye aliyeitisha kikao hicho. ( siku nyingine andika vizuri ,uache kupindisha kama gwajiboy)
Bila kujali matokeo ya hicho kikao, nawashauri mhudhurie ili angalau mpate sababu za reactions zenu baadae.
Kila mtu anajua kusoma
 
Hakuna kikao cha aina hiyo. Labda wamwalike Augustino Lyatonga Mrema (TLP) atadudhuria. Sisi wengine hatuoni umuhimu wa kikao cha namna hii wakati huu.

Tuendelee kuitisha makongamano mpaka dunia ione ushenzi na unajisi wa katiba unaoendelea Tanzania. Makongamano haya yaitishwe kwa wingi zaidi na yalenge maeneo ambayo dunia itaona kwa urahisi ukandamizaji wa polisi.
 
Hakuna kikao cha aina hiyo. Labda wamwalike Augustino Lyatonga Mrema (TLP) atadudhuria. Sisi wengine hatuoni umuhimu wa kikao cha namna hii wakati huu.

Tuendelee kuitisha makongamano mpaka dunia ione ushenzi na unajisi wa katiba unaoendelea Tanzania. Makongamano haya yaitishwe kwa wingi zaidi na yalenge maeneo ambayo dunia itaona kwa urahisi ukandamizaji wa polisi.
Itisheni tuwavunje viuno! Hivi Katibu Mkuu wenu yupo? Siku hizi kaacha hata kuhamasisha maandamano ya kwenda Kisutu kwa Mwamba
 
Vyama vya siasa vipo kisheria, mikutano na kongamano na vyenyewe vipo kisheria, polisi wanahusikaje huko?

Jukumu la Polisi ni usalama wa raia na mali zao, kinachopelekea kuvamia mikutano ya vyama vya upinzani ni kipi?

Mbona mikutano ya CCM hawasogelei?

Tanzania bila Katiba mpya, migogoro/uonevu/uvunjwaji haki za binadamu hauta koma.
 
Washiriki watakuwa ni Mrema, Cheyo, Ayatollah Zitto na yule Shibuda.
Hakuna kikao cha aina hiyo. Labda wamwalike Augustino Lyatonga Mrema (TLP) atadudhuria. Sisi wengine hatuoni umuhimu wa kikao cha namna hii wakati huu.

Tuendelee kuitisha makongamano mpaka dunia ione ushenzi na unajisi wa katiba unaoendelea Tanzania. Makongamano haya yaitishwe kwa wingi zaidi na yalenge maeneo ambayo dunia itaona kwa urahisi ukandamizaji wa polisi.
 
Mkuu maccm na Serikali yao haramu wako katika pressure kubwa sana wamebaki kuhangaika kutoa matamko fyongo. Polisiccm na kukutana na vyama vya siasa wapi na wapi!!! Kwa kifungu kipi cha sheria za nchi au katiba ya nchi.
Vyama vya siasa vipo kisheria,mikutano na kongamano na vyenyewe vipo kisheria,polisi wanahusikaje huko?
Jukumu la Polisi ni usalama wa raia na mali zao,kinachopelekea kuvamia mikutano ya vyama vya upinzani ni kipi?
Mbona mikutano ya ccm hawasogelei?
Tanzania bila Katiba mpya,migogoro/uonevu/uvunjwaji haki za binadamu hauta koma.
 
Back
Top Bottom