Ndg Nape,
Kwa heshima na taadhima, ya hekima yangu niliyobarikiwa na Mungu, naomba leo niseme na wewe.
Nitasema na wewe kwa njia ninayoiita kunong'ona na wewe kwenye kona ya nuruni, ambayo sio ya siri kama ilivyo minong'ono mingine.
Kwanza kabisa nakupongeza kwa kuzaliwa katika viuno vya Mzee Moses Mnauye, Mungu Amlaze Pema(M.A.P), pili nikupongeze kwa uwezo wako mkubwa wa kutoa sauti inayoweza kusikika vizuri kupitia kisema mbali (microphone),hivyo sauti yako hunukuliwa maneno yako yote kama ulivyotamka, na hatutegemei siku moja useme ulinukuliwa vibaya.
Baada ya pongezi hizo, naomba nikutupie japo nasaha, ambazo hata hivyo sio lazima sana ukubali kuzifuata, ingawa zitaweza kukusaidia sana endapo utazitumia.
Mwaka 1993 nikiwa darasa la nne, nilifundishwa wimbo mzuri sana na mwalimu wangu wa sanaa, pale shule ya msingi Burunga, wimbo huu niliushika mpaka sasa ninapoandika hapa naendelea kuimba moyoni mwangu.
Wimbo unaimbwa hivi..."Tazama ramani...utaona nchi nzuri..yenye Mito na mabonde mengi ya nafaka.." kwa wale waliobahatika kufundishwa wimbo huu huko nyuma, watakubaliana nami kuwa wimbo huu ulikuwa na mvuto na kutufanya tutamani kuyaona yale amabyo mwimbaji aliyasifia.
Baada ya kukua na kupata elimu ya uelewa, nilijitahidi kutafuta nyimbo za kizalendo na hotuba za viongozi wa zamani wa taifa letu.
Nilitembelea maktaba ya Taifa, jijini da es salaam, nikabahatika kupata mahitaji yangu baadhi sio yote, lakini nilifarijika sana nilipoupata wimbo huu katika santuri na kaseti, nikanunua ile kaseti yenye wimbo huu, ambayo hadi sasa nausikiliza ninapoandika ujumbe huu kwako Bwana Nape.
Kumbe ni Mzee Moses Mnauye(M.A.P) baba yako mzazi, ndiye mtunzi na mwimbaji wa wimbo huu?!!!
Nilianza kutafuta chochote cha maana alichonufaika mzee huyu kwa utunzi wa wimbo wenye heshima na staha kwa nchi yetu.
Hata hivyo sikupata jibu lolote, na nikadhamiria kuandika Barua kwa waziri wa utamaduni ili lifanyike tukio la kumkumbuka mzee Mnauye, lakini juhudi zangu ziligonga mwamba baada ya kukutana na katibu wa wizara husika aliyeniambia kuwa, yupommtoto wake tena ni mwanasiasa, nijaribu kuonana nae ili yeye apokee wazo langu na kulifanyia kazi, ilikuwa 2004 licha kupewa namaba yako sikujaribu kukutafuta kabisa, kwani nilijua utalifanya ni suala la ki-ccm na sio la kitaifa.
Baada ya miaka miwili nilianza kukusikia Nape ukiwa katika harakati za kugombea wenyekiti wa UVCCM, ambao hata hivyo hukuwa na sifa sitahiki za kugombea na ukaondolewa mapema kabisa.
Hapo nikaanza kufuatalia nyendo zako kisiasa, ili nijue kama una ufanano wowote na mzee Mnauye,lakini nilikata tamaa nilipogundua kuwa huna hekima za kutosha katika maamuzi yako, hasa nilipokusikia ukijitokeza hadharani na kuanza kurusha maneno ya kejeli kwa viongozi wako wakuu wa chama.
Sina maana kwamba usiwakemee mafisadi katika ccm, ila niligundua kuwa ile sio haiba/ uhalisi wako,ila uliamua kufanya vile baada ya kuchakachuliwa katika uchaguzi ule, ambao wewe ulilenga kuwa kiongozi wa vijana.
Tabia hiyo ndiyo iliyomtisha mwenyekiti wako wa chama,kikwete, baada ya wewe kukosa nafasi ya kuwa mgombea pale ubungo 2010, na ikahisiwa kuwa kwa hulka yako ya kupenda utawala kuliko chama, ungeweza kushiriki katika upande mwingine wa chama cha siasa ili tu fanikishe kumwangusha yule aliyekuangusha katika kura za maoni.
Hivyo kwa hali hiyo jk aliamua kukuficha kusini mwa tanzani, akakutupia ukuu wa wilaya ili usihatarishe chama.
Kwa hili unatakiwa umshukuru jk, kwani baada ya mgombea wako ccm ubungo kushindwa vibaya, wewe ndiye ungeitwa suspect No.1, bila shaka ungewekewa vikwazo na kamati yenu ya maadili ya kuwa umemsaidia mgombea wa chadema kupata ushindi.
Nape, hukujua/ulijua sababu ya wewe kutupiwa ukuu wa wilaya, ila bado haikukusaidia kuchambua mbichi na mbivu, baada ya chama chako kubuni mbinu hewa ya kuwa kinajivua gamba, jk akaona tena wewe ndiye mtu muafaka, utaketumika kuwapiga wabaya wake, akakutupia nafasi hiyo uliyonayo ya uenezi, kwani alijua wewe bado una kinyongo kwa waliokuchakachua wakati UVCCM, na alijua kabisa utafanya kazi atakayokuapa bila koma wala nukta.
Kweli kijana mwenye sauti ya juu sana, inayosikika ukajitokeza na kuanza kuwachapa hadharani, na kweli kipigo cha mabua wamekipta, na ndio sababu nilisema kuwa sauti yako hatutarajii useme ulinukuliwa vibaya.
Kwa vita hiyo uliyotumwa kuipigana, imekumaliza na kukufanya uwe maarufu kwa kutoa kauli zinazoonyesha unafiki na uongo wako, hata yote uliyokuwa ukiyasema yote yamechujwa na kugundulika sio maneno yako, bali ni ya kupikiwa na kunyeshwa na kambi zenu za magamba.
Nape, umefika muda uone haya kuropoka hovyo, muda wa kuchunga domo lako, muda wa kukubali kuwa wewe sio zaidi ya mafisadi wenzako, ukubali kuwa huyo anayekuma ukadanganye wananchi atakuacha peke yako na utakapomhitaji. hutamwona, utamwita hataitka.
Na yale uliyotumwa uahidi kwa watanzania na kuwashawishi vijana wetu wakabidhi kadi feki za chadema, watanzania wataanza kukuhoji na utayalipa wewe peke yako.
Nape, umaarufu unatafuta utakupoteza, zigo ulilobebeshwa ni zaidi ya kg zako, pole kwa mijasho na ulemavu wa kudumu unaokunyemelea, kwa nerves zako kuuwawa na uzito wa zigo hilo.
Nakuomba sana, unisikilize japo sio jadi yako kuwasikilza wale usio waafiki, naomba uachane na kazi ngumu isiyo size yako, itakupoteza, itakuadhili na hutasikilizwa hata kwa ukweli utakaojaribu kuuleta baadae.
MIMI, nina uwezo mkubwa wa kukuandikia nyombo nyingi na nzuri utakazoweza kuimba na kuiweka nyota ya mzee Mnauye hewani tena,kwani hata kama hujui kuimba, mimi naweza kukupa somo na utaimba vizuri sana, nazingati kanuni za uimbaji, kwa mtu uliyezaliwa na mwanamuziki, ni lazima utafundishika na utaimba, hapo nitapata picha ya kurejea ile roho ya Mnauye.
EPUKA HILI ZIGO SIO LAKO NAPE, ACHA USHABIKI, ACHA UNAFIKI NA VISASI, HAUNA UPAMBANAJI WA KWELI NAPE..UNAAMBUKIZWA UNAFIKI NA VISASI WEWE UNACHEKELEA TU, HUJUI BADO UNA SAFARI NDEFU EE!!!?
Ila sasa nape nakuomba uonyeshe uhalisi wa vita unayotangaza kuwa unawavua magamba, hapa naomba ujitokeze na utangaze kujiuzuru nafasi hiyo(zigo) kama siku 90 zitapita bila hao mliowakusudia kuondoka ccm.
Vinginevyo....."Mawe ni mepesi mikononi, ila ni mazito yatakapotua usoni"
Aepukae mauti kwa kuogopa kulala ndani, hufia njiani na kuliwa na Tai- Nyakarungu