Naona kama mke ananikwamisha

Naona kama mke ananikwamisha

2028 hiyo nyumba utauza 300m ila akili kumkichwa.
Asipofika 2028? Kimfaacho mtu chake. Apige bei 60M anunue au kujenga nyumba huko anakosema nje ya mji, 30M-50M awape UTT wamtunzie awe anakula 300K-500k kila mwezi hizo 40M zingine aanze hiyo biashara anayoiwaza pamoja na ya mke. Baadae biashara ikikaa vizuri anaweza ongeza mtaji toka kwenye pesa iliyo UTT
 
Wazazi wangu waliwahi kuniambia kwamba usikubali kuuza asset zako muhimu kutatua matatizo yako as long as upo mzima wa afya na una akili timamu

Watu wanauza asset zao kwasababu wameona fursa kubwa zaidi na sio kutatulia matatizo

Wewe hapo umeishiwa mbinu na sio pesa tu,
Angalia unakosea wapi badala ya kukimbilia kuuza nyumba...... ukikosea tu utabeba familia na kurudi kijijini kwenu au utakimbia familia

Tatizo ni kwamba utafunga akili yako ukifiria kuuza nyumba ndio solution pekee na kusahau kupambana

Wanasemaga ukianza kuuza vitu vyako vya ndani ni kama kula nyama ya mtu.... hautaacha
Baadae na hizo nyumba utauza tena mwisho utahamia kwenye fenicha, simu nk nk
Atakimbilia vipi kijijini wakati amekuambia ananunua nyumba sehemu nyingine na kufungua biashara?? Kuna faida gani sasa anapata kwa kuishi hapo na hela ya kula hana???
 
Yes tulikuwa tuko pamoja kwa miaka 10 hivi. Nilipopata hela ya kununua kiwanja, Yeye na madalali ndio walikuwa wanazunguka kutafuta mpaka niliporidhika ndio nikatoa pesa ya kulipa. Na ujenzi kwa kiasi kikubwa kasimamia yeye ndio yupo nyumbani muda wote mimi nikiwa kwenye mihangaiko.
Wenzio huwa tunajenga kwanza ndio tunaleta mke. Hapo 50 50 hukwepi! Chamsingi ongea nae na ikiwezekana yeye ndio ampigie huyo jamaa na jamaa akija mnakaa nae wote mnaridhishia kwamba hamna shida.

NB: kama yuko serious mwambie mtalipa gharama za mwanasheria maana huwa katika mkataba kuna domu ambayo mke nae anasaini kuridhia kwamba hana shida na nyumba kiuzwa!
 
Ni kama inaingia akilini hii!!! 😀😀😀😀😀 Ngoja nijipe muda.
Tumia muda wako wote kaka kufikiria, uzuri wa ardhi huwa haishuki thamani na badala yake huwa inaongezeka so usitumi sana kisa hiyo millions 150.

Wazo lako si baya ni zuri sana ila shida iliyopo ni kwamba wewe tayari unacho cha kupoteza, kwa maana unao watoto ambao watakuchanganya zaidi pindi mtakapokosa pahala pa kukaa.

Unaweza ukauza hapo ukaenda kununua nyumba nyingine then pesa nyingine ukaweka kwenye biashara, sasa umeshajiuliza what if hiyo biashara ikaenda kwa namna tofauti na vile ambavyo wewe ulikua unatarajia?

Jibu ni kwamba utarudi kujipa tena plan B ile ile ambayo ulijipa hapo awali kwa maana ubongo huwa inakawaida ya kurudia matukio ya kujicomfort pindi unapokutana na changamoto zile zile mfanano na kukawa na njia zile zile mfanano na ile ya awali ambayo ilitumika kusolve tatizo la namna hiyo.

Kwahiyo hii kwako inaweza ikaenda kuwa infinity loop, kwa maana utauza utanunua utauza utanunua over and over again.

Yes, huu ni ushauri wa kiprobabiliy na si kwamba nakukatisha tamaa ila nimeona tu labda nikukumbushe upande ambao labda haukuuwaza sana wakati wazo la kuuza hiyo nyumba lilipokita malangoni mwako.

So take your time, fikiria kwa kina then fanya maamuzi ambayo unaona yanafaa.
 
Miaka 15 iliyopita nilinunua kiwanja kwa shilingi milioni 4 nikaanza ujenzi wa nyumba kwa kuunga unga na nikahamia na familia nyumba ikiwa haijakamilika.

Namalizia kidogo kidogo huku nikiwa humo humo ndani. Miaka ya kati hapo nikapoteza channel kabisa, na sijaweza kumalizia hiyo nyumba, lengo ilikuwa kuweka madirisha ya alminium, mpaka sasa kuna grills na wavu tu.

Nyumba sio mbaya na finishing ilibaki madirisha tu. Nakadiria mpaka hapo imegharimu kama milioni 45 hivi. Ghafla tu miaka ya karibuni bei za viwanja na nyumba zimepanda sana huku kwetu, majirani zangu watatu ambao viwanja na nyumba zetu zinafanana wameuza kwa shilingi milioni 150, 160 na 180. Sasa mtu anataka kuninunua mimi kwa mil 150.

Kwa sababu nimepoteza channel nikawaza kupauza nianze upya kwa kununua nyumba mbili Mbezi Msumi, Msakuzi au Mpiji Magoe au hata Kibaha, moja ya kupangisha na moja ya kuishi, chenji nitumie kuanzisha biashara ya tyre service na kuosha magari kwa sababu naiwaziaga siku zote, kama chenji ikibaki nifungue na workshop ya carpentry na wife apate milioni 6 za biashara ya ndoto zake ambayo anaiwazaga miaka zaidi ya 8 sasa.

Tukaongea na wife tukakubaliana, hata yeye anaona tulivyopigika, wakati tumekalia ardhi ya bei mbaya ambayo hatuwezi hata kuindeleza. Sasa siku mteja amekuja kulipa tufanye hiyo biashara, nilikuwa nimetoka kidogo.

Nikafika nyumbani nikakuta mteja amefika kabla yangu na wife ameshamwambia tumeghairi hatupauzi tena!!! Nilitaka hata kulia. Na jamaa anasema ameshaghairi moja kwa moja anaogopa kununua nyumba yenye mgogoro.

Nilishakuwa na mipango kama milioni ya kujikwamua kutoka kwenye hili janga la umaskini sasa hivi naona giza tena. Na wife anasema tuendelee kutafakari kwanza kama miaka 2 hivi tukiona bado tunahitaji kuuza ndio tuuze!

HAPA NAANGALIA NAMNA YA KUFANYA ILI NIPATE HIYO HELA IKIWEZEKANA KWA KUACHANA NA HUYU MAMA TUGAWANE. Naamini nikipata milioni 80 naweza kujipanga upya, hili giza la kiuchumi limekuwa zito sana.
Mke wako mchawi nini hahahahahhahaha
 
Anasema watu wengi wanaouza miji yao hawawezagi kusimama tena kiuchumi na familia huwa zinayumba zaidi. Anataka tuuze mashamba yetu mawili kama ekari 30 ambayo tumeshindwa hata kuyalima. Sasa mashamba hatupati hata mil 30!!! Pamoja na mambo mengine lengo ilikuwa kuhama maeneo haya kwa sababu ya kukwepa dharau za majirani baada kutetereka kimaisha. Sasa tutahamaje huku? Majirani wanakuwaga kichomi sometimes, wanakuheshimu kwa ulicho nacho, ukifulia hata salamu wanaweza wasikupe. Wakati nikiwa na magari yalikuwa yanatumika kama ya kijiji, sasa hivi dharau mbele.
Ndio maana nimekwambia mkeo ako na hoja ya msingi kwasababu pesa siku zote huwa inawazingatia watu ambao hawaizingatii.

Wewe ni baba wa familia, utaanzisha biashara na biashara kikawaida huwa iko na hatua kwahiyo huwezi ukaianza Leo then ukategemea kesho ikupatie pesa ya kuanza kupay bills mbalimbali.

Je, ulishajiuliza utakapoanzisha hiyo biashara utakua tayari kuivumilia huku ukiendelea kuilea kwa muda gani, bila wewe kuitegemea ila yenyewe iendelee kukutegemea wewe?

Kwasababu si Kila biashara ambayo inakufa mkononi mwa mtu huwa ni mbaya ila huwa ni hali tu ya kushindwa kutofautisha kati ya biashara na kazi.

Kazi unaweza ukajitengenezea Leo na Leo hii hii ukawa unaweza kuingia mia mia mbili, ila biashara ni mfumo ambao na hakuna mfumo unaotengenezwa wiki au mwezi bali utahitaji muda kidogo.

Kama ulishawahi kuwa na pesa then zikapotea huwa mentality ya kuhisi watu wanakudharau haijawahi kuisha lakini kitu kikubwa zaidi huwa watu wengi waliowahi kupitia changamoto hiyo hufosi sana ili warudi pale ambapo walikua na kadri wanavyofanya hivyo ndivyo ambavyo hujikuta wanafanya makosa mengi yanayozidi kuwadidimiza chini.

Heka 30 kama ziko sehemu nzuri unaweza kujaribu kujipa challenge ya kuchukulia mkopo bank ili uingie kwenye hiyo biashara unayotaka kufanya uangalie upepo jinsi unavyoenda, ukiona biashara inaenda poa na inahitaji kujipanua zaidi uza hiyo nyumba tia pesa huko Jenga kakibanda somewhere then zungusha pesa katika hiyo biashara.
 
kuna watu wa ajabu kweli hii dunia,...unamshirikisha wife kwenye mambo yako,?🤔🤔❗ yani hapo wife alitakiwa aambiwe hapa tunaondoka na anaondoka bila kuuliza,... mwanamke atakushauri nn?📍📌 hayo ndo madhara ya kumuona mke ni mwenzako,....🚮
Wameoana badala ya yeyejamaa kuoa ndo mana
 
Kuna ndugu zangu waliwahi kuuza mashamba kwa Millioni. 100 mwaka 2007. Pesa iliisha ndani ya wiki tatu. Ama kweli pesa ni makaratasi. Ama kweli huyo mke anaakili. Niliwahi fundishwa na mama yangu kwamba usipende kuuza vitu ulivyo nunua kwaajili ya matumizi yako na familia yako. Utakuja kuuza hadi makabati na vitanda.
 
Mkuu kama jambo mlishalijadiri Kwa pamoja na mkapanga mipango inakuaje abadiri pekeyake bila kukushirikisha kweli kuuza sio kuzuri ila kama wewe ulimshirikisha akakubali iweje abadili gia angani bila kukushirikisha?
Hii nayo inafikirisha mkuu😂😂😂
 
Usiuze hilo eneo endelea kuganga njaa miaka 5 ijayo utamshukuru wife. Na sie kidogo tuachane miaka kadhaa nyuma eneo tulilinunua 10m bei zikapanda hadi 70m mwenza alivyoona hela aliona haiachi nikakataa tukaishi kama maadui muda mrefu sana leo hii ni 250m namkumbusha kuhusu kupauza hataki tena ananiona mie ndo nina tamaa tena. Utapata kazi tu ama biashara zitanyooka tu vumilia ndugu.
 
Miaka 15 iliyopita nilinunua kiwanja kwa shilingi milioni 4 nikaanza ujenzi wa nyumba kwa kuunga unga na nikahamia na familia nyumba ikiwa haijakamilika.

Namalizia kidogo kidogo huku nikiwa humo humo ndani. Miaka ya kati hapo nikapoteza channel kabisa, na sijaweza kumalizia hiyo nyumba, lengo ilikuwa kuweka madirisha ya alminium, mpaka sasa kuna grills na wavu tu.

Nyumba sio mbaya na finishing ilibaki madirisha tu. Nakadiria mpaka hapo imegharimu kama milioni 45 hivi. Ghafla tu miaka ya karibuni bei za viwanja na nyumba zimepanda sana huku kwetu, majirani zangu watatu ambao viwanja na nyumba zetu zinafanana wameuza kwa shilingi milioni 150, 160 na 180. Sasa mtu anataka kuninunua mimi kwa mil 150.

Kwa sababu nimepoteza channel nikawaza kupauza nianze upya kwa kununua nyumba mbili Mbezi Msumi, Msakuzi au Mpiji Magoe au hata Kibaha, moja ya kupangisha na moja ya kuishi, chenji nitumie kuanzisha biashara ya tyre service na kuosha magari kwa sababu naiwaziaga siku zote, kama chenji ikibaki nifungue na workshop ya carpentry na wife apate milioni 6 za biashara ya ndoto zake ambayo anaiwazaga miaka zaidi ya 8 sasa.

Tukaongea na wife tukakubaliana, hata yeye anaona tulivyopigika, wakati tumekalia ardhi ya bei mbaya ambayo hatuwezi hata kuindeleza. Sasa siku mteja amekuja kulipa tufanye hiyo biashara, nilikuwa nimetoka kidogo.

Nikafika nyumbani nikakuta mteja amefika kabla yangu na wife ameshamwambia tumeghairi hatupauzi tena!!! Nilitaka hata kulia. Na jamaa anasema ameshaghairi moja kwa moja anaogopa kununua nyumba yenye mgogoro.

Nilishakuwa na mipango kama milioni ya kujikwamua kutoka kwenye hili janga la umaskini sasa hivi naona giza tena. Na wife anasema tuendelee kutafakari kwanza kama miaka 2 hivi tukiona bado tunahitaji kuuza ndio tuuze!

HAPA NAANGALIA NAMNA YA KUFANYA ILI NIPATE HIYO HELA IKIWEZEKANA KWA KUACHANA NA HUYU MAMA TUGAWANE. Naamini nikipata milioni 80 naweza kujipanga upya, hili giza la kiuchumi limekuwa zito sana.
Una uhakika mlikubaliana vizuri? Laah! Mke wako anakuheshimu vizuri kama kichwa cha familia? Inakuwaje anatoa majibu ambayo yangehitaji mwenye mji kwanza afike? Siku hizi baadhi ya wanawake hawana heshima hata mbele ya ugeni! Hii inaleta shida sanaa.
 
Atakimbilia vipi kijijini wakati amekuambia ananunua nyumba sehemu nyingine na kufungua biashara?? Kuna faida gani sasa anapata kwa kuishi hapo na hela ya kula hana???
Hujanisoma vizuri mkuu

Ukimsoma vizuri mleta hoja tatizo lake wala sio MTAJI
Kama alikua anajishughulisha hadi akajenga nyumba hiyo na kununua magari lakini akaja kufeli..... hapo utabaini hata akiuza apate hizo hela uwezekano wa mambo kumuendea komba tena ni mkubwa, na ataendelea na tabia ya kuuza hata hiyo aliyo nunua akidhani ni MTAJI... hapo ndio atakimbilia kijijini au kuikimbia familia

Assume angekua hana nyumba na anapitia hali hiyo angefanyaje?
Tatizo ni kwamba hawezi kufikiri tena nje ya box zidi ya kudhani nyumba ndio suluhisho la matatizo yeke

Akibali kurudi moja ajipange.... huu ni ushauri tu, muamuzi ni yeye
 
Miaka 15 iliyopita nilinunua kiwanja kwa shilingi milioni 4 nikaanza ujenzi wa nyumba kwa kuunga unga na nikahamia na familia nyumba ikiwa haijakamilika.

Namalizia kidogo kidogo huku nikiwa humo humo ndani. Miaka ya kati hapo nikapoteza channel kabisa, na sijaweza kumalizia hiyo nyumba, lengo ilikuwa kuweka madirisha ya alminium, mpaka sasa kuna grills na wavu tu.

Nyumba sio mbaya na finishing ilibaki madirisha tu. Nakadiria mpaka hapo imegharimu kama milioni 45 hivi. Ghafla tu miaka ya karibuni bei za viwanja na nyumba zimepanda sana huku kwetu, majirani zangu watatu ambao viwanja na nyumba zetu zinafanana wameuza kwa shilingi milioni 150, 160 na 180. Sasa mtu anataka kuninunua mimi kwa mil 150.

Kwa sababu nimepoteza channel nikawaza kupauza nianze upya kwa kununua nyumba mbili Mbezi Msumi, Msakuzi au Mpiji Magoe au hata Kibaha, moja ya kupangisha na moja ya kuishi, chenji nitumie kuanzisha biashara ya tyre service na kuosha magari kwa sababu naiwaziaga siku zote, kama chenji ikibaki nifungue na workshop ya carpentry na wife apate milioni 6 za biashara ya ndoto zake ambayo anaiwazaga miaka zaidi ya 8 sasa.

Tukaongea na wife tukakubaliana, hata yeye anaona tulivyopigika, wakati tumekalia ardhi ya bei mbaya ambayo hatuwezi hata kuindeleza. Sasa siku mteja amekuja kulipa tufanye hiyo biashara, nilikuwa nimetoka kidogo.

Nikafika nyumbani nikakuta mteja amefika kabla yangu na wife ameshamwambia tumeghairi hatupauzi tena!!! Nilitaka hata kulia. Na jamaa anasema ameshaghairi moja kwa moja anaogopa kununua nyumba yenye mgogoro.

Nilishakuwa na mipango kama milioni ya kujikwamua kutoka kwenye hili janga la umaskini sasa hivi naona giza tena. Na wife anasema tuendelee kutafakari kwanza kama miaka 2 hivi tukiona bado tunahitaji kuuza ndio tuuze!

HAPA NAANGALIA NAMNA YA KUFANYA ILI NIPATE HIYO HELA IKIWEZEKANA KWA KUACHANA NA HUYU MAMA TUGAWANE. Naamini nikipata milioni 80 naweza kujipanga upya, hili giza la kiuchumi limekuwa zito sana.


After 2 yrs, utauza hadi 200mil plus, but pia vifaa vya ujenzi na mahali utataka kununua vitapanda at the same rate, hivyo economically hiyo extra 50 mil in 2 yrs haina faida yoyote, hivyo mshawishi mkeo
 
Asipofika 2028? Kimfaacho mtu chake. Apige bei 60M anunue au kujenga nyumba huko anakosema nje ya mji, 30M-50M awape UTT wamtunzie awe anakula 300K-500k kila mwezi hizo 40M zingine aanze hiyo biashara anayoiwaza pamoja na ya mke. Baadae biashara ikikaa vizuri anaweza ongeza mtaji toka kwenye pesa iliyo UTT
Ni ushauri mzuri pia kama hatozuzuka na pesa maana kuna watu wakishika hela mipango insyeyuka anatumia tu hovyo hovyo kwasababu ipo.
 
Back
Top Bottom