Nape na mafisadi wa CHADEMA

Nape na mafisadi wa CHADEMA

Huyu Nape baba yake ni Profesa Mwand..... Mzee Mussa Nnauye alibambikiwa tu.Kwa msimshangae dogo kuropoka.
 
Namshauri Dr. Slaa wala asihangaike kujibishana na huyu mtoto mdogo, swala la msingi ni kwamba amdharau tu inatosha.
 
Watanzania wenzangu,
Dr Slaa aliwahi kunukuliwa akisema mishahara ya Wabunge ni mikubwa sana haiendani na vipato halisi vya Watanzania walio wengi. Tukamshangilia sana humu. Leo tunaambiwa mshahara wake ni zaidi ya milioni7. Tunamtetea kwa nguvu zote. Tunamlaani na kumkejeli Nape. Ni kweli Dr Slaa kachangia pakubwa ruzuku ya sasa ya CHADEMA. Hili halihalalishi mshahara huu.
Labda ni kwa kuwa mkewe wa sasa anatarajia kujifungua! Kwa umri wa Dr Slaa kuzaa mtoto sasa ni shughuli pevu huko mbele.
 
Nape Nnauye amekuja na mpya anawatuhumu Dr Slaa na Mbowe, gazeti la mwanachi limemnukuu.
Nape anasema Dr Slaa ni mnafiki kwa kushinikiza Chama chake kumlipa Ths Mil 7na nusu wakati alipokuwa Mbunge alipinga mishahara wa wabunge kuwa ni mikubwa ambao ni mil 6.
Uwongo wa kwanza wa Nape.
Dr Slaa hajawahi kuomba mshahara huo, badala yake alikuwa anajiandaa kugombea ubunge ambako alikuwa nauhakika wa kushinda.
Uwongo wa pili; Kiwango chochote cha mshahara anaopata ni maamuzi ya kamati kuu kilichomwomba Dr Slaa agombee urais na siyo kiwango alichoomba Dr Slaa.. Zaidi ya hapo ni propaganda.
Tatu, wabunge wakati huo hawakulipwa mil 6 ni zaidi ya hapo – akafanye tena utafiti wake.
Mwisho, Nape kuulinganisha mshahara wa Dr Slaa – Katibu mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini na mbunge mmoja wa viti maalum au jimbo siyo sawa. Hivi, kuufananisha Mshahara Dr Slaa na mbunge mmoja wa CCM k ambaye anaweza kukaa miaka 5 bila kuchangia hata hoja mmoja bungeni kama tafiti zilivyoonesha huko nyuma ni sawa? Je, hajui mchango wa Dr Slaa katika nchi hii ni zaidi wabunge 20 wa chama chake? Hivi Nape anajua kuwa mkurugenzi wa shirika la Nyumba – NHC analipwa karibu mil 15 ambaye mchango wake hauwezi kufananishwa na Mchango wa Dr Slaa?
Kwa hiyo hoja ya Chadema na Dr Slaa kwamba mishahara ya wabunge ni mikubwa iko pale pale lakini siyo mshahara wa Dr Slaa hata kama kiwango hicho kingekuwa cha kwelil.

Kuhusu MboweNap anadai Mbowe anashinikiza Chama chake kimlipe Tsh mil 500 kwa ajili ya magari 3 aina ya Fuso ambayo alitoa kwa Chadema kwa mujibu wa wa gazeti la Mwanachi.

Mosi, Kiwango alichotaja sicho – amekikuza akafanye utafiti wake tena.
Pili, huo ulikuwa ni mkakati wa chama ili haikuwa na pesa hivyo Mbowe akaokoa jahazi la chama chake akanunua magari mapya.
Tatu, kama Mbowe alitoa kama mkiti mkarimu ili tufanyie kampeni kwa sababu hatukuwa na fedha wakati huo, leo tunazo na tuna uwezo wa kumlipa kwa nini tusifanye hivyyo? Hajui kuwa chadema haina mafisadi wa kuifadhili na haiwataki hata kama wangejipendekeza?
Nne Mbowe ni muungwana kwa kuwa hata hakuna mahali nimesikia akidai riba. Hivi Nape anajua riba ya Ths mil 500 kwa mwezi? Na anajua hayo magari tumekaa nayo muda gani? Je, tungedaiwa riba hizo ingekuwaje?

Mwisho Nape lazima ajue, hoja za chadema za Ufisadi wa CCM wa EPA, Downs, bil 200 zilizoibuliwa juzi na Dr Slaa, madai ya Mbowe kuwa 35% fedha zote za za serikali zinapotea kifisadi na tuhuma za Zitto kabwe kuwa Serikali imefilika na imeshindwa kulipa mishahara ya wafanyakazi hayawezi kujibiwa kwa propaganda dhaifu za namna hii. Hata hivyo, kama Nape anateleza maelekezo ya bosi wake JK kuwa kila siku waandikwe gazetini kwa kutoa kauli ili wapumue kidogo, nitamwelewa.
Aluta continua
 
Nape Mnauye .... huyu si mkuu wa wilaya...hivi watu wa hiyo wilaya wapo wapi ...... hivi wilaya kama hii isipokuwa na maendeleo italalamika....? hivi ni wilaya gani hii na ina mchango gani katika pato la nchi kwa juhudi za mkuu wa wilaya .... vinginevyo hii wilaya ifutwe ifanywe kata ...sioni sababu ya wilaya kuongozwa na katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi
 
Chadema hakuna mafisadi,Nape anapoteza mjadala wa mapacha watatu kwa kuingiza chadema. Hajatuambia kama barua za mafisadi zimetoka au la.
 
Nape Mnauye .... huyu si mkuu wa wilaya...hivi watu wa hiyo wilaya wapo wapi ...... hivi wilaya kama hii isipokuwa na maendeleo italalamika....? hivi ni wilaya gani hii na ina mchango gani katika pato la nchi kwa juhudi za mkuu wa wilaya .... vinginevyo hii wilaya ifutwe ifanywe kata ...sioni sababu ya wilaya kuongozwa na katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi

hivi bado analipwa mshahara na malupulupu ya DC?

huenda ni kweli manake sijasikia kajiuzulu au mtu mwingine kateuliwa mahali pake! sasa nini maana ya kuwajibika? huyu anawajibika saa ngapi kama DC? au anatumia simu/remote control? na likatiba letu hili hatuwezi kumwajibisha JK, jamani kweli watanzania tumenasa, sijui nani atatukwamua na matope haya mazito yenye magamba.

kwa kweli hapa duniani siasa za aina hii huenda zinapatikana tanzania pekee, halafu tunashangaa kwa nini hatpigi hatua kwenda mbele!
 
Chadema hakuna mafisadi,Nape anapoteza mjadala wa mapacha watatu kwa kuingiza chadema. Hajatuambia kama barua za mafisadi zimetoka au la.

Hili la barua za mafisadi si lenu CHADEMA. Lenu ni hili: Mnamlipa Dr Slaa sh milioni7 na nusu kwa mwezi? Dr Slaa ndiye Yaya Toure, Lionel Messi wenu? Katibu wako wa Jimbo la Ubungo analipwaje?
 
Nape hv anamaanisha nini kuwa hakuna MSAFI NCHI HII WOTE NIWACHAFU!
SIJAMUELEWA NAPE!
 
Nilishasema kuwa wengi wa hiyo serikali yenu ya ccm ni vilaza tu, yaani hawajui maana ya ufisadi among others.
 
Aaah Makupa!? Bado unatumika tu!? Unatumika hadi unakuwa kipofu. Kama mikutano ni gharama kubwa kwa nini asiache kuifanya na kupeleka maendeleo kwa wananchi!? Au gharama inaihusu cdm peke yao? Ni upuuzi kusema kuwa gharama kubwa wanayoitumia cdm kwenye mikutano wangeitumia kuleta maendeleo wakati nyie ndio mliopewa dhamana! Fungua akili yako usiwe mjinga!


Niboreshe kidogo Mh Filipo, CCM hawakupewa dhamana na wananchi, walijipa wenyewe kwa mkono wa Tume Chakachuzi. Asante
 
Mengi alooyasema Nape kayatoa humu JF. Nadhani naye ni member humu sasa. Muulizeni Dr Slaa ni kweli mshahara wake ni milioni hizo "chache" tu?
 
Nakubaliana na GTs wa JF kuwa CCM hakuna hata mmoja mwenye akili timamu. Wameoza wote, wote kabisa.

Huyu dogo Nape ni mbumbu wa kutupa. Mshahara ni malipo halali kwa kazi halali tena kwa makubaliano kati ya mlipa na mlipwaji.
Ukubwa au udogo wa mshahara sio hoja kwa mwenye utimamu wa fikra, bali matokeo ya kazi na ufanisi wa majukumu. Mifano ni mingi; kwani watu wa cheo kimoja wanaweza kutofautiana mishahara katika Kampuni/idara moja sembuse kampuni/idara tofauti. Kama CCM na serikali yake wangekuwa makini Nape asingesema hayo...wao wanawaza na kuweka sera mbovu na kufanya watu wa Tz kuwa duni sana na kuangamia kwa maskini, maradhi na ujinga.

Swali, je kwani Tz ina salary cap? Kwanini wabunge, mawaziri, RCs, DCs etc wanapata mishahara mikubwa tena mara mbili mbili kwa kuhodhi vyeo ili hali hakuna ufanisi wala maslahi kwa Taifa?

Kwa taarifa ya Nape, wananchi wa Tz wako tayari kuchanga fedha za kulipa mshahara wa Dr. Slaa. WaTz wangekuwa na mwamko wa kulipa kodi na kuleta maendeleo kwa manufaa yao kama wangekuwa na serikali na viongozi makini na waadilifu.

Hizo semina elekezi ni mfano wa karibuni zaidi wa ufisadi wa CCM.
 
Kwani ufisadi ni nini?
au ufisadi unakua ufisadi pale tu unapo kua unaongoza serikali?
Dr.Slaa alimtaja mangula aliye kua katibu mkuu wa ccm kama fisadi,
au naye pia alikua kiongozi wa serikali?

Tatizo sio kutaja,tatizo ni kuwa na uwezo wa kusimama na kutaja,..
naamini siku itaisha hajafanya kitu,ila wakitaja pia ni mwanza wa
chadema kuondoa magugu,..
kusema kwamba ufisadi wa ruzuku ndogo za chama sio ufisadi tuna jidanganya,...
hao unao waona mafisadi wadogo siku wakishika nchi na level ya ufisadi wao itaongezeka,..

It's time to make chadema clean for the take over,and we need some one outside chadema
to point out the weakness chadema has,...and the time is now.


kwanza Nape hanauhakika na anachokisema.Dr hakuomba alipwe huo mshahara kama anavyodai,kwa maana hiyo ukileta maana ya ufisadi yeye ndiye fisadi kwani analipwa mshahara wa cheo tofauti na alichonacho.Dogo Nape you are too young for politics,naomba nikukaribishe nyumbani au ofisini nikupe breakdown ya matumizi na mapato yetu ili unapotamka ujue unatamka nini.

Niliposoma hapa that you are still a baby sikuelewa now am getting it.please you are welcome for more investigation and i will show you everything.
Unapoona tunapambana nikwamba tunajiamini nje na ndani ya mioyo yetu,Hata mshahara unaoulalamikia njoo nikuonyeshe unaishia kwa watanzania wangapi, kumbuka Dr Slaa anachukuliwa kama kiongozi mkubwa wa nchi hivyo wapo watanzania wengi wanaoitaji msaada wake wa fedha.Tafadhali Njoo maana ninaviambatanishi vyote.Tuambie mshahara wako na mapato yako maana Dr anapowataja mafisadi anaeleza nini wamefanya na aina gani ya matumizi yanayopelekea ufisadi.

Mf.Majumba ya kifahari,malimbikizo ya mali mbalimbali na fedha kwenye mabenki.je Matumizi yaliyopitishwa kihalali toka lini yakawa ufisadi?
 
Hiyo milioni 7 ndo ameona kitu cha kuongea mbele ya watu wenye akili timamu?mbona anaongea kama anamatatizo ya kumbukumbu.Tena kama anasoma JF hebu ajaribu kuangalia nini anaongea,tena ajue siku 2015 chama chao cha magamba kikitoka atafute pa kwenda,bila maandamano nani angejua matatizo ya chama chake cha magamba,tena kama amechoka arudi kwao akatumikie wananchi.Asemi viongozi wake wanatumia kiasi gani kwenye anasa.Hii ndo shida ya kupeana uongozi kwa kulipa fadhila
 
Ama kweli newala wamepata Dc kihiyo Nape,ndo huyu huyu Dc aliyemuamuru OCD amkamate mwanakijiji aliyeshindwa kulima shamba la mihogo,gamba dogo linalokua kwa kasii hana jipya huyu mtoto anajua kubwabwaja tuuuuuu!
 
Watanzania wenzangu,
Dr Slaa aliwahi kunukuliwa akisema mishahara ya Wabunge ni mikubwa sana haiendani na vipato halisi vya Watanzania walio wengi. Tukamshangilia sana humu. Leo tunaambiwa mshahara wake ni zaidi ya milioni7. Tunamtetea kwa nguvu zote. Tunamlaani na kumkejeli Nape. Ni kweli Dr Slaa kachangia pakubwa ruzuku ya sasa ya CHADEMA. Hili halihalalishi mshahara huu.
Labda ni kwa kuwa mkewe wa sasa anatarajia kujifungua! Kwa umri wa Dr Slaa kuzaa mtoto sasa ni shughuli pevu huko mbele.

Lakini mshahara wa wabunge umebeba marupurupu mengine mengi km sitting allowances, mikopo maalum bado kuna mfuko wa jimboambao hatujui kama yeye pia haufaidi. Hivyo km Dr Slaa anapata tu 7m labda tujaribu kulinganisha na maofisa wengine katika nafasi kama yake. (Lazima ufanye job evaluation) Kwa mfano Makamba alikuwa anapata kiasi gani bila kuingiza malipo ya pembeni ya kifisadi. Na je ukiongeza za mafisadi alikuwa anapata kiasi gani?
 
Watanzania wenzangu,
Dr Slaa aliwahi kunukuliwa akisema mishahara ya Wabunge ni mikubwa sana haiendani na vipato halisi vya Watanzania walio wengi. Tukamshangilia sana humu. Leo tunaambiwa mshahara wake ni zaidi ya milioni7. Tunamtetea kwa nguvu zote. Tunamlaani na kumkejeli Nape. Ni kweli Dr Slaa kachangia pakubwa ruzuku ya sasa ya CHADEMA. Hili halihalalishi mshahara huu.
Labda ni kwa kuwa mkewe wa sasa anatarajia kujifungua! Kwa umri wa Dr Slaa kuzaa mtoto sasa ni shughuli pevu huko mbele.

Ni kweli ,Hembu tujuze malalamiko hayo yalifanyiwa kazi?

kama hapa naomba kujua unapozungumza hayo unajua vigezo vilivyotumika mpaka Dr Slaa kulipwa kiwango hicho?

Tunapokuwa tunapinga au tunachangia hoja nilazima tuwe na vigezo vya msingi na kujua sababu zote zilizopelekea mazingira hayo,Naomba sababu na vigezo viliwekwa wazi na siyo siri na mjadala ulijadiliwa kamati kuu na kura zilipigwa na hakuwa mmoja wa wapiga kura sasa ufisadi wake uko wapi.

Ni kwamba maneno kama haya hayatakosekana lakini ajenda yetu itabaki palepale

CCM AND HIS GOVERNMENT HAS FAILED TO DELIVER TO TANZANIAN,WE WILL CONTINUE FIGHTING THEM UNTIL THEN.
 
Back
Top Bottom