Nape na mafisadi wa CHADEMA

Jamani jamani, tunataka viongozi manaotoa dira ya dhati kwa maendeleo ya taifa. Kama tunaona ni busara kutaja madhaifu ya mtu m1 m1 kuwa ndiyo mahitaji ya msingi ya mtanzania!? Tumepotea sana. Nyerere ataendelea kuwa "nabii"!
 
Hivi siku 90 walizopewa magamba hazijaisha tu?
Wangekuwa na uwezo wa kuingia kwenye Bongo za watu na kudelete hiyo kumbukumbu ya siku 90 wangesha fanya hivyo!
Hii ni katika vitu vitakavyowadhalilisha sana, mfano wa aibu aliyoipata Riziwan JK juzi baada ya kutisha wakongwe na kushindwa kuwashitaki, na kuishia kung'aka pindi alipoulizwa sababu za kutochukua hatua!
 
Nilidhani Tundu Lisu ndo kachakachuliwa na Nape Nyau-ye!. Kumbe ni vilaza wa ccm, wal'o pretend kuwa cdm!! Nape ataambulia vichaa kama hao walio logwa akili zao na ccm kwa kofia zao. Maana zimefunga fikra zao, wasitambue zipi pumba na zipi ngano. NAPE, imekula kwako!!
 
Usanii tupu!!!! chama cha wasanii kinafanya mambo kisanii tupu. Ni vigumu kuelezea hizo fugure kisayansi. Bendera na kadi hizo zimechapishwa na CCM ili kuonesha umma kama sehemu ya propaganda zao. Siwezi kuamini kuwa bendera 87 zimerejeshwa na kadi 150 tena baadae wakaenda kulazimisha vijana au watu wengine kushusha bendera zao za CDM kwa nguvu. Wanatekeleza mambo hayo kwa nguvu ipi na mamlaka ipi? Hii inaonesha wazi kuwa wahusika ni vijana wa kijiweni waliolipwa fedha na kupewa maelekezo maalum. Hawafanyi hayo kwa mapenzi ya CCM.

Mambo kama hayo ndo yatakayo mmaliza Nape mapema!!
 
Mji wa Singida leo ulitekwa na CCM ndani ya Stendi ya Zamani ambapo Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa -CCM Nape Nnauye alitoa tuhuma mbali mbali zinazofanywa na Viongozi wakuu wa CHADEMA ndani ya Chama hicho na Kuelezea kuwa Viongozi hawa kwanza waangalie usafi wa Nyumba yao badala ya Kujinadi kwa usafi nje!
Jumla ya Wanachama 153 walirudisha Kadi za CHADEMA na bendera 87 za CHADEMA zilirudishwa! Ni pale mmoja wa walio rudisha bendera na Kadi za CHADEMA kukiri kuwa tangu ajiunge na CHADEMA amekuwa akiweweseka usiku na kujihisi ana ishi na kitu cha hatari ndani ya maisha yake kwani hata akigombana na majirani zake basi anajihisi kuandamana! Aliwavunja mbavu watu kwa kusema Chadema ni Chama cha Wahuni ambao hata Katibu wao Mkuu akiamanisha Dr Slaa hajaoa hadi leo na kusema kama mtu familia inamshinda kuishi na mwanamke ni ajabu kwa wanao mfuata kwani kwa Mila za Kiafirika Slaa bado anatakiwa asipewe siri za mambo ya nyumba hadi pale atakapo kua na kujitambua na kuoa!
Baada ya Mkutano huo vijana walizagaa mitaani na kuanza kushusha bendera zote za CHADEMA na kuharibu kila kitu chenye nembo ya CHADEMA. Kutokana na Uvunjifu huo wa amani polisi waliingilia kati na kuna vijana walikamatwa na hadi jioni walikua wameshikiliwa na polisi. Mkutano huu uliendelea huku kukiwa na mvua kubwa Mkoani Singida! Nape amesema Vijana wana haki ya kulinda Taifa na amani ya Nchi yao na kuendelea kuichagua CCM!

Hata mwandika hii thread kumbe ni fisadi tu. Unachukua maneno ya mtoto wa fisadi na kuyageuza kuwa maneno ya watanzania, kweli ukiwa na kinyesi usoni vigumu kuona. Huu ndio umaskini wenyewe, mwandika hii thread mwambie Nape "nani anawapa ukimwi wasichana wetu Tanzania kama si nyie mafisadi na watoto wenu?" Nani anawauwa watanzania? Muulizeni kiongozi wenu ccm fisadi kikwete lini watanzania watapata umeme? Mtanzania yupi anamwamini fisadi?

"Fisadi akishndwa kuongoza anatapatapa kama nyoka"
 
Kunya anye kuku akinya bata kahara ingekuwa ni mikutano ya CDM ungesikia viongozi wako ndani wote kama vile wao ndo wamewaambia watu wafanye hayo. Sasa hizi siasa ni za kishamba sana maana sidhani kama uongozi wa nchi unataka experience ya kuwa na mke maana kama ni hivyo ni hatari sana.
 
UMASKINI NA UJINGA NDIO MTAJI WA CCM mbona asije arusha atuambie hayo au aende shinyanga au hata Babati Singida vijana bado wako nyuma kimaendeleo thats why wanawarubuni kirahisi na pesa za mohamed dewji pita stend ya Singida utaona vijana hawana nguo ni t shirt za ccm watashindwaje kupewa buku wakatapike upupu jukwaani? Nape ya kujivua magamba imemshinda anarukia mambo asiyoyajua hivi kwani ashawaandikia barua? Wale watuhumiwa ka bado namkumbusha kama akiweza kuandika na moja iende pale magogoni kwa luteni kwan nafkiri inamhusu
 
Hawana chao hawa wafuasi wa chama cha Magamba. Wamebanwa kila kona sasa wanaweweseka mchanamchana. Wanajaribu kupunguza imani kwa wanaCDM bila mafanikio, maana kila kukicha wafuasi wanakuwa wengi mno afadhali ya jana. Sasa watu wameamka na wanajua maana ya propaganda na hawawezi kuwaamini hata kidogo. Labda wakiwashughulikia hao akina RACHAEL, na wakifanya hivyo ndio mwisho wao.
 
Hee!! Yaani ufisadi wa CDM ni mshahara wa Dr Slaa? Nape mbona unajizidishia kasi ktk kupoteza umaarufu wako? Nilikupenda ulipowatetemesha mafisadi wa jengo la UVCCM, sasa umesogezewa sahani pembeni na hao mafisadi wa mradi huo umeufyata wala huuzungumzii tena. Vijana wa UVCCM wanashangaa kitu gani kimekubadilisha?
 
Hee!! Yaani ufisadi wa CDM ni mshahara wa Dr Slaa? Nape mbona unajizidishia kasi ktk kupoteza umaarufu wako? Nilikupenda ulipowatetemesha mafisadi wa jengo la UVCCM, sasa umesogezewa sahani pembeni na hao mafisadi wa mradi huo umeufyata wala huuzungumzii tena. Vijana wa UVCCM wanashangaa kitu gani kimekubadilisha?

Wanalazimisha ufisadi wa Chadema na wanalinganisha vitu tofauti. Ufisadi wa CCM uko katika serikali yake na vitu kama EPA, Deep Green, Twin Towers, Richmond, IPTL ni multibillion -- hakika ndivyo vimechangia sana kuifikisha Tanzania tulipo. Au Nape hataki kulikubali hilo?

Nape azungumzia ufisadi wa CDM na sana sana ameona mshahara wa Dr slaa ndiyo unaimaliza nchi!

That is bullshit! CCM you are finished -- in total! Leave us CCM!
 
Kwani ufisadi ni nini?
au ufisadi unakua ufisadi pale tu unapo kua unaongoza serikali?
Dr.Slaa alimtaja mangula aliye kua katibu mkuu wa ccm kama fisadi,
au naye pia alikua kiongozi wa serikali?

Tatizo sio kutaja,tatizo ni kuwa na uwezo wa kusimama na kutaja,..
naamini siku itaisha hajafanya kitu,ila wakitaja pia ni mwanza wa
chadema kuondoa magugu,..
kusema kwamba ufisadi wa ruzuku ndogo za chama sio ufisadi tuna jidanganya,...
hao unao waona mafisadi wadogo siku wakishika nchi na level ya ufisadi wao itaongezeka,..

It's time to make chadema clean for the take over,and we need some one outside chadema
to point out the weakness chadema has,...and the time is now.
Tumia akili bwana, mangula alikuwa katibu mkuu wa chama tawala bwana na alikuwa anaidhinisha kuchota pesa EPA siyo CCM.
Mawili, nikukosa akili au upotoshaji wa makusudi.
Kweli Nape vuvuzela!
 
Watanzania msitegemee mabadiliko yoyote chini ya utawala wa CCM na makuwadi wake. Nchi hii itaweza pata mabadiliko pindi tu CCM ikiondoka au ikondoshwa kwa nguvu.
 
haijalishi gari chakavu ni chakavu tu

Aaah Makupa!? Bado unatumika tu!? Unatumika hadi unakuwa kipofu. Kama mikutano ni gharama kubwa kwa nini asiache kuifanya na kupeleka maendeleo kwa wananchi!? Au gharama inaihusu cdm peke yao? Ni upuuzi kusema kuwa gharama kubwa wanayoitumia cdm kwenye mikutano wangeitumia kuleta maendeleo wakati nyie ndio mliopewa dhamana! Fungua akili yako usiwe mjinga!
 
Nilipopata habari jana kwamba Nape Nauye ataanika ufisadi wa Chadema nilishtuka nikasema kama ni kweli basi Chadema wamekwisha.Wananchi wangeshangaa kuona wapiganaji wa ufisadi nao kumbe ni mafisadi.Nikawa na hamu kubwa kumsikia Nape akiunguruma.
Hatimaye nimepata mshangao mkubwa kumsikia Nape akidai kwamba ana nyaraka za siri zinazoonyesha mshahara wa Katibu Mkuu wa Chadema Dr Slaa ni mil 7.5 kwa mwezi.Nimeshangaa kwa sababu kubwa kwamba mshahara wa Dr Slaa uliwekwa hadharani na halmashauri kuu ya Chadema muda mrefu uliopita.Nimuulize Nape hivi kweli amekosa chochote cha kumpakazia Dr Slaa ikabidi ataje mshahara wake kwamba ndio ufisadi? Nape alitaka Slaa alipwe kiasi gani? Nape ndiye msemaji wa Chadema? Nape hajui kazi anayofanya kuwaelimisha watanzania kuzunguka huku na huko ni kubwa kuliko anacholipwa? Mbona Nape hashangai mshahara na posho wanayolipwa wabunge wa CCM ambao wanalala bungeni na wengine hawafungui midomo miaka mitano? Nape alitaka Slaa asilipwe halafu awe ombaomba mtaani? Au Nape alitaka Slaa aanze kuwapigia magoti mafisadi ili wampe fedha?
Pili eti Nape anadai Mbowe anaidai Chadema mil 500 kwa sababu ya magari yake yanayotumiwa na Chadema.Ebo! Sasa Nape alitaka Mbowe atoe sadaka? Nape ana mamlaka ya kuiamulia Chadema itumieje fedha zake? Naona Nape inamuuma roho anavyoona Chadema ikistawi kupita kiasi.Mbona Nape hatuanikii matumizi ya ruzuku CCM? Mbona hatuambii yeye kama Katibu itikadi na uenezi analipwa shilingi ngapi?
Hakika kama Nape anadai haya ndiyo mambo aliyotaka kulipua basi amechemsha tena vibaya sana.Na namshauri Nape akawaambie hao waliomtuma watafute mbinu nyingine.Kama Nape anadhani kusema mshahara wa Slaa Chadema itaacha kupambana na ufisadi basi ajue amechemsha.Namshauri Nape atafute kwanini chama chake kinachukiwa kila kona ya nchi.Ajue wananchi wamechoshwa na maisha magumu na kamwe asidhani watu watashiba akiwatajia mshahara wa Dr Slaa.
Mwisho:Niseme tu kwamba Dr Slaa ameipaisha Chadema inalipwa mamilioni ya fedha kama ruzuku kwa kazi kubwa aliyofanya na anayoendelea kufanya.Ameingiza wabunge wengi na madiwani wengi,nakumbuka Zitto Kabwe alisema Dr Slaa ameipandisha chati Chadema kwa asilimia 400.Niseme tu kwamba kwa kazi anayofanya Slaa bado Chadema inastahili kumpa heshima kubwa zaidi kuliko hata anacholipwa sasa.
Nape Umechemsha tafuta mbinu nyingine kwani Dr Slaa si saizi yako.
 
haijalishi gari chakavu ni chakavu tu

Aaah Makupa!? Bado unatumika tu!? Unatumika hadi unakuwa kipofu. Kama mikutano ni gharama kubwa kwa nini asiache kuifanya na kupeleka maendeleo kwa wananchi!? Au gharama inaihusu cdm peke yao? Ni upuuzi kusema kuwa gharama kubwa wanayoitumia cdm kwenye mikutano wangeitumia kuleta maendeleo wakati nyie ndio mliopewa dhamana! Fungua akili yako usiwe mjinga!
 
Kwakifupi hawana hoja, sheria ya mamunuzi ya serikali tangu lini ikatumika kwenye chama. Kama ndivyo basi sheria hiyo itumike kwa wananchi pia sijui ni wangapi kati yetu tungeweza kumiliki magari!
 
Back
Top Bottom