impongo
JF-Expert Member
- Feb 18, 2015
- 8,732
- 7,611
Njaa mbaya lakini uzalendo ni jambo la msingi inasikitisha mwakyembe MTU mzima msomi wa PhD hajitambuiNjaa mbaya Mkuu
Njaaa
Sipati picha na huwa siamini kama inchi hii itaendelea, ni ngum
Njaa mbaya lakini uzalendo ni jambo la msingi inasikitisha mwakyembe MTU mzima msomi wa PhD hajitambuiNjaa mbaya Mkuu
Njaaa
Mkuu serikali nzr ni ile inayojali Ushauri na kuwa na weledi wa hali ya juu.. Ili kupata kuungwa mkono na wananchi ambao ndo waliokupigia kura na kukufikisha hapo ulipo! In short hao ndo waajiri wako.. Hivyo mahusiano Kati ya mwajiri na mwajiriwa yanatakiwa kuwa mazuri hasa mwajiriwa kufuata matakwa ya mwajiri... Unapoleta Kiburi na kukurupuka katika maamuzi yako italeta picha mbaya kwa mwajiri wako! Suala la Nape na Bashite kwa mtu yeyote mwenye weledi asingemchomoa Nape akamwacha Bashite.. Hata ungekuwa wewe mkuu.. Tuwe wakweli tu katika hili! Mkulu kachemsha tena sana tu!
Anaendelea na maisha yake atakayo kuwa kapangiwa na Mungu wake aliyehai. Nitaendelea kumuunga mkono kwani Mungu wake huwa hamuongozi katika kuharibu.Akipigwa chini we ndo wakwanza kumtosa.
Samahani MKUU ww ni mmakonde ati?
Kama hamjapendezwa, 2020 mna muda wa kubadilisha Serikali, na kumuweka Nape wenu au yoyote mnayemtaka, sasa kelele za nini?
Ni Paulo Makonda, mkuu wa mkoa wa Dar, ndo alifoji vyeti, haya niletee huo moto.Mmh! Mnahangaika kuzunguka mubuyu c utaje tu jina uone moto wake, hahaa huu ni moto wa kifuu
2020 ya nin
Kama wewe unanufaika na bashite kwenye hizo deals zenu za kuwatisha watu na kuchukua pesa kwa mgongo wa dawa za kulevya hiyo ni juu yenu
Huwez kutupangia..nchi hii walipa kodi ni sisi na tunayo saut ya kusema pale jamaa zenu wanapofanya madudu
Kwan we ni msukuma wa wapi..mbona akili zako finyu sana
Jiandae!Ni Paulo Makonda, mkuu wa mkoa wa Dar, ndo alifoji vyeti, haya niletee huo moto.
Cheti cha daudi bashite kina nin hadi kiwe gumzo kias hicho?
Suala la uvamiz wa clouds media ule ushahid wa camera za cctv hautoshelez kwa mwakyembe kuchua hatua?
Mimi nawaza tu.
Una baba, mtoto unaemtegemea au jitu somi kabisa lakini siku moja unafuatilia nyendo zake mitandaoni unakuta komenti kama "hahahahaha Mange we kiboko, Juma Pondamali Maharage, Bashiteee, utaisomaaa " kwanza jua huyo mtu ana element za ushoga au usagaji na tapu tapu hajielewi, umasikini mpaka takoni anahimili hela ya bando tu. Mtu yuko MTWARA au MOSHI huko na yeye halali kakomaa BASHITE, BASHITE , VYETI VYETI - Ninyi mbona vyeti vyenu hamviweki wazi mitandaoni mkaonesha mfano au WAULIZE WAZAZI WAKO na wao wakuoneshe VYETI VYAO Kwanza ndo uulize vya WANAMUME KUTOKA LAKE ZONE
Elo wa..nangu mmakonde
Kuchidachi..unindolee nangu mmang'wanyu eeeh
Nguholoka Nannyanga...Kutahimba..!
Kuna member mwenzetu humu JF aliandika uzi ambao uliegemea kwenye maudhui kuwa Nape Nnauye ana matatizo ya kisaikolojia kias cha kumpelekea mheshimiwa huyo kila mara kuonekana akikumbuka mambo mbali mbali hususan yanayohusiana na juhud zake ambazo amekuwa akizifanya katika kukipigania chama,hadi kilipomuingiza Juma Poor Manager madarakan hadi kwa yeye kuchukua nafasi ya uwaziri na baadae kuondolewa kwa hila kutokana na kumshikia bango Daudi Bashite katika suala la Uvamiz wa Clouds media group hali iliyopelekea taharuki na hasira kali kwa wananchi na Tasnia ya habari kwa ujumla.
Mimi nachoweza kusema ni kwamba Nape hana tatzo la kisaikolojia...
Kwa sisi wamakonde tunaweza kusema kwamba hana Ntimanyongo..ila kitu kinachomzonga akilini mwake ni kwamba kuna kosa gan ambalo amewahi kulifanya hapo awali dhidi ya Juma Poor Manager hadi afikie hatua ya kumtafutia sababu ya hovyo kabisa ya kumwondoa kwenye position ambayo yeye ameihudumu kwa weledi wa hali ya juu sana i.e ya uwazir wa habari mpaka hatua ya mwisho kabisa katika position hiyo?
Kwanza,ameihudumu ofisi hiyo katika hali ya utiifu sana kwa upande wa serikali hii naweza kutolea mfano kwa tukio la yeye nape hadi kufikia hatua ya kutukwaza sisi wananchi kwa kusimamia ajenda ya kuzuia bunge lisioneshwe live ili mradi tuh amfurahishe Juma Poor Manager hata kama akijua kwamba mamillion ya watanzania hawamuungi mkono.
Pili alisimama kidete kwa wahanga wa sakata la daudi bashite i.e wamiliki wa vyombo vya habari na kuhakikisha anaipigania haki yao na kuhakikisha pia image ya serikali na Rais wake asie msikivu inalindwa na kuweka hali ya hewa kuwa sawia..
Lakin pamoja na juhud zake hizo bado akaonekana ni mtu asiefaa na ambae anatakiwa kuondolewa mara moja ili hali daudi bashite ambae hakuwa na haki ya kubakia hata kwa sekunde moja kwenye nafasi aliyopo amee delea kuwepo tena kwa kusifiwa na yule yule aliemtengua yeye katika nafas ambayo kiukweli amefanya kadir ya uwezo wake woote kuthibitisha kuwa hakupewa nafas ile kama ahsante bali amedeserve na ameonesha viwango vilivyostahili...
Hali hii kibinadam yeyote yule lazima ingemsumbua kama inavyomsumbua nape na kumweka katika mabano kwamba kuna nin?kuna kipi ambacho amekikosea na amefichwa kuelezwa?
Maana kwa mantiki ya kawaida kwa alichokifanya hata yeye Juma Poor Manager moyoni mwake anajua fika kuwa ni sahihi na hata daudi bashite anafaham fika kuwa kama kuzingua basi kazingua na kupitiliza.
Lakin kwa vyovyote vile iwavyo..Daudi bashite achukuliwe hatua leo au hata aachwe hatakuwa na mwisho mzuri ndan ya utawala wake alionao hiv sasa pia hatakuwa na mwisho mzuri kwa jamii anayoiongoza vile vile.
Ametengeneza taharuki kwa viongoz wengine waliobakia kuanzia kwa makamu wa rais,waziri mkuu na hata mawazir wengine mfano tumeona hata mwakyembe akifyata mkia.
Pia ametengeneza taharuki kwa wamiliki wa vyombo vya habari ambao hivi sasa wao na yeye ni kama panya na paka katika mahusiano yao ya kila siku.
Nape Nnauye kikubwa yeye afaham kwamba kipo kilichomuondoa tuh ukiachilia mbali hili la daudi bashite
Kwa kuwa hili alilifanya nape kwa daudi bashite hata Juma Poor Manager anafaham kabisa kuwa yupo sahihi.
Muda Utaeleza wenyewe...Daudi Bashite hauna mwisho mzuri.
Utakuwa mangi wewe. Nawajua tuYani uneonyesha busara ya chini kuliko hata huyo bashite unayemkingia sijui nini, ila una haki ya kutoa yaliyo kichwani mwako. Eti na wewe ni Mtanzania mleta maendeleo
Sasa unasubiri nini kuchukua hatua dhidi ya unayemuita bashite kelele humu hazikusaidii, Kama una cha kufanya fanya siyo kupiga kelele humu hutafanikiwa watu wanataka matokeo ya kazi yake tu siyo vyeti vyake, nyinyi wenye vyeti safi mmefanya nini? Si mmeishia kuwa wezi tuI am real telling you.
We aint gona keep quite with this hata iweje.
Daudi Bashite hawez vamia kituo cha habar kwa mitutu ya bunduki then akaachwa hiv hiv eti kwa kuwa ana protection ya Juma Poor Manager...no one is above the law.
Daudi bashite hawez kuachwa anadunda na madaraka ya kulevya town hapa huku akila kiyoyoz cha jasho la kodi yetu huku wengine wakiondolewa kwa kufoji vyeti hivyo hivyo alivyofoji daudi bashite hilo hatutaliacha hivi hivi
Daudi bashite hata akijifanya kutafuta sympathy kwa kutumia mgongo wa madawa ya kulevya kwa sasa haitawezekanika tena
Hatuhitaj tena double standards katika hilo
Kaa ukijua na kama kakutuma umtetee nenda kamfikishie salaam
wewe huyo ulikuwa unamwita Nape vuvuzela
wewe hayo hautaki kukubali alikosea
"kilichotokea kwa Nape sio habari ya kuwa right or wrong...simply ni kutofautiana na bosi wake"
wala haihitaji essay kujua kuwa lazima angetumbuliwa"
be careful maana utaja umbuku humu
Nape atakuruka....leo kasema alijua kuwa ataondolewa
Sasa unasubiri nini kuchukua hatua dhidi ya unayemuita bashite kelele humu hazikusaidii, Kama una cha kufanya fanya siyo kupiga kelele humu hutafanikiwa watu wanataka matokeo ya kazi yake tu siyo vyeti vyake, nyinyi wenye vyeti safi mmefanya nini? Si mmeishia kuwa wezi tu
Kwani vip mkuu
Imekuwa ugomvi?
Kipi kinachokufanya ushikie bango kuwa watu wapo hapa kwa nia ya kumpigania nape au kumfariji?
What happened to nape has already happened..
Na hicho hakituzuiii sisi kuendelea kudiscuss na kubainisha what was wrong and what was right
Kutumbuliwa kwa. Nape mwenye maamuz ni juma poor manager
Uhalali wa makonda wa kuendelea kukaa hapo alipo hautokan na whether juma poor manager anapenda au hapendi ni kwamba uhalali wa kuendelea kukaa pale haupo
Na huyo Juma Poor manager hamlipi bashite kwa pesa yake ya mfukon la hasha anamlipa kwa kodi zetu
Na tuna haki ya kulisema hilo.
Sasa point yako hasa ni ipi?
Kwamba bashite alipovamia clouds media na bunduki iachwe hiv hiv?
Bashite amefoji vyeti iachwe hiv hiv?
Why iachwe hivyo na wengine wakifukuzwa kazi?
Double standards za nin
Watu wengine mnatumia nin kufikiri
Masaburi au?