Hahahaaa! Kwanza niseme hili la kijinga kabisa kuzungumzwa na watu wazima katika mjadala wa siasa ya nchi lilianzishwa mwaka 2003, wengine hata siasa mlikuwa hamjui ni kitu gani. Lengo likiwa kujaribu kumzuia Nape asiwe Mwenyekiti wa UVCCM, wanaweza kurejea enzi hizo na mpambano ule. Na hili la 2003 linaweza kuwa shule nzuri kwa wale wanaosema Nape katokea wapi, mbona kama kakurupuka tu!!!
Lakini hivi leo nikiitwa Nape .... Inabadili vipi msimamo wangu juu ya matumizi mabaya ya rasilimali za nchi? Maana ndio jambo linaloumiza watu vichwa hasa baada ya kuona ni msimamo usioyumba, hata nikifa leo mbegu niliyoipanda haitapotea, waadilifu na wazalendo watasimamia hili bila kuchoka....
NI KAZI KUBWA SANA KAMA SIO KUTOWEZEKANA KABISA KUTAFUTA MATOPE KWENYE SAKAFU SAFI, BAADA YA KUKOSA MATENDO YA KIFISADI KWA NAPE KWA MUDA WOTE WA SIASA ZANGU ZA KITAIFA, WANABUNI HATA UPUMBAVU ILI MRADI WAMTAJE NAPE WAPATE USINGIZI. NITATETEA RASILIMALI ZA NCHI YANGU MPAKA MWENYEZI MUNGU, NASISITIZA MWENYEZI MUNGU AKIAMUA KUNICHUKUA.
Maneno haya yanaongeza tu morale ya kufanya kazi hasa kwakuwa ni ya kijinga, isipokuwa yananithibitishia kuwa nimepiga kisu kimegusa mfupa so nikiongeza nguvu kidogo naweza vunja mfupa uliowashinda wengi wakaishia kulamba asali mwambani..
Hakika Nape your Brave Boy na unakazi, fahamu hayo ndio maisha yetu Watazania na Taifa letu tuliopofika kuwa hata asiyefaidika na Pesa za Kifisadi naye uamka kutetea ufisadi au kumtetea fisadi,na ndio maana kwenye mitaa yetu utakuta mwanaume mzima kasimama kwenye vilinge vya kahawa "eeh fulani mjanja sana ana hela mbwa haluki".Tumepotea hakika kama Taifa tunaitaji watu ambao ni BRAVEl akini wakati wanatenda mambo ya kutusaidia kutoka kwenye matatizo ya kiataifa dhidi ya UFISADI wataonekana kama Wendawazimu.
Na ndio maana Mwalimu alisema kulitetea
Azimio la Arusha kunaitaji mwendawazimu,hakika mwendawazimu wa leo ni wewe!!!!!!!!na kwa kuwa ni mwendawazimu wa faida ya wengi hakika Mungu atakuwa nawe.Na wanaokuna katika picha ya wendawazimu watakuja kujua faida zake pindi wtakapoona kumbe ufisadi ni laana, uovu na kutokumjua Mungu, a mwisho wa uovu ni aibu.
Kwa wale wanaokuzodoa kuhusu Mzazi wako kati ya Pro na Brigedia,hakika kama kweli wanaondika thread humu ndani za mada kama hiyo nao wakajiita ni great thinkers basi ni aibu sana.Kwa msomi mwenye ulewa akipewa profile ya watu wawili Pro na Brigedia kisha akaambiwa atoe jibu la haraka kuw Nape mtoto mdogo anaepigana na kuangaika na mafisadi wenye fedha nyingi na majina makubwa na achoki kupiga kelele kuwahusu pasipo woga atakuwa ni mtoto wa nani.
Hakika kwa msomi yoyote kwa maana ya intellectul jibu litakuwa Brigedia kwa kuwa inajukulikana kuwa watoto ulithi genetical asilimia 80% ya tabia za wazazi wao na asilimia ishirini 20% uwa ni mazingira [Environment].Ukiona wapuuzi wanakuja na hoja zisizo na mashiko jua maji shingoni na vyanzo vya style waliojenga ya kuishi kwa kutega majungu vinakaribia kushika ardhi toka walikokuwa.
Kwenye nyekundu nimepapenda kwa kuwa wenye ufahamu wa hayo ni wachache sana, wengi wenye tabia za kifisadi na matendo ya kifisadi uwa wanalala wakiota kusikia mabaya yakitokea kwako na pengine wengine wakiendesha mambo mabaya dhidi yako pasi ufahamu wako wewe,lakini kwa kuwa Mungu anasababu na wewe basi wanaishi kukuona kila siku unawaenyesha, hakika siku zote nasema UFISADI utaondolewa na style ya
SISIMIZI KUINGIA KWENYE MKONGA WA TEMBO.
Mtu mwenye Mungu ndio uweza kuiona picha hii,kwa kuwa kama ujui Mungu ufanya kazi vipi ndio hivyo hivyo watu hawajui Unavyofanya kazi ya kupambana na mafisadi [David na Goliath].Na Mungu siku zote anapowaibisha watu wenye mamlaka na nguvu kubwa duniani zenye ouvu mkubwa kwa watu wake utumia watu wanaonekana hopeless na wenye sifa zenye utata kwenye jamii,ambazo Mungu uzianda kwa kuwa anajua zitatumika wapi.
Hivyo kwa Mafisadi ili isiwe aibu kubwa ni vyema kuwai mapema na kutubu kwa viongozi wao wa dini na kuludisha mali zote walizoibia Taifa,na kuachana na siasa,au kusubilia adhabu ya Mungu ya aibu.
Nape kwenye msisitizo wako nami nasisitiza ni kwa Mapenzi ya Mungu na si Mapenzi ya Mwandamu au Wanadamu,japo wanaumia sana kwa kuwa hawajui kwanini aiwi kama wanavyotaka kuna nini?Napapenda hapo kwa kuwa uwa ni siri ya watu wa Mungu Tu.