Filipo
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 9,342
- 5,536
Katika kile kilichoonekana kama ni muendelezo wa wananchi wa Arusha kuikataa serikali, muda mfupi uliopita dereva wa daladala iliyokuwa imesimamishwa na polisi pamoja na gari nyingine eneo la Aicc hosp, ili kupisha msafara wa makamu wa rais ambaye alikuwa anakwenda kupata lunch kibo palace hotel, alijikuta matatani baada ya kuwekwa chini ya ulinzi kwa muda.
Daladala hiyo ilikuwa inapiga wimbo wa bongo fleva unaosema "naongea na Riz1, ongea na mshua" kwa sauti ya juu sana wakati gari zilipokuwa zimesimamishwa. Alifuatwa na askari waliokuwa karibu na kumhoji sababu za kupiga wimbo huo pale na kwa sauti kubwa. Walimlazimisha azime na aseme aliyemtuma.
Hata hivyo alikubali kuzima na kukana kutumwa. Walimwacha baada ya abiria kumtetea kuwa wimbo unatoka kwenye kituo cha redio.
Duh! Kaaazi kwelikweli!?
Daladala hiyo ilikuwa inapiga wimbo wa bongo fleva unaosema "naongea na Riz1, ongea na mshua" kwa sauti ya juu sana wakati gari zilipokuwa zimesimamishwa. Alifuatwa na askari waliokuwa karibu na kumhoji sababu za kupiga wimbo huo pale na kwa sauti kubwa. Walimlazimisha azime na aseme aliyemtuma.
Hata hivyo alikubali kuzima na kukana kutumwa. Walimwacha baada ya abiria kumtetea kuwa wimbo unatoka kwenye kituo cha redio.
Duh! Kaaazi kwelikweli!?